28 March 2025
Goma, Kivu ya Kaskazini
DR Congo
Viongozi wakuu kijeshi wa SADC SAMIDRC na AFC mubashara katika shughuli ya maridhiano iliyofanyika hoteli ya Serena Goma ...
View: https://m.youtube.com/watch?v=8CaXVcTyRJg
Mmoja wa viongozi wakuu wa kijeshi kutoka nchi za SADC kutoka Tanzania Major General Ibrahim Michael Mhona wa TPDF / JWTZ akiwa ameshika nyaraka za maridhiano.
Makubaliano hayo yalifanyika huku viongozi wakuu wa pande hizo mbili za SADC SAMIDRC na waasi wa AFC / M23 kwa bashasha na kuheshimiana huku furaha ikionekana baada ya maafikiano hayo...
Wengine waliohudhuria hafla hiyo ni General Rudzani Maphwanya, mkuu wa majeshi ya ulinzi ya Afrika ya Kusini SANDF; Lieutenant General Geoffrey C. Zyeele, kamanda wa jeshi la Zambia ; Major General Saiford Kalisha, mwakilishi wa mkuu wa majeshi wa Malawi ; Professor Kula I. wa kamati ya Stroika ya SADC ya siasa, ulinzi na mambo ya usalama
Pia mbali ya Major General Sultani Makenga; alikuwepo Brigadier General Bernard Byamungu, naibu mkuu wa majeshi ya waasi ARC / M2R; na Bahati Musanga Erasto, Governor wa jimbo la Kivu ya Kaskazini DR Congo .
TOKA MAKTABA :
19 January 2022
KOZI USALAMA NA STRATEJIA
Major General Ibrahim Michael Mhona wa TPDF / JWTZ alipata kuwa mkuu wa Chuo cha Ulinzi wa Taifa, chuo mahiri kwa mafunzo ya mapana yanayohusiana na stratejia mkakati mbalimbali
View: https://m.youtube.com/watch?v=YGH4z19yylk
Katika video hii maktaba jenerali Ibrahim Michael Mhona wa anafafanua masomo ya NDC Chuo cha Ulinzi wa Taifa yanayotolewa, ambayo yana mambo mtambuka mengi