Saa inatakiwa kuvaliwa mkono gani?

Saa inatakiwa kuvaliwa mkono gani?

Bavaria

JF-Expert Member
Joined
Jun 14, 2011
Posts
53,109
Reaction score
53,626
attachment.php


Hapo ukiangalia kwa makini unaona JK amevaa saa mkono wa kulia na Kenyatta amevaa wa kushoto.

Yupi yupo sahihi?
 
Tunavalia saa mkono wa kushoto (logic) kwa sababu kwanza iwe rahisi kuona mda wakati unaandika na pia mkono wa kushoto hauna movements nyingi kama mkono wa kulia. Hivyo kuifanya saa idumu miaka mingi and that's the fact
 
Inategemea unatumia sana mkono gani. Kwa mfano wale wote wanaotumia mkono wa kulia kuandika inashauriwa wavae saa mkono wa kushoto. Na wale wanaoandika kutumia mkono wa kushoto kama Rais obama wanatakiwa kuvaa saa mkono wa kulia.
 
Yote ni kutaka kumtoa kasoro raisi, jamani tuacheni umbea mengine hayatuhusu
 
Mimi huwa navaa left hand, na naona it suits me sababu uko inactive ukilinganisha na mkono wa kulia ambao kwa mimi hufanya shughuli nyingi, iwe kuandika, kusalimia etc etc.

Wakati mwingine ni vile mtu unavyo_feel uvae mkono upi, hakuna kanuni maalum.
 
Mm navaa mkono wa kushoto ila kuna baadhi nawaona wanavaa kulia nadhan ni uamuzi tu au ulivyozoea kuvaa mkono gan
 
Saa unavaa mkono wowote unaojisikia ata ukivaa mguuni ni sawa wengi huvaa saa kama pambo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom