Rwanda - Tanzania Tensions Flare Again

Rwanda - Tanzania Tensions Flare Again

Status
Not open for further replies.
Ndugu yangu MimiBaba...naomba kuwekwa sawa kidogo...you have been repetedfly pointing out about Tutsis and the genocides they commited...naomba kueleweshwa hapa kidogo niko gizani...Kwa uelewa wangu Genocide ni mauaji yanaoyoandaliwa yenye malengo ya kuua na kutokomeza watu wenye kabila au chimbuko Fulani. Genociode ya Rwanda ya mwaka 1994 iliandaliwa na kufanywa na wahutu kwa ajili ya kutokomeza watusi. Watu zaidi ya milioni moja waliuliwa kwa kuwa tu ni aidha watusi au wahutu wenye mlenmgo wa kati. Sasa ndugu yangu unaposisistiza watusi walifanya genocide unamaanisha walijiua? Au waliuwa watusi wenzao? Unaposisitiza Kagame alifanya Genicide ina maana aliandaa genocide kumaliza watusi wenzie? Hapo umeniacha kidogo. Guys listen...Kila inapofikia karibia na maadhimisho ya kukumbuka mauaji ya kimbari waliyofanyiwa watusi na wahutu wachache wenye msimamo wa kati kama Waziri Agatha (RIP) huko Rwanda, maadhimisho ya KIMATAIFA ambayo hufanyika kila mwaka Aprili, mambo mawili hutokea...kwanza watusi waliofikwa na majanga hayo haswa waliokuwepo Rwanda kipindi hicho wanakuwa traumatized...wewe na mimi ambao tumetokea kupoteza mtu mmoja au wawili katika familia kwa ugonjwa ajali au chochote kisicho mauaji ikifika anniversary ya kifo huwa kumbukumbu zinarudi upya machungu unayapata kama ilikuwa jana, sembuse wengi Rwanda ambao unakuta alibaki peke yake katika familia au hata ukoo...huwa wana uchungu sana sana na wanakuwa very sensitive. Jambo la pili linalotokea huwa ni upande wa wauwaji/ndugu zao au wale wanao support hayo mauaji na wenye chuki dhidi ya watusi wanaodhani watusi hawastahili kuishi. Watu hawa roho zinawauma kuwa hawakufanikiwa kuwamaliza watusi wote! Niwie radhi ndugu yangu MimiBaba ila na wewe nakuweka kundi hili. Wao ikifika kipindi hiki huwa wanakuwa hiper! Wanaongea na kuzungumza kila wawezalo kuondoa international attention from remembering what exactly happened in 1994. Wengine hufanya hivi aidha kwa guilty consciousness au kutaka kufuta historia. Listen mkuu historia iko hivo...mliuwa watusi katika mauaji ya kimbari ya 1994 and this will haunt you for the rest of your lives. And this goes out to anyone who intentionally decides to end another person's life! It haunts you forever. Lucky are those who confess and seek for forgiveness...with readiness to be punished for the wrong done! Kwetu/kwenu nyinyi msiohusika...hapa namanisha wasio wanyarwanda...narudia...tusiingilie mambo ya ideology za watu bila kufanya research...research haimaanishi kusikiliza MimiBaba JMali au Mukamasimba kaongea nini ndipo na wewe useme yako...There is well documented research on Rwanda genocide...kesi hadi leo ziko mahakamani...Haya mengine ya nani kamtembelea nani yako way beyond us unless wewe ni mhusika wa moja kwa moja. Hatujasikia tamko la kagame au Rwanda kulaani hiyo safari na wala ikulu ya hapa sijasikia ikizungumzia mgeni huyo 'rasmi'. Basi mambo hayo tuwaachie baba na mama. Watu/media walipiga domo weeeee wakati wa tension zilizopita...mwisho ulikuwa nini? Mkulu si alituambia tuache ushabiki? Jeshi si lilitoa tamko lenyewe ndo linastahili kutoa updates za vita Kongo? Halafu hii vita ya mtandao ya wahutu na watusi tuwaachie wenyewe, very cautiously maana kama Nyerere alivoasa kuwa ubaguzi ni ugonjwa, tukumbuke unaambukiza! Haya jengeni taifa! Na nyie wenye vita yenu ya mdomo ya wahutu na watusi kwani huko kwenu mitandao hamna? Si naskia mmetandaziwa WIFI hadi vijijini? Si mkalumbane huko mtuache na yetu?

Nashukuru kwa hoja zako fasaha

1. Rudia tena kwenye tafiti zako jiridhishe kuwa PK na watutsi hawajawauwa watu kwa sababu si watutsi.

2. 6000000 inocent congolese waliouawa na Kagame pamoja na askari wa Uganda waliosingiziwa ni Intarahamwe na kuwa paraded na askari wa PK hiyo si genocide.

3. Wapinzani wa Kagame wengine wakiwa watutsi wenzie na pk hao ni mbwa si binadamu? Na inafanyika hivyo kwa kujihami na uhalifu tu.

4. Kwa nini maadhimisho yawe kwa ajili ya watutsi tu wahutu hawajauawa? Jibu ni rahisi kulingana na watutsi, wao wanaua na kulia wanauawa na kuhadaa dunia.

5. Mimi Mtanganyika toka central Tanganyika nachukia dhulma ya maisha atayofanyiwa mtu ye yote pahali po pote na mtu ye yote kwa sababu yo yote. Naamini kuna njia bora zamaelewano kuliko kutoa maisha. Hii imani yangu ni tofauti sana na viongozi akiwemo pk na jk. Nasisitiza dhukma ya maisha hata ya mtu mmoja kwangu inanisababishia maumivu kwa sababu naamini kuna mbadala wa kupata haki kutoka kwa mhalifu.

6. Narudia chokochoko za Rwanda dhidi ya Tanzania si za wanyarwanda wote bali ni za pk na genge lake la watutsi kumtishia rais wa tz hata kama ana madhaifu yake. Hilo halitavumiliwa litasemwa hadharani na ikibidi kuzipiga poa tu lakini tz iheshimiwe.

7. Umeelza vizuri kuwa hakuna tamko la serikali ya rwanda lakini aliyetishi kufanyia jk akiingia kwenye anga zake ni pk. Na alisema hadharani akaenda mbali kusema atakaesaliti rwanda atakiona(atauwawa) na niwakati alipouwawa mtutsi mwenzie SA. Ungetaka serikali itoe tamko lipi?

Mission ya MUKAMASIMBA iliyoleta malumbano haya kila upande ilikuwa na lengo. Lengo hili ni kujihami kwa uhalifu wa watutsi ambao ni zaidi ya genocide. Lakini mashambulizi kwa jk ambaye kwa sasa ni alama ya tz yalikusudia tumdharau rais wa nchi yetu HICHO HAKIWEZEKANI pamoja na tofauti zetu.

Mwisho watutsi waendelee tu na maadhisho ya genocide walioshiriki na kuhadaa dunia. OGOPA SANA WATU WANAVYOKUONA KIMATENDO NDIVYO SIVYO NA UNAYOYASEMA.

USHAURI

Kuanzisha hoja za chuki kama hii ya mukamasimba itajibiwa kwa chuki na nguvu ile ile tu hasa kutokana na kujaribu kumchafua mtu kama jk rais wetu. Halafu pamoja na credible research nazungumza kutoka na uzoefu na ushuhuda wa kujionea
 
1. Sijui kama nni kweli Rais wetu amemwalika Twagiramungu, na siamini kama kweli Rais wa Tanzania amemwalika
Twagiramungu. Kama kweli Twagiramungu amealikwa inawezekana ni kwa sababu za kisiasa, kutokana kijibu vitendo vya Paul Kagame.

2. Sababu inayowafanya watu wanaoipinga serikali ya Rwanda waje Tanzania kwa kufuatana (kama ni kweli), inaweza
kuwa ni kutokana na sababu za kiuslama na kutaka kujua kutoka kwa watu wanaoijua vizuri serikali ya PK maana ya vitisho alivyotoa PK, matusi waliyotoa wanasiasa waandamizi wa Rwanda kwa Tanzania, serikali
ya Tanzania na Rais wa Tanzania.
3. Ukiona jirani yako anaalika maadui wako, kweli katika hali ya kawaida kuna maana mbaya, au anatuma ujumbe fulani kwako. Lakini hawa jamaa hawaingii kisiri, walaingia wazi wazi tu kwa mtindo wa kuwafanya majasusi wa rwanda wajue kuwa wameingia.

Something to note though, it is justified from Rwandan vintage point to be worried which what Kigali authorities percieve to be a retaliation from JK, it is understandable if Kigali crys foul or even act.

However, you have to remember that when you are a leader, whenever you cause a diplomatic spat and for whatever reason, and whatever you says in public that may be subejct to open interpretation, you bear full responsibility of the outcome of your actions and words. PK as the President, Mushikwabo as FM know this very well.

In normal cases (not diplomatically) when someone insults you, vilify you, threatens to hit you, or even equates you to interhamwe, just for telling you a right thing (which for your own political reasons) which you think it is not, is it very understandable for you to react. But insulting back a person who insults you, does not make you any different from him, that is why i think my president and his entire government were very right not to engage themselves in verbal exchanges with authorities in Kigali. Paul Kagame can comfortably threaten Yoweri Museveni and can happily threaten Joseph Kabila, and how the two chose to react was their business. JK or Tanzania has her own way of reacting. When PK stood before militarymen in Kigali and vilify JK he definately knew what he was doing, and he bears full responsibility for what is happening.

Murutongore wewe unaongea kiswahili vizuri, naamini umeishi Tanzania, au ni mtanzania by affiliation, kwa hiyo naomba hili jambo uliangalie kwenye muktadha wake na kwa mentality ya mtanzania. Unajua kabisa kuwa JK hapa Tanzania sio Mungu, ndio maana anapiga hesabu vizuri sana kudeal na jambo hili bila kutukasirisha watanzania. JK hana beef hata kidogo na Rwanda, wanyarwanda, (watutsi au wahutu), na hakuna mtanzania mwenye chuki na wanyarwanda. Wanyarwanda ni ndugu wa watanzania kwa muda mrefu tena ni jirani zetu wema, long before Kagame hajazaliwa and that will be the case long after he leaves. Sioni kama ni jambo la busara kuanza kuangalia uhusiano kati ya wanyarwanda na watanzania kwa jicho la mvutano kati ya PK na JK, huku kwetu JK amebakiza siku 700 hivi za urais, tutakuwa na jina lingine, so we can not have an atomistic view of Rwanda-TZ relations, we have to look at at beyond PK na JK. Hata hivyo kutokana na ukaribu wa Rwanda na Tanzania, kinachotokea kati ya PK na JK, baadhi yetu tunakifananisha na kile kati ya JK na wanasiasa wengine wa Tanzania, au JK na Dr Slaa, bahati mbaya ni kuwa hili la JK na PK lina harufu ya diplomasia ndani yake.

Lakini vile vile ukumbuke kuwa Tanzania ni soveregin country, whoever comes to Tanzania is up to us to Tanzania to decide, not Kigali. Hyabyarimana tuliwahi kumwambia kuwa hawezi kutuambia watutsi wasije Tanzania, eti kwa kuwa wanapigana na serikali yake, we can tell PK the same hawezi kutuambia nani asije Tanzania kwa kuwa anataka kuiondoa serikali yake. Na kuja kwa hao watu, kama kweli wamekuja, hakuna maana kuwa Tanzania inaunga mkono vitendo vyao. PK anasumbuliwa na guilty conscious.

The problem is arrogance ya PK na baadhi ya watu Kigali, ya kutotaka kukubali kuwa hawa-kudeal vizuri na pendekezo la JK kuongea na FDLR, ndio inasumbua sasa. You can not believe how strong can respect be.

Bongolander, nashukuru kwa majibu yako ijapokuwa sijaridhika na baadhi. Mimi sio msemaji wa Serikali ya rwanda ila ni raia ambae kwa namna moja au nyingine ni muathirika wa mauaji ya kimbari ya 1959,1972,1994. Suala ambalo sisi hatuwezi kulifumbia macho kamwe ni uchochezi wa aina yoyote dhidi ya kabila lolote ndani ya nchi yetu. Mtazamo wangu na wengi humu ni kwamba tukiwaachia watu wachache humu wakasambaza sumu ya chuki dhidi ya wanyarwanda mwishowe hata watu wenye uelewa mkubwa wa masuala ya kisiasa wataanza kuamini kuwa wayasemayo ni ya kweli. Sisi tuna mfano hai hapa wa ile redio RTLM ambayo ilichochea mauaji ya kimbari.

Mimi naamini sana kuwa katika forum hii kuna watu wengi ambao hawajui historia ya rwanda ila kwa kupitia magazeti na mitandao. Wengi hapa aidha walikuwa wadogo wakati wa mauji ya 1994 au hawajui chimbuko na nia ya wanyarwanda kutaka kurudi kwao.

Mimi ningewasihi wana JF kuwa katika threads zinazohusu Rwanda na siasa zetu, wajaribu kufanya utafiti kidogo na wasiamini sana hawa "war mongers" kama akina jMali,Rushasha,Mokala1989,Majeshi 1981 and Co. lakini wachambue kwa kina huu uchochezi wao.

Vile vile I believe kwamba raisi wenu ana lake jambo! Ni dhahiri kabisa kuwa hawa akina Twagiramungu na huyo kanali wa FDLR, walialikwa kuja hapa kama vile yule kamanda wa FDLR Nzeyimana alivyo alikwa hapo Tanzania. Huu ni mtiririko wa matukio mengi ya kujaribu kuwakumbatia maadui wetu na yote haya yamefanyika kwenye awamu ya raisi wenu Kikwete. Hili linatupa wasi wasi sana na wahenga wana msemo "where there is smoke, there is fire". Tahadhari kubwa ichukuliwe na viongozi wenu wenye uelewa mkubwa nchi zetu zisije zikajikuta ziko kwenye vita ambayo inasababishwa na watu wachache ambao nina uhakika moto ukianza kuwaka, ndio watakuwa wa kwanza kukimbilia uswisi walikoficha hizo hela zao za wizi.
 
Vile vile I believe kwamba raisi wenu ana lake jambo! Ni dhahiri kabisa kuwa hawa akina Twagiramungu na huyo kanali wa FDLR, walialikwa kuja hapa kama vile yule kamanda wa FDLR Nzeyimana alivyo alikwa hapo Tanzania. Huu ni mtiririko wa matukio mengi ya kujaribu kuwakumbatia maadui wetu na yote haya yamefanyika kwenye awamu ya raisi wenu Kikwete. Hili linatupa wasi wasi sana na wahenga wana msemo "where there is smoke, there is fire". Tahadhari kubwa ichukuliwe na viongozi wenu wenye uelewa mkubwa nchi zetu zisije zikajikuta ziko kwenye vita ambayo inasababishwa na watu wachache ambao nina uhakika moto ukianza kuwaka, ndio watakuwa wa kwanza kukimbilia uswisi walikoficha hizo hela zao za wizi.

Hapa ndipo mnapofanya makosa. Tanzania haiwezi kuwa dictated na matakwa yenu never ever. Mbona kuna waliopewa hifadhi Uganda SA na rwanda ikafanikiwa kuwaua. Mbona baadhi yenu wengi sana mlikuwa wakimbizi tz na mlipanga vita yenu tz? Huo uwezo wenu wa kuwaua maadui zenu ndiyo inafanya maadui zenu wajiimarishe kuwaua.

Unapo "personalise" rais wa awamu hii jk ndiye anakutana na madui zenu unapotoka sana. Hamuwezi kumuamulia rais wetu akutane au asikutane na nini. Kuna kitu kinaitwa BUSARA kingine kinaitwa HEKIMA. Rwanda kwa uzoefu wangu hamna hata kimoja kati ya hivyo na ndivyo mlivyo binafsi na hususan watutsi.

EBU JIFUNZENI KUHESHIMU WENGINE
 
Nashukuru kwa hoja zako fasaha

1. Rudia tena kwenye tafiti zako jiridhishe kuwa PK na watutsi hawajawauwa watu kwa sababu si watutsi.

2. 6000000 innocent congolese waliouawa na Kagame pamoja na askari wa Uganda waliosingiziwa ni Intarahamwe na kuwa paraded na askari wa PK hiyo si genocide.

3. Wapinzani wa Kagame wengine wakiwa watutsi wenzie na pk hao ni mbwa si binadamu? Na inafanyika hivyo kwa kujihami na uhalifu tu.

4. Kwa nini maadhimisho yawe kwa ajili ya watutsi tu wahutu hawajauawa? Jibu ni rahisi kulingana na watutsi, wao wanaua na kulia wanauawa na kuhadaa dunia.

5. Mimi Mtanganyika toka central Tanganyika nachukia dhulma ya maisha atayofanyiwa mtu ye yote pahali po pote na mtu ye yote kwa sababu yo yote. Naamini kuna njia bora zamaelewano kuliko kutoa maisha. Hii imani yangu ni tofauti sana na viongozi akiwemo pk. Nasisitiza dhulma ya maisha hata ya mtu mmoja kwangu inanisababishia maumivu kwa sababu naamini kuna mbadala wa kupata haki kutoka hata kwa mhalifu.

6. Narudia chokochoko za Rwanda dhidi ya Tanzania si za wanyarwanda wote bali ni za pk na genge lake la watutsi kumtishia rais wa tz hata kama ana madhaifu yake. Hilo halitavumiliwa litasemwa hadharani na ikibidi kuzipiga poa tu lakini tz iheshimiwe.

7. Umeelza vizuri kuwa hakuna tamko la serikali ya rwanda lakini aliyetishia kumfanyia jk akiingia kwenye anga zake ni pk. Na alisema hadharani akaenda mbali kusema atakaesaliti rwanda atakiona(atauwawa) na niwakati alipouwawa mtutsi mwenzie SA. Ungetaka serikali itoe tamko lipi?

Mission ya MUKAMASIMBA iliyoleta malumbano haya kila upande ilikuwa na lengo. Lengo hili ni kujihami kwa uhalifu wa watutsi ambao ni zaidi ya genocide. Lakini mashambulizi kwa jk ambaye kwa sasa ni alama ya tz yalikusudia tumdharau rais wa nchi yetu HICHO HAKIWEZEKANI pamoja na tofauti zetu.

Mwisho watutsi waendelee tu na maadhisho ya genocide walioshiriki na kuhadaa dunia. OGOPA SANA WATU WANAVYOKUONA KIMATENDO NDIVYO SIVYO NA UNAYOYASEMA.

USHAURI

Kuanzisha hoja za chuki kama hii ya mukamasimba itajibiwa kwa chuki na nguvu ile ile tu hasa kutokana na kujaribu kumchafua mtu kama jk rais wetu. Halafu pamoja na credible research nazungumza kutoka na uzoefu na ushuhuda wa kujionea

Blah blah blah blah blah... peleka huu ujinga kwa mabwege wenzako wenye akili za darasa la pili kama wewe ndio watakuamini sio hapa.
 
Ndugu yangu MimiBaba...Usijali hata kidogo wewe sijakuweka kwenye kundi la wanaozungumza bila research...kama ulivojisemea mwenyewe nilikisia sahihi kwamba wewe unazungumza kwa kujionea/kushiriki hiyo genocide whatever the case is. Hapo nilikuwa nawazungumzia wadau ambao wanajikuta katika ushabiki wasioujua. Wala nia yangu si kukunyooshea kidole kwa kuwa haisaidii kitu hapa. Kwa mtazamo wangu nakuweka katika kundi la wanaotaka sympathy ya waTZ wasioijua historia ili kupata back up ya kufuta ukweli wa genocide. Ndio maana kila comment yako una highlight wamuache JK blablabla...JK hahitaji utetezi wako for ur information. Mambo yake na majirani zake yana intelligency na diplomasia ya kushughjulikia hategemei utetezi wako. Ila kwa kauzoefu kako hako ambako umekiri kushuhudia ebu tupe kwa kifupi genocide ya 1994 ilikuwaje? Je ni sahihi kusema ilifanywa na kagame au ilisababishwa na watusi? Mbona hujanijibu? Ninachojua ilifanywa na wahutu dhidi ya watusi au sio? Hilo kwa upeo na ufahamu wangu halina compromise. Isipokuwa wahutu wana justify kuwa walifanya hivo kwa kuwa watusi walimuua Rais Habyarimana. What amazes me ni kwamba ilikuwaje just the same day Habyarimana alikufa kila mhutu akawa tayari ana panga na shoka awe wa mjini awe wa kijijini na mauaji yakafanyika systematically kila pembe ya nchi...hapo bado sijaelewa. Tunazungumzia genocide hapa...kama kuna ushahidi wa kwamba Wahutu walifanyiwa genocide naona kidogo umepwaya maana 20 years after bado haijakubalika na kutambulika hivyo! Kwa hiyo kwa mtazamo wangu you can't change history bahati mbaya...you can only work on it to establish a better future...you can always learn from your mistakes for a better tomorrow. Mlifanya genocide...yes RPF iliisimamisha na unapopigana na muuaji obviously sio amicable embrace...muuaji huyo asipojihami na kukimbia unaweza ukamjeruhi au hata akafa na kuwafanya wauaji wengine wakimbie kwa kuogopa mkombozi. Kuhusu mauaji yanayosadikika kufanywa na serikali ya Rwanda...Mimi na wewe si wasemaji wa Rwanda na wala hatuna huo ushahidi...Hayo ya Kongo unless ukiniletea statistics verified kuwa wakongo wangapi waliuliwa na KAGAME na watusi wangapi waliuliwa na nani sijui still nitakuweka katika kapu la propaganda. Kama ambavyo hatuwezi kuthibitisha JK kum host Twagiranini sijui....hata kama kafika aendako akathibitisha still tunaipa serikali yetu benefit of doubt si ndio? Haya tuwaachie Baba na Mama watajuana wenyewe...:A S 103:
 
Huu ugomvi lini utafika mwisho??? Wote ni Raia wa Rwanda kaeni kitako mzungumze. Hilo ndilo suluhisho litakalo kuwa na faida kwa watoto wenu baadae. Matusi na kashfa mnazozuliana si msaada kwenu. Msamaha utawavusha pande zote.

Ugomvi upi? Sisi hatuna ugomvi na mtu. Tunachosema, hawa FDLR waweke silaha chini warudi rwanda.
 
Jmali hivi hlo gazeti New Times nani analimiliki,maana nijue ili nione nafaa au sifai kushiriki kwenye mjadala huu.

Linamilikiwa na chama tawala cha RPF kupitia kampuni yake ya crystal ventures (which is also the biggest company in Rwanda, lakini hawaishi kutuambia Rwanda inaongoza kwa uwekezaji, wakati makampuni yote manene ni ya chama tawala).
If you go to the 'about us' page right now through here(new times-about) utakuta eti 'page being updated', wakati website yao imeanza toka mwaka 2003! yani miaka yoote hiyo kumi na moja bado wana-update only this specific page!
 
DR.SLAA AMKOSOA RAIS KIKWETE KUHUSU RWANDA

Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbroad Slaa, amemkosoa Rais Jakaya Kikwete, kuhusu kauli ya kumshauri Rais wa Rwanda, Paul Kagame, kuzungumza na waasi wa serikali yake.

Dk. Slaa amesema haoni busara kwa Rais Kikwete kuwaambia viongozi wa Rwanda, akiwamo Rais Kagame, kuzungumza na wafuasi wa chama cha FDRL walioko Congo kwa vile wanatambulika kama wauaji.

Alisema hayo wakati akizungumza katika kongamano la vijana wa Chadema (BAVICHA) la uchumi na ajira lililofanyika jana jijini Dar es Salaam.

Alimshangaa kuwataka kuzungumza na watu ambao Kagame anawaita wauaji wenye asili ya kundi la jeshi la Nterahamwe, lililokuwa linaangamiza Watutsi.

“Rais Kikwete hapa nyumbani hawezi kuzungumza na wapinzani, hajachukua hatua dhidi wauaji wa mwandishi Daudi Mwangosi, alishauriwa amuwajibishe Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa Michael Kamuhanda, amempandisha cheo,” alisema.

Alisema Rais alitakiwa kuwaambia waje awapatanishe lakini si kuwaambia wazungumze na watu anaowatuhumu kuua Watutsi.

Kumezuka sitofahamu ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Rwanda, baada ya Rais Kikwete kutoa ushauri huo wakati wa mkutano wa Umoja wa Afrika (AU) uliofanyika Addis Ababa, Ethiopia hivi karibuni.

Ushauri huo ulionekana kumchukiza Rais Kagame, anayedaiwa kuhutubia mikutano kadhaa nchini kwake na kutumia lugha ya matusi, kejeli na dhihaka dhidi ya Rais Kikwete na Tanzania.

[h=1]Dr. Slaa: Tukishika Dola tutaruhusu utengenezaji wa pombe ya gongo kisheria[/h]
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimetoa mpya baada ya kueleza kuwa kitakapofanikiwa kushika dola kitaruhu Shirika la Viwanda Vidogo Vidogo (SIDO) kutengeneza mitambo ya kutengenezea pombe aina ya gongo.


 
Linamilikiwa na chama tawala cha RPF kupitia kampuni yake ya crystal ventures (which is also the biggest company in Rwanda, lakini hawaishi kutuambia Rwanda inaongoza kwa uwekezaji, wakati makampuni yote manene ni ya chama tawala).
If you go to the 'about us' page right now through here(new times-about) utakuta eti 'page being updated', wakati website yao imeanza toka mwaka 2003! yani miaka yoote hiyo kumi na moja bado wana-update only this specific page!

Gazeti la Uhuru linamilikiwa na nani? you dimwit
 
Blah blah blah blah blah... peleka huu ujinga kwa mabwege wenzako wenye akili za darasa la pili kama wewe ndio watakuamini sio hapa.

Although I don't agree with what you are saying but I will defend to death your right of saying it - this is human right, the right of freedom of speech . This is what you lack my friends Rwandese . Ndo maana unajibu kwa emotions , hutaki hoja za watu wengine yaani wewe bozoo kweli!!!! Haya ya kutokutaka mawazo kinzani peleka huko huko Rwanda. This is JF hosted in the cyberspace. Free space where any one is free to write and publish anything. It is a gate without gate keeper.
 
:


Ungejibu swali kwani Kagame kamfanya nini Kikwete,
Watu kama nyiej Jmali FDRL sympathisers ndio mnakuza mgogoro huu, ushahidi ni nyie kubadili speech ya Kagame nakuongeza neno i will hit you! kitu ambacho Kagame hakusema, wengine nao wanadandia tu bila kujua kuwa kuna watu kama Jmali ambao kazi yao ni propaganda kwenye mitandao ya jamii, hiyo ndiyo kazi yao, hata kwenye mikutano ya FDRL hili wanalipa kipaumbele, kutumia mitandao ya kijamii kwenye nchi jirani ya Rwanda, ili sura yao ionekane kama wao ndio waonewa(FDRL) yani Genocide isahaulike wao ndio wawe attention:
Chini nimeweka speech ya Kagame ilivyo, post yangu iliyopita nilikuomba atleast uweke hiyo youtube link Kagame anaposema i will hit you:
Sasa nyie mnaongeza hiyo statement kwa sababu gani, kama hamna faida kwenye mgogoro huu??
kwa yule ambaye hakusikia hii speech, nenda youtube uandike Kagame remarks on Kikwete statement utapata statement ya ukweli:
Kutaka kuhalalisha msimamo wenu kila mara uhusiano wa Rwanda na Tanzania ukiongelewa hapohapo mnaleta sijui M23,RDC eeh!hapa inaongelewa Rwanda na Tanzania, kumbuka vifaa vya kijeshi vya Tanzania vilivyotumika kuipiga M23 vilipita Kigali Airport:
Kumbuka Ntaganda mliyekuwa mnasema anasaidiwa na Rwanda alijisalimisha kwenye ubalozi wa Marekani Kigali, sasa kwanini Rwanda haikumficha na tayali alikuwa nchini:
Nani kamkamata Nkunda? kwani unadhani alikuwa ameshindwa kukamata nchi:
Unaushahidi wowote wa askali hata mmoja wa Rwanda(RDF) aliyekamatwa mateka au kuuawa vitani kwenye hivi vita vya M23?:
Ukweli nikwamba rwanda haukipigana upande wa M23 ingekuwa hivyo mambo yangekuwa mengine sasa hivi:
Wa nyaRwanda wengi, nanina Imani pia Wa Tanzania wengi hawapendi vita tunataka amani, sijui nikwa faida gani Kikwete anaendekeza chokochoko hii dhidi ya Rwanda;
tayari wafanyabiashara wa Tanzania washakutana na matunda ya huu uongozi wa Kikwete(Road toll imeongezwa) kumbuka rwanda ilikuwa inatoza kodi ya chini kabisa kwa maroli kutoka Tanzania lakini sasa yote yamebadilika:
Sisi ni wapenda amani, na ni busara kuwa na uhusiano na nchi badala ya vikundi vya upinzani vyenye silaha:

Hivi hii statement ya hapa chini inatosha kumfanya mkuu wa nchi, kuanza kujadiliana na vikundi vya kigaidi ili kuipindua serikali ya nchi jirani, hivi unadhani hata akifanikiwa (though its totally impossible) Tanzania haitakutana na madhala yoyote?


Kagame statement
I had some had things to say about Rwanda having to negotiate, to talk to the murderers of our people, people talk FDRL as casually as that and they know they are talking about the mass graves of our people and that the ones who did it we owe them something:
First of all i did`t talk about it because of the contempt i had for it:
Second i thought it was utter nonsense
Third i thought it was ignorance
Fourth, if it is an ideological problem which i think it may largely be, then it better stay with those who have it
But we will have another day to deal with it, We Rwandans knows who we are in our way, we are doing our best to achieve what we want to achieve and this is not a myth it is a reality:

Kama kawaida kwa unafiki tu hamjambo! Wewe hiyo unayosema ni nyingine kabisa. Unayoongelea wewe ni speech aliyotoa katika graduation ya chuo cha jeshi Nyakimana.
Maneno ya 'i will hit you' yako kwenye speech aliyotoa tarehe 30 juni, 2013 katika youth konnect summit iliyoandaliwa na mkewe. Na alikuwa anaongea na vijana. Kitu cha wazi kinachoonekana ni kuwa uko kazini. You can't seriouly say hii issue wewe kwako ni mpya au ni propaganda. Hii ni common tactic kwenu mapropagandist. Mnaposhindwa mjadala mnaaza diversionary tactics kwa kuanza kuuliza vitu ambavyo ni facts na vingine common-sense. Anyway ili nisije nikajishusha kufikia hadhi yako kwa vile wewe 'muungwana' fanya mojawapo kati ya haya vinginevyo sepa tu, tumeshakushtukia, urudi na ID nyingine!:

1. Kataa au kubali kuwa kulikuwa na hiyo event ya youth konnect iliyoandaliwa na Mrs kagame tarehe 30, juni 2013.
2. Pili, kama unakataa hakusema maneno nitayakoandika hapa chini, basi lete wewe ya kwako, vinginevyo tukubaliane kuwa kasema.

NANUKUU:

Those people [Tanzanian President Jakaya Kikwete] you just heard siding with Interahamwe and FDLR and urging negotiations… negotiations? Me, I do not even discuss this topic, because I will just wait for you [Tanzanian President Jakaya Kikwete] at the right place and I will hit you! He[Tanzanian President Jakaya Kikwete] did not deserve my answer. I did not waste my time answering him…It is well known. There is a line you cannot cross, there is a line, a line that you should never cross. It is impossible…”


kazi ni kwako....

cc: JokaKuu, NasDaz, Mimibaba
 
Last edited by a moderator:
Kama kawaida kwa unafiki tu hamjambo! Wewe hiyo unayosema ni nyingine kabisa. Unayoongelea wewe ni speech aliyotoa katika graduation ya chuo cha jeshi Nyakimana.
Maneno ya 'i will hit you' yako kwenye speech aliyotoa tarehe 30 juni, 2013 katika youth konnect summit iliyoandaliwa na mkewe. Na alikuwa anaongea na vijana. Kitu cha wazi kinachoonekana ni kuwa uko kazini. You can't seriouly say hii issue wewe kwako ni mpya au ni propaganda. Hii ni common tactic kwenu mapropagandist. Mnaposhindwa mjadala mnaaza diversionary tactics kwa kuanza kuuliza vitu ambavyo ni facts na vingine common-sense. Anyway ili nisije nikajishusha kufikia hadhi yako kwa vile wewe 'muungwana' fanya mojawapo kati ya haya vinginevyo sepa tu, tumeshakushtukia, urudi na ID nyingine!:

1. Kataa au kubali kuwa kulikuwa na hiyo event ya youth konnect iliyoandaliwa na Mrs kagame tarehe 30, juni 2013.
2. Pili, kama unakataa hakusema maneno nitayakoandika hapa chini, basi lete wewe ya kwako, vinginevyo tukubaliane kuwa kasema.

NANUKUU:

Those people [Tanzanian President Jakaya Kikwete] you just heard siding with Interahamwe and FDLR and urging negotiations… negotiations? Me, I do not even discuss this topic, because I will just wait for you [Tanzanian President Jakaya Kikwete] at the right place and I will hit you! He[Tanzanian President Jakaya Kikwete] did not deserve my answer. I did not waste my time answering him…It is well known. There is a line you cannot cross, there is a line, a line that you should never cross. It is impossible…”


kazi ni kwako....

cc: JokaKuu, NasDaz, Mimibaba
Aise umeoa mkuu kama hujaoa nina dada yangu mzuri sana ili mzae nipate wajomba wenye akili kama wewe teh teh ha ha !!!!!!!!!!!!!
 
Last edited by a moderator:
Bongolander, nashukuru kwa majibu yako ijapokuwa sijaridhika na baadhi. Mimi sio msemaji wa Serikali ya rwanda ila ni raia ambae kwa namna moja au nyingine ni muathirika wa mauaji ya kimbari ya 1959,1972,1994. Suala ambalo sisi hatuwezi kulifumbia macho kamwe ni uchochezi wa aina yoyote dhidi ya kabila lolote ndani ya nchi yetu. Mtazamo wangu na wengi humu ni kwamba tukiwaachia watu wachache humu wakasambaza sumu ya chuki dhidi ya wanyarwanda mwishowe hata watu wenye uelewa mkubwa wa masuala ya kisiasa wataanza kuamini kuwa wayasemayo ni ya kweli. Sisi tuna mfano hai hapa wa ile redio RTLM ambayo ilichochea mauaji ya kimbari.

Mimi naamini sana kuwa katika forum hii kuna watu wengi ambao hawajui historia ya rwanda ila kwa kupitia magazeti na mitandao. Wengi hapa aidha walikuwa wadogo wakati wa mauji ya 1994 au hawajui chimbuko na nia ya wanyarwanda kutaka kurudi kwao.

Mimi ningewasihi wana JF kuwa katika threads zinazohusu Rwanda na siasa zetu, wajaribu kufanya utafiti kidogo na wasiamini sana hawa "war mongers" kama akina jMali,Rushasha,Mokala1989,Majeshi 1981 and Co. lakini wachambue kwa kina huu uchochezi wao.

Vile vile I believe kwamba raisi wenu ana lake jambo! Ni dhahiri kabisa kuwa hawa akina Twagiramungu na huyo kanali wa FDLR, walialikwa kuja hapa kama vile yule kamanda wa FDLR Nzeyimana alivyo alikwa hapo Tanzania. Huu ni mtiririko wa matukio mengi ya kujaribu kuwakumbatia maadui wetu na yote haya yamefanyika kwenye awamu ya raisi wenu Kikwete. Hili linatupa wasi wasi sana na wahenga wana msemo "where there is smoke, there is fire". Tahadhari kubwa ichukuliwe na viongozi wenu wenye uelewa mkubwa nchi zetu zisije zikajikuta ziko kwenye vita ambayo inasababishwa na watu wachache ambao nina uhakika moto ukianza kuwaka, ndio watakuwa wa kwanza kukimbilia uswisi walikoficha hizo hela zao za wizi.

Hao unaowaita "maadui zetu", walikuwa ndiyo serikali ya Rwanda 1994. na wenyewe pia walikasirika tulipo "wakumbatia" maadui zao kina kagame vile vile, na kushauri mazungumzo wakati kagame kishafanya mauaji kwa miaka 4! (seuze siku 100).

Hivyo elewa kwamba we will be the last people kuwatenga FDLR ambao by the way wanaongelea amani. Hivi do you think kwamba Tanzania inahitaji FDLR ili kuwapiga nyinyi? Do you think kama kuna any ill motivekwa upande wetu, Twagiramungu angesema hadharani kuwa kaja Tanzania, au hata wewe (na mimi) tungejua kuwa wamekuja? Sababu ya public kujua juu ya ujio huu ni kwa sababu hakuna lengo baya lolote ndio maana hakuna mtu anajificha. Lakini you people act as if hii habari imejulikana kiitelijensia hivi or something.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom