Mamlaka ya DPP ni kufuta kesi kama kufanya hivyo kutakuwa ni kwa masilahi ya taifa au kwa nia ya kulenga kupata haki, hivyo hatua za kufuta kesi jana hazikuwa kwa masilahi ya taifa bali ilikuwa ni kuizuia mahakama kutoa haki, kilichofanyika jana ni matumizi mabaya ya mamlaka ya DPP,
HATUA TULIZOCHUKUA.
1. Leo tumefungua kesi mahakama kuu kwa hati ya dharura , kwa kuiomba mahakama iitishe mafaili yote mawili ,ili iyachunguze ione kama haki imetendeka kwa mujibu wa sheria za nchi yetu.
2. Wameiomba kama itakubali ifute ile hati ya DPP ya kufuta mashitaka, na ifute amri ya mahakama ya kufuta kesi iliyofanyika jana ,
3. Ielekeze mahakama ya hakimu mkazi kisutu , iendelee na utaratibu wa kutoa hukumu kama ilivyokuwa imepangwa , na hii ni kwa masilahi yab haki ionekane inatendeka.
Kilichofanyika n a mwendesha mashitaka wa serikali ni kuingilia uhuru wa mahakama katika kutenda haki.