Saa 11:20 alfajiri unapishana na schoolbus zenye watoto wa miaka 4

Imekaaje hii

Saa 11:20 alfajiri Unapishana na schoolbus zimebeba wanafunzi wadogo wa miaka 4-6 wakipelekwa mashuleni.

Unabaki unajiuliza maswali mengi sana kichwani,

-Hivi Hawa watoto wameamshwa saa ngapi?
-Hivi Hawa watoto wameandaliwa kwa MDA gani?
-Hivi Hawa watoto wamekaa vituoni kusubiria school bus kwa MDA gani?

Wazazi, waalimu,Serikali, jamii na wahusika wote wa Hizi DAYCARE na PRIMARY SCHOOLS mnaofanya hivi mjitafakari sana kwa hili.

HAIINGII AKILINI KABISA
Tunatengeneza 'kizazi cha Wasafiri' badala ya wasomi. Matokeo yake yataonekana miongo miwili au mitatu ijayo.
 
Kuna hawa pia wa darasa la nne nao ni mateso tu. Wanaambiwa waripoti shuleni saa 12 asubuhi kila siku. Wanarudi nyumbani saa 11 jioni halafu wanarudi tena shuleni saa 12 jioni mpaka saa 3 usiku kila siku. Jumamosi pia wanaenda.
Hivi mtoto wa darasa la nne anasoma nini muda wote huo?
Elimu imekuwa mateso kwa watoto kisa shule zinatafuta sifa za kuonekana zinafaulisha zinabaki kukaririsha watoto.
 
Baba zenu walioa mama zenu wakawa wa mama wa nyumbani wakawasimamia nyie mkaenda shule mkarusi mkakuta chakula, mkapata mda mkaenda kucheza mkajumuika na ndugu na jamaa kwenye shughuli mbali Ile nyie Sasa Leo maisha kusaidizana mnataka kuzaa uku malezi mnawachia wadada wakazi na makonda wa school bus maana mama anamkaa saa kumi baba hivyo hivyo na mkitoka kazini hamuendi nyumbani mama anapita bar baba naye hivyo hivyo

Matokeo yake watoto wanakuwa na tabia mbaya pamoja na kusoma shule nzuri ila wanaishia pabaya ebu nenda uswahili au vijijini kama utakuta mtoto kundi kubwa la mashoga au wasagaji au watumia unga
 
Kwenda shule sio ishu kama ni 3yrs ishu shule isiwe mbali na eneo mnaloishi,wangu ana 3yrs anasoma jirani na nyumbani basi linamfata saa 1 na 30 asubui!
Anakua ashaamka mwenyewe mida hiyo wala haamshwi awahi basi
 
Huu ni ujinga
Kuna hawa pia wa darasa la nne nao ni mateso tu. Wanaambiwa waripoti shuleni saa 12 asubuhi kila siku. Wanarudi nyumbani saa 11 jioni halafu wanarudi tena shuleni saa 12 jioni mpaka saa 3 usiku kila siku. Jumamosi pia wanaenda.
Hivi mtoto wa darasa la nne anasoma nini muda wote huo?
Elimu imekuwa mateso kwa watoto kisa shule zinatafuta sifa za kuonekana zinafaulisha zinabaki kukaririsha watoto.
 
Wengine wanaona ujanja mtoto miaka miwili anaanza kupelekwa day care..principle yangu ni mtoto akae home awajue siblings, ajue viumbe vya dunia, atembee ahave fun, ajue milima mito na bahari, ajue abc -z akiwa home, 1 to 100 akiwa home.. alale, acheze, ale.

Nursery nataka asome mwaka mmoja tu..sitaki kuskia ya baby class, kg 1, kg 2, pre grade 1 ..Halaf baada ya hapo ndo agraduate aende class 1 lol..watu wanafanywa mtaji
Watu wanafanywa fursa bila kijijua. mmoja aliniambia hana mtu wa kumwachia watoto akienda kazini. Nikamwambia ni cheap kumwajiri mwalimu mmoja aje kucheza na watoto nyumbani kuliko kuwapeleka day care.
Ni kutesa watoto tu
 
Wazazi tumepata pesa ya kuwatesa watoto badala ya kuwatunza watoto. Mtoto anakua kwenye school saa11 alfajiri ameamka saa ngapi?

Halafu unampeleka mtoto mdogo miaka 3,4 shule saa 11 alfajiri ili iweje? Anaenda kukuletea pesa au mshahara.

Watoto kusoma katika umri mdogo ni sawa lakini sio kumuamsha alfajiri. Mtoto alale usingizi wake uishe, akue vizuri, apate muda wa kucheza, kulala na kusoma

Binafsi naprefer homeschooling kwa watoto wangu hadi 6yrs, na baada ya hapo sipeleki mtoto shule ya kumuamsha saa11.

Watasoma shule ya karibu na nyumbani au mimi nitahamia karibu na shule watakayosoma

Mtoto miaka2, 3, 4 aamke saa 11 mimi niamke saa11, HAPANA
Mama d wa ukweeee
Mama mwenye busara zake
Nmekubali
Si umeona ulivyoshusha nondo

Ova
 
Kuna shule huku inafosi mtoto darasa la nne akae shule kama mzazi hutaki umpeleke mwanao saa 12 asubuhi kasorobo awe shule na kutoka saa mbili usiku.
Darasa la nne? Kwanza hata huo mtihani wa darasa la nne ni kupoteza pesa na kusumbua watoto. Hauna maana yeyote ile. La nne mtoto bado ni wa kubembeleza aipende shule sio kumpa ratiba kama anasomea rocket science.
 
Darasa la nne? Kwanza hata huo mtihani wa darasa la nne ni kupoteza pesa na kusumbua watoto. Hauna maana yeyote ile. La nne mtoto bado ni wa kubembeleza aipende shule sio kumpa ratiba kama anasomea rocket science.
Changamoto sana
 
Wazazi tumepata pesa ya kuwatesa watoto badala ya kuwatunza watoto. Mtoto anakua kwenye school saa11 alfajiri ameamka saa ngapi?

Halafu unampeleka mtoto mdogo miaka 3,4 shule saa 11 alfajiri ili iweje? Anaenda kukuletea pesa au mshahara.

Watoto kusoma katika umri mdogo ni sawa lakini sio kumuamsha alfajiri. Mtoto alale usingizi wake uishe, akue vizuri, apate muda wa kucheza, kulala na kusoma

Binafsi naprefer homeschooling kwa watoto wangu hadi 6yrs, na baada ya hapo sipeleki mtoto shule ya kumuamsha saa11.

Watasoma shule ya karibu na nyumbani au mimi nitahamia karibu na shule watakayosoma

Mtoto miaka2, 3, 4 aamke saa 11 mimi niamke saa11, HAPANA
Uko sawa 100% Mama D. Mtoto wa miaka 4 unamwamsha kwa alarm? Huyu anatakiwa alale mpaka aamke mwenyewe usingizi unapomwisha.
Kuna haja ya waalimu kuanza kuspecialise kwenye private schooling kwa watoto. Watapata sana watu
 
Shule nzuri huuza maeneo inayoizunguka, kwa mfano umejenga nyumba Tabata na shuke nzuri iko Kibaha.

Kwa muda watoto wanaihitaji shule ya Kibaha tafuta nyumba Kibaha upangishe.

Tabata unatafuta mpangaji na kodi ya Tabata inalipa nyumba Kibaha. Hofu zenu kuwa flexible.
Tabata kuna shule nzuri kibao mf Tusime, St Mary, Crist the King,Reminant nk na bado kama ikiwezekaa unampeleka Loyola ambayo ipo Mabibo, kwani Mabibo na Tabata ni pua na mdomo.

Sometimes ni show off na ujinga ujinga.
 
Hakuna kitu kinanikera kama kumwamsha mtoto saa 11 alfajiri, unawahi nini? Masaa mawili ya alfajiri?

Mtoto aamke saa moja kamili asubuhi, then muda wa kuondoka shule kurudi nyumbani ongeza masaa mawili.
 
Back
Top Bottom