Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 17,804
- 24,437
Hizi ndo akili zetu...sijui umetumia kigezo gani kusema Putin anatumia akili ya zamani sana,in short tutapiga kelele humu ila hatutajua chanzo chake hasa hadi wamefika/amefikia hapo......We are African lets solve our problem 1st before looking outside our boundary ambayo hata tungeachiwa changamoto zao hata robo tu tutakesha miaka mia mbili hatumalizi hata robo ya tatizo.
Kama una akili kuliko huyo Putin tusaidie kuondoa matatizo ya kiuchumi hapa Tanzania au jambo kubwa kuliko hilo dogo la huko Russia la msongamano wa magari Dar-Es-Salaam.
Hebu tulia ujadili hoja iliyoko mbele yetu, siyo kukurupuka na ku-question akili zangu. Kama unataka nitatua matatizo ya Dar es Salaama, niko tayari kufanya hivyo iwapo utanipa madaraka hayo. Siwezi kutatua matatizo ya Dar wakati umewapa madaraka watu wasiokuwa na akili.
Kama wewe unadhani kuwa tendo la Putin ni sawa basi tuambia uhalali wake ni nini. Huwezi kuchukua jeshi lako na kuliingiza nchi ya jirani yako wakati hamjagombana. Matatizo ya Ukraine yalikuwa yao ya ndani, yeye kuingilia ni kosa ambalo litakuwa ni hasara kwa urusi. Kuvamia nchi ya jirani kwa sababu tu rafiki yake kaondolewa madarakani na wabunge wa nchi hiyo kwa mujibu wa katiba ya nchi hiyo ni kusa sana. Ni akili ya kizamani kudhani kuwa Ukraine bado ni sehemu ya USSR wakati ni wao Russia wakiongozwa na Yelstin ndio waliovunja muungano ule na kuacha kila nchi ijiendeshe yenyewe.
Amejenga mazinigira ambayo nchi nyingine zote zilizokuwa sehemu ya USSR kuanza kujijenga kijeshi kwa kuogopa kuvamiwa na urusi; waliwahi kuivamia Georgia, na sasa wamefanya hivyo kwa Ukraine kwa hiyo nchi nyingine zilizobaki zinajua kuwa wana bully jiranni yao. Kumbuka kuwa Ukraine ndiyo iliyokuwa na silaha nyingi sana za Nyuklia kuliko republic nyinginje yoyote huko USSR, wakaombwa sana waziharibu na hapo mwaka 1994 wakawekeana mkataba wa kuziharibu mradi tu usalama wao usitishiwe na urusi. Kwa vile Putin amekiuka mkataba huo, basi Ukraine inaweza kuanza tena kujilimbikiza silaha hzio, jambo ambalo linakuwa ni hatari siyo tu kwa usalama wa dunia bali kwa Urusi pia.
Nchi nyingi zilizokuwa za USSR na zile za Warsaw pact zinaanza kuhamia NATO haraka haraka kwa sababu ya matendo ya Putin; hilo halitakuwa jambo zuri kwa Urusi.