Sabah Muchacho

Kaolewa na Muchacho...

Kama hujui kitu bora ukae kimya.

Muchacho ambae ni maarufu sana Tanzania kwa watu wa zamani, kaka yake Sabah, kwa jina anaitwa Abdulrahman na alikuwa meneja wa timu ya simba iliyokuwa na mafanikio makubwa sana wakati wa awamu yake, enzi hizo za 70s.

Sabah, amewahi kuolewa na mume wa kwanza jina Hussein, nae ni marehemu, waliachana kabla hajafa. Na akaolewa tena na Mume mwingine aitwae Salum, huyu ni mpiga kinanda maarufu wa taarab hapo miaka ya nyuma, nae ikatokea kuitwa kwa umaarufu wa Muchacho kwa ajili ya mkewe na si yeye mwenye jina hilo la Muchacho.

Jina la Muchacho alilipata huyu meneja wa Simba, kutokana na sinema za zamani za ki western "cowboy", kuna actor maarufu aliyekuwa aki act kama Gang Leader wa ki Mexicano (Fernando Sancho) na alikuwa akilitumia sana hilo neno Muchacho.

Kwa umbo la huyo mcheza filam Fernando Sancho na ni gang leader, na kwa kuwa Abdrahman Muchacho ni kaka mkubwa na mwenye umbo kubwa kama la Fernando Sancho, katika ukoo wao wenye vijana wa kiume wengi sana, na mwanamke mmoja tu Sabah, basi hilo jina la Muchacho likamkaa na mpaka kesho ni umaarufu wake huo na hakuna mtu wa zamani wa Tanzania na mpenda soka asiyemjuwa Muchacho. Pia Abdrahman muchacho ni mpenzi wa Taarab na alikuwa muimbaji, nadhani bendi yao ya kwanza ilikuwa ikiitwa MAMESH iliyomilikiwa na Ahmed Azzan, na hapo walikuwa wana waimbaji watatu na wote ndugu, Sabah, Abdrahman na Ibrahim Muchacho (Marehem) na ndipo alipopatikana mpigaji kinanda Salum ambae akaja kumuoa Sabah na akajulikana kama Salum Muchacho.

Sabah ana mume na watoto watatu, Samira, Nuru na Ahmed. Samira na Nuru wameshaolewa na wanaishi nje ya Tanzania, Ahmed bado anasoma (secondary).

Kwa hiyo ukweli ni kwamba mumewe Sabah ndiye aliyechukuwa jina la umaarufu la kina Muchacho kutoka kwa kina Sabah na si vinginevyo.

Habari za siku nyingi Game Theory. Umeadimika!
 
Kaolewa ila ana mtoto wake changu kama nini

Usilolijuwa ni usiku wa kiza. Sabah ana watoto wawili wa kike na wote wameolewa na wako kwa waume zao nje ya Tanzania. Mmoja US mmoja Canada.

Wacha kutukana watu usiowajuwa na kuwaharibia character zao. Huo ni ujinga wa hali ya juu.
 
Usilolijuwa ni usiku wa kiza. Sabah ana watoto wawili wa kike na wote wameolewa na wako kwa waume zao nje ya Tanzania. Mmoja US mmoja Canada.

Wacha kutukana watu usiowajuwa na kuwaharibia character zao. Huo ni ujinga wa hali ya juu.

Usipaniki mkuu kwani vicheche hawaolewi??
 

Duh mkuu una data utadhani WIKIPEDIA
 
Mzizi Mkavu wewe chiboko!! Uzi wa mwaka gani? Ume mmiss saana jamaa? lol....
 

asante kwa ufanunuz mzuri..
cc FaizaFoxy
 
Last edited by a moderator:
Inna li Llahi wa Inna Illahi Rajiun, Muchacho, meneja wa zamani wa simba anaeongelewa hapo amezikwa jana.

Huyo Muchacho wa Simba aliefariki ndo huyo aliyetajwa na Zomba kwa jina la Abdurhaman?
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…