Rwanda yalegea, malori ya TZ yaruhusiwa

Rwanda yalegea, malori ya TZ yaruhusiwa

Manyerere Jackton

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
2,438
Reaction score
4,463
Tumezungumza na Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk. Tzeba, amethibitisha kuwa Serikali ya Rwanda imeruhusu malori ya Tanzania yaendelee na safari kwa kulipa dola 152 badala ya 500 zilizoanza kutozwa jana. Kasema Waziri wa Fedha wa Rwanda, aitwaye Gatete, na wa Uchukuzi, Rwakabamba, wameridhia tozo ya dola 152 iendelee.

Source: mimi mwenyewe-dodoma
 
Tumezungumza na Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk. Tzeba, amethibitisha kuwa Serikali ya Rwanda imeruhusu malori ya Tanzania yaendelee na safari kwa kulipa dola 152 badala ya 500 zilizoanza kutozwa jana. Kasema Waziri wa Fedha wa Rwanda, aitwaye Gatete, na wa Uchukuzi, Rwakabamba, wameridhia tozo ya dola 152 iendelee.

Source: mimi mwenyewe-dodoma

na kasema ilikuwa imewekwa kwa sababu gani?
 
Aksante kwa taarifa, tunahitaji ufafanuzi zaidi wa kilichopelekea hiyo hali na pia kilichofanyika wakabadili msimamo. Usikute tumewapigia magoti.
 
na kasema ilikuwa imewekwa kwa sababu gani?


Kasema ofisa mmoja katika Wizara ya Fedha ya Rwanda ndiye aliyezomoka na kutangaza mabadiliko hayo kwa mdomo. Waziri wa Fedha Rwanda alipoulizwa na mwenzake wa Tanzania, alishituka, na akaahidi kulipatia ufumbuzi. Tzeba kasema ndani ya dakika 30 jibu likawa limepatikana kuwa agizo la ofisa wa Rwanda halikuwa halali.

Muhimu: Nadhani Rwanda wanajua bila Tanzania hawana maisha. Huo ndiyo ukweli. Rais Kagame asituvuruge uhusiano wa nchi hizi mbili.
 
Je ametoa sababu ya ongezeko la ghafla? Nini kimebadili msimamo wao mkuu?
 
Kasema ofisa mmoja katika Wizara ya Fedha ya Rwanda ndiye aliyezomoka na kutangaza mabadiliko hayo kwa mdomo. Waziri wa Fedha Rwanda alipoulizwa na mwenzake wa Tanzania, alishituka, na akaahidi kulipatia ufumbuzi. Tzeba kasema ndani ya dakika 30 jibu likawa limepatikana kuwa agizo la ofisa wa Rwanda halikuwa halali.

Muhimu: Nadhani Rwanda wanajua bila Tanzania hawana maisha. Huo ndiyo ukweli. Rais Kagame asituvuruge uhusiano wa nchi hizi mbili.

Nina wasiwasi huyu anaweza kuwa murutongore au Balali.

 
Last edited by a moderator:
Mi nadhani wengine wasipeleke tena mizigo Na hao wakifikisha hiyo mizigo wasirudi tena hadi suluhu ya kudumu ipatikane
 
Kichwa cha habari kimekaa kishabiki!

Pia unajua makubaliano yamefikiwaje? fuatilia vyema utajua TZ imepiga magoti na kupoteza baadhi ya haki zake kufikia maamuzi hayo.
 
Kasema ofisa mmoja katika Wizara ya Fedha ya Rwanda ndiye aliyezomoka na kutangaza mabadiliko hayo kwa mdomo. Waziri wa Fedha Rwanda alipoulizwa na mwenzake wa Tanzania, alishituka, na akaahidi kulipatia ufumbuzi. Tzeba kasema ndani ya dakika 30 jibu likawa limepatikana kuwa agizo la ofisa wa Rwanda halikuwa halali.

Muhimu: Nadhani Rwanda wanajua bila Tanzania hawana maisha. Huo ndiyo ukweli. Rais Kagame asituvuruge uhusiano wa nchi hizi mbili.

Hapa inaonekana wazi walikwishaongea lakini afisa aliongeza ushuru prematurely. Ipo siku watafanya hivyo, watanzania tujiandae tusibweteke
 
Kichwa cha habari kimekaa kishabiki!

Pia unajua makubaliano yamefikiwaje? fuatilia vyema utajua TZ imepiga magoti na kupoteza baadhi ya haki zake kufikia maamuzi hayo.

wewe kama unajua si utuambie au unaishi maisha ya dhahania.
 
Kichwa cha habari kimekaa kishabiki!

Pia unajua makubaliano yamefikiwaje? fuatilia vyema utajua TZ imepiga magoti na kupoteza baadhi ya haki zake kufikia maamuzi hayo.
Mkuu hebu fafanua vizuri, je hayo makubaliano hayahusu kusitishwa kwa kuwafurusha wahamiaji haramu?
 
Mkuu hebu fafanua vizuri, je hayo makubaliano hayahusu kusitishwa kwa kuwafurusha wahamiaji haramu?


Muziki wa wahamiaji haramu upo pale pale! Rwanda hana ujanja wa kuitenga Tanzania. Rwanda kwa Tanzania ni sawa na kichwa na bega. Rwanda ni bega-kamwe haliwezi kukivuka kichwa!
 
Hehee kumbe tishio letu limeigusa Rwanda,

Tukiwa kama taifa lenye kura ya Veto tunayo kila sababu ya kuwa na karipio kwa yeyote EAC

Tulitoa saa 24 za angamizo kwa Kagame

Aagh wacha kutishia nyau bro....!!
 
Tumezungumza na Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk. Tzeba, amethibitisha kuwa Serikali ya Rwanda imeruhusu malori ya Tanzania yaendelee na safari kwa kulipa dola 152 badala ya 500 zilizoanza kutozwa jana. Kasema Waziri wa Fedha wa Rwanda, aitwaye Gatete, na wa Uchukuzi, Rwakabamba, wameridhia tozo ya dola 152 iendelee.

Source: mimi mwenyewe-dodoma

Tanzania yalegea kwanza.

Bado nipo hapa Rusumo mpakani mwa Tanzania na Rwanda, kwa habari ambazo ni rasmi Serekali ya Rwanda imefuta ongezeko la ushuru wa barabara ( Road Toll) la USD 500 kwa kila gari lenye usajili wa Tanzania na kuanzia leo kila gari litavuka kwa ushuru wa zamani wa USD 152. Uamuzi huu umefikiwa baada ya Mamlaka Ya Mapato Tanzania (TRA) kulazimika kupunguza ushuru wa barabara ( Road Toll) kwa magari yenye plate numbers za Rwanda kutoka USD 500 mpaka USD 150. Hatua hii inaoenakana ni ushindi mkubwa kwa Rwanda ikizingatiwa kuwa umbali kutoka Dar mpaka Rusumo sio sawa na umbali kutoka Rusumo mpaka Kigali....kwahiyo ushuru wa barabara hauwezi kuwa sawa kwa simple basics za economics.....
 
Back
Top Bottom