Sababu hasa zinazofanya wanajeshi wawapindue watawala

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Jan 31, 2021
7,235
12,748
Mara nyingi wanajeshi husema kuwa wanapindua nchi sababu ya uongozi mbaya, kwa ajili ya wananchi blah blah. Ukweli hizo si sababu kabisa zinazofanya wafanye hivyo.

Mara nyingi wanajeshi hupindua nchi baada ya kuona mtawala hana maslahi tena kwao au hawezi kuendelea kulinda maslahi yao. Mfano, kama kiongozi ni mgonjwa sana, kuna uwezekano mkubwa wa kupinduliwa. Sababu wanajeshi wanakuwa na mashaka na mustakabali wao.

Hili lilifanyika sana kwa masultani wa Milki ya Ottoman. Unakuta Sultani ana watoto wengi kwa mama mbalimbali. Siku akishikwa na ugonjwa na watu/watoto wakawa hawana uhakika na future yao, huwahi kumpindua mapema ili kuwawahi watoto wengine kushika madaraka.

Mobutu alitawala miaka kibao lakini alikuja kugeukwa baadaye, inadaiwa kuwa alipatwa na ugonjwa wa kansa ya kibofu. Majenerali wake wakaona hapa nguzo inaenda kuanguka, ni kuchukua chako mapema.

Hata Bongo wa Gabon kuna uwezekano mkubwa kapinduliwa sababu ya afya yake mgogoro.

Sababu nyingine ni uzee. Watu wakishaona unakuwa mzee wanaanza kuulizana nani atarithi. Maneno hayo yanapamba moto na kusababisha watu kuwahi chao mapema. Ni kama kilichotokea kwa Mugabe.

Mapinduzi yote ni watu wanaangalia maslahi yao kwanza. Ndiyo maana ukipindua kitu cha kwanza ni kushika hazina ya nchi ili uweze kuwalipa machawa wako.

Kitu cha kwanza ambacho wa Ottoman walifanya baada ya kufanya mapinduzi ilikuwa ni kushika hazina. Ukishindwa kufanya hivyo unapinduliwa tena. Na ukipindua na kujidai kuleta utawala bora na kubana mafisadi, hao chawa wako watakupindua. Kama kilichomkuta Sankara.

Pamoja na yote hayo, utawala wa madikteta wa kijeshi ni bora kuliko wa kidemokrasia, sababu hasa ni kuwa kwenye demokrasia kuna chawa wengi sana wa kuwalisha.
 
Mfano wako ottoman ni wa kijinga kabisa , ni kama unatusimulia masuala ya tamithiliya , west Africa imepamba Moto Kwa mapinduz sababu wale jamaa wanajielewa , Sisi akili tushashikiwa na watu wa Pwani wapenda vya bure
hakuna kujielewa kokote.ndio sababu hakuna jipya hata baada ya wao kuingia.
 
Kama unaona nchi kuongozwa kijeshi ni bora kuliko utawala wa kidemokrasia,basi lianzishe wewe wengine wafuate,usiwe mwepesi TU wa kuchezea keyboard ya smartphone Yako twende kwenye vitendo.
 
Mkuu Ali Bongo ana miaka 64 tu hata mimi mkubwa 😄 🤣
Kwa starehe hizo mbona bado sana

Wanajeshi wanaona salute hazijengi ndio maana wanaamua na wao kutafuta mlo
Masalute wanaona wanatoa tu ila keki inaliwa na wengine wao wanawalinda tu
Ni tamaa tu hakuna lingine
 
Mkuu Ali Bongo ana miaka 64 tu hata mimi mkubwa 😄 🤣
Kwa starehe hizo mbona bado sana

Wanajeshi wanaona salute hazijengi ndio maana wanaamua na wao kutafuta mlo
Masalute wanaona wanatoa tu ila keki inaliwa na wengine wao wanawalinda tu
Ni tamaa tu hakuna lingine
Ni mgonjwa. Alipigwa na kiharusi hapa juzi kati.
 
Zacharia Hans Poppe: The untold story of a Kagera war veteran

Zakaria Hanspope anasema sababu ya wao kupanga mapinduzi ni kuwa hadi kufika mwaka 1982 hali ya uchumi nchini ilikuwa mbaya sana na Nyerere alikuwa anatupa lawama kwa maadui wa kufikirika wa ndani na nje ya nchi.

Hans poppe anasema wapanga mapinduzi waliamini Nyerere alishindwa kutatua matatizo ya uchumi kwa kuwa alizungukwa na wanafiki ambao hawakutaka kupoteza vyeo vyao kwa kumwambia Nyerere ukweli.

Chawa wanaweza kusababisha ukapinduliwa.
 
Zacharia Hans Poppe: The untold story of a Kagera war veteran

Zakaria Hanspope anasema sababu ya wao kupanga mapinduzi ni kuwa hadi kufika mwaka 1982 hali ya uchumi nchini ilikuwa mbaya sana na Nyerere alikuwa anatupa lawama kwa maadui wa kufikirika wa ndani na nje ya nchi.

Hans poppe anasema wapanga mapinduzi waliamini Nyerere alishindwa kutatua matatizo ya uchumi kwa kuwa alizungukwa na wanafiki ambao hawakutaka kupoteza vyeo vyao kwa kumwambia Nyerere ukweli.

Chawa wanaweza kusababisha ukapinduliwa.
Hangeweza kusema kuwa alitaka kupindua ili naye arambe asali kirahisi.
 
Back
Top Bottom