SABC washangaa Rais Samia kumteua Tony Blair kuwa mshauri wake

Ni ujinga wa kiwango Cha juu kufikiri kuwa tukihitaji chanjo lazima tupitie Kwa secretary of state, Magufuli alinunua Boeing mbili USA je tulipitia Kwa secretary of state? Samia ni mweupe tu Wala sioni agenda yeyote.

Ni vizuri tukajibizana kwa hoja na sio matusi huko ni kuonesha uvivu wa kufikiri. Unafananisha kununa ndege Boeing na kupata chanjo? Ndege ni hela yako tu lakini Vaccines sio hivyo kwani hazitoshelezi kwa kila muhitaji. Serikali ya marekani inasimamia hizo vaccines jinsi zinavyogawiwa na ndio maana nchi maskini wanalalamika kuwa hawatendewi haki katika mgawo wa hizi chanjo!!! Wakubwa wanataka wajiridhishe wao kwanza halafu ndio masikini wapate hapo baadae, wakati huo watu wao wanateketea!

Sawa Magufuli alikwenda BOEING na hela zake kwenye sandarusi akanunua ndege kwasababu ziko nyingi; hizi chanjo sio hivyo, the supply cannot meet the world wide demand hence the skewed rationing!! Lakini mkitaka za WARUSI au WACHINA mnaweza kununua nazo zipo!!!
 
Kubeba fedha za umma kwenye sandarusi ni kosa la jinai
 
Kuna kitu umechanganya hapa.
Kuna mtu anaitwa Tony Blair (huyu ndio mshauri wa mama Samia wa sasa) na kuna waziri mkuu wa Uingereza aliyekuwa anaitwa Tony Blair (huyu ndio alishirikiana na Mkapa kuhakikisha Tz tunasamehewa madeni). Hawa ni 'watu' wawili tofauti ukiwatazama kwa jicho la kidiplomasia.

Kama ilivyokuwa kwa mama Samia, kuna mama Samia aliyekuwa makamu wa rais na kuna mama Samia rais wa Tz. Hawa ni 'watu wawili' tofauti ukiwatazama kwa jicho la kimamlaka.
 
SIo Kweli, chanjo hazitengenezwi na USA state , ni private companies ambazo zimekuwa authorized kuuza popote duniani, south Africa wamenunua chanjo kutoka katika makampuni hayo bila kuwa na direct contacts za Biden or so called secretary of state, vaccines ni biashara kama biashara zingine, Samia kachemka, uwezo mdogo
 

Serikali ya Marekani imetumia fedha nyingi sana kuyawezesha haya makampuni kufanya utafiti wa hizi chanjo hivyo wana sauti kubwa katika usambazaji wake. Sio kweli kuwa South Africa wamenunua chanjo toka makampuni huko Marekani bali wao wanatengeneza wao wenyewe under license!! Biashara nyingine ni strategic [ kama vile silaha] hivyo hazifanywi kiholela bila mkono wa Serikali na hii ya chanjo ni moja wapo!!!

Mama Samia hajachemka lolote kwani vaccines za kutosha zipo nchini hivi sasa anaetaka chanjo anapata; nyie mnaopinga chanjo ndio mmechemka! Mna ajenda yenu ya siri, mwishowe mtalegea na kushindwa.
 

Nakubaliana na wewe kuwa kimamlaka ni watu tofauti lakini kiutu wao ni watu wale wale!!! Huwezi kuwa na Mamlaka bila utu bali waweza kuwa na utu wako bila Mamlaka!
 
Mwaka 2016 mzee mmoja aitwa John Chilcot alifanya assessment ya kitendo cha Tony Blair kuiingiza nchi yake kwenye uvamizi wa Iraq.

Tathmini ile ilimmaliza kabisa Tony Blair pale iliposema kwamba yeye (Blair) na George Bush waliudharau Umoja wa Mataifa na kuamua (wao wenyewe) kuivamia Iraq.

Tony Blair mwenyewe akihojiwa na Fareed Zakaria wa CNN mwaka 2015 aliomba radhi kwa makosa aloyafanya na akakubali kwamba kulikuwa na ukweli kwenye madai uvamizi ule ulisababisha kuibuka kwa kundi la ISIS.

Tukiachana na hayo, Tony Blair ni mwanasheria nguli, msemaji na mzungumzaji mzuri yaani "keynote speaker and Performer" na hualikwa kwa kutoa mihadhara mingi ya faragha kwa pesa ndefu sehemu mbalimbali duniani.

Tony Blair amewahi kuwa mhadhiri wa masuala ya utandawazi na imani katika vyuo vikuu vya Yale na Divinity na baadae akashiriki kuanzisha stashahada katika masuala hayo iitwayo Globalisation Initiative kwenye vyuo hivyo vya Yale, Durham cha UK na national University cha Singapore.

Iliripotiwa kuwa Tony Blair ana kamba zilizounganishwa kwenye kampuni iitwayo UI Energy Corporation na huvuta mpunga wa kutosha kutoka huko.

Hii kampuni inajishughulisha na utafutaji na uchimbaji wa mafuta, madini, uwekezaji wa vituo vya kufulia umeme na pia inajishughulisha na usambazaji wa vifaa vya mahospitalini yaani medical equipment.

Hawa UI Energy ni sehemu ya mtandao mkubwa yaani Consortium wa makampuni mengine mengi tu humo uitwao KNOC Bazian Limited.

Hili la Tony Blair kuwa mshauri wa serikali ya Tanzania si geni, kwani nchi zingine kama Khazakhstan zimemtumia kusafisha taswira ya nchi hiyo ambayo ilikuwa na rekodi chafu kabisa ya ukiukaji haki za binadamu na rekodi hiyo bado ipo palepale.

Kuna mauaji makuwa yalifanywa nchini humo yaloitwa "Zhanaozen Massacre" na Tony Blair akatumiwa na raisi wa nchi hiyo Nazabayev kufanya kitu chaitwa damage-limitation advice.

Tony Blair amewahi kuwa mshauri wa masuala ya biashara kwa serikali ya Misri.

Tony Blair ni mjasiriamali na ana hisa katika makampuni kadha wa kadha na kiasi cha fedha za kutoka katika akiba ya benki.

Juzijuzi mzee huyu ametajwa katika orodha ya watu ambao ni mashuhuri lakini wanaweka fedha nje ya nchi zao, orodha ilopewa jina la Pandora Papers.

Uwezo wake wa fedha na ushawishi wake mkubwa umemfanya kuwa na marafiki au watu wengi ambao hujihusisha nae kwenye masuala ya biashara yaani Associates na alianzisha kitu chaitwa Tony Blair Associates.

Hawa hukusanya fedha na kuzielekeza katika miradi au shughuli mbalimbali barani Afrika na nchi za mabara mengine.

Ndipo akaanzisha taasisi iitwayo Institute for Global Change.

Pamoja na mambo mengine mengi taasisi hii kwa sasa imejikita kwenye janga la COVID-19.

Hivyo hii waita Government Advisory Practice ambapo taasisi hii ina watu kama 200 hivi ambao wamesambazwa katika nchi hizi za Afrika na zingine.

Kwa Afrika kuna nchi 14 kama za Senegal, Rwanda, sasa Tanzania na Zanzibar wamejiingiza humo hivi karibuni.

Vaccine Management for Africa.

Huu ndo mpango wenyewe ambapo Tony Blair kwa kupitia taasisi yake wanashirikiana na Oracle ambao ni wataalam wa kanzidata kuboresha mifumo ya kuweka kumbukumbu za afya katika mpangilio wa kisasa.

Hii Oracle Health Management System itasaidia kurahisisha usambazaji na utoaji wa chanjo na rekodi za watu wote walochanjwa zitahifadhiwa kwenye kanzidata iitwayo Cloud.

Kwa kifupi ni kwamba kama umechanjwa Afrika na wataka kwenda Ulaya au Marekani basi itakuwa rahisi kupata taarifa zako kwa wakati muafaka.

Hivyo hiyo yaweza kuwa ni moja ya masharti kwa serikali ya Tanzania kuondolewa kwenye ile Red List.

Pili hii kanzidata ya OHMS ikiimarishwa itasaidia nchi za Afrika kuweza kuwa na mipango mingine zaidi ya kupambana na si tu COVID-19 bali magonjwa mengine kama polio na surua.

Ikumbukwe kuwa nchi za Afrika kwa kukubali kushiriki katika mpango wa COVAX na mingine kama huu wa OHMS zimepewa miaka 10 kutumia mfumo huo na kupata msaada wa kitaalam na bila malipo.

Hivyo kwangu mimi sioni kama kuna tatizo kwani sisi kama nchi bado tupo nyuma sana kiteknolojia na kufikiri nje ya boksi.

Na ndo maana hata raisi wetu ametangaza kujengwa kwa chuo kikubwa sana cha Tehama Tanzania ambacho kitafundisha vijana masomo ya sayansi na kompyuta ingawa tayari wasomi wa tasnia hizi wapo na wanazurura mitaani.

Hivo tukijadili tuangalie zaidi Context ya mradi ( IFGC) na sio mtu binafsi maana yeye bado aruka na ndege huku na huko duniani kupiga pesa ya maana.
 
Ww na wee unataka mada tu ya kuongelea sasa nafasi yenyewe ya ushauri ni ya ushauri kuhusu Covid 19 ? Kweliii ? Alafu huyo anaekwambia Tony Blair hana credibility pengine amfahamu Tony Blair .. huyu ndiye alibahatika kuaminjwa na chama chake cha labor akiwa kijana tu ..akasema yy akipewa nafasi bac kipaumbele chake cha kwanza ni Elimu, cha pili ni elimu na tatu ni elimu

Kwa UK kuna mambo mazuri kawafanyia pale England.

Alafu mwisho kabisaa ili swala la chanjo mbonaa hata wa tz wenyewe sie wengi hatuja chanja na sio case ...angekiwa kkateuliwa kuwa mshauri ktk mambo ya uchumi au madini hapo kweli tungesema toba toba yaraaabi yaraaabyaaa
 
Kapotea kabisa. Tony Blair is worthless kabisa kuwa mshauri.

Ina maana hajamwona mwanamke mwenzake Githa Gopinath ? Au Mohammed El Erian ? Vipi kuhusu Condoleezza Rice?

Anazidi kupoteana kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…