Ni sababu zipi zilikufanya kukipenda chama cha siasa unachokiunga mkono?

The Sheriff

JF-Expert Member
Oct 10, 2019
617
1,800
Kila mmoja wetu ana sababu zake za kuchagua na kupenda chama cha siasa anachoona kuwa kinamwakilisha vyema. Huku kila mmoja akiwa na sababu tofauti, ni muhimu kujiuliza: Je, ni sababu zipi zinazotuongoza kuchagua na kukipenda chama fulani cha siasa?

Moja ya sababu kuu inaweza kuwa ni sera na itikadi za chama. Mara nyingine watu huchagua chama chenye sera na itikadi zinazofanana na mitazamo yao kuhusu mambo yanavyopaswa kufanyika. Inawezekana ni masuala yanayohusu elimu, afya, ajira au chochote kile. Masuala kama vile uhuru wa mtu binafsi au usawa wa kijamii pia zinaweza kuwa jambo linalowavuta watu kwenye chama fulani.

Lakini pia, kuna suala la historia ya chama. Baadhi yetu huwa na uhusiano wa kihistoria na chama fulani, iwe ni kutokana na misingi ya chama kilipoanzishwa au mchango wa chama katika matukio muhimu ya kitaifa. Hali hii inaweza kufanya chama fulani kuwa sehemu ya utambulisho wetu wa kisiasa.

Mara nyingine viongozi wa chama wanaweza kuwa kigezo kikubwa cha uungwaji mkono. Watu hupendezwa na viongozi wenye uongozi imara, wanaojitolea kwa dhati kwa wananchi wao. Kauli na matendo ya viongozi wa chama huathiri jinsi watu wanavyochukulia chama na uwezekano wa kuendelea kuwa wafuasi wake.

Watu wanaweza kukipenda chama kutokana na mipango na mikakati inayopendekezwa na chama hicho kwa maendeleo ya nchi. Ikiwa chama kinatoa suluhisho la changamoto za jamii na maendeleo ya uchumi, hii inaweza kuwa kichocheo kikubwa cha kuwavuta wafuasi.

Hata hivyo, ni muhimu kujiuliza: Je, ni vipi unapima utendaji wa chama chako cha siasa? Je, unachunguza kwa kina sera zake na utekelezaji wake, au unapendelea chama fulani kwa ushabiki tu? Je, unafuata mkumbo kwakuwa marafiki, wazazi au ndugu zako wanakifuata? Je, unakifuata kwakuwa ndugu marafiki na jamaa zako wana maslahi huko? Je, sababu za kukifuata chama hicho ni za msingi?

Hebu jiulize maswali hayo leo na kisha ujijibu na uone kama sababu yako ni ya msingi au hujui ni kwanini unaunga mkono chama hicho.

Kujitafakari kuhusu sababu zetu za kuchagua na kuipenda chama cha siasa kunaweza kutufanya kuelewa kama sababu zetu ni za msingi au la, kama zina maslahi kwa jamii zetu au vinginevyo.
 
Nilikuwa shabiki wa Zitto alivyokuwa CHADEMA lakini sikuwa mwanachama wa CHADEMA. Alivyounda ACT Wazalendo ndipo niliamua kuwa mwanachama wa ACT. Zitto ukiachana na madhaifu mengine ya kibinadamu, ana ushawishi wa kisiasa hasa kwa vijana.
 
Nilipenda Chadema sana wakati nakua, walinikosha sana kuikosoa serikali, uthubutu wao, point zao, yan ilikuwa akisimama mbunge wa upinzani unaogopa. Ghafla kikaja kizazi cha matusi, kizazi pinga pinga, kizazi hakina hoja,
Najikuta nakuwa bored na siasa daily.

Kwa sasa nipo tu nje ya siasa, natazama tu sina chama cha siasa.
 
Nilikuwa shabiki wa Zitto alivyokuwa CHADEMA lakini sikuwa mwanachama wa CHADEMA. Alivyounda ACT Wazalendo ndipo niliamua kuwa mwanachama wa ACT. Zitto ukiachana na madhaifu mengine ya kibinadamu, ana ushawishi wa kisiasa hasa kwa vijana.
Zitto alivutia vijana wengi sana CHADEMA na kwenye siasa. Jamaa alikuwa anatema facts bila shida yeyote ile, alifanya niipende Chadema kipind changu.
 
Nilikuwa shabiki wa Zitto alivyokuwa CHADEMA lakini sikuwa mwanachama wa CHADEMA. Alivyounda ACT Wazalendo ndipo niliamua kuwa mwanachama wa ACT. Zitto ukiachana na madhaifu mengine ya kibinadamu, ana ushawishi wa kisiasa hasa kwa vijana.
Zito nilijua mpinzani kweli, nikajitosa nikatafuta namba yake nikampigia nikampa mbinu za kushinda jimbo fulani, we!! Jinsi alivyojibu sikuamini kama yeye ndo Zito kweli. Any way, usilolijua ni sawa na usiku wa giza. Tutafute hela tulishe familia zetu.
 
Nilikuwa shabiki wa Zitto alivyokuwa CHADEMA lakini sikuwa mwanachama wa CHADEMA. Alivyounda ACT Wazalendo ndipo niliamua kuwa mwanachama wa ACT. Zitto ukiachana na madhaifu mengine ya kibinadamu, ana ushawishi wa kisiasa hasa kwa vijana.
Kwahiyo ilikuwa ni ushabiki tu kwa Bw. Zitto bila kuzingatia Sera?
 
Wengine sisi na siasa ni maji na mafuta, sina chama ninachokiamini wala kukisapoti, sijaona pia mwanasiasa mkweli wa kumuamini.
 
Nilipenda Chadema sana wakati nakua, walinikosha sana kuikosoa serikali, uthubutu wao, point zao, yan ilikuwa akisimama mbunge wa upinzani unaogopa. Ghafla kikaja kizazi cha matusi, kizazi pinga pinga, kizazi hakina hoja,
Najikuta nakuwa bored na siasa daily.

Kwa sasa nipo tu nje ya siasa, natazama tu sina chama cha siasa.ole sana, ndugu yangu. Kwahivyo sasa hauna

Nilipenda Chadema sana wakati nakua, walinikosha sana kuikosoa serikali, uthubutu wao, point zao, yan ilikuwa akisimama mbunge wa upinzani unaogopa. Ghafla kikaja kizazi cha matusi, kizazi pinga pinga, kizazi hakina hoja,
Najikuta nakuwa bored na siasa daily.

Kwa sasa nipo tu nje ya siasa, natazama tu sina chama cha siasa.

Dah! Pole sana, ndugu yangu. Kwahivyo sasa hauna sera yoyote ambayo unadhani "inakubariki"?
 
Niliipenda CHADEMA kipindi wanatetea rasilimali za nchi na kupinga ufisadi. Niliichukia CHADEMA pale walipoanza kumpinga JPM katika mambo yale yale waliokuwa wakiyapigania mda wote.
 
Niliipenda CHADEMA kipindi wanatetea rasilimali za nchi na kupinga ufisadi. Niliichukia CHADEMA pale walipoanza kumpinga JPM katika mambo yale yale waliokuwa wakiyapigania mda wote.
Ni mambo yapi walikuwa wanampinga JP?
 
Back
Top Bottom