ACHA UONGO wewe, utakuwa kijana wa siku za hivi karibuni. Umelishwa Propaganda hadi hujielewi.
Hadi leo, bunduki pekee iliyouwa watu wengi duniani ni AK-47 - MRUSI. Hata NATO walii-copy.
Submarine ya kwanza inayotumia Atomic Energy ilikuwa ya USA, ila kwa leo hii mwenye dude kubwa ni Russia. Inavyokuja kwenye Missiles, Mrusi yupo mbali sana.
Ningelikubaliana na wewe ungelisema, USA wanashinda kwenye silaha nyingi ila siyo zote.
Wakati USA ana Bomu liitwalo "Mother of all Bombs -GBU-43/B Massive Ordnance Air Blast", Mrusi yeye analo la kwake linaitwa "Father of all Bombs - Aviation Thermobaric Bomb of Increased Power ". Vipi kuhusu TSAR Bomb?
Ila ukweli ni huu kwamba, RUSSIA na USA hawawezi kupigana. Ni MJINGA tu anaweza kufikiri hawa jamaa watapigana. Kwa miaka mingi wamekuwa wakigawana Pande mbili na kuwapa silaha ili wajaribie waone zinavyofanya kazi. Vita baridi ya dunia, hawa jamaa walikuwa wakishirikiana kwa nyanja nyingi sana. Imeshasemwa wazi kuwa hata APOLLO wakati inakwenda mwezini, Warusi walisaidia kuitengeneza.
Mrusi aliweka Space Station yake peke yake angani (MIR) na USA akashindwa. Walipotaka kuweka ya Kimataifa, ilibidi wamuombe Mrusi awasaidie kwa kuwa ndiyo mtu pekee alikuwa na uzoefu huo. Hata kukitokea Vita kati ya USA vs sijui nani, Mrusi atashika upande wa USA, na hivyo hivyo kwa Russia. Ni Mabest sana hawa jamaa na msifuate wanavyozuga kwenye TV. Hata kabla ya uchaguzi, Microphone ilimnasa Obama akimwambia Kigogo wa Russia "Mwambie President, uchaguzi ukiisha, nitakuja tutete..."