Kaliua urambo
JF-Expert Member
- Apr 21, 2009
- 603
- 127
Wabongo kitu moja(misimamo) hadi raha
mabomu kuangukia nchi ya mwenzako huo ni uchokozi! Ni vema kuheshimu mipaka ya mwenzako labda kama ni sababu ya kutaka kupima maamuzi ya rwanda!
Tanzania imetoa tahadhari kwa wajumbe wa Kudumu wa UNSC kuwa vikosi vyetu havitavumilia nchi yoyote itakayoingia DRC kusaidia M23 - Bernard Membe on Twitter
Lakini leo imebainika kuwa mabomu hayo yanarushwa na M23! ili kuwapa excuse rwanda kuivamia congo na ku-neutralize brigade ya UN source: AljazeeraMzozo wa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo unaonekana kuchukua sura mpya na ambayo inaanza kutia wasiwasi baada ya Rwanda kutishia kuchukua hatua za kijeshi endapo DRC itaendelea kurusha mabomu kwenye ardhi yake. Rwanda imeyasema hayo baada ya mabomu kumi kuanguka nchini Rwanda mfululizo na kumuua mtu mmoja na kujeruhi wengine kadhaa
source DW(KISWAHILI)
ahahahahaa,angola,zimbabwe,tz,DRC,south africa,mimi sina lakuongea lakini dunia itapigwa butwaaaaaaaaaaaa,mimi yangu macho.
Ni kweli kabisa.......hii si vita na M23 bali ni vita na Rwanda na swahiba wake mkuu Uganda.tanzania ilipeleka majeshi drc ikijua fika inaenda kupambana na rwanda, no m 23 without rwanda, vita kongo itakoma baada ya kagame kuondoshwa madarakani.
Bila shaka kawaambia M23 warushe mabomu kwake na ionekane ni askari wa DRC ili apate sababu ya kuingia huko. Asisahau kuna askari 3,000 wa Tz na South Africa na ikibdi SADC yote hasa wanaume wa Angola na Zimbabwe wanaweza kuingia huko
asubuhi nimeona malori ya jw yamepakia vifaru maeneo ya chalinze, nikabaki na maswali kibao.!
Nadhani weye umeiona vita katika sinema tu, au kwenye ndoto mororo usingizini. Ukweli ni kuwa nchi nyingi zimeanza vita kwa kuona zina uwezo wa ushindi wa haraka haraka!==>> Thubutu....karwanda tunapiga na kudandia juu...kagame KACHANGANYIKIWA....TUNAPIGA HADI DUNIA ITASHANGAA...
asubuhi nimeona malori ya jw yamepakia vifaru maeneo ya chalinze, nikabaki na maswali kibao.!
aisee vifaru vyetu ni vya kizamani kama vile vya drc, duh...tuko nyuma. Ndo maana museveni kaamua ku-modernize jeshi lake. Sasa hivi jeshi la uganda lina ndege za 4th generation kwenye air force. Sisi huku bado tuna ndege zilizotengenezwa sixties na 70s! Tusiombee vita kamili maana siyo ya advantage kwetu bongo. Uchumi wetu ni kusua sua na hatujajitosheleza hata kwa chakula. Vita vya ku-engage ni vile ambavyo vitaonekana kweli kutishia usalama na utangamano wa taifa. Hivi vita vingine ni vya kutafuta umaarufu usiokuwa na malipo!
lakini leo imebainika kuwa mabomu hayo yanarushwa na m23! Ili kuwapa excuse rwanda kuivamia congo na ku-neutralize brigade ya un source: Aljazeera
Iddi Amini alikuwa na jeshi zuri mwanzoni wakati anapindua serikali ya Obote 1971 kabla hajaanza kuwaua cream waliosoma na wazoefu; akaja kuwajaza kabila lake waliokuwa na elimu kama yake! Jua kwenye vita sio makelele tu na majigambo. Israel huwa inawashinda waarabu kwa akili na mazoezi ya jeshi ya muda wote. Kelele hizi za nyuma ya keyboard hazisaidii. Endelea kuwa shabiki wa vita kama vile unashabikia Man U ama Barca!jidanganyeni, hata amini 1978 alijiaminisha ana jeshi la kisasa na silaha za kisasa lakini aliishia kuangukia pua.