1000 digits
JF-Expert Member
- Oct 16, 2012
- 7,802
- 10,290
Mkuu 1000 digits kazi ya polisi ni.
. Kuzuia
. Kupambana na hatimaye kukamata na kufikisha mbele ya sheria.
Unataka kuniambia kuwa mkoa wa mwanza hapakuwa na matukio mengne mabaya zaidi?
Unafikir hili tukio la kuzuia kuagwa mwili wa mawazo unadhan ndio tukio kubwa zaidi?
Mwanza ni mkoa mkubwa wenye matukio mengi sana ya ujambaz, mauaji n.k je umeona kuwa huyo kamanda wa polis ameeshindwa kuyazuia na kuyafanyia kazi?
Una ushahidi wowote wa kutoka mahakaman kuwa hakuna kabisa za kesi za robbery, mudder, ubakaji, unyang'anyi wa kutumia nguvu, ukiukwaji wa haki za binadamu mpaka useme hakuna alichokifanya?
Amefanya Mengi sana.
Lakini mtumishi wa umma anapotangazwa na mahakama kwamba amevunja sheria hakuna namna ya kumlinda kwa sababu ya aliyokuwa amefanya .
Sheria ni msumeno.
Jeshi la polisi halitabadilika kama wakubwa wao wanapewa promosion kwa kuvunja haki na sheria za nchi.
Kuna askari maskini ya Mungu walipiga tu picha wakiwa wamekumbatiana wakafukuzwa kazi mara moja na hakuna aliyejali utendaji wao wa huko nyuma. Sheria ilifuata mkondo bila ajizi. Wote tulishangilia askari wale maskini wasio na mshahara wa kuwafanya hata waishi mtaani kwa wiki mbili mbele.
Leo wakubwa wao wanatajwa na hukumu ya mahakama kuwa wamevunja sheria halafu wanapandishwa vyeo badala ya kukaa benchi bila kitengo.
Tena sijasema huyo mkumbo afukuzwe kazi bali aachie wengine hizo nafasi kubwa za kitaifa.
Hata haya majipu yanayotunbuliwa na Dr. Magufuli yamefanya mambo mengi tu katika utumishi wao lakini pale wakipokiuka wanatumbuliwa ,why wengine wanapokosea wanatumbuliwa na wengine wanapongezwa tena mahakama ikiwa imeshatoa na mwongozo wa kukiuka sheria.
Huoni kuwa hawa watendaji wanaofanya kazi kwa matakwa na malengo binafsi ya vyeo ni hatari kwa amani ya nchi?
Na pia mtu anayefanya kazi kwa maslahi binafsi hata hayo matukio mengine anaweza kupindusha ukweli pale anapoona atanufaika.
Kama tumeamua kujenga nchi yenye haki kwa wote na hasa wanyonge basi hatuna budi kuwa na viongozi watakaohakikisha wanyonge wanapata haki zao.
Unapovunja haki ya mnyonge kwa lengo la kumlinda mtawala ni uonevu na ndio dhulma inapoanzia.
Huyo kamanda anaonekana yuko kwa ajili ya kulinda maslahi ya watawala na yuko tayari kuvunja haki za wanyonge. Jambo ambalo linamuuma sana Mh. Rais Magufuli.
Sheria ikisimamiwa kwa haki kila mtu atamuheshimu mwenzake na nchi itakua na umoja.
Hata hao majipu wanaotumbuliwa wataridhika kwa kuona hawaonewi bali ni sheria lakini huyu anatumbuliwa halafu huyu anapandishwa cheo, tutaanza kuona kwamba kuna dalili ya kukomoana na sio kazi ya kusimamia haki.
Last edited by a moderator: