Safari yangu mkula irrigation scheme

UMASKINI HAPANA

Senior Member
Jan 3, 2017
105
47
Kuchelewa kwa mvua msimu huu ulinipa changamoto ya kutafuta mashamba katika Irrigation schemes kwani huko huwa hakutegemi mvua, kulima ni mara mbili kwa mwaka na kuvuna ni uhakika. Katika hangaika hangaika zangu nilipata wasaa wa kufika kijiji kimoja kinaitwa Mkula kwenye Mkula Irrigation scheme. Kwa kweli wanakijiji wa Mkula wana neema, maji ya uhakika pale mashamba yao yana rutuba kuvuna ni uhakika kwa kweli ni raha wana Mkula wamependelewa kwa kiasi chake sidhani kama wanaijua njaa kabisa. Tatizo ni kuwa mradi una cover ekari chache sana, niliuliza nikaambiwa ni ekari 600 tu ambazo zinamilikiwa na wanakijiji takribani 148. Mwenye kujua Irrigation schemes zingine wazimwage hapa ili tukipata wasaa watu tunatembelea na kwenda kujifunza kilimo huko.

JF Members, wakulima na wajasiriamali karibuni kuchangia.
Asanteni.
 
Hizi ndio mambo Magu na wenzie walitakiwa kuanza nazo badala ya kukimbilia kununua mapangaboi. Serikali ingewekeza kwenye infrastructure za kilimo kama hizi tuondokane na kutegemea mvua na kulialia njaa.

Watengeneze hizi scheme za kutosha na wanaotaka kulima wanaweza kukodishwa au kuuziwa. Na kwa kilimo cha kisasa kabisa huitaji eneo kubwa sana kupata mazao mengi. Kwa watu wa subsistence farming akiwa na eka zake mbili anazoweza kulima mara mbili kwa mwaka zinamtosha kabisa. Eka moja ya mbunga, kwa mfano, inaweza kutoa mpaka gunia 50 (kwa msimu mmoja) kwa kilimo kinachozingatia mbinu bora na za kisasa za kilimo.

Tanzania haipaswi kuwa na njaa. Tuna tatizo la vipaumbele tu.
 
Tuombe mwenyezi Mungu ampe neema rais wetu magufuri ya kuliona hili maana lipo ndani ya uwezo wake. Kama ameweza kununua ndege kwa cash, kujenga hostel udsm kwa cash, kujenga nyumba za maaskari ukonga kwa cash ni dhahiri anaweza jenga irrigation schemes za maana kwa cash. E mwenyezi Mungu mujaarie Rais wetu alione hili.
 
Kuchelewa kwa mvua msimu huu ulinipa changamoto ya kutafuta mashamba katika Irrigation schemes kwani huko huwa hakutegemi mvua, kulima ni mara mbili kwa mwaka na kuvuna ni uhakika. Katika hangaika hangaika zangu nilipata wasaa wa kufika kijiji kimoja kinaitwa Mkula kwenye Mkula Irrigation scheme. Kwa kweli wanakijiji wa Mkula wana neema, maji ya uhakika pale mashamba yao yana rutuba kuvuna ni uhakika kwa kweli ni raha wana Mkula wamependelewa kwa kiasi chake sidhani kama wanaijua njaa kabisa. Tatizo ni kuwa mradi una cover ekari chache sana, niliuliza nikaambiwa ni ekari 600 tu ambazo zinamilikiwa na wanakijiji takribani 148. Mwenye kujua Irrigation schemes zingine wazimwage hapa ili tukipata wasaa watu tunatembelea na kwenda kujifunza kilimo huko.

JF Members, wakulima na wajasiriamali karibuni kuchangia.
Asanteni.
Hiyo mkula ipo wapi hebu funguka mkuu
 
Tuombe mwenyezi Mungu ampe neema rais wetu magufuri ya kuliona hili maana lipo ndani ya uwezo wake. Kama ameweza kununua ndege kwa cash, kujenga hostel udsm kwa cash, kujenga nyumba za maaskari ukonga kwa cash ni dhahiri anaweza jenga irrigation schemes za maana kwa cash. E mwenyezi Mungu mujaarie Rais wetu alione hili.
Hii komenti ilibidi iwepo jukwaa la siasa sio hapa!
 
Naming'ongo Irrigation Scheme Momba - Songwe ambayo ina ekari zaidi ya 6000 ila kwa sasa imecover ekari 1500 tu
 
Scheme ya Naming'ongo ni moja ya Scheme ya Umwagiliaji ya muda mrefu,kutokana na sababu mbalimbali za kifedha na kiutendaji ilishindwa kukamilika kwa wakati lakini kwa sasa Scheme imekamilika kwa asilimia 70 bado ukamilishaji wa mifereji inayoingia mashambani na upimaji wa mashamba.

Scheme hii ya Naming'ongo inapatikana ndani ya Mkoa mpya wa Songwe,Wilayani Mombo katika vijiji vya Makamba na Chitete.

Hadi sasa ni ekari 1500 zilizolimwa kati ya ekari 6000,awamu ya pili inategemewa kukamilisha upimaji wa ekari 4500 zilizobakia.

Bado nafatilia taarifa za upatikanaji wa mashamba lakini kwa sasa ni wakulima wachache wa vijiji vya jirani wanaofaidika na Scheme hii.

Kwa maelezo Zaidi Inbox au Wasiliana na ofisi ya Mkurugenzi wa halmashauri ya Momba.
 
Nenda Kashagulu Irrigation Scheme ipo Uvinza eneo lipo takribani 1200Ha linalolimwa ni 200Ha tuu.Lakini utalazimika kutumia Boti/ Meli maana hakuna barabara za uhakika.
 
JE KM NAITAJI KULIMA KWENYE HIZO SCHEME NI HATUA GANI NIFUATE AU MASHARTI YAKE YAKOJE
 
Kwa ufafanuzi: Mkula ni kijiji ambacho kipo katika tarafa ya mang'ula, wilaya ya kilombero mkoani morogoro. Ni kilometa chache tu kutoka kilipo kiwanda cha sukari cha kilombero kama unaelekea ifakara.
Nyumbani hapo baada ya kuanza wilaya ya kilombero unapita vijiji vya mkamba, Kidatu, msolwa, sanje halafu mkula, serikali ingejaribu kulizingatia hili.
 
Hizi ndio mambo Magu na wenzie walitakiwa kuanza nazo badala ya kukimbilia kununua mapangaboi. Serikali ingewekeza kwenye infrastructure za kilimo kama hizi tuondokane na kutegemea mvua na kulialia njaa.

Watengeneze hizi scheme za kutosha na wanaotaka kulima wanaweza kukodishwa au kuuziwa. Na kwa kilimo cha kisasa kabisa huitaji eneo kubwa sana kupata mazao mengi. Kwa watu wa susbstistence farming akiwa na eka zake mbili anazoweza kulima mara mbili kwa mwaka zinamtosha kabisa. Eka moja ya mbunga, kwa mfano, inaweza kutoa mpaka gunia 50 (kwa msimu mmoja) kwa kilimo kinachozingatia mbinu bora na za kisasa za kilimo.

Tanzania haipaswi kuwa na njaa. Tuna tatizo la vipaumbele tu.
shikamoo SMU
 
  • Thanks
Reactions: SMU
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom