Sababu za vegetarians kutokula nyama


Dunia inaelimu za kila aina, wasiokula nyama kwa sababu za kiimani ukiwasikiliza wana maelezo yanayo onekana yana logic kibinadamu,kiafya na kiumbaji. wapo kiroho zaidi na wanaujua mfumo wa mahitaji ya mwili, mfumo wa uyeyushaji chakula, mfumo wa upumuaji. Wanasababu nyingi ikiwemo za kukataa kutoa uhai lakini pia wanasema.
Mfumo wa taya na meno ya binadamu haujaumbwa kula nyama, pia
Inachelewa kusagwa mwilini hivo kutengeneza sumu. Japo baadhi ya hoja zina ukweli, lakini kama issue ya uhai hata mimea na matunda ina uhai isipokuwa haina roho. Na kwa Elimu yao mwisho wa Siku wanaishia kwenye Miungu yao kama krishna, n.k
Tunaokula nyama tunazo sababu za kula nyama kama ifuatavyo.
Kwa wakristo aliyewaumba aliwapa muongozo na mipaka (haramu na halali) katika nyanja za chakula, kuoana, mavazi, n,k.(rejea kitabu cha torati, mambo ya malawi). Jambo lolote kama halikufanywa kwa kiasi litaleta madhara. hata kama ni vegetarian kama hukula kwa kiasi pia litaleta madhara. na nyama ukila kwa kiasi na yenye ubora unaotakiwa haiwezi kuleta madhara
 
Unamaanisha Wakristo,waislam na wengineo ma-roho yetu ni mabaya zaidi ya shetani lakini yote inachangiwa na kudhurumu/kutoa roho na kula nyama za viumbe wapumuao kama sisi wenyewe?
 
Kuna Utafiti unasema mimea NATO lina hisia wakati inaliwa...na wengine wakaenda mbali wakisema vegans waanze kula hewa kwakuwa ndiyo pekee mpka sasa haijaonesha kuwa inahisia zozote
 
Mada nzuri; lakini tujiulize kidogo, hizo karma wanazo wanyama tu; je mimea haina haja ya kuishi? Kama issue imeanza kwa kujiuliza sisi wanadamu against wanyama wengine; kwa vipi isiwe hivo kwa mimea pia? Ama tunaonea mimea ili tusikose chakula? ....vipi Simba anayemla Swala , je yeye hawezi kuja kuliwa siku akizaliwa kama swala? Nakubaliana na sababu za kiafya za kuacha nyama kuliko za kidini
 
Mi nataka kuacha kula nyama lakin nashindwa nifanyeje?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vipi samba au Chui anapomla Swala hii nayo ni Ego au hawa Carnivores wao hawakuwa ENLIGHTED kama sisi tulao Nyama?
 
Vipi samba au Chui anapomla Swala hii nayo ni Ego au hawa Carnivores wao hawakuwa ENLIGHTED kama sisi tulao Nyama?
Wanakula kushibisha mwili.. Sisi tunatafuta mpaka ladha... Wao hawana mbadala sisi tuna mibadala
 
Wanakula kushibisha mwili.. Sisi tunatafuta mpaka ladha... Wao hawana mbadala sisi tuna mibadala
Mi nadhani hata sisis ni kama wao tu, maana historia inasema kabla ya ugunduzi wa moto nasi tulikula mbichi. Hii ya kukaanga, kuchoma na kupika ni manjonjo tu, lakini bado nasi tunakula kwa hitaji hilo hilo kama wao. Hizo choices zinaongezeka na elimu, lakini bila hivyo tungekuwa kama carnivores wengine still.
 
Bado nasisitiza kwenye uchaguzi sisi tuna uchaguzi ama mbadala lakini wao hawana
 
Sect ipi mojawapo
Sijui but niliona wahindi wanakula mutton. But budha wenyewe wanasema nyama wanakula ..ambacho hawali Ni nyama ambayo imeandaliwa specific kwa wao..Yani mtu amchinje kuku kwa ajili yao.
 
Sijui but niliona wahindi wanakula mutton. But budha wenyewe wanasema nyama wanakula ..ambacho hawali Ni nyama ambayo imeandaliwa specific kwa wao..Yani mtu amchinje kuku kwa ajili yao.
Buddhism ina sect mbili kubwa
Mahayana... Hawa ni karibia wote wenye asili ama kaliba na uchina
Vajrayana hawa ni wenye asili wote na uhindi....
Buddhism ina misingi kama imani yoyote ile ila huathiriwa na mila desturi na tamaduni
Hoja ya mabudha kula nyama umeijibu vizuri ila ufafanuzi wake huu hapa
M'budha ataruhusiwa tu kula endapo
. hakuna means yoyote ya chakula kingine
. hakikuandaliwa kwa ajili yake
. sio chakula cha biashara
. hakuona mnyama husika akichinjwa na hakuona hata damu yake ngozi ink
. hakuona akiandaliwa mpaka kupikwa
 

Kweli. Na kingine cha kuepuka katika nyama
- Usiagize uchinjiwe. Ukimwambia mtu akuchinjie mnyama sio sahihi pia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…