Haaa aaaahhh...kelele tuu mbona,waambie walianzishe tuu,anyway acheni kujidanganya na story zenu za kishabiki,war btn TZ and Rwanda will never happen period! Vita sio lelemama mjomba
Mkuu si story za kujidanganya, hapa JF kuna wengi tu hawampendi JK, but when it comes to Tanzania utashangaa. Huko Rwanda Kagame ni kama mungu. lakini hapa Tanzania JK ni rais tu, pamoja na hayo kumkejeli Rais wetu ni kutukejeli sisi.
Tanzania inajua vita si ushabiki, kwani tumewahi kupigana vita na si mara moja, wala mara mbili na si mara tatu. Tunajua vita si lele mama, karibu na kwenu huko kuna kaka zetu wamelala sehemu moja inaitwa Kaboya, kwa hiyo tunajua sana vita si lele mama, hasa baada ya vita kuvuruga uchumi wetu. But when it comes to us, we will not flatter.
Hivi ile energy and spirit btn Rwanda and TZ waliyoshirikiana kwenye multi billion projects like Rusumo Hydro power imeenda wapi?najua kulikuwa kuna mradi mkubwa wa reli pia Dar Isaka Kigali (what happened?),nafikiri its time kuangalia positives ambazo zinaweza kusaidia hizi nchi kuendelea mbele kuliko negativity zinazoendelea sasa,its not too late na ukiangalia vizuri sioni any serious conflict/problems btn these 2 countries
For some reasons Kigali imeamua kuwa Tanzania si rafiki, si jirani na si ndugu. My meaning of Kigali here is, PK and Co, na sio wanyarwanda au watutsi. Ili tuwe wakweli ni lazima tuseme wazi kuwa uhusiano kati ya Tanzania na Rwanda una mtikisiko, vitendo vya Kigali na kauli zao zinaonesha wazi kabisa kuwa Tanzania inatakiwa ku-act, otherwise PK and Co, wataendelea kusumbua Tanzania. How to do so, that is up for discussion.
Unajua kambare akishaota sharubu anajiona gege, lakini inawezekana kuwa sharubu sio ukubwa. Tanzania na watanzania hawajawahi kutegemea hata siku moja kuwa Rwanda itakuwa na tabia kama ya leo, ya dharau, kejeli, matusi na vitisho. Kwa mtu mwenye akili timamu hili jambo ni la kuliangalia kwa undani wake na kwa muktadha wa muda mrefu.
Hata siku moja Tanzania haijawahi kuamuliwa nani aje na nani asije, hata Marekani yenyewe haikuwahi kufanya hivyo. Leo kuwaalika watu wawili watatu kutoka Rwanda inakuwa tatizo, eti kisa Kigali anataka wasikaribishwe.....that is a pack of BS.
Ni tabia gani ya kusema adui yako ni adui yangu, ina maana wakati Habyarima alipokuwa madarakani tungesema watutsi hawatakiwa kuja Tanzania? Au kwa kuwa Kagame alikuwa mpinzani tungesema hatakiwi kuja Tanzania? au kwa kuwa RPF ilikuwa kundi la uasi lenye lengo la kupindua nchi tungesema halitakiwi Tanzania?
Unajua PK na bahati mbaya sana wengine ambao wanapenda kujiaidentify kuwa watutsi wanatoa lugha chafu sana, zinazwafanya baadhi ya watu hapa Tanzania waanze "kuwaelewa" machinjachinja. This is extremely dangerous, sick and bad. Kama kweli tuna nia ya kupambana na mchinjachinja, tusioneshe tabia zao.
When you exhibit exteremly ideologies, you are no different to an extremist. There is no where written that extreme genocidal ideologies and mentalities are restricted to Interhamwe. We now hear, see and smell extreme and genocidal (suicidal) tendencies in Kigali...in similar proportions to those we heard in 1992, 1993 and 1994 from Colonel Bagosora and Co. The worst part of all is that, the current Kigali tone is well playing into the interhamwe's core ideology, and have some believe that Bagosora's were right. This is very very dangerous.
Yule msh..nzi aliyesupervise genocide Rwanda alikuwa anasema haya haya ambayo baadhi ya watu humu (sorry to say...wanaojiita watutsi) wanafanya. Badala ya kuelemisha watu kuchangia kwa akili wanakuja na kejeli, matusi as if Tanzania ni kundi la wajinga, kama serikali ya Rwanda inavyofikiri. Ni hatari sana, ni bora watanzania tendelee kuwa neutral, kuhumiza wazungume kwa kuheshimiana, licha ya matauusi na kejeli zao. In the end kama likilipuka la kulipuka hatuwezi kufunga mipaka
Inasikitisha sana kuona baadhi ya member wenzetu kutoka Rwanda wanakamatika kirahisi sana kwenye mchezo wa interhamwe.