Mgirik
JF-Expert Member
- Apr 27, 2013
- 13,260
- 13,368
Your stupid.
nakusamehe ngombe ww
Your stupid.
Habari zenu wakuu.
Kwa wenye uelewa zaidi juu ya hili tushirikishane namna tunavyo/tulivyo kabiliana nalo.
Kwa mwana chuo yeyote(japo kila sehemu lipo), hatakuwa mgeni na hili tatizo hasa kwa ladies.
Nikisema tamaa nitakosea kwasababu kila mtu anatamaa ila tunatofautiana mipaka, vyuoni dada zetu(wanaojiheshimu) wanapata shida kutokana na ma lecturers(SI WOTE) kupenda kuomba rushwa ya ngono.
My sister ni victim na amejikuta anapewa SAP 4 kisa aligoma kutoa hii rushwa yenye majuto sana.
Now ndio anasoma Bachelor accounting lakini ilibidi awe na degree yake kitambo.
Rafiki zaku wana kazi na familia tayari. Nini kifanyike ndugu zangu?
Humu Jamiiforums wapo wanao lielewa vizuri hili sasa tushirikishane mawazo maana ukiacha swala la tabia binafsi ya mtu, dada zetu wanaojiheshimu wanapata tabu sana toka kwa hawa watu wasioridhika (hata wanawake walioolewa wanaombwa hii kitu.
Leo dada yangu kesho huwezi jua nani next.
Tusemezane wakuu
Ni hilo limenigusa kwa leo, UKIZINGATIA HILI LINA ATHIRI MAHUSIANO YA WATU.
ndo maana kuna mtu kauliza ni chuo gani. Kuna chuo nakijua dean kapigwa chini hivi karibuni baada ya mwanafunzi kuripoti tabia hiyo na alikuwa na uthibitisho. Pia kama chuo si cha "kata" rufaa hutendewa haki kabisa kwa mitihani husika kupelekwa kwa msahihshaji mwingine. Halafu mtu anakuwaje na supp 4 zinazotokana na kukataa kuzini na mhadhiri wake? Ni chuo gani mhadhiri anaweza kufundisha kozi zaidi ya moja na zikizidi sana 2 kwa darasa moja? Au katongozwa na kuadhibiwa kwa supp na mhadhiri zaidi ya mmoja? Na supp 4 kwa chuo cha kueleweka huyo mwanafunzi asingekuwa chuoni bali mtaani maana hawezi kuwa na wastani unaomruhusu kuingia mwaka mwingine. Kama ana hakika anafeli kwa sababu hiyo na mamlaka ya chuo husika imeshindwa kumpa haki yake wakati ushahidi anao basi aende hata t.c.u. akaombe msaada huko. Wahadhiri wa kuime nao wanalalamika jinsi mabinti wanavyojipeleka. Wakifeli au kutofanya majaribio kwa wakati wanaenda na kutanguliza kauli kama hii "mwalimu mi niko tayari kwa chochote"!! Wahadhiri nao ni binadamu. Wamo mabazazi pia. Anaona wenzie wamepewa, yeye akiomba ananyimwa kwa hiyo anatafuta jinsi ya kuambiwa "mwl niko tayari kwa chochote". Kwa ufupi binti mwenye bidii na anayechukia short cuts akionewa apige kelele, lazima kuna atakayemsikia. Hii nchi kweli imeoza lakini si kiasi cha kutupwa jalalani. Wenye haki wachache bado wapo.akate rufaa wapi ambapo anaweza kusikilizwa na kupata haki yake!!!!
Anaweza akawa lecture at the same at akawa co- ordinator , so anaweza kufanya chochote anachoweza ata kukuwekea disco. Hizi kesi zilikuwepo sana chuo kwetu, mademu wengi walimaliza na vyeti fake, unakuta mtu chuo aonekani mwezi na paper hajafanya, matokeo yakitoka unaona kafaulu, hii nchi elimu ni uozo mtupu, elimu inanunuliwa
kitakuwa chuo cha aina gani hiki? vyuo vinavyojua taaluma hakuna mtu yeyote hata mkuu wa chuo anayeweza ku-temper na matokeo ya mwanafunzi maana mtu pekee mwenye mamlaka na somo au mtihani husika ni mwalimu wa somo tu. Matokeo huratibiwa kwa mfumo maalum wa kompyuta ambayo hurekodi nyendo zote ikiwa ni pamoja na jina la mtu aliyeingia kwenye mfumo na saa ngapi, kufanya nini. Kwa hiyo hata afisa wa mitihani hawezi kubadili chochote bila kujulikana. Ndo maana akitokea mwanafunzi hajaridhika na matokeo shahidi wa kweli ni karatasi yake ya mtihani. Mhadhiri mwenye akili timamu hata kama ni bazazi hawezi kuweka x sehemu ya tiki maana hiyo karatasi inaweza kupitiwa na external examiner na mtu atakayeteuliwa endapo rufani itatokea.
Mimi mwenyewe nashangaa, siku iz vyeti watu wananunua, sasa najiuliza, inakuwaje mtu anunue cheti kama sio jopo la ma lecture kupitia au kuhusika na kutengeneza vyeti fake, maana sidhan kama lecture mmoja anawez kutengeneza cheti fake bila kushirikiana na co ordinator, elimu ya bongo hamna kitu, bora nchi za wenzetu
kuna mtu namjua aligundulika kuwa na cheti feki cha chuo flani. NI kweli alisoma hapo ila matokeo yake hayakuwa mazuri, kwa hiyo akafoji matokeo mazuri zaidi ila wahusika ni watu wa mtaani. Unawapelekea cheti halisi, sijui wanatumia nini kufuta baadhi ya maandishi unayotaka yafutwe na kisha kuweka maandishi unayotaka wewe. Kuna waliogundulika wakati mwakyembe anasafisha bandari. wale walikuwa wanachukua nakala halisi za t.r.a wanabadilisha figure za hela tu.
Kwa hali ya vyuoni niijuayo mimi hakuna lecturers wanaoweza kujiunga eti watengeneze vyeti feki. Mwanafunzi wa ki-tz anayesoma hapa nyumbani ana uwezo wa kuwapa shilingi ngapi? Lecturer kazi yake haina sana tofauti sana na ya mwalimu wa shule ya msingi. Hana anachoweza kuchukua ili ajiongezee kipato zaidi ya muda. Kwa hiyo wengi wataenda vyuo vingine kufanya part time ambapo huweza kupata hela robo tatu au mara 2 ya take home yake, au miradi yake binafsi lakini si kuhangaika na kufoji foji vyeti ambavyo risk yake ni kubwa na return ni kipande cha karanga.
Aiseerr.......niliwahi kutojaziwa course work yangu na mwalimu wa somo fulan nikiwa chuo,nia ilikuwa niwe na incomplete course work nisifanye final na hyo ni technical supp kisa ananitaka kimapenzi.
Kama mara 2 nilikwenda kudai marks zangu alikuwa ananizungusha nakuniambia anataka ninachokimiliki,nilimrecord mara zote mbili.Mara ya mwisho nikaenda nakuonesha msimamo wangu wa kudai changu akanivuta nakutaka kunishika.
Ndipo kesi ilipoanza.....mpaka navyoongea sasa hv yule mwalimu kafukuzwa hapo chuoni,kafukuzwa kwenye nyumba ya chuo.Chuo nmemaliza lakin alinishtaki mahakamani.
Bado nakomaa nae mahakamani.Kama dada yako alistahili hzo marks basi alipaswa kujiamini na kukusanya ushahidi na kumlipua huyo mtu.
Ipo but sizani ni hadi kupeana sup tano! Coz lecturer unakuta anakufundisha somo moja au mawili sizani kama hilo linawezekana! Na pia kama lina wezekana ange appeal coz wanasahihisha wengine.
Kwa nini alikushtaki sasa??kwa kosa gani??
Rushwa ya ngono inaua elimu ya bongo, ma lectures n professors wanapenda mno uchi
Wanaume wote wanapenda uchi... we hupendi?