Rwanda Vs Uganda nani atashinda Vita?

Rwanda Vs Uganda nani atashinda Vita?

Marekani hakushindwa Vita Vietnam,aliyeshindwa Vita Vietnam Ni Wanasiasa wa Marekani waliorudisha majeshi Nyuma ili waweze kuchaguliwa. Hata Afghanstan tunaambiwa Marekani Kashindwa Vita,Lakini aliyeshindwa Vita Afghanstan Ni Rais Joe Biden na Wala Sio Jeshi la Marekani. Jeshi la Marekani lilikuwa na uwezo wa kuendelea kuikalia Afghanstan hata kwa miaka mingine 20 endapo Wanasiasa wasingeliingiza Jeshi kwenye kampeni zao za Kisiasa za kutafuta Kura. Kwahiyo uwe unatofautisha vitu hivyo.
😄😄😄 Basi tufanye US ilishinda Vita ya Vietnam,Russia iliwashinda Muhajidina huku USA ikiwashinda Taliban 😄😄
 
Rwanda aliipiga mara 3 Uganda kwny kisangani war,maelfu ya wanajeshi wa Uganda waliuwawa na mageneral wa jeshi la Uganda walitekwa wakapelekwa Rwanda baadae wakapandishwa ndege from Kanombe to Kampala kwa aibu Sana,Kagame alishakua CMI(Chief of Military Intelligence) wa Jeshi la Uganda anawafahamu Uganda nje ndani yaani kifupi wanajeshi wengi walioko kwny jeshi la Rwanda RDF(Seniors) walilitumikia jeshi la Uganda tangu likiwa Msituni wakiwa waasi wakiitwa NRA mpk Sasa wanaitwa UPDF kwa hio wanalijua nje ndani.

Mwisho wa siku Hawa hawatapigana,watafanyiana vitimbi vya kuchokonoana kiinteligensia then ndo basi tena.
Huyu anayesema Tz vs Rwanda jasho litatutoka hivi haya si matusi mkuu kwa tpdf?

Au tunajioverrate bure?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ya Rwanda na Uganda, watajuana wenyewe. Ila ikitokea Rwanda wakajichanganya kwa TZ, wataenda kusimuliana huko Jehanam.

Tutapeleka vifaa kadhaa hapo Kigoma, then tunawaachia ndugu zetu "Waha" kazi ya kumnyoosha Kagame, huku mikoa yetu mingine ikiendelea na shughuli mbalimbali za ujenzi wa taifa!

Na tunavyozitamani pisi zao, wajichanganye tu!
 
Rwanda aliipiga mara 3 Uganda kwny kisangani war,maelfu ya wanajeshi wa Uganda waliuwawa na mageneral wa jeshi la Uganda walitekwa wakapelekwa Rwanda baadae wakapandishwa ndege from Kanombe to Kampala kwa aibu Sana,Kagame alishakua CMI(Chief of Military Intelligence) wa Jeshi la Uganda anawafahamu Uganda nje ndani yaani kifupi wanajeshi wengi walioko kwny jeshi la Rwanda RDF(Seniors) walilitumikia jeshi la Uganda tangu likiwa Msituni wakiwa waasi wakiitwa NRA mpk Sasa wanaitwa UPDF kwa hio wanalijua nje ndani.

Mwisho wa siku Hawa hawatapigana,watafanyiana vitimbi vya kuchokonoana kiinteligensia then ndo basi tena.
Wanajeshi wa tangu 1980s ndio unasema wanajulikana na siri zao zinajulikana. Ukishajua Uganda wana Su-30 fighters na Mil Mi-24 attack helicopters ndio unashinda vita bure?

Rwanda sio wazembe ila hii sio point. Ni sawa na kusema Tanzania itaishinda Angola kwa kuwa tuliwahi toa support kwenye vita yao na makaburu
 
Safi..kumbe hata Kenya ni kelele tu sio na KDF yao..

No wonder operations nyingi za kimataifa mkono wa tpdf unakuwa na umuhimu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwanza Kenya ktk majeshi yako very indiscipline kwa East Africa nadhani la kwanza Ni Jeshi la Burundi then linafuata La Kenya,hata wapewe vifaa gani pale Ni bure kabisa.

TPDF Ina mizizi mirefu tena Sana tu.
 
Wanajeshi wa tangu 1980s ndio unasema wanajulikana na siri zao zinajulikana. Ukishajua Uganda wana Su-30 fighters na Mil Mi-24 attack helicopters ndio unashinda vita bure?

Rwanda sio wazembe ila hii sio point. Ni sawa na kusema Tanzania itaishinda Angola kwa kuwa tuliwahi toa support kwenye vita yao na makaburu
Point yako ni Nini?
 
Siwezi kubishana Sana khs Hilo,ingawa ukweli Ni kwamba hata Kampuni kubwa kubwa nyingi Rwanda Zina mkono wa jeshi kuanzia za kujenga mabarabara,za Maziwa na ma hotel etc.

BTW Juzi nimeona Rwanda wamenunua 12 drones model ya TB2 kutoka Turkey.Naona Ile vita ya Azerbaijan and Armenia drone za turkey zime prove ufanisi kwny kuleta ushindi kwa Azerbaijan na demand yake imeongezeka sokoni.
Hizo Bairaktar TB2 zinauzwa bei ndogo sijui kama Turkey hawatazipandia bei maradufu. Zina bei ndogo kiasi kwamba vichaa wa procurement kama Egypt wakinunua wanaweza chukua units hata 200 kwenye planned budget ileile. Na hazina masharti magumu kwa wanunuzi, unless supplier wa components kama Canada waweke vizuizi
 
Point yako ni Nini?
Rwanda haiifahamu Uganda kisa Kagame aliwahi kuwa CMI. Mambo mengi yamebadilika tangu miaka Kagame yuko Uganda. Hapo kuna seniors kibao wamestaafu na wamebadilishwa majukumu. Hata hivyo ukijua taarifa na huna namna ya kuzichakata hazikufai kitu. Rwanda itajua airbase za Uganda zilipo, ishambulie sasa kwa kutumia nini?
 
Rwanda haiifahamu Uganda kisa Kagame aliwahi kuwa CMI. Mambo mengi yamebadilika tangu miaka Kagame yuko Uganda. Hapo kuna seniors kibao wamestaafu na wamebadilishwa majukumu. Hata hivyo ukijua taarifa na huna namna ya kuzichakata hazikufai kitu. U
Rwanda itajua airbase za Ugandana zilipo, ishambulie sasa kwa kutumia nini?
Jua hivi Kampala ilikamatwa na 1st, 7th, 11th, 13th, 19th, and 35th battalions ambazo hizo zote zilikua chini ya wanyarwanda, Sasa hapo sijui location ya Kampala itakua imebadilika?BTW Kampala ilikamatwa na hao wkt M7 akiwa zake Sweden ilikokua familia yake.

Wanyarwanda kwny jeshi la Uganda wameondoka officially 1995,baada ya hapo Hali ikawa tete huko Entebbe, Jinja na Kampala ikabidi M7 awaombe wanajeshi wa Rwanda(RPA) warudi kumsaidia kutuliza Hali,ikabidi vikosi vitumwe chini ya Maj. Alex Kagame(usimchanganye na Paul Kagame) akiwa na kikosi cha artillery na anti-aircraft wakapigana na kuikamata Entebbe airport,eneo lenye rada la Nsamizi,Owen Falls Dam, Kule Lugazi kwny Viwanda vya sukari etc wakashikilia hayo maeneo kwa miezi 12 Hali ilipotulia wakayakabidhi kwa serikali ya Uganda.

Hata kikosi Cha ulinzi Cha M7 kulikua chini ya wanyarwanda wakina Captain Charles Muhire(OPTO) and Captain Charles Ngoga, the PPU Commander (OC).

Kifupi tu,nimetaka nikuonyeshe RDF Wanaijua Uganda nje ndani.
 
Hizo Bairaktar TB2 zinauzwa bei ndogo sijui kama Turkey hawatazipandia bei maradufu. Zina bei ndogo kiasi kwamba vichaa wa procurement kama Egypt wakinunua wanaweza chukua units hata 200 kwenye planned budget ileile. Na hazina masharti magumu kwa wanunuzi, unless supplier wa components kama Canada waweke vizuizi
So far Morocco wanazo 13,Ethiopia nao wameagiza kadhaa,Rwanda wameagiza 12 etc hizi nyingine Ni story za kanyabazongo.
 
Wale magaidi kule Msumbiji hawakutoka hadi Rwanda walipotia timu. Kutokana na hilo, kuna haja ya kuichamnua vizuri na kiundani hii mada kuliko suala la population na ukubwa au udogo wa geographical location
 
Ya Rwanda na Uganda, watajuana wenyewe. Ila ikitokea Rwanda wakajichanganya kwa TZ, wataenda kusimuliana huko Jehanam.

Tutapeleka vifaa kadhaa hapo Kigoma, then tunawaachia ndugu zetu "Waha" kazi ya kumnyoosha Kagame, huku mikoa yetu mingine ikiendelea na shughuli mbalimbali za ujenzi wa taifa!

Na tunavyozitamani pisi zao, wajichanganye tu!
'waha' wenyewe Red tabara inawatoa jasho kila Mara mabomu ya hapa na pale hayaishi Mara yanarushwa mtaani,kwny airport,kwny vituo vya mabus 😁😁 wako dhoofu bin Khali.
 
Vikitokea vita kati ya Rwanda na Uganda nani atashinda?

Wameanza kuparuana tena hawa wezi wa Madini ya Congo

Nahisi hawa mwisho wao utakuja kuwa kwenye hizi battle

Kati ya Uganda na Rwanda nani atashinda vita?

Nasema hivi kwasababu msitumie kigezo cha Rwanda ni ndogo! Rwanda sio ndogo kiidadi ina watu milioni 12!

Watu milioni 12 sio kidogo ni wengi sana


Na hata battle na Rwanda na tz lingetokea hata possiblity ya kutandikwa na Rwanda ingekuwepo tu nchi ikishakua na watu milioni 10 na kuendelea wakijiandaa vizuri wana uwezo wa kuzichapa na nchi yenye watu milion 120

Turudi kwenye mada Rwanda Vs Uganda nani atashinda vita?
Unaongea pumba.
Kwanza Rwanda hawezi kuchapana na baba yake M7.
Pili huku kwetu anajua shughuli iliyopo .
 
Back
Top Bottom