Jannatul Firdaus
JF-Expert Member
- Aug 4, 2026
- 352
- 770
Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Ruby, kupitia kipindi cha wasafi fm (the switch) tarehe 24 august, amefunguka kuhusu maisha magumu aliyopitia wakati akipambana kutafuta kutoboa kwenye tasnia ya muziki, ikiwemo kufikia hatua ya kulala kwenye kibaraza cha nyumba ya msanii mwenzake, Diamond Platnumz.
Ilikuwa ni mahojiano maalum (interview) ambapo Ruby alikuwa akieleza safari ya maisha yake ya muziki, changamoto alizopitia, na jinsi alivyopambana kujiendeleza kabla ya kufanikiwa na kujulikana nchi nzima. Mahojiano haya yalikuwa katika vipindi vya hivi karibuni vya masuala ya burudani kwenye kituo hicho cha Wasafi.
Ruby alieleza kuwa baada ya kurejea jijini Dar es Salaam akitokea mkoani, alikumbana na pigo kubwa kutoka kwa ndugu na jamaa zake wa karibu waliokuwa wakiishi jijini hapa. Ndugu hao walimkataa na kumnyima hifadhi, jambo lililomfanya akose kabisa mahali pa kujistiri.
Baada ya kukataliwa na ndugu, msanii huyo alilazimika kutafuta hifadhi mbadala na kuamua kukimbilia kwenye nyumba moja ya kulala wageni (gesti) iliyopo maeneo ya Sinza, Dar es Salaam.
Katika gesti hiyo, alilazimika kulipia kiasi cha shilingi 5,000 kila siku ili kupata hifadhi ya usiku na kuepuka kuzurura mitaani.
Hata hivyo, kutokana na ukata na ukosefu wa kipato cha uhakika, kulikuwa na siku ambazo alikosa kabisa fedha za kulipia gesti hiyo. Siku yoyote alipokosa fedha hiyo, alilazimika kutoka na kwenda kulala kwenye kibaraza cha nyumba iliyokuwa inatazamana na gesti hiyo.
Ruby alibainisha kuwa wakati anatumia kibaraza hicho kama hifadhi yake ya dharura ya usiku, hakuwa na ufahamu wowote kwamba mjengo huo ulikuwa ni wa mwanamuziki Diamond Platnumz. Ndoto yake ya kutoka kimaisha na kufanya vizuri kwenye muziki ilikuwa ndio nguzo pekee iliyompa uvumilivu wa kupita kwenye changamoto hizo kabla ya kupata mafanikio anayojivunia hivi sasa.
"Nilivyorudi Dar es salaam ndugu zangu wote wa huku walinikataa hivyo nikakosa sehemu ya kulala, nilipata gest flani maeneo ya sinza kwa siku nilikuwa nalipa elfu 5, sasa kumbe ile gest ilikuwa inaangaliana na nyumba ya Diamond Platnumz."
“Sasa nilivyokuwa nakosa hela ya kulipia gest nikawa naenda kulala kwenye kibaraza cha nyumba ya Diamond bila kujua kuwa ni nyumba yake, kuna siku akanikuta akanisamilia. mimi na Diamond tumeanza kujuana mda mrefu sana" amesema hayo msanii ruby.
Ilikuwa ni mahojiano maalum (interview) ambapo Ruby alikuwa akieleza safari ya maisha yake ya muziki, changamoto alizopitia, na jinsi alivyopambana kujiendeleza kabla ya kufanikiwa na kujulikana nchi nzima. Mahojiano haya yalikuwa katika vipindi vya hivi karibuni vya masuala ya burudani kwenye kituo hicho cha Wasafi.
Ruby alieleza kuwa baada ya kurejea jijini Dar es Salaam akitokea mkoani, alikumbana na pigo kubwa kutoka kwa ndugu na jamaa zake wa karibu waliokuwa wakiishi jijini hapa. Ndugu hao walimkataa na kumnyima hifadhi, jambo lililomfanya akose kabisa mahali pa kujistiri.
Baada ya kukataliwa na ndugu, msanii huyo alilazimika kutafuta hifadhi mbadala na kuamua kukimbilia kwenye nyumba moja ya kulala wageni (gesti) iliyopo maeneo ya Sinza, Dar es Salaam.
Katika gesti hiyo, alilazimika kulipia kiasi cha shilingi 5,000 kila siku ili kupata hifadhi ya usiku na kuepuka kuzurura mitaani.
Hata hivyo, kutokana na ukata na ukosefu wa kipato cha uhakika, kulikuwa na siku ambazo alikosa kabisa fedha za kulipia gesti hiyo. Siku yoyote alipokosa fedha hiyo, alilazimika kutoka na kwenda kulala kwenye kibaraza cha nyumba iliyokuwa inatazamana na gesti hiyo.
Ruby alibainisha kuwa wakati anatumia kibaraza hicho kama hifadhi yake ya dharura ya usiku, hakuwa na ufahamu wowote kwamba mjengo huo ulikuwa ni wa mwanamuziki Diamond Platnumz. Ndoto yake ya kutoka kimaisha na kufanya vizuri kwenye muziki ilikuwa ndio nguzo pekee iliyompa uvumilivu wa kupita kwenye changamoto hizo kabla ya kupata mafanikio anayojivunia hivi sasa.
"Nilivyorudi Dar es salaam ndugu zangu wote wa huku walinikataa hivyo nikakosa sehemu ya kulala, nilipata gest flani maeneo ya sinza kwa siku nilikuwa nalipa elfu 5, sasa kumbe ile gest ilikuwa inaangaliana na nyumba ya Diamond Platnumz."
“Sasa nilivyokuwa nakosa hela ya kulipia gest nikawa naenda kulala kwenye kibaraza cha nyumba ya Diamond bila kujua kuwa ni nyumba yake, kuna siku akanikuta akanisamilia. mimi na Diamond tumeanza kujuana mda mrefu sana" amesema hayo msanii ruby.