Rwanda yalegea, malori ya TZ yaruhusiwa

Rwanda yalegea, malori ya TZ yaruhusiwa

wamelazimika kufungua baada ya bidhaa kupanda ghafla km vile mafuta (fuel) na vyakula,nimewasiliana na m2 ambaye yuko rwanda akasema endapo ingeendelea siku mbili mafuta ya magari yangepanada mara mbili na pengine pangetokea upungufu mkubwa sana wa bidhaa mbalimbali ha kigali
 
muziki wa wahamiaji haramu upo pale pale! Rwanda hana ujanja wa kuitenga tanzania. Rwanda kwa tanzania ni sawa na kichwa na bega. Rwanda ni bega-kamwe haliwezi kukivuka kichwa!

this is very true,...
 
Kichwa cha habari kimekaa kishabiki!

Pia unajua makubaliano yamefikiwaje? fuatilia vyema utajua TZ imepiga magoti na kupoteza baadhi ya haki zake kufikia maamuzi hayo.

Mkuu hebu fafanua vizuri, je hayo makubaliano hayahusu kusitishwa kwa kuwafurusha wahamiaji haramu?

Muziki wa wahamiaji haramu upo pale pale! Rwanda hana ujanja wa kuitenga Tanzania. Rwanda kwa Tanzania ni sawa na kichwa na bega. Rwanda ni bega-kamwe haliwezi kukivuka kichwa!
Kama hoja ya Tume ya katiba ina ukweli, ni kitu gani zaidi ni stake kiasi cha rwanda kukifanya kiwe sharti kwa Tanzania zaidi ya wahamiaji haramu?
 
wamelazimika kufungua baada ya bidhaa kupanda ghafla km vile mafuta (fuel) na vyakula,nimewasiliana na m2 ambaye yuko rwanda akasema endapo ingeendelea siku mbili mafuta ya magari yangepanada mara mbili na pengine pangetokea upungufu mkubwa sana wa bidhaa mbalimbali ha kigali
Hii hoja inamashiko.
 
Sababu ya kupanda ghafla.....!!???

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Nilichogundua ni kwamba kuna wanaofurahia mgogoro kati ya Rwanda na Tanzania...kwa sababu wanazojua wenyewe. Uamuzi wa Rwanda kurekebisha kodi hiyo ulipaswa kupongezwa na sio kukejeliwa kuwa WAMETUOGOPA. Uamuzi wa Wizara husika huko Rwanda kujulishwa kuwa kuna tamko lenye utata, na wizara hiyo kulifanyia kazi mara moja unapaswa kuigwa na wababaishaji wetu walioweka pamba kwenye masikio.

Acheni kulazimisha uhasama na Rwanda. Hata kichwa cha habari cha "Rwanda YALEGEA..." kimekaa mkao wa ki-shari. What about "Rwanda YALEGEZA/YABADILI msimamo?

And by the way, mie si Mnyarwanda bali naamini maadui wetu wakubwa ni wapuuzi kama Prof Muhongo anayetuaminisha kuwa sie tunaweza kuwekeza kwenye juisi tu sio gesi, au huyo Rais wetu mzururaji ambaye kila kukicha yupo kiguu na njia kutalii huku nchi inazidi kutafunwa na mafisadi
 
Tanzania yalegea kwanza.

Bado nipo hapa Rusumo mpakani mwa Tanzania na Rwanda, kwa habari ambazo ni rasmi Serekali ya Rwanda imefuta ongezeko la ushuru wa barabara ( Road Toll) la USD 500 kwa kila gari lenye usajili wa Tanzania na kuanzia leo kila gari litavuka kwa ushuru wa zamani wa USD 152. Uamuzi huu umefikiwa baada ya Mamlaka Ya Mapato Tanzania (TRA) kulazimika kupunguza ushuru wa barabara ( Road Toll) kwa magari yenye plate numbers za Rwanda kutoka USD 500 mpaka USD 150. Hatua hii inaoenakana ni ushindi mkubwa kwa Rwanda ikizingatiwa kuwa umbali kutoka Dar mpaka Rusumo sio sawa na umbali kutoka Rusumo mpaka Kigali....kwahiyo ushuru wa barabara hauwezi kuwa sawa kwa simple basics za economics.....

Jeuri hiyo hamna.....mizigo hiyo sio ya watanzania ni migizo ya wanyarwanda.....! Usitukane wakunga na uzazi ungalipo
 
Kasema ofisa mmoja katika Wizara ya Fedha ya Rwanda ndiye aliyezomoka na kutangaza mabadiliko hayo kwa mdomo. Waziri wa Fedha Rwanda alipoulizwa na mwenzake wa Tanzania, alishituka, na akaahidi kulipatia ufumbuzi. Tzeba kasema ndani ya dakika 30 jibu likawa limepatikana kuwa agizo la ofisa wa Rwanda halikuwa halali.

Muhimu: Nadhani Rwanda wanajua bila Tanzania hawana maisha. Huo ndiyo ukweli. Rais Kagame asituvuruge uhusiano wa nchi hizi mbili.

Kwani Kagame ndo alitoa hilo agizo?
 
Kasema ofisa mmoja katika Wizara ya Fedha ya Rwanda ndiye aliyezomoka na kutangaza mabadiliko hayo kwa mdomo. Waziri wa Fedha Rwanda alipoulizwa na mwenzake wa Tanzania, alishituka, na akaahidi kulipatia ufumbuzi. Tzeba kasema ndani ya dakika 30 jibu likawa limepatikana kuwa agizo la ofisa wa Rwanda halikuwa halali.

Muhimu: Nadhani Rwanda wanajua bila Tanzania hawana maisha. Huo ndiyo ukweli. Rais Kagame asituvuruge uhusiano wa nchi hizi mbili.

tunashukuru kwa ufafanuzi, watusi washaanza kupotosha mada humu ndani tayari.
 
nilijua tu mbio za baiakeli ya mbao mwisho kilimani!!
 
Tanzania yalegea kwanza.

Bado nipo hapa Rusumo mpakani mwa Tanzania na Rwanda, kwa habari ambazo ni rasmi Serekali ya Rwanda imefuta ongezeko la ushuru wa barabara ( Road Toll) la USD 500 kwa kila gari lenye usajili wa Tanzania na kuanzia leo kila gari litavuka kwa ushuru wa zamani wa USD 152. Uamuzi huu umefikiwa baada ya Mamlaka Ya Mapato Tanzania (TRA) kulazimika kupunguza ushuru wa barabara ( Road Toll) kwa magari yenye plate numbers za Rwanda kutoka USD 500 mpaka USD 150. Hatua hii inaoenakana ni ushindi mkubwa kwa Rwanda ikizingatiwa kuwa umbali kutoka Dar mpaka Rusumo sio sawa na umbali kutoka Rusumo mpaka Kigali....kwahiyo ushuru wa barabara hauwezi kuwa sawa kwa simple basics za economics.....
Kumbe hawajamaa walifanya makusudi baada ya Tz kuwa wakaidi ....
 
Tumezungumza na Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk. Tzeba, amethibitisha kuwa Serikali ya Rwanda imeruhusu malori ya Tanzania yaendelee na safari kwa kulipa dola 152 badala ya 500 zilizoanza kutozwa jana. Kasema Waziri wa Fedha wa Rwanda, aitwaye Gatete, na wa Uchukuzi, Rwakabamba, wameridhia tozo ya dola 152 iendelee.

Source: mimi mwenyewe-dodoma
Tena huyo Prof Lwakabamba ni mtoto wa UDSM miaka hiyo!!
 
Tumezungumza na
Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk. Tzeba, amethibitisha kuwa Serikali ya
Rwanda imeruhusu malori ya Tanzania yaendelee na safari kwa kulipa dola
152 badala ya 500 zilizoanza kutozwa jana. Kasema Waziri wa Fedha wa
Rwanda, aitwaye Gatete, na wa Uchukuzi, Rwakabamba, wameridhia tozo ya
dola 152 iendelee.

Source: mimi mwenyewe-dodoma

Kwa serekali hii dhaifu haichelewe kusema,waruhusuni kwa $152 hizo $348 tutakuwa tunazitop up kila mwezi.
 
Back
Top Bottom