Miaka mingi ya nyuma (labda 30 iliyopita au zaidi), Gozi langu lilikuwa linafanya kazi Yemen kwenye kampuni ya ki Canada iliyokuwa inafanya exploration ya mafuta huo.
Nakumbuka aliniiita niende kwa mwezi mmoja nikamfaariji, na nikapata visa ya kwenda huko ya mwezi mmoja lakini baada ya mwezi ikabidi niendelee kubaki huko na visa ni lazima iongezwe, basi tukaenda "immigration office" za huko ili kuongeza muda wa visa.
Tulivyofika mlangoni tukamkuta askari na kumuuliza ofisi ya "mudir" (manager), iko wapi? akatuchangamkia sana akaacha geti na kutuambia tumfate, tukaona hii ni huduma VIP kabisa, akatupekea mpaka kwa "mudir", akatufungulia mlango wa ofisi na "mudir"na yeye akaingia na sisi ofisini akatuambia huyu ndiyo "mudir", na kweli mudir ana nyota tatu mabegani, tukamueleza shida yetu, na "mudir" bila ajizi akatuongezea miezi mingine mitatu ya visa.
Yule askari aliyetuleta yupo hapo hapo na sisi, ile tumemaliza akatuuliza "khalas?" yaani mmemaliza? tukamjibu "naam khalas" akasema "bakhshish" mbele ya boss wake, sisi tukashangaa anaomba bahashishi mbele ya "mudir"? kumtazama "mudir", anatwambia "just give him something, its OK here".
Huko bado hatujafikia Tanzania.