SADC yaingia makubaliano na AFC/M23

SADC yaingia makubaliano na AFC/M23

Ni kweli. Lakini, huyo mbelgiji anawazidi nguvu hawa SADC? Jibu ni hapana. Pia, jambo usilotakiwa kusahau, siasa ni mchezo mchafu. Hata marekani kupitia tume yake, imeshasema serikali haina uwezo wa kulinda raia na mali zao mashariki mwa nchi hiyo. Hivyo, M23 wana sababu za kupigania haki zao. Na kumbuka. Dunia nzima, inategemea eneo hilo. Nani akubali kupoteza biashara yake? Hapo rais keshapata pigo, na akikubali tu, ameisha. Bora tu nchi waigawe, wazungu watakula meza moja na M23.
SADC imfanye nini Mbelgiji?
SADC hawa Msumbiji walishindwa na Kivu wameshindwa tena. Kama wameshindwa dhidi ya M23 ndio waiweze Belgium ikiamua.
 
AFC/M23 kusaidia majeshi ya SADC kuondoka nchini
-SADC kuondoka na silaha zao, huko za serikali ya DRC zikikabidhiwa AFC/M23.

1743216215759.jpeg

Tanzania’s Major General Ibrahim Michael Mhona and Alliance fleuve Congo AFC military commander Major General Sultani Makenga sign the agreement on SADC troops’ withdraw, on Friday, March 28, 2025 during their meeting at Serena Hotel, in Goma DR Congo
 
28 March 2025
Goma, Kivu ya Kaskazini
DR Congo

Viongozi wakuu kijeshi wa SADC SAMIDRC na AFC mubashara katika shughuli ya maridhiano iliyofanyika hoteli ya Serena Goma ...


View: https://m.youtube.com/watch?v=8CaXVcTyRJg
Mmoja wa viongozi wakuu wa kijeshi kutoka nchi za SADC kutoka Tanzania Major General Ibrahim Michael Mhona wa TPDF / JWTZ akiwa ameshika nyaraka za maridhiano.

Makubaliano hayo yalifanyika huku viongozi wakuu wa pande hizo mbili za SADC SAMIDRC na waasi wa AFC / M23 kwa bashasha na kuheshimiana huku furaha ikionekana baada ya maafikiano hayo...

Wengine waliohudhuria hafla hiyo ni General Rudzani Maphwanya, mkuu wa majeshi ya ulinzi ya Afrika ya Kusini SANDF; Lieutenant General Geoffrey C. Zyeele, kamanda wa jeshi la Zambia ; Major General Saiford Kalisha, mwakilishi wa mkuu wa majeshi wa Malawi ; Professor Kula I. wa kamati ya Stroika ya SADC ya siasa, ulinzi na mambo ya usalama



Pia mbali ya Major General Sultani Makenga; alikuwepo Brigadier General Bernard Byamungu, naibu mkuu wa majeshi ya waasi ARC / M2R; na Bahati Musanga Erasto, Governor wa jimbo la Kivu ya Kaskazini DR Congo .


TOKA MAKTABA :
19 January 2022

KOZI USALAMA NA STRATEJIA
Major General Ibrahim Michael Mhona wa TPDF / JWTZ alipata kuwa mkuu wa Chuo cha Ulinzi wa Taifa, chuo mahiri kwa mafunzo ya mapana yanayohusiana na stratejia mkakati mbalimbali

View: https://m.youtube.com/watch?v=YGH4z19yylk
Katika video hii maktaba jenerali Ibrahim Michael Mhona wa anafafanua masomo ya NDC Chuo cha Ulinzi wa Taifa yanayotolewa, ambayo yana mambo mtambuka mengi
 
Meja jenerali Ibrahim Michael Mhona wa kutoka TPDF (JWTZ) moja ya majeshi chini ya mwamvuli wa SADC SAMIDRC akibadilishana nyakara za makubaliano na Meja jenerali Sultani Makenga wa majeshi ya waasi wa AFC / M23

1743218763519.jpeg
 
Hii ni aibu kwa Tanzania

Walikuwepo maofisa wa wakuu wa kijeshi kutoka South Africa, Malawi, Zambia na Tanzania, hili ni suala la kikanda na siyo la taifa moja yaani Tanzania.

TOKA MAKTABA :

UCHAMBUZI WA HALI HALISI YA OPERESHENI ZA SAMIDRC
25 February 2025
Dar es Salaam, Tanzania

Hakuna jeshi lililokuwa na ndege yenye uwezo wa kuwasafirisha wanajeshi waliojeruhiwa vitani DRC kurudi nyumbani - Theletsane


View: https://m.youtube.com/watch?v=-SLqLuk8rXg
hayo yamebainishwa katika mahojiano.

Mkurugenzi wa Ogani ya Masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa SADC Profesa Kula Theletsane anasema hakuna kikosi chochote cha kijeshi cha nchi katika kanda hiyo ya SADC ikiwa ni pamoja na jeshi la ulinzi la South Africa SANDF, kilikuwa na ndege yenye uwezo wa kuwasafirisha kurudi nyumbani wanajeshi waliojeruhiwa vitani kutoka DRC. Anasema badala yake ilitumiwa ndege ya kibinafsi charter .

Habari zaidi zinasema kuwa jijini Dar es Salaam mkutano wa wakuu wa kijeshi wa nchi za SADC wanakutana kutekeleza maazimio ya mkutano wa wakuu wa nchi za SADC na EAC uliofanyika Dar es Salaam 08 February 2025 ambapo wakuu hao wa nchi walikubaliana kuwa sahihi ni kufungua jukwaa la mazungumzo kwa kuwa njia za kijeshi pekee haziwezi kumaliza mzozo wa Mashariki ya Congo...

SADC’s Director of Organ on Politics Defence and Security Affairs Professor Kula Theletsane says none of the military units in the region including SANDF, had a plane with the capacity to transport back home the wounded soldiers from DRC. He says a private plane was used instead.
 
TOKA MAKTABA :

Jeshi imara la South Afrika tangu 2016 misheni zake Congo zimeshindwa pamoja na kuwa wana zana kali za kisasa :

View: https://m.youtube.com/watch?v=x6BYYyukjDI
Hii 𝘀𝘁𝗼𝗿𝘆 ilirushwa mara ya kwanza 𝟭𝟴 𝗦𝗲𝗽𝘁𝗲𝗺𝗯𝗲𝗿 𝟮𝟬𝟭𝟲.

Akisindikizwa na helikopta maarufu ya Rooivalk mfano wa ngome yenye ulinzi uliosheheni silaha kali , Carte Blanche anasafiri hadi kambi ya kijeshi iliyotekwa hivi majuzi ndani ya misitu ya tropiki kaskazini mwa Beni katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

John Webb anapata ruhusa ya kipekee kuvifikia vituo vya mstari wa mbele vya jeshi la South Africa SANDF katika eneo maarufu la liliopachikwa jina la kuogofya la Pembe Tatu ya Mauti (Triangle of Death) katika Mkoa wa Kivu Kaskazini tunapowatembelea wanajeshi wetu walio mstari wa mbele katika vita dhidi ya waasi wa ADF.

Tunakutana na wanajeshi ambao uMauti umeshindwa kuchukua roho zao katika uwanja wa vita na vile vile katika majukumu muhimu ya usaidizi wa mapigano, na marubani wa SANDF wanaofanya kazi kama sehemu ya kitengo cha anga cha Umoja wa Mataifa ambao wamekuza sifa ya ustadi na ujasiri wa kufika maeneo haraka kupambana na adui.

Carte Blanche pia anakutana na Jenerali wa SANDF Derrick Mgwebi ambaye aliteuliwa kuongoza operesheni ya jumla ya Umoja wa Mataifa ya kulinda amani nchini DRC - ambayo bado ni Misheni kubwa zaidi ya kulinda amani duniani.

View: https://m.youtube.com/watch?v=x_SYts84EGM
 
Meja jenerali Ibrahim Michael Mhona wa kutoka TPDF (JWTZ) moja ya majeshi chini ya mwamvuli wa SADC SAMIDRC akibadilishana nyakara za makubaliano na Meja jenerali Sultani Makenga wa majeshi ya waasi wa AFC / M23

View attachment 3286488
kitambo sana huyu makenga hajaonekana hadharani walidai alikuwa mgonjwa, sasa kaja kutokezea huku
 
Maono ya rais mstaafu Joseph Kabila yamezingatiwa

TOKA MAKTABA :

23 February 2025

View: https://m.youtube.com/watch?v=FEiyHSsFXjM
DRC Crisis needs more than a military solution.

"Given the history of its member states, Sadc should know better.The grievances of the Congolese people against their government must be addressed"

-Joseph Kabila in the Sunday Times opinion column writes.
 
SA wanatamani wangekuwa na hata robo ya uwezo wa jeshi lao la wakati wa kaburu. jeshi la kaburu lilikuwa noma sana.

Jeshi hilo liliundwa na mercenaries wa Angola 🇦🇴. jamaa wakiitwa 32 (unatamka three two) Battalion wakijulikaana pia kama "Terrible Ones". 🤣

Hawa wamba ilikuwa hawashindwwi vita. wamekiwasha sana miaka hiyo hata hizi vita za Congo. lilivunjwa ulivokuja utawala wa mweusi.
Screenshot_20250329-071709_Chrome.jpg
 
Kwenye mkutano wa viongozi wakuu wa majeshi ya nchi wanachama wa SADC, huko Goma, Serena Hotel, badhi ya makubaliano yamefikiwa, ikiwa ni pamoja na haya:

-AFC/M23 kusaidia majeshi ya SADC kuondoka nchini
-SADC kuondoka na silaha zao, huko za serikali ya DRC zikikabidhiwa AFC/M23.

-wataalam wa SADC na M23 kukagua hali ya uwanja wa ndege wa Goma kwa sasa

-SADC imekubali kukarabati uwanja wa ndege wa Goma

-AFC/M23 imeikubalia SADC, kwamba, baada ya ukarabati, itumie uwanja huo kuondoka wanajeshi wake na silaha zao (SAMIDRC).


Kwa kifupi, AFC/M23 ndo mshindi wa vita, na eneo ililopigania, ni haki yake.
Niliandika humu kuwa AFC /M23 wataikalia Goma katika harakati za Kivu Republican
 
Back
Top Bottom