mbenge
JF-Expert Member
- May 15, 2019
- 4,573
- 9,809
"Kukuza sekta za huduma hususan utalii ili kutumia fursa zilizopo kikamilifu na kuongeza mchango wake katika uchumi wa Taifa. (Uk.14)"KUKUZA UTALII
F. Kutengeneza ajira zisizopungua 7,000,000 (milioni saba) katika sekta
rasmi na isiyo rasmi kwa ajili ya vijana:-
(i) Kuchochea ukuaji wa uchumi, hususan katika sekta ya viwanda vinavyotumia malighafi za kilimo, mifugo, uvuvi, madini, maliasili na sekta ya huduma za kiuchumi pamoja na utalii;
(ii) Kuwawezesha vijana kushiriki katika shughuli za ujasiriamali,
ikiwemo kuwapatia mafunzo na kuwaunganisha na taasisi na
asasi za utoaji mikopo yenye riba na masharti nafuu;
(iii) Kuwahamasisha na kuwawezesha vijana kushiriki kikamilifu
katika utamaduni, michezo na sanaa kwa ajili ya afya bora na
burudani na pia kuongeza fursa za ajira na kipato; na
(iv) Kuhakikisha kuwa miradi mikubwa ya kimkakati inaajiri
vijana wengi zaidi wa Kitanzania.
UKURASA WA 8
(xi) Kukuza sekta za huduma hususan utalii ili kutumia fursa
zilizopo kikamilifu na kuongeza mchango wake katika uchumi
wa Taifa. ( UKURASA WA 14)
Ndiyo! Imetajwa hivyo katika ilani, lakini utekelezaji wa wake ni lazima Mheshimiwa mwenyewe ndiye aende "front line" ama hili ni jukumu la wizara yenye dhamana ya utalii kwa kushirikiana na wizara ya mambo ya nje.
Urais ni taasisi yenye majumu makubwa sana kiuendeshaji. Tunategemea Rais atumie zaidi "abstract skills" zaidi ya "administrative & technical skills" katika suala kama vile ambavyo inaonekana yupo "field" akifanya.
Matumizi ya "administrative & technical skills" ni jukumu la wizara na wataalamu wake kuhakikisha linatekelezwa kwa ukamilifu na umakini mkubwa chini ya maelekezo ya ofisi ya Rais. Rais ni lazima ahakikishe yale yote anayoyaelekeza yanafanyika kupitia kwa wale aliowaamini na kuwapa majukumu hayo. Si sahihi kwa yeye kwenda mwenyewe "field" kufanya kazi za wasaaidizi wake.