Bongolander, nashukuru kwa majibu yako ijapokuwa sijaridhika na baadhi. Mimi sio msemaji wa Serikali ya rwanda ila ni raia ambae kwa namna moja au nyingine ni muathirika wa mauaji ya kimbari ya 1959,1972,1994. Suala ambalo sisi hatuwezi kulifumbia macho kamwe ni uchochezi wa aina yoyote dhidi ya kabila lolote ndani ya nchi yetu. Mtazamo wangu na wengi humu ni kwamba tukiwaachia watu wachache humu wakasambaza sumu ya chuki dhidi ya wanyarwanda mwishowe hata watu wenye uelewa mkubwa wa masuala ya kisiasa wataanza kuamini kuwa wayasemayo ni ya kweli. Sisi tuna mfano hai hapa wa ile redio RTLM ambayo ilichochea mauaji ya kimbari.
Mimi naamini sana kuwa katika forum hii kuna watu wengi ambao hawajui historia ya rwanda ila kwa kupitia magazeti na mitandao. Wengi hapa aidha walikuwa wadogo wakati wa mauji ya 1994 au hawajui chimbuko na nia ya wanyarwanda kutaka kurudi kwao.
Mimi ningewasihi wana JF kuwa katika threads zinazohusu Rwanda na siasa zetu, wajaribu kufanya utafiti kidogo na wasiamini sana hawa "war mongers" kama akina jMali,Rushasha,Mokala1989,Majeshi 1981 and Co. lakini wachambue kwa kina huu uchochezi wao.
Vile vile I believe kwamba raisi wenu ana lake jambo! Ni dhahiri kabisa kuwa hawa akina Twagiramungu na huyo kanali wa FDLR, walialikwa kuja hapa kama vile yule kamanda wa FDLR Nzeyimana alivyo alikwa hapo Tanzania. Huu ni mtiririko wa matukio mengi ya kujaribu kuwakumbatia maadui wetu na yote haya yamefanyika kwenye awamu ya raisi wenu Kikwete. Hili linatupa wasi wasi sana na wahenga wana msemo "where there is smoke, there is fire". Tahadhari kubwa ichukuliwe na viongozi wenu wenye uelewa mkubwa nchi zetu zisije zikajikuta ziko kwenye vita ambayo inasababishwa na watu wachache ambao nina uhakika moto ukianza kuwaka, ndio watakuwa wa kwanza kukimbilia uswisi walikoficha hizo hela zao za wizi.
Mkuu nakuelewa sana. Nafurahi unaeleza kwa utulivu na staha, hapa inakuwa rahisi sana kukuelewa. Naamini unajua kabisa kuwa watanzania, hata rais wetu hana hila wala hiyana na Rwanda. Lakini we must appreciate the fact that there is something going on, regardless of who started it.
At least umeeleza bigger picture ya suala zima, na sio kuliangalia kidogo tu kwa jicho la mvutano kati ya JK na PK. Nasisitza mara kwa mara kwenye jukwaa hili, kuwa Rais sio Mungu, wetu sisi anaondoka mwaka kesho, lakini uhusiano na Rwanda au ujirani na Rwanda hautaondoka. Kwa hiyo yanaoendelea sasa sidhani kama ina anyway yatakuwa balaa.
AMINI hata kama JK ataamua kuwasaidia FDLR, hakuna kitu kinachoitwa genocide, or even close to that, ataruhusu. JK can be accused of anything lakini sio hofu mliyonayo wanyarwanda.
NI kweli kuwa kwa sasa JF inatumiwa na baadhi ya watu ku-chochea mambo, sababu ni kuwa ukianza kuangalia kwa undani kuna watu wanaojifanya representatives wa watutsi (who are not), ambao badala ya kueleza hali halisi, kueleza sababu ya kuwa na wasiwasi na hatari iliyopo ya kucheza na FDLR, wanachofanya ni kutoa matusi,dharau na kejeli, badala ya kuwa wavumilivu na kuwafahamisha watu polepole sababu za wasiwasi wa kinachoendelea kati ya JK na PK, na at least to get us into the mind of Rwandese government or PK, wao wanatukana. This is neither helping nor educating.
Lakini ninachoweza kukuhakikishia ni kuwa Tanzania na Rwanda hazitapigana vita. Lakini kuna uwezekano mkubwa kukatokea mabadiliko kwenye uhusiano kati ya nchi zetu.
Ningependa usi-comment kuhusu hili. Kauli ya PK na kauli za Bibi Louise Mushikwabo kutokana na pendekezo la JK kuongea na FDLR zimetufikisha hapa.
Angalia Marekani wanaongea na Taleban, Angalia Israel wanaongea na Palestina, Renamo na wanaweza kukaa na Frelimo, FARC na serikali ya Colomboa wanaongea, this will be the trend in the future.