Sababu za wameru kumkataa Siyoi Sumari

Sababu za wameru kumkataa Siyoi Sumari

Muda na sanduku la kura ndiyo mwamuzi wa mwisho

Kwa Tz yetu isiyokuwa na democrasia sidhani kama sanduku la kura ndilo huwa linasema ukweli kwani tume ndiyo inaamua kwakupindisha kura
 
Muda na sanduku la kura ndiyo mwamuzi wa mwisho

Hakutakuwa na kuchakachua? maana hata Wameru wakiamua kufanya kweli na kuwatosa wale jamaa wa chanikiwiti, lakini je ule mchakachuo?
 
Sijui ni nani atashinda, lakini nakumegea siri kuwa wameru wamekudanganya, wangekuwa wakweli wasingemnyima Sarakikya kura kwa kishindo.

Pale ni nguvu ya pesa iliyotumika. Kwa hiyo kama jamaa anaweza kuhonga wameru wote basi atashinda Sioi.
 
sioi ni pandikizi limeletwa ili kuja kuitawala Meru. Hatuwezi ruhusu hili, si kweli kwamba meru yote haina viongozi, sii kweli kwamba koo zote hapa meru zimelaaniwa ila kina sumari na sii kweli kwamba matumbo ya mama wote wa meru yamelaaniwa ila tumbo hilo,... Kamwe hatuta ruhusu ufalme huu kuendelea, hatutaruhusi kuendelea kuzaraulika kiasi hiki, hatuta ruhusu masikira ngama.. na wamasai waendelee kutupangia wawakilishi. Imetosha na imefikia kikomo.
Tutampa mmeru, aliezaliwa meru na anaejua mazingira na mahitaji ya meru..kama hayupo bora tupige kura za maruhani. Wameru wa nairobi na huko Dar hatuwataki na tusiwaone.

Sisi ndio wameru na meru tutampa mmeru mwenzetu tulie mchagua na kamwe hatutaruhisu yeyote atuchagulie mbunge.
Umenifurahisha sana eti wameru wa Nairobi....
 
Kuna ulazima gani wa kujua kusalimia kimefu? Old school politics! Njooni na points dhidi ya mgombea siyo hizo irrelevants
 
Mkuu kuna wakati lazima ukubali kwamba vitu vingine haufahamu, binafsi mimi ni Mtanzania lakini sijui mila na desturi za kila kabila na kila mkoa, lakini nijuavyo mimi ziko sehemu swala la lugha ni moja ya sifa ya mgombea, hili lilimletea shida sana Joseph Kabila kwa kutojuwa Lugha ya Kilingala mpaka ikambidi afanye Alliance na Zanga Mobutu ili apate kura za upande wa wanaozungumza kilingala, kwahiyo si vyema kujifanya unafahamu kila kitu hapa jamvini. wewe unajuwa hili na huyu anajuwa lile, ukiona mtu anajuwa kila kitu basi ana tatizo huyo

Kuhusu swala la Nassari kusema anaishi Marekani ni sawa na kutuambia Lipumba nae anaishi Marekani na Uswiswi, huku ni kupungikiwa na uelewa na sidhani kama unafahamu vyema status ya mtu mpaka aitwe ni mkazi wa nchi fulani, nina uhakika huna ufahamu huo ndio maana unaropoka tu, badilika kifikra mkuu.

Mapenzi mabaya sana Aisee! Sasa mie kujenga hoja kupingana na maneno ya muanzisha hii thread unaniambia na ropoka..

Jamaa yako anasema Siyoi sio mkazi wa Arumeru.

Siyoi hajui Kimeru.

Siyoi amekosa utu.

Siyoi katumia milioni 700..

Sasa hapa sijui nani karopoka au haya maneno maneno unayapenda sababu yanakuliwaza.

Mkuu ushauri wako huu umejaa chuki badalika.
 
Ni kweli hayo yanasemwa.. Ila yanasemwa na wachache walio na uelewa... Ila asilimiaa kubwa ya wazee wao hawamwangalii mtu... Wao wanajua ccm basi... Pia kuna hoja mbili kubwa wanazozisema.. Ya kwanza sioi hajawai kuwa na interest za kisiasa.. Hana record ya kisiasa ndani ya arusha pia kuna ishu ya wabunge wengi kuwa wanatokea eneo na barabara ya Akeri.... Kuna mengi yanazungumzwa ila lazima tukubali kuna changamoto nyingi sana...
 
Mapenzi mabaya sana Aisee! Sasa mie kujenga hoja kupingana na maneno ya muanzisha hii thread unaniambia na ropoka..

Jamaa yako anasema Siyoi sio mkazi wa Arumeru.

Siyoi hajui Kimeru.

Siyoi amekosa utu.

Siyoi katumia milioni 700..

Sasa hapa sijui nani karopoka au haya maneno maneno unayapenda sababu yanakuliwaza.

Mkuu ushauri wako huu umejaa chuki badalika.

Kama unaona ushauri wangu umejaa chuki basi achana nao, ila mimi binafsi Simjui Sioyi Sumari mpaka alipojitokeza kuchukuwa fomu CCM na wala sizifahamu siasa za Arumeru na sijui Majority ya wakazi wa Meru percent kubwa ni kabila gani, lakini kama Percent kubwa ni Wamasai basi hili haliitaji Degree kujuwa CCM itashinda pale kwa offer za kuwachinjia ng'ombe Wamasai kila siku.
 
Sijui ni nani atashinda, lakini nakumegea siri kuwa wameru wamekudanganya, wangekuwa wakweli wasingemnyima Sarakikya kura kwa kishindo.

Zile 700m zilikuwa za nini sasa, hakuna kishindo hapo.
 
Yale yale ya mshili mmoja kuwasemea wengine kutoka upande ule na sasa kuna wameru wengine wamewasemea wengine wa upande huu. Naomba niwe wa mwisho kuamini haya yamesemwa kwa niaba ya majority ya wameru.
 
Sample size gani hiyo ?

How can one conclude by just talking to a few people ?
 
wote uliowataja hawaishi meru.kwa wameru hili ni jambo kubwa.lakini ni lazima tujue meru ni jimbo lenye wamasai na wameru kwa wingi hata hivyo sikumbuki ni lini mmasai aliwahi kushika jimbo hili!
Ole saitabau?
 
Zile 700m zilikuwa za nini sasa, hakuna kishindo hapo.

oooh! Kumbe wameru wananunulika!
Kwa hiyo zikiletwa milioni 700 nyingine au zaidi wataendeleza kawaida yao ya kugeuzwa/kufanywa bidhaa?
 
Back
Top Bottom