Rwanda yatishia kuishambulia kijeshi DRC

Rwanda yatishia kuishambulia kijeshi DRC

Unapotoa hoja kuwa na fikra kidogo hivi kama ni kweli mabomu yamerushwa ndani ya ardhi ya Rwanda kutoka DRC hapo mchokozi ni nani? na tukumbuke Idd amin alianza kuishambulia Tanzania kwa mbinu za kichokozi kama hizo mwisho wa siku akaingiza majeshi kabisa na kuua watanzania wengi kule Kagera kama ni kweli wamerusha mabomu ni vema Rwanda nayo ikajihami na uvamizi huo.
Unahitaji kujua zaidi ya hizo propaganda za mabomu kurushwa ndani ya Rwanda. Moja sehemu wanayopigania ni mpakani kabisa mwa Rwanda. Mji wa Goma (Kongo) na Gisenyi (Rwanda) ni mmoja uliotenganishwa na mpaka tu. Kwa hiyo ni ngumu kupigana Goma na Gisenyi isidhurike. Lakini kubwa ni kuwa kuna uthibitisho kuwa M23 ni kikosi cha Rwanda. Umoja wa mataifa wanasema mabomu hayo yanarushwa na wao M23, pengine kutafuta sababu ya kulalamika au kuingia ndani ya Kongo.
 
Unapotoa hoja kuwa na fikra kidogo hivi kama ni kweli mabomu yamerushwa ndani ya ardhi ya Rwanda kutoka DRC hapo mchokozi ni nani? na tukumbuke Idd amin alianza kuishambulia Tanzania kwa mbinu za kichokozi kama hizo mwisho wa siku akaingiza majeshi kabisa na kuua watanzania wengi kule Kagera kama ni kweli wamerusha mabomu ni vema Rwanda nayo ikajihami na uvamizi huo.

Mbona majeshi yatanzania ndio yanatumia mizinga congo! hiyo inajulikana,subirini jamaa wakizama congo mtausikia mziki wao,mnasema m 23 inasaidiwa na rwanda,hamujui mziki wao,mkisikia wameingia hakutakua cha angola,zimbabwe,drc,fdlr,tz yani ni kiboko mbele kwa mbele,waache waendelee kuchokoza.

Mawazo hayo hayana tofauti na mawazo na maneno ya CCM juu ya tukio la Soweto hivi kuna uwezekano kweli ukajirishia mabomu na kuua raia wako? hayo ni mawazo ya kipuuzi

Sikilizeni nyie Wanyarwanda
Msiwe mnasahau kirahisi hivyo. Miaka kadhaa Kagame na jeshi wamekuwapo DRC wakipiga mabomu na risasi na kuua watu.............Nikuulizeni kuna sheria gani inaruhusu Jeshi la Rwanda kuingia ndani ya Nchi nyingine?

Kgame na Jeshi lake alishawahi kupigana na Wanajeshi wa Uganda kwenye ardhi ya Congo wakigombea madini.....Nani aliwapa mamlaka hayo.

Kagame & Co. watulie tu, wembe uleule uliowakata Wacongo kwa zaidi ya muongo mmoja ndiyo huohuo utawakata.
 
ahahahahaa,angola,zimbabwe,tz,DRC,south africa,mimi sina lakuongea lakini dunia itapigwa butwaaaaaaaaaaaa,mimi yangu macho.

Kwa nini tusiwe kama Zambia tu ..................... tuwaachie wenyewe na nchi yao, tulinde mipaka yetu!!

Kabila alipokufa kuna nchi kama saba zilikuwa huko kupigana. Jamaa wako wengi (Zaidi ya million 80) hamtawamaliza. Wakiondoka hao M23 fter 2 years wataibuka wengine. Wasije wakafanya siri tu askari wetu watakapoanza kupukutika.
 
Rwanda inajua m23 karibia washindwe sasa anajipanga kuingia mwenyewe kwa hicho kisingizio!! Wataalam wa siraha wahusishwe katika hili haingii akilini Congo yenye matatizo Kila siku iivamie Rwanda kijeshi! Kagame wa kuangalia Sana muda wote mwili unamuwasha anataman damu ya watu imwagike!
 
MUKAMAAIMBA: Kama M23 sio wa Paulo kwanini asishirikiane na MONUSCO tukawabananisha hawa magaidi M23 na FDLR??
 
Bila shaka kawaambia M23 warushe mabomu kwake na ionekane ni askari wa DRC ili apate sababu ya kuingia huko. Asisahau kuna askari 3,000 wa Tz na South Africa na ikibdi SADC yote hasa wanaume wa Angola na Zimbabwe wanaweza kuingia huko
Na huo ndio ukweli uliopo RDF sasa itaingia vitani kwa Madai ya kujilinda.wamesema kama mabomu yataendelea kurushwa Rwanda wanaingia vitani.siku mbili tatu hizi utasikia mabomu yamerushwa tenta hivyo inawabidi kujilinda kumbe wanayalipua wenyewe.
 
Muda wa kagame naona unaisha hivyo anatapatapa. Akithubutu tu nahisi ndio utakuwa mwanzo wa mwisho wake kwa sababu akiigusa Tanzania atakuta kumbe hatuko peke yetu, kuna Msumbiji, Zimbabwe, Angola na Afrika kusini ambao wana usongo wa kuondoa jeuri yake. Tusubiri tuone.
 
mabomu kuangukia nchi ya mwenzako huo ni uchokozi! Ni vema kuheshimu mipaka ya mwenzako labda kama ni sababu ya kutaka kupima maamuzi ya Rwanda!
Sidhani kama hayo mabomu yanalengwa kwa maksudi lazima itakuwa ni bahati mbaya,lakini pia kumbuka mabomu hayana macho.
 
.Tulishasema humu ndani na tutaendelea kusema kuwa mwisho wa Kagame na kagenge chake unahesabika.......maji sasa yamefika shingoni
..Majuzi baada ya M23 kuelemewa walijaribu kupeleka toka Rwanda reinforcement ambayo pia kikosi cha Afrika Kusini kilidhibidi kwa kutumia helcopter gunships
...Hatimaye makao yao makuu pale Kibati yametekwa na wanaume wa shoka
...Tunasuburi M23 wote kuvuka mpaka kukimbilia Rwanda, huko tutahitaji wakamatwe warudishwe Congo, la sivyo naiona Gisenyi kuwa next step..!
...Update toka twitter ya JW inathibitisha utekwaji wa Kibati

Jeshi la Wananchi Tz ‏@JW_TZ 31m Mapigano yaliyodumu saa 24 tangu 28/8/2013 tumefanikiwa kuichukua ngome kuu ya waasi wa M23 ya Kibati (Nyirangongo Territory - Goma, E- DRC)
 
Kagame anacheza mechi asiyoijua ila waswahili walisema mfa maji ahachi kutapa tapa na jinsi anavyotapa ndivyo anavozidi kujichimbia kaburi, ITS TIME NOW FOR KAGAME TO GO
 
Yaani huyu Kagame, ni kurusha mabomu mpaka kile Kigali ikiwezekana mpaka hata Uganda ili waingie vitani then sisi tutakuwa tunawatandika tukiwa tunajua hawa ni M23 tunazama Rwanda tunamfukuzia Uganda au akipatikana anauawa, tunaweka mtu wetu pale Rwanda.
Kinachotafutwa hapa ni kisababishi cha kuzama Rwanda
 
M23 wanakimbia front line JW wagongenimpaka Rwanda.msiwaachie!.
 
mwambie awe straight kwamb anataka apigane na wanajesh wa tz,aachane kuruka ruka
 
Kagame anacheza mechi
asiyoijua ila waswahili walisema mfa maji ahachi kutapa tapa na jinsi
anavyotapa ndivyo anavozidi kujichimbia kaburi, ITS TIME NOW FOR KAGAME
TO GO

Kama Kagame akiwa msituni na genge lake la kigaidi la RPF aliweza kupanga na kufanikisha mauaji ya marais wa nchi mbili kwa mpigo sisi tunashindwa nini kumuua yeye?
 
Mwambieni Kimbaumbau ajaribu kuingilia hii vita kwa kutuma majeshi yake kupigana na JWTZ aone chamoto tutakapoanza kumchapa kupitia Ngara na Karagwe mpaka Kigali.
 
Nadhani hao M23 wanatumia mbinu ya kurusha mabomu huko Rwanda na kuifanya Rwanda ione wanaofanya hayo ni Serikali ya DRC. Hata uko Syria inawezekana matumizi ya silaha za kemikali yakawa yalifanywa na wapinzani wa Serikali ya Syria.
 
tulia wee kiboga mnyarwanda, tukio la soweto huwezi kulinganisha na hilo la Rwanda,
Kiboga nafikiri utakuwa wewe unayeshabikia vita nyuma ya keyboard huku ndugu wa yule Major aliyeuawa wanamajonzi na masikitiko juu ya mpendwa wao hii yote ni sababu ya sifa za kijinga wanazotaka hawa viongozi wetu.
 
Back
Top Bottom