Nimesikia sasa Polisi wanatawanya Mikutano, Sherehe, na hata Misiba ya Wanasiasa Ati kulinda amani. Sasa Hiyo inaitwa Kulinada amani au Ni Kuvuruga amani, Watu wako kwenye sherehe, au msiba au ibada, au mkutano wa Chama Unawapiga Mabomu, Je Ni Kulinda amani huko? au ni Kuvuruga amani?
Kama Kulinda amani ndio huko, Kama Niaa yao ni ya kweli, Kama hawafanyi hivi kwa Kutumwa na Serikali Kuwasaidia Wanaccm Kisiasa kwa Njia ya Uharamia, Basi wanithibitishie hili, naomba Polisi Tanzania Muandae Mabomu ya Kutosha na Maji ya Washawasha Muwapige Mkutano Mkuu wa CCM Unaanza Dodoma nadhani ni Mwezi wa saba ili kuwe na Amani. Na Mtaonekana 1) Mnapowapiga wengine Mabomu hamtumwi na CCM 2) Kuwa Kweli huo ndio Mtindo wenu wa kulinda amani.
Vinginevo Wakuu wote wa Polisi Tanzani, Pamoja na Kuwa Kweli Mnafanya kazi ya Kweli ya Kulinda amani, Lakini Katika hili Mtatufanya Kuendelea Kuamini Kuwa Mmekuwa Vibaraka na Wanyapara wa CCM Tendo ambalo ni Kinyume na sheria ya Vyama Vingi, Na Ni fedheha Kwa Mtu anayejiheshimu Tena Polisi Kutumwa Kukandamiza haki.
Yupo wapi Mkuu wa Polisi Mmoja atakayejitolea Muhanga Kujiuzulu, Watanzania Tutamchangia Mamilioni aishi Kwa raha na heshima na Awe ni Mfano wa Historia.Haki ya Mama hata Mimi Nitauza ikiwezekana, Mbusi, Kuku, mbwa, hata Paka na Gari yangu na mimi nivurutishie kamchango!
Vinginevyo Zoezi haramu wanalolifanya Polisi la Kuzuia Mikutano, sherehe na hata Mazishi ilimradi tu sherehe hizo ziwe na harufu ya Zitto wa ACT, au Chadema au CUF. POLISI MKOME NA MNAOWATUMA MKOME.