North pole mna shida sana! Alivunja sheria? Ipi? Ya kugombea maiti? Halafu hakimu aliyeendesha kesi anaitwa nani vileee. Mnafikiri wanaotafsiri sheria wanatoka mbinguni. No ni game tu imechezwa....sasa msikariri hukumu zenu za madai mkafikiri zinavuka mipaka kila sekta..... Mwacheni afanye KAZI..... SAWA SAWA? Ha ha haa
Kumbe bado kuna watu wanawaza ukabila kwenye haki na utendaji wa kazi.
Asili ya haki ni Mwenyezi Mungu na wote wanaosimamia haki kamwe hawayumbishwi hata kama ni ndugu wa damu.
Kwani Mawazo ni kabila gani?Mtu mwovu ni kama kipofu. Yani hata ukweli unaletewa ushabiki.
Hii nchi ina siasa za kizamani sana bado .
Hukumu ya mahakama wewe unaleta ukabila kweli. Majaji wamekaa siku tatu kupitia sheria na vifungu mbalimbali wewe unaleta ukabila.
Kama ni kupindisha wale majaji ndio wangepindisha kuifurahisha dola lakini wakasimamia ukweli
Na siku zote haki inapingwa na shetani na mawakala waje pekee.
Sisi wengine hatuchangamani kamwe na dhulmati. Historia hijawahi kumhukumu mtu anayesumamia hake kwa mnyonge.
Nyerere alisema kwamba Polisi ni chombo cha mabavu kisiposimamia haki za wanyonge vizuri basi kitageuka kuwa chombo cha kuwaonea na kuwagandamiza wanyonge. Na wanyonge watakosa pa kukimbilia.
Mashabiki wengi wa vyama huvipenda vyama kiushabiki na mara nyingine wanakua tayari kushangilia umwagaji wa damu kwa binadamu wenzao walioumbwa na Mungu. Wanasahau kuwa utu wa mwanadamu ndio jambo bora na la msingi kuliko vyama vilivyoundwa kwa maslahi ya vikundi vya watu na mara nyingine waanzilishi wake wanaviacha kwa kugundua makosa kisera.
Kuna watu mmeamua kujitoa akili na kwa sababu ya maslahi na kuona kuwa vyama ni kama dini na vitawafikisha peponi. Mnasahau kutenda yaliyomema.
Kumbuka siku Utakapokufa hutaulizwa habari za sera na cheo chako bali utaulizwa matendo yako ya haki yalikuaje. Kama ulikua kiongozi ulisimamia vipi haki kwa wanaoonewa.