Mahakama Masjala Ndogo ya Dar es salaam April 30, 2026 imekataa ombi la Tundu Lissu la kuunganishwa katika shauri namba 8323/2025 lililofunguliwa na Said Issa Mohamed na wenzake dhidi ya Bodi ya Wadhamini wa Chama pamoja na Katibu Mkuu wa Chama.
Awali, baada ya Lissu kuwasilisha ombi hilo, mawakili wa upande wa Said Issa Mohamed na wenzake waliwasilisha mapingamizi wakipinga ombi hilo. Hata hivyo Mahakama Machi 03, 2026 iliyatupilia mbali mapingamizi hayo, hivyo ombi la msingi likaruhusiwa kuendelea kusikilizwa.
Kwa mujibu wa Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Dkt. Rugemeleza Nshala, ambaye pia alikuwa sehemu ya jopo la mawakili wa Lissu, amesema kuwa leo asubuhi April 30, 2026 Lissu alifikishwa Mahakamani lakini uamuzi uliotolewa umetupilia mbali hoja za Lissu kutaka kuunganishwa katika kesi hiyo.
Brenda Rupia: Ni kweli kuwa, Mwenyekiti alifikishwa mahakamani kusomewa uamuzi mdogo kufuatia Maombi yake ya kuunganishwa kwenye kesi ya said Issa Mohamed na wenzake wawili dhidi ya Bodi ya wadhamini na Katibu Mkuu wa Chama.
Katika uamuzi wake, Mahakama kuu imekataa Maombi ya Mhe Lissu kuunganishwa kwenye kesi hiyo.
===============
Walalamikaji: Said Issa Mohamed (Makamu Mwenyekiti mstaafu), Ahmed Rashid Khamis, na Marehemu Maulida Anna Komu.
MHE LISSU AFIKISHWA MAHAKAMANI LEO
Leo Asubuhi, Mheshimiwa Lissu amefikishwa Mahakamani kusomewa uamuzi mdogo kufuatia Maombi yake ya kuunganishwa kwenye kesi ya Said Issa Mohamed na wenzake dhidi ya Bodi ya wadhamini wa Chama na Katibu Mkuu.
Kuna mambo mawili hapa ya kukumbuka; Mosi, Maombi ya Mhe Lissu yalisikilizwa na Mwanga hivyo kisheria yeye alipaswa kutoa uamuzi wa Maombi hayo.
Pili, Ikumbukwe kwamba jalada la kesi ya Said Issa Mohamed na wenzake dhidi ya Bodi ya wadhamini na Katibu Mkuu, lilishaondoka mezani kwake, lipo kwa Jaji Ngunyale.
Sasa, Jaji Mwanga katika uamuzi wake amekataa Maombi ya Lissu kuunganishwa kwenye hiyo kesi.
Ufafanuzi zaidi utatolewa na Chama.
Wakili @ShundoGaston,
Mkurungenzi wa sheria wa CHADEMA HQ.