Yaliyojiri Clubhouse katika mjadala wa wazazi na walimu kuhusu kuwapa wanafunzi kazi za shuleni wakati wa likizo

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Aug 7, 2018
625
938
1638457365518.png

Baadhi ya Wachangiaji ndani ya JamiiForums wamezua Mjadala kuhusu 'Homeworks' nyingi wanazopewa Watoto toka Shuleni hasa kipindi cha likizo

Ikiwa wewe ni Mzazi, Mlezi au Mwalimu ungana nasi katika Mjadala huu utakaofanyika leo Desemba 2, 2021 kupitia Clubhouse.

Kushiriki mjadala huu bonyeza link

BAADHI YA MAONI NA MAWAZO YALIYOTOLEWA NA WADAU WAKATI WA MJADALA

Baraka (Mwalimu): Mtaala wetu wa Elimu una mambo mengi ndio maana unasababisha Walimu wengi kutomaliza wanayotakiwa kufundisha hivyo kuanzisha mfumo wa masomo ya ziada.

Tunatakiwa kurahisha Mfumo wa Elimu yetu. Tuna mambo mengi Wanafunzi wanafundishwa ambayo hayana maana kwetu.

Bazo Komu: Aliyetangulia kuongea amesema point za Msingi sana. Natamani tamko la Waziri lisifanye kazi kwenye Shule za Serikali tu bali Shule zote.

Watoto siku hizi hatuwajengi bali tunawabebesha mizigo ili mambo yaende. Mtoto wa darasa la 5 anabeba begi ambalo mimi siliwezi.

Bazil Komu: Tunawadumaza Watoto badala ya kuwajenga. Mtoto anahitaji kujifunza mambo ya kidunia, kidini na ku-refresh mind. Siku hizi wanapata Elimu ya darasani na kula.

Akirudi ana homework na anawahi school bus asubuhi. Hatujengi kizazi cha kupambana na changamoto za Dunia.

Simon Msenga: Tunaposema tusitishe huduma ya Masomo wakati wa likizo lakini inabidi tuangalie na namna ya kuwasaidia hawa Wanafunzi.

Sio Madarasa yote huwa yanabaki Shuleni ila unakuta ni Madarasa yale yenye mitihani. Shule za Serikali hazifanyi vizuri sana kwenye matokeo.

Zawadi Mkweru: Nizungumzie Enlish medium, kuna changamoto kubwa watoto huwa wanapewa kazi nyingi sana. Inawezekana walimu wana lengo zuri lakini zile kazi zinakuwa nyingi sana.

Unakuta likizo inapokaribia kuisha watoto wanaanza kustruggle kuzimaliza.

Zawadi Mkweru: Mfumo wa Elimu una mambo mengi sana, hata mimi nakumbuka kuna vitu vingi nilivisoma lakini sivitumii hivi sasa

Kuna mambo mengi ya muhimu ambayo nilipaswa kufundishwa lakini sikuyapata. Kwa hiyo iangaliwe namna ya kupunguza masomo.

Glory Tausi: Glory Tausi: Kuna shughuli nyingi za kijamii tunazoweza kufanya ambazo zitafanya watoto wawe bora zaidi kuliko hizo 'Homework'

Pia watoto wanahitaji kupata muda wa kuwa watoto kwa kucheza, kuna wakati tunataka kusafiri na watoto wetu kwenda kwa babu/bibi ili ajuane na ndugu wengine.

Sultan: Vijana wa siku hizi wamekuwa na kauzito kwenye kushika yale wanayofundishwa hivyo inabidi Mwalimu aende taratibu ili kuwapata Wanafunzi wote

Wanafunzi wengi akishasogea darasa la mbele anasahau vitu vyote vya darasa la nyuma. Pia, Walimu wana mambo mengi ya kufundisha.

Sultan: Nadhani tunaweza kupunguza muda wa hizi 'tuition' wakati wa likizo. Labda badala ya kufundisha Mwezi mzima iwe wiki 2

Vijana wanaangalia vitu vingi kwenye Jamii na Television jambo linalofanya Ubongo uwe mzito kushika vitu Darasani. Mzazi anaacha Mtoto anaangalia 'Series'.

Abdul Nondo: Maamuzi haya yanaegemea upande mmoja ambayo yanaenda kutatua matatizo yanayotokea maeneo tofauti. Maamuzi yamefanyika kana kwamba kuna tafiti iliyofanya kuonesha hii ni changamoto kwa wanafunzi wote.

Mimi nimesoma Kigoma, nilipata division 3 huku wanafunzi wengine wakiwa wamepata 4 na 0, shuleni hakukuwa na vipindi vya ziada. Mimi nilipambana ninavyojua, kwa hiyo wanaokubali suala la likizo inategemea na maeneo yao, sio suala la nchi nzima.

Abdul Nondo: Tamko la Waziri ni zuri na linaonesha Moyo wa Uzazi. Lakini hakuna tafiti iliyofanyika Tanzania nzima kufahamu haya Masomo ya likizo yameleta athari kwa kila sehemu.

Mimi nilipata division III, hakukuwa na 1 wala 2 kwasababu hatukuwa na 'remedial classes'.

Abdul Nondo: Siku 164 ambazo Wanafunzi wanatakiwa kuwepo Shule huwa hazitimii kwasababu huwa kuna sikukuu humo katikati

Huku Kigoma Wazazi wenyewe wamekubali hizo tuition na Walimu wako tayari. Kuna Wanafunzi akisikia neno likizo ndio anasahau kila kitu kabisa.

Justine Kakoko: Watoto huendelea kusoma hata wakati wa likizo ni kwa sababu tunaamini sana katika kufundisha kuliko kujisomea. Hii hofu ni changamoto kwa kuwa tunaamini watoto hawawezi kujisomea.

Justine Kakoko: Hofu ya mtoto kushindwa kujisomea kwa kuwa hatujajenga tamaduni ya kujifunza wenyewe bila mtu kusimama mbele yao.

Wazazi hawana muda wa kukaa na watoto hata wakati wa likizo, wazazi wanaamini shuleni ni sehemu salama ya mtoto kukaa.

Justine Kakoko: Kuna baadhi ya shule wazazi hulilia watoto wabaki shuleni, sio mara zote kuwa shule inalazimisha watoto kubaki shuleni.

Kuna watoto pia hubaki shule kama njia ya kufanya masoko hasa kwa shule binafsi, wazazi hupenda kuona shule inasoma muda wote.

Justine Kakoko: Masomo yana mambo mengi kiasi cha kuhitaji muda wa ziada kumaliza mambo yote. Madarasa ya mitihani yana mitihani mingi, hivyo wamiliki huona njia ya maandalizi ni kuwabakisha shule.

Justine Kakoko: Tunahitaji kuwapima watoto kwa njia zote tatu na kujenga nidhamu binafsi. Kipimo pekee kinachotumika ni kutumia mitihani ambapo tunashindwa kupima masuala mengine yanayohusu kuendelea kwa mtoto

Justine Kakoko: Wazazi wajengewe uwezo wa kuweza kusimamia watoto wakiwa nyumbani. Shule zinaweza kutengeneza semina au kwenye vikao vya wazazi kwa kuwa kusimamia sio kufundisha, mtu anaweza kufundisha hata kama hana uwezo wa kusoma na kuandika.

Godfrey Boniventura (Haki Elimu): Kiukweli mitihani inachangia woga kwa Wanafunzi, Walimu na Wazazi hasa kwa madarasa ya mitihani. Mitihani kwa sasa huonekana ni kila kitu, Wazazi hujiuliza itakuwaje mtoto akifeli

Boni wa Haki Elimu: Shule za binafsi zinafanya biashara hivyo hulazimisha sana watoto kufaulu. Kwa kuwa watoto wakifaulu huvutia zaidi biashara, na hii huleta changamoto kubwa.

Godfrey Boniventura (Haki Elimu): Shule za blBinafsi zinafanya biashara hivyo hulazimisha sana watoto kufaulu. Kwa kuwa watoto wakifaulu huvutia zaidi biashara, na hii huleta changamoto kubwa.

Godfrey Boniventure (Haki Elimu): Nashauri watoto wafanyiwe Assessment sio Examinations. NECTA wafanye Assessment ili kuondoa woga kwa hawa watoto. Pia, tuachane na kusema shule ipi ya kwanza shule ipi ya mwisho.

Alpha: Mfumo wa Elimu unamtaka Mwanafunzi atoke shuleni akiwa amefaulu mtihani sio kuwa ameongeza maarifa. Suala la kufaulu mitihani ndio hufanya Walimu wabakishe Watoto shuleni.

Assah: Mwalimu bora ni yule anayeweza kufundisha watoto ndani ya muda halisi ambapo wale wanaelewa kwa haraka kupata faida ya kujifunza mara mbili.

Kuhakikisha darasa zima wanaelewa kwa hiyo hakuna maana ya kutetea muda wa ziada ambapo watoto hupaswa kupumzika.

Ummy Mwalimu (Waziri wa TAMISEMI): Ummy Mwalimu: Mimi kama Waziri, kauli yangu ililenga katika kutekeleza maelekezo ya kisera kutoka kwa mawaziri kisekta.

Marufuku ya wanafunzi kubaki shuleni wakati wa likizo ilitoka kwa Waziri wa Elimu, Prof. Ndalichako.

Ummy Mwalimu (Waziri wa TAMISEMI): Elimu sio vita mtoto apate muda wa kupumzika. Kama kuna tatizo lolote linalohitaji siku za ziada Shule au Mamlaka italazimika kuomba kibali kutoka kwa Kamshna wa Elimu.

Umm Mwalimu (Waziri wa TAMISEMI): Sisi kama TAMISEMI tumeandaa kalenda ya mtaala inayonesha mwanafunzi atafundishwa kitu gani ndani ya siku zinazoelekezwa. Ndani ya siku 194 tunajua tuliyoyapanga kufundishwa yatamalizika.

Umm Mwalimu (Waziri wa TAMISEMI): Sisi kama TAMISEMI tumeandaa kalenda ya mtaala inayoonesha mwanafunzi atafundishwa kitu gani ndani ya siku zinazoelekezwa.

Ndani ya siku 194 tunajua tuliyoyapanga kufundishwa yatamalizika.

Ummy Mwalimu (Waziri wa TAMISEMI): Sio tu likizo hata siku za kawaida watoto wanajifunza mpaka Jumamosi wanakosa muda wa kujifunza mambo mengine. Kwa mamlaka yangu kama Waziri wa TAMISEMI naagiza shule zote ziheshimu likizo za Wanafunzi.

Ummy Mwalimu (Waziri wa TAMISEMI): Kwa sasa umezuka mchezo mbaya, shule ikifanya vibaya Afisa Elimu kata na Halmashauri wanashushwa vyeo. Nimepiga marufuku tabia hii kwa wakurugenzi kwa kuwa kabla hujamshusha cheo lazima uangalie ulimuwezesha kiasi gani.

Ummy Mwalimu (Waziri wa TAMISEMI): Kwa sasa umezuka mchezo mbaya, shule ikifanya vibaya Afisa Elimu Kata na Halmashauri wanashushwa vyeo. Nimepiga marufuku tabia hii kwa Wakurugenzi kwa kuwa kabla hujamshusha cheo lazima uangalie ulimuwezesha kiasi gani
 
Wanafunzi wapumzike wakati w Likizo, elimu yetu imekuwa ya nadharia zaidi za kujibia mtihani kwa muda mrefu sana.
 
Hello JF,
Nimetafuta hii topic sijaiona kama ipo nielekezeni huko...lol

Binafsi nadhani nchi yetu bado haijawa na resources fully zinazotakiwa ziwe invested kwenye education, leo maabara changamoto,walimu shule za secondary za serikali hawakanyagi.....leo unamwambia mwanafunzi asijiongeze wakati wa likizo, hii ni sawa kweli?? Tutarejea huu mjadala once factors zote ziko constant, kila kitu kiko mahali pake..sio sasa hivi wakuu...lol

Nimefurahishwa na mchangiaji mmoja,aliyesema tubadilishe form of assessment, sio iwe exams, watoto wanakuwa na fear na wanaandaliwa kufanya mitihani,na sio kuelewa, I agree with him partially,sipingi mitihani iwepo,ila kuwepo na mbadala, kwa mfano kungekuwa na alternative courses ambazo ziko equivalent na Olevel ama A level, such as diploma ambako labda assessment ni coursework, group work etc.....

Ningependa kuongeza kwa huyu huyu mchangiaji,aliyesema kuhusu inclusive education, jinsi ilivyo difficult ku identify watoto wenye special needs, hili naona linaenda back to course syllabus za watu wanaousomea ualimu, iwe moja ya topics katika course za ualimu, jinsi ya kuwa identify na kuwe na referral system ambapo hawa watoto wanaiweza kuwa referred to.......inashangaza mtu mpaka anamaliza la saba hajui kuandika wala kusoma, hii inaonyesha kuna tatizo mahali, angeweza kuwa referred mapema na kusaidika kuliko kupoteza muda wake wote

Tunawashukuru wachangiaji wote,tumejifunza mengi kutoka kwenu. Binafsi mchango wangu ni huu; swala la likizo lisiwe mikononi kwetu bali kwa watoto wenyewe, wengi especially waliosoma boarding huwa wako kwenye strict routines, sidhani kama wanahitaji masomo ya ziada,sababu huko shuleni huwa wanapewa na muda wa kujisomea, kwa hio likizo ni sehemu ya kupumua,serikali kupanga au ku dectate wanatumiaje muda wao wa likizo haijakaa vizuri...mtaishia wapi mkifanikiwa hili? Kwa wafanyakazi wa umma? Au?...

What if mtoto ana struggle na physics anajiona kabisa yuko weak kwenye hilo somo anahitaji msaada, na anaona likizo yake aitumie kusoma zaidi, mkiweka restrictions huoni kama mnam FAIL huyu mtoto na system yenu?

Tuition pia zinaongeza CONFIDENCE...in the end, hii iwe kwa mtoto ku DECIDE aitumie muda wake kufanya nini wakati wa likizo, akijiona yuko weak somo fulani afanye masomo ya ziada, sawa. Akijiona anataka kupumzika basi sawa. The STATE,WAZAZI wasiingilie likizo za watoto...huu ndio mchango wangu..
 
Asante mkuu..lol
 
Hello JF,
Nimetafuta hii topic sijaiona kama ipo nielekezeni huko...lol

Binafsi nadhani nchi yetu bado haijawa na resources fully zinazotakiwa ziwe invested kwenye education, leo maabara changamoto,walimu shule za secondary za serikali hawakanyagi...
Watoto.wanahitaji kupumzika pia wafanye vitu vingine ndiyo maana watoto wanashindwa kujua mambo mengine ya kijamii. Elimu ya jamii pia ni muhimu sana.
 
Mtoto akiwa shuleni anaweza kutumia masaa hata 10 ukiunganisha muda wa kuwa shuleni, muda wa kujisomea, n.k.

Likizo akitumia hata masaa mawili kuna ubaya gani??

Tuishen za likizo zina faida sana tu, Nakumbuka enzi zetu kuna watu hizi likizo wakimaliza, shule zikifungua wamesha cover nusu ya vitu, kwao inakuwa marudio tu.

Kwa wale waliosoma shule za vipaji maalum hali ndio ilikuwa tete sana, mtu anatumia likizo hii kusomea vitu vyote vya mwaka mzima, kuna wengine walikuwa form 3 wanafanya mitihani na form 4.
 
Sijaelewa hii, hili swala la masomo ya ziada (Tuition) wanalazimishwa kufanya au ni hiari tuu? ni kubaki shule wakati wa likizo wanalazimishwa au ni hiari na lenyewe? tueleweshane
 
Sijaelewa hii, hili swala la masomo ya ziada (Tuition) wanalazimishwa kufanya au ni hiari tuu? ni kubaki shule wakati wa likizo wanalazimishwa au ni hiari na lenyewe? tueleweshane
Wanataka kupiga marufuku masomo ya ziada (tuition) wakati wa likizo kwa watoto wote. Ninachoona mimi serikali kuacha maswala muhimu kama kutoa syllabus inayoendana na mazingira yetu, kuongeza ufaulu, kuhakikisha shule especially za serikali zinakuwa na vifaa vyote eti wenyewe wanaweka maguvu kwenye petty issues kama likizo....by the way sioni kama wanawatendea haki watoto, huku ni kuingilia maisha yao,wameelezea tuition haih8tajiki, wakati kuna baadhi ya watoto extra tuition inawapa CONFIDENCE hivyo kufanya vizuri kwenye masomo, in the end wangewaachia watoto wachague wenyewe, kwenda tuition ama not,sio kupiga Marufuku kabisa
 
Back
Top Bottom