Kuna kitu gani cha ajabu hapa?.
Kwa mtu anayeifahamu historia ya Tanganyika/Tanzania katika kupigania haki za wanyonge wa kisiasa siyo barani Africa peke yake, bali duniani kote hawezi kupatwa na mshangao kusikia kuna kundi la watu au wakimbizi nchini wanaoishi au kupanga mikakati ya namna ya kuondokana na unyanyaswaji katika nchi yao.
Rais Paul Kagame akiwa ni mmoja wa wanufaika wa hisani ya Tanzania kabla ya kwenda Uganda na Rwanda na kuanza kubadili sura yake kiutawala na kuwa oppressor lazima atakuwa anafahamu vizuri mtazamo wa Tanzania katika kupigania haki za msingi za wanyanyaswaji na hasa cadres of the liberation movement.
Marehemu Mandela zaidi ya kumpa a warm welcome, ilibidi pia tumsindikize kwa kumpatia pasi ya kusafiria while also availing places to live and train Umkhonto we Sizwe. Hatukuwajibika kujibu kwa yoyote yule.
Rais Kagame na Mseveni wakati wanapata mafunzo ya kivita nchini, hatukuwajibika kujibu kwa yoyote yule.
Tanzania hatujawahi kuchaguliwa rafiki au adui na ndiyo maana hata tuliamua mwaka 1964 kuwa kwenye Non-Aligned countries. Hatuawajibiki kuiambia nchi nyingine nini tunakifanya na hasa kama kile tunachokifanya kitakuwa kwanza kwa maslahi yetu kama nchi na kikubwa kabisa, hakuna international or East African member countries arrest warrant kwa hawa candres wa mapambano nchini Rwanda.