Ruhusa ya mikutano ni mtego kwa CHADEMA

Ruhusa ya mikutano ni mtego kwa CHADEMA

Hivi hakuna namna ukawa jukwaani ukasema maneno ya upinzani bila kuzua utata, yaani bila lugha za kichochezi wala matusi?
Mapepo yaliyompagawa mtu huwa hayaondolewi kwa lugha nyororo na ya kulemba. Ni lugha ngumu na amri kuu, na kwa mamlaka ya mbingu. PEPO ULIOLAANIWA TOKA.
 
Hivi hakuna namna ukawa jukwaani ukasema maneno ya upinzani bila kuzua utata, yaani bila lugha za kichochezi wala matusi?
Kauli za kisiasa, hasa za kishindani zilinganishe na wewe unaposhindana na wenzako kupata mchumba.

Mpo vijana wawili ama watatu kwa mfano, mnagombania mchumba mmoja ili kukubaliwa kumuoa.

Je utakapokuwa unajieleza kwa huyo msichana, utawapamba kwa maneno hao mahasimu zako?

Ni kawaida sana 'kupondana' na hakuna matusi yoyote viongozi wa CDM wanatoa, sema matendo yanayofanywa na Serikali kwa raia ndiyo matusi halisi na ni zaidi ya matusi, ni unyama!

Sasa Cdm wanapokuwa wanaexpress matusi yanayofanywa na Serikali pamoja na viongozi wake, ndipo wanapoonekana kama wachochezi!

Sisi wadau mbona hatuyaoni matusi hayo wala uchochezi wowote bali twaona tafsiri yenye kuyapembua matendo maovu ya Serikali?

Kusema: 'baba funga zipu umekaa uchi', je hapo mtoa taarifa atakuwa katukana au katoa taarifa ya kuzuia huyo baba asiendelee kuonesha matusi?

Tuwe tunapima dhamira ya maneno atoayo mtu, hata kama mtu huyo haumpendi.
 
Ruhusa hii imetolewa na jeshi la polisi ambao hawakukataza mikutano! Mikutano ilikatazwa na waziri wa mambo ya ndani.

Hivi sasa kuna ukamataji ambao huenda umelengwa kwa wafuasi wa Chadema, kinachokosekana ni viongozi wake na njia ya kuwapata ni kupitia majukwaa ya mikutano, hali ya kisiasa kwa hivi sasa ni tete kwani kila neno jukwaani linaweza kukutia matatani hata kama si kosa, ila dhamana haipo kwa utashi tu wa wakamataji!
Sasa kama ni hivyo:
Huyo Katambi atatembea nchi nzima kuwasaka watu wa CHADEMA bila polisi? Kama polisi wameruhusu, Katambi akatae,itabidi yeye mwenyewe akatekeleze katazo lake, au siyo?

Pili, kama viongozi wa CCHADEMA watakuwa na hofu hiyo unayoeleza wewe, ya kukamatwa kwenye mikutano; kuna kipi kitazuia hao hao kukamatwa mahali popote. Au watafunga midomo yao wasitamke tena neno lolote kwa kuogopa kukamatwa?

Kama hali inakuwa hii unayoieleza wewe hapa, si hao CHADEMA pekee watakamatwa. Kila atakayeonekana hakubaliani na wanayoyataka hao wakamataji, watakamata tu, bila kujali ni CHADEMA au la.
 
Na kwa elimu yangu, ni kiumbe mmoja tuu ambaye yeye na uongo ni damu damu mpaka akaitwa baba wa uongo.

Kwa kiumbe kisichotaka ukweli, maana yake kinataka na kinapenda uongo.

Baba wa uongo ni shetani, hivyo kama CCM ni baba wa uongo, maana yake CCM ni .....
CCM ni Chama Cha Mashetani
 
Hivi hakuna namna ukawa jukwaani ukasema maneno ya upinzani bila kuzua utata, yaani bila lugha za kichochezi wala matusi?
Hiyo ni lugha ya aina gani; kuna kipimo cha lugha hiyo kinachoopambanua ukisema hili ni tusi na hili siyo tusi?
Ni nani huyo anayeshikilia kipimo hiki cha "lufgha ?

maneno yoyote yatakayomuudhi Samia hayo ni matusi hata kama ni maneno ya kweli?
 
Waziri ndo anaakiiwa kutoa tamko japo alivunja katiba hakuna kifungu kinaruhusu waziri kuzuia mikutano ya kisiasa kwa sababu zake binafsi au Katambi kaona aibu kutoka kuruhusu mikutano angeoneka homnanzo japokua yote yanawezekana anatumia police kutengua kauli ya ovyo je kuna barua kutoka kwa IGP wa police Wambura kuruhusu mikutano?
Na ndio maana gazeti la NIPASHE la leo Alhamis tarehe 30/7/2026 limeruka na habari " WAZIRI AKINZANA NA POLISI"...wasije tu wakaitwa
 
Zuio bado lipo palepale kwani lilitolewa na waziri mambo ya ndani, halikutolewa na polisi ambaye yuko chini ya waziri kiutendaji.
Hii nchi haieleweki Mkuu.
Nisije nikasema Uongo.
Katiba inasiginwa na Kubakwa.

Waziri hana Mamlaka ya kutangaza hali ya Hatari.
Kuna chombo kinaitwa Balaza la Usalama.

Waziri hana mamlaka ya kuzuia mikutano ya kisiasa

Waziri hana mamlaka mbele ya IGP
Kumuamlisha atakavyo.
Mambo ni mengi.
 
Zuio bado lipo palepale kwani lilitolewa na waziri mambo ya ndani, halikutolewa na polisi ambaye yuko chini ya waziri kiutendaji.
Hii nchi haieleweki Mkuu.
Nisije nikasema Uongo.
Katiba inasiginwa na Kubakwa.

Waziri hana Mamlaka ya kutangaza hali ya Hatari.
Kuna chombo kinaitwa Balaza la Usalama.

Waziri hana mamlaka ya kuzuia mikutano ya kisiasa

Waziri hana mamlaka mbele ya IGP
Kumuamlisha atakavyo.
Mambo ni mengi.
 
Hii nchi haieleweki Mkuu.
Nisije nikasema Uongo.
Katiba inasiginwa na Kubakwa.

Waziri hana Mamlaka ya kutangaza hali ya Hatari.
Kuna chombo kinaitwa Balaza la Usalama.

Waziri hana mamlaka ya kuzuia mikutano ya kisiasa

Waziri hana mamlaka mbele ya IGP
Kumuamlisha atakavyo.
Mambo ni mengi.
Tuwaache wapambane wenyewe, sisi ni watazamaji tu.
 
Back
Top Bottom