Rwanda yalegea, malori ya TZ yaruhusiwa

Rwanda yalegea, malori ya TZ yaruhusiwa

Kasema ofisa mmoja katika Wizara ya Fedha ya Rwanda ndiye aliyezomoka na kutangaza mabadiliko hayo kwa mdomo. Waziri wa Fedha Rwanda alipoulizwa na mwenzake wa Tanzania, alishituka, na akaahidi kulipatia ufumbuzi. Tzeba kasema ndani ya dakika 30 jibu likawa limepatikana kuwa agizo la ofisa wa Rwanda halikuwa halali.

Muhimu: Nadhani Rwanda wanajua bila Tanzania hawana maisha. Huo ndiyo ukweli. Rais Kagame asituvuruge uhusiano wa nchi hizi mbili.

Manyerere wewe ndio unavuruga watu kwa hadithi zako alfu ulela ulela msimsingizie kagame toeni boriti kwenye jicho lenu ndipo mtaona kibanzi cha kagame
 
Tumezungumza na Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk. Tzeba, amethibitisha kuwa Serikali ya Rwanda imeruhusu malori ya Tanzania yaendelee na safari kwa kulipa dola 152 badala ya 500 zilizoanza kutozwa jana. Kasema Waziri wa Fedha wa Rwanda, aitwaye Gatete, na wa Uchukuzi, Rwakabamba, wameridhia tozo ya dola 152 iendelee.

Source: mimi mwenyewe-dodoma

Lakini kwanini viwango viwe tofauti na kupewa favour Tanzania pekee? Au ni kwa ajili ya hali ya kisiasa inayoendelea kati yetu? Kama ndivyo basi Rwanda wanamengi wanaitaji kutoka kwetu. Kwani ukweli huwezi kubadilisha sera zako kwa ajili ya nchi moja tu na wengine kutumia sera nyingine lazima kuna sababu.
 
uTumezungumza na Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk. Tzeba, amethibitisha kuwa Serikali ya Rwanda imeruhusu malori ya Tanzania yaendelee na safari kwa kulipa dola 152 badala ya 500 zilizoanza kutozwa jana. Kasema Waziri wa Fedha wa Rwanda, aitwaye Gatete, na wa Uchukuzi, Rwakabamba, wameridhia tozo ya dola 152 iendelee.

Source: mimi mwenyewe-dodoma

Wewe mbunge?
 
Tuache kuukuza huu mgogoro bila sababu za msingi
 
Badilisha kichwau cha habari kiwe, 'TANZANIA YALEGEA, YAPUNGUZA USHURU WA MAGARI YA RWANDA'. Ushabiki wa kipuuzi hautusaidii. Kumbe tatizo lilikuwa ni la Tanzania kuweka ushuru mkubwa wa dola 500 kwa malori ya Rwanda, nao wakajibu mapigo. Tanzania ikasalimu amri.

Wanyarwanda kwenye hilo nitawapongeza, wana akili. Siyo kama sisi hapa serikali inajiongezea ushuru kwa kila kitu sisi tupo kimya. Mburula watanzania ni kama kondoo.

Bams wewe kweli bum ha ha ha
 
Kichwa cha habari kimekaa kishabiki!

Pia unajua makubaliano yamefikiwaje? fuatilia vyema utajua TZ imepiga magoti na kupoteza baadhi ya haki zake kufikia maamuzi hayo.

Kwa shida gan Tz iliyonayo hadi kuipigia got rwanda?mizingo inayoingia rwanda n sawa na ile inayokwenda mikoa ya kanda ya ziwa,acheni kuwalinganisha mbuz na ng'ombe bhana.
 
Kichwa cha habari kimekaa kishabiki!

Pia unajua makubaliano yamefikiwaje? fuatilia vyema utajua TZ imepiga magoti na kupoteza baadhi ya haki zake kufikia maamuzi hayo.

Ni vema unapopinga hoja basi uje na ile unayoiamini ili kutunza heshima ya wasomi.
 
ushabiki wa aina hii hautuongezei gdp, naamini kulikuwa na namna nyingi na nzuri zaidi za kuiwasilisha hii habari.
 
Kasema ofisa mmoja katika Wizara ya Fedha ya Rwanda ndiye aliyezomoka na kutangaza mabadiliko hayo kwa mdomo. Waziri wa Fedha Rwanda alipoulizwa na mwenzake wa Tanzania, alishituka, na akaahidi kulipatia ufumbuzi. Tzeba kasema ndani ya dakika 30 jibu likawa limepatikana kuwa agizo la ofisa wa Rwanda halikuwa halali.

Muhimu: Nadhani Rwanda wanajua bila Tanzania hawana maisha. Huo ndiyo ukweli. Rais Kagame asituvuruge uhusiano wa nchi hizi mbili.

Pamoja na hayo, bado ninao wasi wasi kuwa huyo jamaa kweli alikurupuka bila maelekezo. Mi nadhani walikuwa wanatikisa kiberiti.
 
Tanzania yalegea kwanza.

Bado nipo hapa Rusumo mpakani mwa Tanzania na Rwanda, kwa habari ambazo ni rasmi Serekali ya Rwanda imefuta ongezeko la ushuru wa barabara ( Road Toll) la USD 500 kwa kila gari lenye usajili wa Tanzania na kuanzia leo kila gari litavuka kwa ushuru wa zamani wa USD 152. Uamuzi huu umefikiwa baada ya Mamlaka Ya Mapato Tanzania (TRA) kulazimika kupunguza ushuru wa barabara ( Road Toll) kwa magari yenye plate numbers za Rwanda kutoka USD 500 mpaka USD 150. Hatua hii inaoenakana ni ushindi mkubwa kwa Rwanda ikizingatiwa kuwa umbali kutoka Dar mpaka Rusumo sio sawa na umbali kutoka Rusumo mpaka Kigali....kwahiyo ushuru wa barabara hauwezi kuwa sawa kwa simple basics za economics.....

Manyerere aliwahi kupata utapia mlo anatakiwa afundishwe kufikiri vizuri
 
Jackton Manyerere tunaomba uulizie na hili jambo jamaa kaliweka hapa ili story nzima iwe balanced
Ni kweli hebu fuatilia Manyerere Jackton
Hii thread tulishaijadili humuhumu JF na inaendelea ndio maana mm siamini maneno ya Dk Charles Tizeba
Akizungumza na gazeti hili jana, Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk Charles Tizeba, alikiri Wizara yake kupata taarifa za kupanda kwa ushuru huo kupitia wafanyabiashara, lakini hadi sasa wizara hiyo haijapewa taarifa rasmi na Rwanda.
Kuna Thread iliyoletwa na Member nahisi ni Dreva aliyekwama kuanzia jana na leo mchana akaleta majibu kuwa ni mamlaka ya mapato TRA ndio wamerekebisha, Hivyo Mzee wa Kwembe p/se fuatilia uje na ukweli kati ya huyo dreva na Naibu Waziri nani ni mkweli?


https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...magari-ya-mizigo-yanayotokea-tanzania-15.html

Wana Jamiii
Nipo hapa Rusumo mpakani mwa Tanzania na Rwanda.....siamini ninachokiona machoni mwangu....kuanzia jana tarehe 1/09/2013 serekali ya Rwanda imeongeza ushuru wa barabara ( ROAD TOLL)

UPDATES - 03.09.2013
Bado nipo hapa Rusumo mpakani mwa Tanzania na Rwanda, kwa habari ambazo ni rasmi Serekali ya Rwanda imefuta ongezeko la ushuru wa barabara ( Road Toll) la USD 500 kwa kila gari lenye usajili wa Tanzania na kuanzia leo kila gari litavuka kwa ushuru wa zamani wa USD 152. Uamuzi huu umefikiwa baada ya Mamlaka Ya Mapato Tanzania (TRA) kulazimika kupunguza ushuru wa barabara ( Road Toll) kwa magari yenye plate numbers za Rwanda kutoka USD 500 mpaka USD 150. Hatua hii inaoenakana ni ushindi mkubwa kwa Rwanda ikizingatiwa kuwa umbali kutoka Dar mpaka Rusumo sio sawa na umbali kutoka Rusumo mpaka Kigali....kwahiyo ushuru wa barabara hauwezi kuwa sawa kwa simple basics za economics.....
 
hii nchi hapo awali ilikuwa Tanganyika EastAfrika naona sasa ni mda muwafaka kurudisha ramani ya mwaka 1885. na Rwanda kuwa mkoa wa Tanganyika kama itakavyokuwa Zanzibar.
 
Muziki wa wahamiaji haramu upo pale pale! Rwanda hana ujanja wa kuitenga Tanzania. Rwanda kwa Tanzania ni sawa na kichwa na bega. Rwanda ni bega-kamwe haliwezi kukivuka kichwa!
Wewe tulishakuambuia kaombe kazi FDLR wanatafuta propaganda officer,huna business or anything of value hapa JF
 
hii nchi hapo awali ilikuwa Tanganyika EastAfrika naona sasa ni mda muwafaka kurudisha ramani ya mwaka 1885. na Rwanda kuwa mkoa wa Tanganyika kama itakavyokuwa Zanzibar.
Angalia akili za makamasi hizi,michosho kweli kweli.
 
Jamani naomba sana tujitahidi kutoshabikia mambo tusiyoyajua. Na yanayoendeleza uhasama.
Swala hili sio la leo umoja wa wadanyabiashara wa rwanda na tanzania wanalijua fika.mazungumzo yamekuwepo muda mwingi. Magari yenye usajiri wa rwanda yanalipa 500usd yakija tanzania na ya tanzania yanalipa 152 hivyo unaona hakuna uwiano na kilichofanyika ni rra kupandisha ili k i wepo uwiano ama na magari ya rwanda kuwepo na uwiano ktk biashara nao walipe 152. Sitisho hili ni la wiki moja ili mawaziri husika wakae na kuafikiana baada ya hapo 500. Tuwe tunaandika kwa kujua ukweli bila upotoshaji.
Shukrani.
 
Angalau sasa mambo yamekaa sawa,nilishtuka sana kuskia tozo za barabara kwa 'malori ya tz' kwenda Rwanda zimepanda ghafla kutoka dola 152 had 500?! hongera Jf hongera NW Bw Tzeba
 
'tuliongea na Naibu waziri ambaye aliongea na Waziri na baada ya dakika 30 tatizo lilikuwa limekwisha'......I like this kind of intervention.

Unajua ingekuwa upande mwingine mambo yangekuwa hivi, '.tuliongea na nananaaaa....hata hivyo bado ilo suala linajadiliwa na mchakato wake bado....kikao cha mwisho ktk tatizo hilo ni kesho na tutawajulisha.....'
 
Back
Top Bottom