Rostam MUST Resign; CCM Must Act

mkuu tatizo siyo RA, tatizo ni sheria za nchi hii ambazo ni kama mdomo wa mamba. wajanja walitangulia kutupiga bao kutengeneza sheria zinazowalinda waliopo kwenye mfumo. huyo jamaa ni matokeo tu.

Inawezekena ni kweli unayosema. Lakini hatuwezi kudhiadhibu sheria bali kuzibadilisha. Rostam ametumia dhamana ya uongozi wake vibaya ni lazima tumuadhibu na sio kumbadilisha. We need to act on this guy now whether analipwa au halipwi lakini tunaanza na Rostam, no way out this time. Tunaanza na Rostam then wengine wanafuata huku tukiendelea kupitia sheria zetu na kuzibadilisha kwakupitia mapendekezo ya wananchi.
 
Misri imeonyesha njia baada ya Tunisia..kuwakataa watawala wabovu...hatujafikia huko lakini wanaotukoroga waanze kuandimkwa ili wasitufikishe huko!!! CCM must act... kwani bunge halina sheria za kuchunguza maadili ya wabunge??? Tume ya maadili je nao wanasmeaje juu ya hili..Kweli hizi zote bado ni tuhuma tu??? RA mwenyewe hajipimi akaona kwamba yuko njia panda kuhudumuia wananchi wa nzega na kuhudumia biashara zake?? This chapter must be closed....
 
Kweli kabisa , utekelezaji wa ilani utaingia utata, maana huyo ndo engineer wa ilani na ahadi zote za JK anajua wapi fund zitapatikana , zitoke namna gani chama kipate mgawo upi etc
 

Naunga hoja mkuu,ifike sehemu wananchi tunataikiwa kuja kuwa sisi tumeshika mpini,na watawala wameshika makali,hawawezi kuzima nguvu ya umma.Wala si Rostam pekee anayetakiwa kung'oka,viongozi wote na CCM yao tuwang'oe,sioni sababu ya kubagain nao.Nguvu ya umma ndio dawa pekee vinginevyo,tutabaki kuandika na kuandika bila mafanikio.
 
Colleagues,

I always have the same feelings as that of Mwana-Kijiji. However, I noted that majority of Tanzanians are poor and ignorant. Few 'educated' leaders continue to exploit the majority on the context of PEACE. Whatever good point that will be presented here for letting Tanzanians liberate themselves from the exploitative hands of these few leaders, the CCM will always come out and tell the 'Majority' that they are cheated by opposition parties to destabilize PEACE.
Under the umbrella of PEACE, few leaders continue to accumulate unimaginable wealth.

I am of the following takes:
1) Every JF member continues to sensitize and educate whoever is met on the way in regards to the situation we are in. It may take time but without majority supports no change is expected soon
2) Workers' Union, opposition politcal leaders to give out serious messages of CHANGE in leader ship.
3) By the way, did you see one energetic young man from 'UDSM' on strike yesterday? (Source 'ITV-Hapa na Pale' If we have more than ten young men of that nature, I believe CHANGE on the country leadership is at door.
 


lilikuwa dongo la kinyumenyume kwa UVCCM si wamejitokeza na kuonesha kuwa hawaridhishwi na mambo yalivyo? let them go all the way. Tuliongoza kwenye suala la bodi ya mikopo wao wakafuata na kwenye hili waje tu.. it is a logical progression ya hili suala.
 
If Rostam falls the other puppets of corruption will fall behind him..
 


Mkuu, hasa hapo kwenye red, you have made my day. Kinachoniletea kizunguzungu zaidi ni kusikia wazee wa CCM wakisema hilo ni suala la kisheria; siasa isiingie kabisa huku anayekwenda kukinga mkwanja huo wa Dowans ni member wa Kamati Kuu ya CCM kwa uwezo (power of attorney) aliokirimiwa na wenye kampuni. Really disgusting!
 
Asante Mwanakiiji, ila jitahidi kuandika kwa lugha ambayo wengi wanaijua itasaidia zaidi. Kwani wengi wa mtandao huu ni watanzania wanaotumia lugha ya taifa kiswahili.
 
Asante Mwanakiiji, ila jitahidi kuandika kwa lugha ambayo wengi wanaijua itasaidia zaidi. Kwani wengi wa mtandao huu ni watanzania wanaotumia lugha ya taifa kiswahili.

Nadhani Watanzania waliopitia angalau shule ya sekondari wanajua Kiingereza. Tusiwafanye watu wetu duni kiasi cha kushindwa kuelewa.
 
Nadhani Watanzania waliopitia angalau shule ya sekondari wanajua Kiingereza. Tusiwafanye watu wetu duni kiasi cha kushindwa kuelewa.

Unajua ni wangapi wamepita shule za sekondari?

Kutojua au kujua Kiingereza hakuna uhusiano na uduni, ni lugha tu mkuu. Tatizo ni kwamba hata wanaoweza kusoma Kiswahili wanaweza wasielewe, ni uwezo tu wa mtu.

By the way, when you say CCM must act who are you actually talking about?
Naona ni watatu tu ndio wanaoweza kufanya hivyo,

Chairman? That is not possible, you know why!
Secretary General? Give me a break!
CC? Just said RA should be given billions, it did not say he should be dealt with.
 

Mwenyekiti hana ubavu, Katibu of course hana ubavu.. nazungumzia Kamati Kuu au Wabunge wa CCM si mwenzao huyo?
 
Thats why I believe it will be good if Rostam himself decide to quit.

Una maana aachie ulaji mwenyewe kwasababu tu umesema mkuu?Naamini hawezi kufanya hivyo kama hakuna usumbufu kutoka kwa wananchi.Hawezi kuondoka mwenyewe kama maslahi yake haya hatarishwi.

Unaposema it will be good una maana gani mkuu?It will be good for him or for the people?If it is for the sake of the people,then i think he will care less,but if it is good for him then i am sure he might consider your advice.

And bottom line ni kuhakikisha kuwa whatever he's doing now is not good for himself,means that he will suffer the consequences of responsibilities and accountabilities. However the way i see it,at least as of now,it is waay better for him to keep on doing what he's doing.This is unless proven otherwise.
 
Mwenyekiti hana ubavu, Katibu of course hana ubavu.. nazungumzia Kamati Kuu au Wabunge wa CCM si mwenzao huyo?

Rostam ni political kingpin and master manipulator na mara nyingi namlinganisha na Escobar na sasa hivi nadhani ni kama Edgar Hoover kwa sababu anazo siri nying za wakuu.

Nashangazwa sana kuona wananchi wengi sana magazeti mengi yamekemea kitendo cha kulipwa Dowans lakini hakuna kiongozi yoyote wa juu amekemea hata kusikitika kwa hukumu ya ICC...hi ina maana viongozi na CC wanajua kabisa.

Yaani mimi nimesikitika sana kuona kimya cha mkulu yaani ameshindwa hata kutupiga kiini macho?.
 
Ni ujasiri wa kifisadi aliojijengea muda mrefu ambao ulianza taratibu kwa kushirikisha watu wachache ndani ya CCM. Ilipoonekana hajashtukiwa akaendelea kujenga himaya yake ndani ya chama na kufikia hatua hiyo ya kuendesha chama na nchi kwa ujumla.

Tu mateka ndani ya nchi yetu hatuna tunachoweza kukemea na kusikilizwa na watawala wetu,wote wamefungwa midomo na mfadhili huyu haramu. Raisi wetu yu kifungoni,anahitaji msaada wetu sisi wananchi ndo maana hata waziri wake kakiri kuwa raisi hawezi kuzungumzia suala la Dowans sababu wanaelewa mkuu kaelemewa na mzigo mzito.

Eee Mola,jalia upepo wa nchi za kaskazini upulize huku kusini wananchi waamke tufanye mabadiliko muhimu kwa mustakbal wa nchi yetu na vizazi vijavyo. Hakika tumechoka.
 

Rostam,Chenge,Mramba,Mungai.........hakuna aliyefunguliwa kesi ya uhujumu uchumi...mnajua sababu ni nini?...kwa sababu wameiba not vijisenti.....
 
Kuna kitu kinaitwa National Security. The moment nchi inakuwa na mtu au watu wanaohatarisha hicho kitu kuna laid down procedure ya nini kufanya, na ni watu wachache sana akiwemo Rais, mkuu wa Tiss wanaojua ikiwa procedure zinatakiwa kufuatwa.

SasaTanzania badala ya kuprotect nchi na wananchi wasiwe kwenye hatari ya machafuko, viongozi wetu wamewakumbatia hao wanaotakiwa kushughulikiwa.

Solution then inakuja toa hao viongozi na kuweka wengine watakaoprotect nchi kama waliopo wanachekacheka wakati wakijua nini kinatakiwa kufanywa.
 
MM,
Dhambi ni mbaya sana. Ukimaliza kuitenda hamu ya kuitenda tena inarejea mara moja. Rostam amefikia 'a point of no-return' katika kujineemesha kwa gharama ya watanzania maskini. Kumwambia ajiuzulu ni kumpigia mbuzi gitaa. Similarly, viongozi wa ccm wenye uwezo na mmlaka ya kujenga hoja ya kumtimua kwenye chama au hata kumkemea nao wamefikia 'a point of no-retun'.

Wamelishwa na wamenyweshwa wao na ndugu na jamaa zao mpaka wamevimbiwa. Nafsi zao zinawasuta. Kwa hatua waliyofikia, kumnyoshea Rostam kidole ni sawa na kujinyoshea wao wenyewe. Orodha ya viongozi hao ni ndefu ikianzia na M'kiti mwenyewe pale juu kabisa. Kwa hiyo, MM ondoa mawazo yako kwamba Rostam atajiuzulu kwa uamuzi wake mwenyewe. Haiwezekani na haitakuja iwezekane.

Sasa tufanye nini:
Nguvu ya umma ichukue mkondo wake. Kwenye mojawapo ya threads zangu zimewahi kuongelea suala hili kwamba pasipo nguvu ya umma, Rostam ataendelea kuifilisi nchi hii kupitia kwenye migongo ya viongozi wanaochaguliwa na wananchi. Lazima umma uingie mitaani upige kelele pande zote za Dunia na kusema sasa tumechoka. Ifike mahala wananchi waseme sasa ccm basi kwa maana kwamba ichague mawili au kufa au kuendelea kumlea fisadi Rostam.

Vyama vya upinzani na jumuia na vikundi mbalimbali vya kijamii pamoja na jumuia za wanataaluma ndizo zinazoweza kuratibu maandamano makubwa yatakayo-draw attention ya vyombo vikubwa vya habari vya kimataifa BBC World, CNN, Aljazeera, DW, CFI, Skynews, n.k. Tukifikia hatua hiyo, jk na maajenti wake wa ufisadi watachukua hatua wapende wasipende.
 

.......Thats Rostam!!!....right dere!............
 

Thank you for speaking for Rostam. May I please ask if you are from this country? Do we need to doubt the court ruling that mentions and shows the Involvement of Rostam? Do we need to doubt our parliamentary committee?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…