masopakyindi
Platinum Member
- Jul 5, 2011
- 17,882
- 13,172
Mimi ni.msikilizaji mzuri wa kipindi cha Usalama barabani,kila asubuhi Radio One, saa moja na robo baada ya taarifa ya habari.
Askari wote kila siku wanasikika vizuri ,hata yule wa Mwanza Sajenti Ninga leo kasema kuna ka mvua Mwanza, so madereva wawe makini.
Kimbembe kipo kwa Sajenti Ahijo wa Mbeya, kila siku hasikiki vizuri. Simu ina mikwaruzo, mara inakatika, mara hasikiki kabisa.
Tunakushauri Sajenti Ahijo na Kamanda Trafiki Mbeya, Sjenti aache kutumia simu kimeo na abadili line .
Nikiifikiria simu anayotumia Sajenti Ahijo ni kama imefungwa rubber band kuishikilia, na mtandao anaoutumia wa bei chee.
Kama unalitangaxia Taifa, tumia simu au mtandao unaoeleweka kwa sehemu za milima kama Mbeya.