Sababu hizi zitatufanya ichukue muda sana kupata viongozi kama Hayati Magufuli na Mwalimu Nyerere

RNA

JF-Expert Member
Mar 27, 2013
1,584
2,683
Habari JF,

Ukiaachana na nguvu kubwa inatumika kuonesha umma kwa Hayati Magufuli hakufanya kitu huku vitu vinaonekana na tuhuma nzito ambazo hazina ushahidi bado haiwezi ondoa ukweli kwamba hawa viongozi wawili watabaki kuwa bora kuwahi kutokea nchini mwetu.

Kwa kifupi bado tunawahitaji lakini Je, ni rahisi kuwapata ? Jibu hapana na zifuatazo ni sababu kwanini ni Ngumu kuwapata -

1. Demokrasia: Ni mfumo wa kuangalia mawazo ya wengi na kupuuza wachache huu mfumo hautufai Afrika kabisa sababu unatupa viongozi wasiofaa. Pili unapuuza mawazo ya wachache ambayo muda mwingine ni msingi mwisho ni chanzo kikubwa cha migogoro na vita lakini kikubwa zaidi maamuzi mengi sana huwa yanachukua muda mrefu sana sababu inahitajika vikao vingi vya makubaliano. Hivyo AFRIKA INAHITAJI DEMOKSIA INAYOENDANA NA TAMADUNI NA MAZINGIRA YETU.

2. Nguvu ya Mataifa ya nje: Umewahi jiuliza hivi wazungu au mataifa ya nje wanatupenda sana Africa au ni watu wema sana kiasi cha kuacha kusaidia wananchi wao na kutoa misaada na mikopo? La hasha wanafanya hivyo kwa maslahi yao hivyo ni lazima waweke mkono kuhakikisha mtu anapatikina analinda maslahi yao.

3. Ujinga bado mwingi sana: Ujinga ni adui mkubwa sana. Tanzania unaweza fanyika ufisadi mkubwa sana lakini watu wakawa kimya wanaendelea na maisha lakini ukizima data au ukaifungia whatsapp au Twitter basi utawanyima raha sana. Kwa kifupi ni bora uwape uhuru wa kutukanana mitandaoni kuliko maendeleo, sasa watu kama hawa ni ngumu sana kukupa kiongozi bora hasa kwa njia ya demokrasia.

Hivyo tupambane na ujinga.

Je, unadhani kuna siku tutapata watu wazalendo na watakao pigana kwa ajili ya maslahi ya Taifa letu? au tayari tunao tuendelee kuwaamini?
 
Nguvu ya mataifa ya nje: nchi yetu naamini haijitawali katika sekta zoote bado. Bado Kuna mtu ananguvu Zaid ya raisi, Kuna vitu atuwezi fanya bila wao.

Uhuru sio kuiemdeleza aliokuachia mnyonyaji wako. Ni kama mwalimu alitamani utawala wa mzungu, hivyo alitaka Yy ndio ashike nafasi ya huyo mzungu(mnyonyaji)

Au alikua puppet wa huyo mzungu (mnyonyaji) 🤷
 
Ukiona mtu anakupa msaada hakupendi na hataki ujitegemee.
Zamani wazee wa kichaga Mtoto akimaliza darasa la Saba anafukuzwa nyumbani kwa kuambiwa mkataba wako umeisha wa kula na kukaa hapa nyumbani,hii ili wapush wachaga wengi kupambana kwa uchungu na maumivu kwa njia yeyeto hadi wakawa juu.
watoto wao walikuja kuelewa wazee wao baada ya kufanikiwa kimaisha.
Misaada ni tools ya kuzidi kumfanya Muafrika atopee kwenye umasikini
, wazungu wanawasaidia Waafrika kwa kuwapa pesa na misaada,si kwamba wanawapenda sana waafrika la ili wazidi kuwa masikini zaidi ili waweze kuwatawala.
Siku ulaya itakapo acha kuipa pesa afrika ndipo afrika itakapoanza kuinuka, wanatumiaa misaada kupush ajenda zao za Siri mfano ushoga,nk.
Kwa kanuni za asili pia wanatumiaa misaada ili kuchukua baraka zetu kupitia kanuni ya ukitoa unabarikiwa zaidi.Atoae upata zaidi kuliko anaepokea.
Wanajua kabisa hizi pesa hazitofika chini zitadakwa juu kwa juu na kurudi kufichwa bank za ulaya na mafisadi,then wananchi ndio watabebeshwa mzigo wa madeni hadi waingie kaburini.
 
Habari JF,

Ukiaachana na nguvu kubwa inatumika kuonesha umma kwa Hayati Magufuli hakufanya kitu huku vitu vinaonekana na tuhuma nzito ambazo hazina ushahidi bado haiwezi ondoa ukweli kwamba hawa viongozi wawili watabaki kuwa bora kuwahi kutokea nchini mwetu.

Kwa kifupi bado tunawahitaji lakini Je, ni rahisi kuwapata ? Jibu hapana na zifuatazo ni sababu kwanini ni Ngumu kuwapata -

1. Demokrasia: Ni mfumo wa kuangalia mawazo ya wengi na kupuuza wachache huu mfumo hautufai Afrika kabisa sababu unatupa viongozi wasiofaa. Pili unapuuza mawazo ya wachache ambayo muda mwingine ni msingi mwisho ni chanzo kikubwa cha migogoro na vita lakini kikubwa zaidi maamuzi mengi sana huwa yanachukua muda mrefu sana sababu inahitajika vikao vingi vya makubaliano. Hivyo AFRIKA INAHITAJI DEMOKSIA INAYOENDANA NA TAMADUNI NA MAZINGIRA YETU.

2. Nguvu ya Mataifa ya nje: Umewahi jiuliza hivi wazungu au mataifa ya nje wanatupenda sana Africa au ni watu wema sana kiasi cha kuacha kusaidia wananchi wao na kutoa misaada na mikopo? La hasha wanafanya hivyo kwa maslahi yao hivyo ni lazima waweke mkono kuhakikisha mtu anapatikina analinda maslahi yao.

3. Ujinga bado mwingi sana: Ujinga ni adui mkubwa sana. Tanzania unaweza fanyika ufisadi mkubwa sana lakini watu wakawa kimya wanaendelea na maisha lakini ukizima data au ukaifungia whatsapp au Twitter basi utawanyima raha sana. Kwa kifupi ni bora uwape uhuru wa kutukanana mitandaoni kuliko maendeleo, sasa watu kama hawa ni ngumu sana kukupa kiongozi bora hasa kwa njia ya demokrasia.

Hivyo tupambane na ujinga.

Je, unadhani kuna siku tutapata watu wazalendo na watakao pigana kwa ajili ya maslahi ya Taifa letu? au tayari tunao tuendelee kuwaamini?
Watu wa dizaini ya Mwendazake na ni mtu wa hivyo hakuna anaemtaka..

Walau Nyerere ana unafuu hakuwa fisadi japo alikuwa mroho wa madaraka aliyejikita kwenye propaganda
 
..demokrasia inakupa nafasi ya kuchagua na kubadilisha viongozi mara kwa mara.

..pia demokrasia inatoa nafasi sawa kwa vyama na wagombea kujijenga na kuwasilisha hoja zao kwa wananchi.

..kwa hiyo mazingira hayo yanatoa nafasi kubwa zaidi kumjenga na kumpata Magufuli mwingine kuliko kukiwa hakuna demokrasia au chaguzi za haki zinazofanyika mara kwa mara.

..pia katika hoja yako ungezungumzia umuhimu wa mihimili kama Bunge na Mahakama ktk kusimika utawala bora ktk nchi mbalimbali.
 
Back
Top Bottom