Invisble275
JF-Expert Member
- Nov 28, 2014
- 982
- 1,166
Mkuu unaliona hili kama ninavyoliona.Ndo maana nasema nchi inaenda kusiko.Napenda kutoa wito kwa CCM kuhairisha mkutano wetu mpaka pale katazo la mikutano ya siasa litakapobatilishwa.
Tanzania imeisha. wazee wetu wote hovyo kabisa. Hakuna anayesimama kukemea mambo kama haya. Yaaani hawaoni hii misuguano ya kisiasa haitufikishi mbali. Magufuli pia ajue kuwa Baada ya kuziba mianya ya walaji sasa ana maadui wengi sana ndani na nje. Kumbuka mitandao ya ufisadi, madawa ya kulevya network yao ni kubwa sana ndani na nje ya nchi. Hii haizuia, kwa kutumia hao wapinzani wake wa kisiasa inaweza kuwa trick ya kuingiza nchi kwenye machafuko ili yeye alaumiwe kuwa kauwa amani ya Tanzania. Unakumbuka michezo ya utotoni shule ya msingi makundi rival, anatangulizwa yule mnyonge ili rival wajue huyu tutapiga tu. Kumbe nyuma kuna wababe haswa ambao vurugu zikianza lazima kijasho kiwatoke. Mie nadhani Serikali na hivi vyama vingine wangekaaa meza moja kutafuta suluhu ya hii misuguano. Wote tuko kwenye jahazi moja halafu mnagombana mwingine anataka atoe mbao hivi kuna anakayepona jahazi likizama?