Roman Abramovich: Utajiri wa Damu, Risasi na Umafia

ROMAN ABRAMOVICH: UTAJIRI WA DAMU, RISASI NA UMAFIA









SEHEMU YA NANE







Hakuna kitu kizuri kama kiongozi ambaye anaweza kujitathimini na kukubali mapungufu yake na kukubali kukaa pembeni kupisha wengine. Mtu wa namna hii hata kama kuna madudu aliyafanya unajikuta unapata nafasi ya kumsamehe moyoni.

Licha ya mapungufu yake yote na vituko juu ya vimbwnga alivyovifanya kuidharaulisha Russia, lakini ulipofika wakati na kuelezwa ukweli kwamba ni muda muafaka akae pembeni kupisha mtu mwingine, Boris Yeltsin hakuifanya shingo yake kuwa ngumu.



Roman Abramovich akakutana na ma-oligarch wenzake. Akawapa pendekezo lake la nani anadhani anafaa kuwa rais mpya wa Russia. Akaweka sababu zake mezani… ma-oligarch wakakubaliana naye.



Nilieleza kwamba wale wanaojiita ‘The Family’ ambao ni ma-oligarch na wanafamilia ya Yeltsin kimsingi ndio ambao walikuwa wanaendsha nchi. Na ndani ya The Family kulikuwa na ule ‘Utatu Mtakatifu’… Abramovich, Tatyana na Yumachev. Na katika kipindi hiki Abramovich alikuwa na nguvu ya ushawishi kwa Yeltsin kuwazidi wote hata ndani ya The Family na Utatu Mtakatifu.

Kwa hiyo ulipofika wakati wa kuzungumza suala hili zito na Yeltsin… ni Abramovich pekee yake… yeye na Yeltsin pekee walijifungia ofisini na ‘kuyajenga’.

Kwanza Abramovich alimueleza Yeltsin kwa nini huu ni muda muafaka yeye kukaa pembeni na kumpisha kiongozi mpya. Baada ya Yeltsin kuukubaliana na hili, Abramovich akamueleza kuhusu pendekezo la mrithi wake. Abramovich akamueleza kwamba anapendekeza Vladimir Vladimirovich Putin, Mkurugenzi Mkuu wa FSB aanze kuandaliwa kurithi kiti hicho cha Urais. Kama ambavyo aliwafafanulia ma-oligarch ndivyo pia ambavyo alimfafanulia Rais Boris Yeltsin.



Tarehe 9 August mwaka 1999 Rais Boris Yeltsin alimteua Vladimir Putin kuwa Naibu wa Kwanza wa Waziri Mkuu. Yaani kipindi hicho ilikuwa kunakuwa na Waziri Mkuu alafu anakuwa na Manaibu watatu au wawili. Yaani mfano mzuri kama Zanzibar walivyo na ‘Makamu wa Kwanza na Makamu wa Pili wa Rais’. Kwa hiyo Putin aliteuliwa kuwa Naibu wa Kwanza wa Waziri Mkuu wa Russia. Nimeeleza kwamba kipindi hiki Russia ilikuwa kwenye mparaganyiko fulani hivi wa kimfumo. Wakati Putin alikuwa anateuliwa kuwa Naibu wa Kwanza wa Waziri Mkuu lakini nafasi ya Waziri Mkuu ilikuwa wazi. Ndani ya muda wa chini ya miezi kumi na tatu, walikuwa wameteuliwa Mawaziri Wakuu wane tofauti na kufukuzwa. Uteuzi huu wa Putin kuwa Naibu wa Kwanza wa Waziri mkuu ulitangazwa asubuhi ya tarehe hiyo 9… lakini ajabu sana ilipofika majira ya jioni siku hiyo hiyo Putin aliteuliwa kuwa Waziri Mkuu wa Russia.





Mkakati… Abramovich… Abracadabra…



Uteuzi wa Putin kuwa Waziri Mkuu mwanzoni haukushitua sana watu japokuwa hakuwa na umaarufu kwa wanasiasa wala wananchi kwa sababu kama ambavyo nimeeleza kuwa kwa muda wa kama miezi kumi na tatu tu tayari kulikuwa na Mawaziri Wakuu wane walioteuliwa na kufutwa kazi. Kwa hiyo watu walikuwa wanamuhesabia siku tu Putin kabla yay eye pia ‘kutumbuliwa’… ni kama vile hapa kwetu nchini, ukiteuliwa kuongoza Wizara ya Maliasili na Utalii au Wizara ya Nishati na Madini… watu wanakuhesabia miezi tu.



Lakini siku tatu tu baada ya uteuzi wa Putin, Rais Boris Yeltsin alifanya kitu cha tofauti kulinganisha na Mawaziri Wakuu waliopita ambao aliwahi kuwateua. Katika hotuba yake kwa wananchi alitamka kwamba anatamani Putin awe mrithi wake wa kiti cha Urais siku akiondoka kwenye cheo hicho… wenye kusoma alama za nyakati wakaelewa nini kilikuwa kinaendelea. Hii haikuwa ile ‘teau kisha fukuza’. Putin alikuwa anaandaliwa kuchukua nchi.



Kwa hiyo wapinzania wa Yeltsin au tuseme wapinzani wa ‘The Family’ wakaanza kujipanga kuzuia hicho ambacho kilikuwa kinataka kutokea. Iikuwa wazi kwamba Yeltsin amebakiza muda mchache madarakani, kwa wapinzani wa ma-oligarch hii ilikuwa habari njema kwao kwamba walau sasa na wao watapata zamu yao kufaidi mema ya nchi. Lakini baada ya kauli ya Yeltsin kwamba anatamani kurithiwa kiti cha Urais na Putin walielewa kwamba huu ulikuwa ni mkakati wa kuanza kumnadi Putin kwa wananchi. Kwahiyo nao wakaanza mipango ya kukwamisha suala hilo lisifanikiwe.



Sasa,

nimeeelza kwenye sehemu zilizopita kwamba Yeltsin alikuwa na upinzani mkubwa sana kwa wanasiasa wengine. Upinzani huu ulikuwa na historia ndefu hata kabla hajaanza kuwalimbikizia mali ma-oligarch.



Tutazame kidogo kwa ufupi sana… Shirikisho la Russia lilivunjika December, 1991. Kama mwezi mmoja hivi baadae, yaani January, 1992 Rais Yeltsin alianzisha program mpya kukabiliana na hali ya mbaya ya kiuchumi ambayo ilisababishwa na kuvunjika kwa Shirikisho la Russia. Badala ya program ile kusaidia badala yake ilifanya hali ya kiuchumi kuwa mbaya zaidi. Yeltsin alipingwa vikali mno kwa sera hizo mpya ambazo alizianzisha kiasi kwamba mpaka makamu wake wa Rais alikuwa anazikosoa hadharani kabisa. Likatokea wimbi la wanasiasa wengi hata wa chama chake kujiweka mbali na Yeltsin na kujipambanua kupinga sera hizo mpya za kiuchumi za Yeltsin. Matokeo yake ni kwamba Yeltsin alikuwa akipeleka miswada au mapendekezo Bungeni ili yapitishwe yalikuwa yanakwamishwa makusudi ili kumkata makali ya kutekeleza sera zake za kiuchumi. Kipindi hicho Bunge la Russia lilikuwa linaitwa “Supreme Soviet”. Baada ya mvutano wa muda mrefu kati ya Yeltsin na Bunge hatimaye Yeltsin akatangaza kulivunja Bunge. Sasa katiba ya Russia kipindi hicho ilikuwa haimpi mamlaka Rais kulivunja Bunge, kwa hiyo wabunge wakagoma na wakawa wanaendelea na shughuli za kibunge. Yeltsin akaingiza vifaru vya kijeshi kwenye viwanja vya bungeni kutaka kuwatoa wabunge kwa lazima. Wabunge wakagoma… wafuasi wao wakaandamana mitaani pale Moscow… kukatokea mapigano makali kati ya wananchi waliokuwa wanaunga mkono bunge dhidi ya wafuasi wa Yeltsin na jeshi. Inakadiriwa karibia watu 1,500 walipoteza maisha kwenye yale mapigano na kuyafanya kuwa moja ya tukio baya zaidi kwenye historia ya Russia.



Loh.! Nanogewa nichambue zaidi historia hii ya Russia… but let’s cut a long story short. Mapigano yale yalidumu kwa muda wa kama wiki mbili hivi kabla ya Rais Yeltsin na Bunge kufikia muafaka. Bunge walimpa masharti kadhaa ili waendelee kufanya naye kazi ‘smoothly’ na yeye Rais Yeltsin akatoa matakwa yake.

Moja ya makubaliano makuu ilikuwa ni kuunda upya mfumo wa Bunge la ‘Supreme Soviet’. Yeltsin alihisi kwamba Bunge lilikuwa limepewa mamlaka makubwa mno kutokana na mfumo wa kijamaa ambao ulikuwa unatumika kuendesha nchi huko nyuma. Chini ya mfumo huu mpya, kwanza ‘supreme soviet’ litavunjwa na kuundwa ‘Federal assembly’ ambayo itakuwa na ‘chamber’ mbili. Kutakuwa na ‘Lower House’ kwa jina State Duma (au GosDumas kama warusi wenyewe wanavyooita), na pia kutakuwa na ‘Upper House’ kwa jina la Council of the Federation. (Mfumo huu bado ungali unatumika mpaka sasa).



Kwanini nimegusia historia hii? Kuna vitu viwili ambavyo nataka uvione… kwanza ni uhasama wa Bunge na rais Yeltsin kwani hata baada ya mfumo mpya kuwekwa Bunge bado lilikuwa na kinyongo naye kutokana na kile ambacho kilitokea.

Na jambo la pili nataka tufahamu kwamba ile lower house ya Bunge (State Duma) ndiyo ambayo ilikuwa na malamlaka ya kumthibitisha Waziri Mkuu mara baada ya kuteuliwa na Rais.



Sasa,



Bada ya kauli ya Yeltsin kwamba anatamani Putin awe mrithi wake wa kiti cha Urais, wapinzani wa ‘The Family’ wakaanza kampeni ya chini kwa chini kushawishi wabunge wa GosDumas kumpiga chini Putin.



Putin alikuwa anahitaji kura 226 ili kuthibitishwa kuwa Waziri Mkuu.



Kambi ya Yeltsin ikagundua njama hii na mara moja wakaanza kuifanyia kazi. Wanasema pesa sabuni ya roho… haijalishi ni kabila gani au nchi gani… pesa inaweza kubadili moyo wa binadamu. Ma-oligarch wakaingia kazini kumwaga fedha kwa wabunge wa GosDuma.

Siku ya August 16 kura zilipopigwa Putin aliponea chupu chupu kwa kupata kura 233. Kura saba tu zaidi.



Kwa hiyo rasmi sasa Putin alikuwa ni waziri Mkuu wa Russia.



Hatua ambayo ilikuwa inafuata ilikuwa ni kumjenga Putin kwenye mioyo ya wananchi. Kama ambavyo nimeeleza… vyombo vya habari vyote vilikuwa vinamilikiwa na ma-oligarch. Kwa hiyo kila siku vilikuwa vinaandaliwa vipindi malumu vya redio na televisheni… makala kwenye magazeti na makongamano na mikutano ya hadhara… vyote kumuhusu Vladimir Putin.

Lakini moja ya matukio ambayo yalisaidia kumuweka Putin kwenye mioyo ya warusi ilikuwa ni namna ambavyo alishughulikia tafrani ambayo ilitokana na kulipuka kwa mabomu kwenye nyumba za kupanga kwenye miji mitatu nchini urusi… tukio ambalo linajulikana kwa jina maarufu la ‘Russia Appartment Bombings’. Tukio ambalo lilizua hofu kubwa ndani ya Urusi. Putin alionyesha ukakamavu wa hali ya juu na umahiri kulishughulikia suala hilo mpaka mwisho. Lakini pia Putin aliwakosha warusi kwa msimamo wake thabiti juu ya vita waliyokuwa wanaipigana Chechenya.



Miezi mitatu baadae, yaani mwezi December 1999 Rais Boris Yeltsin alijiuzulu ghafla na kwa mujibu wa katiba ya Rusia Waziri Mkuu ndiye anachukua nafasi yake na kuikaimu mpaka uchaguzi mkuu uitishwe.



Yeltisn alijiuzulu tarehe 31 December 1999… siku hiyo hiyo Putin akatangazwa kuwa Kaimu Rais wa Russia. Na siku hiyo hiyo akasaini ‘decree’ ya kwanza na muhimu sana kwenye historia ya Urusi. Decree hii ilikuwa na kichwa kinachosema, “On Guarantees of former President of the Russian federation and members of his family”. Decree hii iikuwa inatoa kinga kwa Rais Yeltsin na wanafamilia wake wote kwamba hawatashtakiwa kwa makosa yoyote yale kama ikionekana labda kulikuwa na makosa yoyote ambayo yalitendeka kipindi cha Urais wa Yeltsin.

Na hii ilikuwa ni moja ya makubaliano kati ya Yeltsin na Abramovich kwa niaba ya ma-oligarch wenzake walipomtaka aachie ngazi… alitaka ahakikishiwe kwamba mali zake hatopokonywa na kamwe asishtakiwe.



Miezi mitatu baadae, Putin aliitisha uchaguzi mkuu ambao alishinda kiulaini kabisa. Tarehe 7 May 2000, Vladimir Vladimirovich Putin alikula kiapo kuwa Rais wa Russia.



Kazi ilikuwa imekamilika…. Abramovich… abracadabra.!!



Swahiba wake ambaye ‘amemfinyanga’ kwa mikono yake na kumtengenezea njia sasa alikuwa amekalia kiti cha urais wa nchi.



Kuna kitabu kitakatifu kinasema “tunakua kutoka utukufu mpaka utukufu”. Na haswaaa, hii ndio hulka yetu binadamu… haijalishi tuko kileleni kiasi gani… siku zote tunataka kuipanda ngazi inayofuata. Hata uwe na kikubwa kiasi gani, nafsini tunaona tulichanacho bado hakitoshi… haijalishi tunacho kingi kiasi gani. Tunatamani, tunatafuta, tunakipata alafu tunataka zaidi… wanadamu tumeumbwa na kiu ya “kukua kutoka utukufu mpaka utukufu”.



Huu sasa ulikuwa ni wakati wa Abramovich kuhamia katika hatua ya pili ya ndoto zake… ndoto kubwa zaidi. Unaweza kudhani kumiliki Sibneft kampuni kubwa zaidi ya kuzalisha mafuta nchini Russia ilikuwa inatosha.. la hasha… Roman Abramovich alikuwa anataka zaidi, na alichikuwa anakitaka safari hii kilikuwa kimono zaidi pale Russia.. Abrfamovich alikuwa anataka kujimilikisha sekta ya Aluminum ndani ya nchi ya Russia. Sekta yenye utajiri mkubwa zaidi nchini Russia lakini pia ikiwa ni sekta hatari zaidi.

Kuingia kwa Abramovich kwenye sekta hii kutakuja kuibua moja ya nyakati za hatari zaidi kuwahi kushuhudiwa nchini Russia na Ulaya mashsriki yote kiasi kwamba mpaka leo hii kipindi hicho kinajulikana kama nyakati za ‘Vita za Aluminum’.



Tutajadili…




Kuhusu ishu ya Vitabu...



Noana kuna jambo nasisitizwa sana, VITABU.

Niliwahi kutangaza kutoa kitabu lakini sijawapa tena update yeyote.



Kuna changamoto imetokea na nilikuwa sitaki kuizungumzia ndio maana kwa mwaka mzima sijasema chochote kuhusu kile kitabu ambacho niliwapostia mpaka picha yake kwamba tayari kinachpwa. Lakini nadhani ni vyema nilisemee mara moja ili walau mnielewe nini kimetokea…

Ni kwamba kwenye kile kitabu kuna hii makala ya ya Ujasusi Sebuleni Kwetu na makala ya The Richest Man. Hizi makala zote zinahusu masuala ya kiusalama hapa Afrika Mashariki.

Nadhani mnaona hali za kiuslama hapa katikati ilikuwa tete kidogo Afrika Mashariki… Kuna mabwana wakubwa wanahisi kwamba hizo makala zina taarifa sensitive na kwamba si vyema zikienda public... so kitabu kikapigwa stop kabla ya kuuza hata nakala moja. Nikafosi kutoa nakala mia moja tu na kuwapa watu waliopo kwenye group langu whatsapp kwa masharti. But sijawahi kumpatia mtu mwingine yeyote nje ya hao na ndio maana hata humu sijawahi kuwaeleza kinapatikanaje.







Taarifa gani hizo sensitive? Wajua, mie humu JF nikionana akiana 'chogo' wanakuja kubeza sijui oooh hii iko google sijui nini nini... huwa nawaangalia nabaki nacheka tu hiiiiiiii... ubaya tumekutana tu hapa JF hakuna anayejua undani wa mwenzake.



Niseme tu kwa haya masuala ya intelijensia Afrika Mashariki nina access ya kupata taarifa kubwa ambazo hata haziko mitandaoni au mtaani. Na kwa kusema hivyo sitaki kumaanisha kwamba labda mie niko pale Oysterbay/K.nyama... hapana, siko huko na sijawahi kuwepo. But nikihitaji intelijensia kuhusu masuala ya Afrika Mashariki najua naipataje… wale mlioko kwenye group nadhani mnafahamu vitu ambavyo mara kadhaa huwa najadili kule kuhusu masuala ya ulinzi na usalama hapa Afrika Mashariki.



Anyways… hiki ndicho kilitokea na sababu kwa nini mpaka sasa nashindwa kutoa kitabu. Ningeweza kutoa kitabu kwa kuondoa makala hizo mbili but nahisi ule ‘umaalumu’ wa kitabu utaondoka. Kwa hiyo bado nakomaa, maana kuna watu wapya pale sasa hivi naamini tutaenda sawa…na mimi mtiifu sana kwa nchi yangu, nawasubiri wao wanipe go ahead ndio nikitoe...



Sikutaka kusema haya muda wote huu maana JF imejaa wajuaji na ungeibuka mjadala ambao hauna maana wala tija… but imebidi niseme maana naona kama hapo juu kuna comment nyingi sana kuhusu kitabu na kwa nini sikitoi wakati nilishatangaza.






Bold - 0718096811

To Infinity and Beyond
 
SEHEMU YA NANE



Nifah Divine... glory to yhwh BansenBurner Alisen Papushikashi Magazine Fire miss chagga SANCTUS ANACLETUS mngony Excel Mussolin5 Jimena Inferiority Complex gwijimimi wambura marwa Hoshea shareef conscious wambeke The Boss Deejay nasmile gkileo Juma chief Mangi flani hivi Ngongo makaveli10 KENZY kadada wa pili Root aretasludovick jonnie_vincy Clkey KAFA.cOm mbewe makedonia Afande Nyati peterchoka Leonard Robert Nchi Kavu STUNTER Chrizo jully Van persie Khalidoun Tetramelyz punje haradari Mazigazi @Alybaba babu na mjukuu platozoom jimmyfoxxgongo Nicodemas Tambo Mwikozi Ls man Heaven Sent sifongo Infantry Soldier haa mym 20acres MTS MarkHilary compos Tembo2 Erick the future nancy1983 Bulah binsaad Fazzaly the wolf everhurt Melvine Mgibeon kijana wa leo samsun Coolant Jagood pacesetter apologize payton George Betram kisengeli Kiranga Jiwe Linaloishi Madame B jay john Guasa Amboni Dinazarde Analyse Diva Beyonce snowhite Mmanu Expected Value onechromosome Missy rose Innocenthezron Immortal_MH Ficus sunola Robot la Matope mamaafacebook II JEKI likikima Compact scorpio me G'taxi YNWA adna yuzo ntamaholo Otorong'ong'o naan ngik-kundie kandukamo1 AFRICA101 mwalidebe Kobe Blaki Womani kalendi savius The Great Emanuel r2ga Ntaluke.N. Transcend Msemachochote Mchumiajuone mwampepec MTOTO WA KUKU Fukara proto cute kawombe zinginary MLALUKO JR Vupu barafu BlackPanther Ntuzu Matola impongo ntamaholo Mkoroshokigoli Deadbody KING easy mahoza Msolo kkenzki deborah1 KIDUDU buffalo44 winlicious riziki Allys MUHUNZI Moses2015 nacktary Liuumi dochivele Renzo @barbers hmjamii mbere TATIANA famicho LUCKDUBE mwanadome Straton memphis ghazar Graph Theory Honey Faith Shunie Slave ddcmanesto zinginary pacesetter Nkanaga KOMUGISHA mikatabafeki johnsonmgaya lee empire wigo MJINI CHAI Asprin mtzmweusi Erasto kalinga Chrizo kichakaa man LULU bike FORTALEZA poleni shibumi ZE DONE umande Edger Sr sir joshua sammoo Roram Password Bavaria hambiliki mwanangu Asili100 Evarist Massawe nice1 Jumong S Rogie 1babake nasreen uberito baest dustless Kilemachocho Tumosa mtembea kwa miguu Debbs Joe scorpnose musacha shibumi seeker of knowledge Simuchi Veni Vidi Vici TUJITEGEMEE abuu garcia Hon Nkundwe Festo Festo marion09 mike2k The dream bro kay vandelintz kirikou1 POINT LOAD lusaka city Dirham Rodcones bato MANCNOO multiphill90 GEORGE Dalali mwanamalundi90 MwaFreeca Roram Ta-kibombo troublemaker mambo KOMUGISHA calabocatz Papaa Azonto Msemachochote Mdomo bakuli tizo1 option dikembe iL Buono fakalava ABDUL KAREEM @Gobe Justine Marack Goodluck Mchika MR UNINFORMED darcity nkasoukumu nG'aMBu thatonegAl kabanga MPARE KIBOGOYO Edward Sambai Rassa mnonje srinavas last king of uscoch proto cute Kennedy krava Rais2020 kbosho Mzee wa BsN sam2000 fuma 999 Bableee dawa yenu The Certified DON SINYORI mij addenbwii ONTARIO Kobe The Vein Mondray jaxonjaxon successor mzee wa liver sawariya Sitaki ukuda Domhome Mpatanishi MKANDAHARI mtugani wa wapi huyo wealthier cluecell Toyota escudo mgumu2 troublemaker Linamo shedede kamtu33 SteveMollel ngushi Donald stewart Mshuza2 Glycel mnonje Ochuanilove SingleFather Santi DEOD 360 ngushi anatory antony ukhuty chris van chicha auxillius Goma Son Hubeb pes KING DUBU VILLAIN mwayena donbeny Aleppo JipuKubwa shoo61 BOMBAY John mungo Nyakageni bato Dogo 1 sufra chamlungu painscott wegman Bravo Engliash MOSELBAY wa stendi FaizaFoxy bigmind cadabraa Internal Kelvin mwalukas mnonje Kelvin X Somoche Wgr30 Miiku Poise Jabman kalamuyamwalimu BOMBAY the say juxhb witnessj Gide MK Mmanyema mgogoone Mnongane Mandingo koncho77 afsa ngaboru Paradoxer Heavy Metal KIMBURU 06 Raaj kichekoh ngumba njeche kikale DullahTza Goodluck Mshana julius Darcy Denis Kasekenya mashonga kitalembwa Khaleed Shaban middle east SirChief jiwe jeusi Mkambarani mansakankanmusa gambada ynwa ney kush mossad 03 white wizard xtaper Mzigua90 Ollachuga Oc Gidbang Mateja M.G Yango jipu abaa4all DIBAJI Agenda1 Grahnman The MaskmaN Slim5 Xubzero agprogrammer JoJiPoJi Architectus blance86 Mamtolo monde arabe Ngao Ya Imani stardust JK naiman64 Dharra seledunga ABB SHAMMA Richard Waziri wa Kaskazini Mwinjuma1 Kanungila Karim baracuda Mwamba028 besaro Pyepyepye Bilionea Asigwa ibn Kiti Chema Tugas Royal Warrior mederii mmangO manzi james LIKUD adrenaline Royal Son Mhadzabe salaniatz Natasha Ismail jiwe jeusi chibalangunamchezo
John Mloy conjuget Van Pauser great G Mtoto wa nzi Zeus1 hindustan Sci-Fi MAN OF PEACE kashata emnly danny baraka bb MTOTELA kbosho TEMLO DA VINCA
 
Kuhusu ishu ya Vitabu...



Noana kuna jambo nasisitizwa sana, VITABU.

Niliwahi kutangaza kutoa kitabu lakini sijawapa tena update yeyote.



Kuna changamoto imetokea na nilikuwa sitaki kuizungumzia ndio maana kwa mwaka mzima sijasema chochote kuhusu kile kitabu ambacho niliwapostia mpaka picha yake kwamba tayari kinachpwa. Lakini nadhani ni vyema nilisemee mara moja ili walau mnielewe nini kimetokea…

Ni kwamba kwenye kile kitabu kuna hii makala ya ya Ujasusi Sebuleni Kwetu na makala ya The Richest Man. Hizi makala zote zinahusu masuala ya kiusalama hapa Afrika Mashariki.

Nadhani mnaona hali za kiuslama hapa katikati ilikuwa tete kidogo Afrika Mashariki… Kuna mabwana wakubwa wanahisi kwamba hizo makala zina taarifa sensitive na kwamba si vyema zikienda public... so kitabu kikapigwa stop kabla ya kuuza hata nakala moja. Nikafosi kutoa nakala mia moja tu na kuwapa watu waliopo kwenye group langu whatsapp kwa masharti. But sijawahi kumpatia mtu mwingine yeyote nje ya hao na ndio maana hata humu sijawahi kuwaeleza kinapatikanaje.







Taarifa gani hizo sensitive? Wajua, mie humu JF nikionana akiana 'chogo' wanakuja kubeza sijui oooh hii iko google sijui nini nini... huwa nawaangalia nabaki nacheka tu hiiiiiiii... ubaya tumekutana tu hapa JF hakuna anayejua undani wa mwenzake.



Niseme tu kwa haya masuala ya intelijensia Afrika Mashariki nina access ya kupata taarifa kubwa ambazo hata haziko mitandaoni au mtaani. Na kwa kusema hivyo sitaki kumaanisha kwamba labda mie niko pale Oysterbay/K.nyama... hapana, siko huko na sijawahi kuwepo. But nikihitaji intelijensia kuhusu masuala ya Afrika Mashariki najua naipataje… wale mlioko kwenye group nadhani mnafahamu vitu ambavyo mara kadhaa huwa najadili kule kuhusu masuala ya ulinzi na usalama hapa Afrika Mashariki.



Anyways… hiki ndicho kilitokea na sababu kwa nini mpaka sasa nashindwa kutoa kitabu. Ningeweza kutoa kitabu kwa kuondoa makala hizo mbili but nahisi ule ‘umaalumu’ wa kitabu utaondoka. Kwa hiyo bado nakomaa, maana kuna watu wapya pale sasa hivi naamini tutaenda sawa…na mimi mtiifu sana kwa nchi yangu, nawasubiri wao wanipe go ahead ndio nikitoe...



Sikutaka kusema haya muda wote huu maana JF imejaa wajuaji na ungeibuka mjadala ambao hauna maana wala tija… but imebidi niseme maana naona kama hapo juu kuna comment nyingi sana kuhusu kitabu na kwa nini sikitoi wakati nilishatangaza.
 
ROMAN ABRAMOVICH: UTAJIRI WA DAMU, RISASI NA UMAFIA









SEHEMU YA NANE







Hakuna kitu kizuri kama kiongozi ambaye anaweza kujitathimini na kukubali mapungufu yake na kukubali kukaa pembeni kupisha wengine. Mtu wa namna hii hata kama kuna madudu aliyafanya unajikuta unapata nafasi ya kumsamehe moyoni.

Licha ya mapungufu yake yote na vituko juu ya vimbwnga alivyovifanya kuidharaulisha Russia, lakini ulipofika wakati na kuelezwa ukweli kwamba ni muda muafaka akae pembeni kupisha mtu mwingine, Boris Yeltsin hakuifanya shingo yake kuwa ngumu.



Roman Abramovich akakutana na ma-oligarch wenzake. Akawapa pendekezo lake la nani anadhani anafaa kuwa rais mpya wa Russia. Akaweka sababu zake mezani… ma-oligarch wakakubaliana naye.



Nilieleza kwamba wale wanaojiita ‘The Family’ ambao ni ma-oligarch na wanafamilia ya Yeltsin kimsingi ndio ambao walikuwa wanaendsha nchi. Na ndani ya The Family kulikuwa na ule ‘Utatu Mtakatifu’… Abramovich, Tatyana na Yumachev. Na katika kipindi hiki Abramovich alikuwa na nguvu ya ushawishi kwa Yeltsin kuwazidi wote hata ndani ya The Family na Utatu Mtakatifu.

Kwa hiyo ulipofika wakati wa kuzungumza suala hili zito na Yeltsin… ni Abramovich pekee yake… yeye na Yeltsin pekee walijifungia ofisini na ‘kuyajenga’.

Kwanza Abramovich alimueleza Yeltsin kwa nini huu ni muda muafaka yeye kukaa pembeni na kumpisha kiongozi mpya. Baada ya Yeltsin kuukubaliana na hili, Abramovich akamueleza kuhusu pendekezo la mrithi wake. Abramovich akamueleza kwamba anapendekeza Vladimir Vladimirovich Putin, Mkurugenzi Mkuu wa FSB aanze kuandaliwa kurithi kiti hicho cha Urais. Kama ambavyo aliwafafanulia ma-oligarch ndivyo pia ambavyo alimfafanulia Rais Boris Yeltsin.



Tarehe 9 August mwaka 1999 Rais Boris Yeltsin alimteua Vladimir Putin kuwa Naibu wa Kwanza wa Waziri Mkuu. Yaani kipindi hicho ilikuwa kunakuwa na Waziri Mkuu alafu anakuwa na Manaibu watatu au wawili. Yaani mfano mzuri kama Zanzibar walivyo na ‘Makamu wa Kwanza na Makamu wa Pili wa Rais’. Kwa hiyo Putin aliteuliwa kuwa Naibu wa Kwanza wa Waziri Mkuu wa Russia. Nimeeleza kwamba kipindi hiki Russia ilikuwa kwenye mparaganyiko fulani hivi wa kimfumo. Wakati Putin alikuwa anateuliwa kuwa Naibu wa Kwanza wa Waziri Mkuu lakini nafasi ya Waziri Mkuu ilikuwa wazi. Ndani ya muda wa chini ya miezi kumi na tatu, walikuwa wameteuliwa Mawaziri Wakuu wane tofauti na kufukuzwa. Uteuzi huu wa Putin kuwa Naibu wa Kwanza wa Waziri mkuu ulitangazwa asubuhi ya tarehe hiyo 9… lakini ajabu sana ilipofika majira ya jioni siku hiyo hiyo Putin aliteuliwa kuwa Waziri Mkuu wa Russia.





Mkakati… Abramovich… Abracadabra…



Uteuzi wa Putin kuwa Waziri Mkuu mwanzoni haukushitua sana watu japokuwa hakuwa na umaarufu kwa wanasiasa wala wananchi kwa sababu kama ambavyo nimeeleza kuwa kwa muda wa kama miezi kumi na tatu tu tayari kulikuwa na Mawaziri Wakuu wane walioteuliwa na kufutwa kazi. Kwa hiyo watu walikuwa wanamuhesabia siku tu Putin kabla yay eye pia ‘kutumbuliwa’… ni kama vile hapa kwetu nchini, ukiteuliwa kuongoza Wizara ya Maliasili na Utalii au Wizara ya Nishati na Madini… watu wanakuhesabia miezi tu.



Lakini siku tatu tu baada ya uteuzi wa Putin, Rais Boris Yeltsin alifanya kitu cha tofauti kulinganisha na Mawaziri Wakuu waliopita ambao aliwahi kuwateua. Katika hotuba yake kwa wananchi alitamka kwamba anatamani Putin awe mrithi wake wa kiti cha Urais siku akiondoka kwenye cheo hicho… wenye kusoma alama za nyakati wakaelewa nini kilikuwa kinaendelea. Hii haikuwa ile ‘teau kisha fukuza’. Putin alikuwa anaandaliwa kuchukua nchi.



Kwa hiyo wapinzania wa Yeltsin au tuseme wapinzani wa ‘The Family’ wakaanza kujipanga kuzuia hicho ambacho kilikuwa kinataka kutokea. Iikuwa wazi kwamba Yeltsin amebakiza muda mchache madarakani, kwa wapinzani wa ma-oligarch hii ilikuwa habari njema kwao kwamba walau sasa na wao watapata zamu yao kufaidi mema ya nchi. Lakini baada ya kauli ya Yeltsin kwamba anatamani kurithiwa kiti cha Urais na Putin walielewa kwamba huu ulikuwa ni mkakati wa kuanza kumnadi Putin kwa wananchi. Kwahiyo nao wakaanza mipango ya kukwamisha suala hilo lisifanikiwe.



Sasa,

nimeeelza kwenye sehemu zilizopita kwamba Yeltsin alikuwa na upinzani mkubwa sana kwa wanasiasa wengine. Upinzani huu ulikuwa na historia ndefu hata kabla hajaanza kuwalimbikizia mali ma-oligarch.



Tutazame kidogo kwa ufupi sana… Shirikisho la Russia lilivunjika December, 1991. Kama mwezi mmoja hivi baadae, yaani January, 1992 Rais Yeltsin alianzisha program mpya kukabiliana na hali ya mbaya ya kiuchumi ambayo ilisababishwa na kuvunjika kwa Shirikisho la Russia. Badala ya program ile kusaidia badala yake ilifanya hali ya kiuchumi kuwa mbaya zaidi. Yeltsin alipingwa vikali mno kwa sera hizo mpya ambazo alizianzisha kiasi kwamba mpaka makamu wake wa Rais alikuwa anazikosoa hadharani kabisa. Likatokea wimbi la wanasiasa wengi hata wa chama chake kujiweka mbali na Yeltsin na kujipambanua kupinga sera hizo mpya za kiuchumi za Yeltsin. Matokeo yake ni kwamba Yeltsin alikuwa akipeleka miswada au mapendekezo Bungeni ili yapitishwe yalikuwa yanakwamishwa makusudi ili kumkata makali ya kutekeleza sera zake za kiuchumi. Kipindi hicho Bunge la Russia lilikuwa linaitwa “Supreme Soviet”. Baada ya mvutano wa muda mrefu kati ya Yeltsin na Bunge hatimaye Yeltsin akatangaza kulivunja Bunge. Sasa katiba ya Russia kipindi hicho ilikuwa haimpi mamlaka Rais kulivunja Bunge, kwa hiyo wabunge wakagoma na wakawa wanaendelea na shughuli za kibunge. Yeltsin akaingiza vifaru vya kijeshi kwenye viwanja vya bungeni kutaka kuwatoa wabunge kwa lazima. Wabunge wakagoma… wafuasi wao wakaandamana mitaani pale Moscow… kukatokea mapigano makali kati ya wananchi waliokuwa wanaunga mkono bunge dhidi ya wafuasi wa Yeltsin na jeshi. Inakadiriwa karibia watu 1,500 walipoteza maisha kwenye yale mapigano na kuyafanya kuwa moja ya tukio baya zaidi kwenye historia ya Russia.



Loh.! Nanogewa nichambue zaidi historia hii ya Russia… but let’s cut a long story short. Mapigano yale yalidumu kwa muda wa kama wiki mbili hivi kabla ya Rais Yeltsin na Bunge kufikia muafaka. Bunge walimpa masharti kadhaa ili waendelee kufanya naye kazi ‘smoothly’ na yeye Rais Yeltsin akatoa matakwa yake.

Moja ya makubaliano makuu ilikuwa ni kuunda upya mfumo wa Bunge la ‘Supreme Soviet’. Yeltsin alihisi kwamba Bunge lilikuwa limepewa mamlaka makubwa mno kutokana na mfumo wa kijamaa ambao ulikuwa unatumika kuendesha nchi huko nyuma. Chini ya mfumo huu mpya, kwanza ‘supreme soviet’ litavunjwa na kuundwa ‘Federal assembly’ ambayo itakuwa na ‘chamber’ mbili. Kutakuwa na ‘Lower House’ kwa jina State Duma (au GosDumas kama warusi wenyewe wanavyooita), na pia kutakuwa na ‘Upper House’ kwa jina la Council of the Federation. (Mfumo huu bado ungali unatumika mpaka sasa).



Kwanini nimegusia historia hii? Kuna vitu viwili ambavyo nataka uvione… kwanza ni uhasama wa Bunge na rais Yeltsin kwani hata baada ya mfumo mpya kuwekwa Bunge bado lilikuwa na kinyongo naye kutokana na kile ambacho kilitokea.

Na jambo la pili nataka tufahamu kwamba ile lower house ya Bunge (State Duma) ndiyo ambayo ilikuwa na malamlaka ya kumthibitisha Waziri Mkuu mara baada ya kuteuliwa na Rais.



Sasa,



Bada ya kauli ya Yeltsin kwamba anatamani Putin awe mrithi wake wa kiti cha Urais, wapinzani wa ‘The Family’ wakaanza kampeni ya chini kwa chini kushawishi wabunge wa GosDumas kumpiga chini Putin.



Putin alikuwa anahitaji kura 226 ili kuthibitishwa kuwa Waziri Mkuu.



Kambi ya Yeltsin ikagundua njama hii na mara moja wakaanza kuifanyia kazi. Wanasema pesa sabuni ya roho… haijalishi ni kabila gani au nchi gani… pesa inaweza kubadili moyo wa binadamu. Ma-oligarch wakaingia kazini kumwaga fedha kwa wabunge wa GosDuma.

Siku ya August 16 kura zilipopigwa Putin aliponea chupu chupu kwa kupata kura 233. Kura saba tu zaidi.



Kwa hiyo rasmi sasa Putin alikuwa ni waziri Mkuu wa Russia.



Hatua ambayo ilikuwa inafuata ilikuwa ni kumjenga Putin kwenye mioyo ya wananchi. Kama ambavyo nimeeleza… vyombo vya habari vyote vilikuwa vinamilikiwa na ma-oligarch. Kwa hiyo kila siku vilikuwa vinaandaliwa vipindi malumu vya redio na televisheni… makala kwenye magazeti na makongamano na mikutano ya hadhara… vyote kumuhusu Vladimir Putin.

Lakini moja ya matukio ambayo yalisaidia kumuweka Putin kwenye mioyo ya warusi ilikuwa ni namna ambavyo alishughulikia tafrani ambayo ilitokana na kulipuka kwa mabomu kwenye nyumba za kupanga kwenye miji mitatu nchini urusi… tukio ambalo linajulikana kwa jina maarufu la ‘Russia Appartment Bombings’. Tukio ambalo lilizua hofu kubwa ndani ya Urusi. Putin alionyesha ukakamavu wa hali ya juu na umahiri kulishughulikia suala hilo mpaka mwisho. Lakini pia Putin aliwakosha warusi kwa msimamo wake thabiti juu ya vita waliyokuwa wanaipigana Chechenya.



Miezi mitatu baadae, yaani mwezi December 1999 Rais Boris Yeltsin alijiuzulu ghafla na kwa mujibu wa katiba ya Rusia Waziri Mkuu ndiye anachukua nafasi yake na kuikaimu mpaka uchaguzi mkuu uitishwe.



Yeltisn alijiuzulu tarehe 31 December 1999… siku hiyo hiyo Putin akatangazwa kuwa Kaimu Rais wa Russia. Na siku hiyo hiyo akasaini ‘decree’ ya kwanza na muhimu sana kwenye historia ya Urusi. Decree hii ilikuwa na kichwa kinachosema, “On Guarantees of former President of the Russian federation and members of his family”. Decree hii iikuwa inatoa kinga kwa Rais Yeltsin na wanafamilia wake wote kwamba hawatashtakiwa kwa makosa yoyote yale kama ikionekana labda kulikuwa na makosa yoyote ambayo yalitendeka kipindi cha Urais wa Yeltsin.

Na hii ilikuwa ni moja ya makubaliano kati ya Yeltsin na Abramovich kwa niaba ya ma-oligarch wenzake walipomtaka aachie ngazi… alitaka ahakikishiwe kwamba mali zake hatopokonywa na kamwe asishtakiwe.



Miezi mitatu baadae, Putin aliitisha uchaguzi mkuu ambao alishinda kiulaini kabisa. Tarehe 7 May 2000, Vladimir Vladimirovich Putin alikula kiapo kuwa Rais wa Russia.



Kazi ilikuwa imekamilika…. Abramovich… abracadabra.!!



Swahiba wake ambaye ‘amemfinyanga’ kwa mikono yake na kumtengenezea njia sasa alikuwa amekalia kiti cha urais wa nchi.



Kuna kitabu kitakatifu kinasema “tunakua kutoka utukufu mpaka utukufu”. Na haswaaa, hii ndio hulka yetu binadamu… haijalishi tuko kileleni kiasi gani… siku zote tunataka kuipanda ngazi inayofuata. Hata uwe na kikubwa kiasi gani, nafsini tunaona tulichanacho bado hakitoshi… haijalishi tunacho kingi kiasi gani. Tunatamani, tunatafuta, tunakipata alafu tunataka zaidi… wanadamu tumeumbwa na kiu ya “kukua kutoka utukufu mpaka utukufu”.



Huu sasa ulikuwa ni wakati wa Abramovich kuhamia katika hatua ya pili ya ndoto zake… ndoto kubwa zaidi. Unaweza kudhani kumiliki Sibneft kampuni kubwa zaidi ya kuzalisha mafuta nchini Russia ilikuwa inatosha.. la hasha… Roman Abramovich alikuwa anataka zaidi, na alichikuwa anakitaka safari hii kilikuwa kimono zaidi pale Russia.. Abrfamovich alikuwa anataka kujimilikisha sekta ya Aluminum ndani ya nchi ya Russia. Sekta yenye utajiri mkubwa zaidi nchini Russia lakini pia ikiwa ni sekta hatari zaidi.

Kuingia kwa Abramovich kwenye sekta hii kutakuja kuibua moja ya nyakati za hatari zaidi kuwahi kushuhudiwa nchini Russia na Ulaya mashsriki yote kiasi kwamba mpaka leo hii kipindi hicho kinajulikana kama nyakati za ‘Vita za Aluminum’.



Tutajadili…





Bold

To Infinity and Beyond
Nimekusoma Origacha mkubwa
 
Siku moja nilikaa na rafiki yangu mmoja, mara akaja mlevi mmoja akaanzisha mazungumzo na yule rafiki yangu lakini wakati wote wa mazungumzo yao yule mlevi alionesha utulivu wa hali ya juu sana. Sasa wakati wanaagana yule rafiki yangu akamuuliza yule mlevi `utamwambia nani kakutuma?´ (alitumwa apeleke salamu mahali) akasema nimetumwa na yule AFISA USALAMA!
 
Kuhusu ishu ya Vitabu...



Noana kuna jambo nasisitizwa sana, VITABU.

Niliwahi kutangaza kutoa kitabu lakini sijawapa tena update yeyote.



Kuna changamoto imetokea na nilikuwa sitaki kuizungumzia ndio maana kwa mwaka mzima sijasema chochote kuhusu kile kitabu ambacho niliwapostia mpaka picha yake kwamba tayari kinachpwa. Lakini nadhani ni vyema nilisemee mara moja ili walau mnielewe nini kimetokea…

Ni kwamba kwenye kile kitabu kuna hii makala ya ya Ujasusi Sebuleni Kwetu na makala ya The Richest Man. Hizi makala zote zinahusu masuala ya kiusalama hapa Afrika Mashariki.

Nadhani mnaona hali za kiuslama hapa katikati ilikuwa tete kidogo Afrika Mashariki… Kuna mabwana wakubwa wanahisi kwamba hizo makala zina taarifa sensitive na kwamba si vyema zikienda public... so kitabu kikapigwa stop kabla ya kuuza hata nakala moja. Nikafosi kutoa nakala mia moja tu na kuwapa watu waliopo kwenye group langu whatsapp kwa masharti. But sijawahi kumpatia mtu mwingine yeyote nje ya hao na ndio maana hata humu sijawahi kuwaeleza kinapatikanaje.







Taarifa gani hizo sensitive? Wajua, mie humu JF nikionana akiana 'chogo' wanakuja kubeza sijui oooh hii iko google sijui nini nini... huwa nawaangalia nabaki nacheka tu hiiiiiiii... ubaya tumekutana tu hapa JF hakuna anayejua undani wa mwenzake.



Niseme tu kwa haya masuala ya intelijensia Afrika Mashariki nina access ya kupata taarifa kubwa ambazo hata haziko mitandaoni au mtaani. Na kwa kusema hivyo sitaki kumaanisha kwamba labda mie niko pale Oysterbay/K.nyama... hapana, siko huko na sijawahi kuwepo. But nikihitaji intelijensia kuhusu masuala ya Afrika Mashariki najua naipataje… wale mlioko kwenye group nadhani mnafahamu vitu ambavyo mara kadhaa huwa najadili kule kuhusu masuala ya ulinzi na usalama hapa Afrika Mashariki.



Anyways… hiki ndicho kilitokea na sababu kwa nini mpaka sasa nashindwa kutoa kitabu. Ningeweza kutoa kitabu kwa kuondoa makala hizo mbili but nahisi ule ‘umaalumu’ wa kitabu utaondoka. Kwa hiyo bado nakomaa, maana kuna watu wapya pale sasa hivi naamini tutaenda sawa…na mimi mtiifu sana kwa nchi yangu, nawasubiri wao wanipe go ahead ndio nikitoe...



Sikutaka kusema haya muda wote huu maana JF imejaa wajuaji na ungeibuka mjadala ambao hauna maana wala tija… but imebidi niseme maana naona kama hapo juu kuna comment nyingi sana kuhusu kitabu na kwa nini sikitoi wakati nilishatangaza.
Safi 😀😀😀
 
Kuhusu ishu ya Vitabu...



Noana kuna jambo nasisitizwa sana, VITABU.

Niliwahi kutangaza kutoa kitabu lakini sijawapa tena update yeyote.



Kuna changamoto imetokea na nilikuwa sitaki kuizungumzia ndio maana kwa mwaka mzima sijasema chochote kuhusu kile kitabu ambacho niliwapostia mpaka picha yake kwamba tayari kinachpwa. Lakini nadhani ni vyema nilisemee mara moja ili walau mnielewe nini kimetokea…

Ni kwamba kwenye kile kitabu kuna hii makala ya ya Ujasusi Sebuleni Kwetu na makala ya The Richest Man. Hizi makala zote zinahusu masuala ya kiusalama hapa Afrika Mashariki.

Nadhani mnaona hali za kiuslama hapa katikati ilikuwa tete kidogo Afrika Mashariki… Kuna mabwana wakubwa wanahisi kwamba hizo makala zina taarifa sensitive na kwamba si vyema zikienda public... so kitabu kikapigwa stop kabla ya kuuza hata nakala moja. Nikafosi kutoa nakala mia moja tu na kuwapa watu waliopo kwenye group langu whatsapp kwa masharti. But sijawahi kumpatia mtu mwingine yeyote nje ya hao na ndio maana hata humu sijawahi kuwaeleza kinapatikanaje.







Taarifa gani hizo sensitive? Wajua, mie humu JF nikionana akiana 'chogo' wanakuja kubeza sijui oooh hii iko google sijui nini nini... huwa nawaangalia nabaki nacheka tu hiiiiiiii... ubaya tumekutana tu hapa JF hakuna anayejua undani wa mwenzake.



Niseme tu kwa haya masuala ya intelijensia Afrika Mashariki nina access ya kupata taarifa kubwa ambazo hata haziko mitandaoni au mtaani. Na kwa kusema hivyo sitaki kumaanisha kwamba labda mie niko pale Oysterbay/K.nyama... hapana, siko huko na sijawahi kuwepo. But nikihitaji intelijensia kuhusu masuala ya Afrika Mashariki najua naipataje… wale mlioko kwenye group nadhani mnafahamu vitu ambavyo mara kadhaa huwa najadili kule kuhusu masuala ya ulinzi na usalama hapa Afrika Mashariki.



Anyways… hiki ndicho kilitokea na sababu kwa nini mpaka sasa nashindwa kutoa kitabu. Ningeweza kutoa kitabu kwa kuondoa makala hizo mbili but nahisi ule ‘umaalumu’ wa kitabu utaondoka. Kwa hiyo bado nakomaa, maana kuna watu wapya pale sasa hivi naamini tutaenda sawa…na mimi mtiifu sana kwa nchi yangu, nawasubiri wao wanipe go ahead ndio nikitoe...



Sikutaka kusema haya muda wote huu maana JF imejaa wajuaji na ungeibuka mjadala ambao hauna maana wala tija… but imebidi niseme maana naona kama hapo juu kuna comment nyingi sana kuhusu kitabu na kwa nini sikitoi wakati nilishatangaza.
Untumia jina gn insta bg bro?
 
ROMAN ABRAMOVICH: UTAJIRI WA DAMU, RISASI NA UMAFIA









SEHEMU YA NANE







Hakuna kitu kizuri kama kiongozi ambaye anaweza kujitathimini na kukubali mapungufu yake na kukubali kukaa pembeni kupisha wengine. Mtu wa namna hii hata kama kuna madudu aliyafanya unajikuta unapata nafasi ya kumsamehe moyoni.

Licha ya mapungufu yake yote na vituko juu ya vimbwnga alivyovifanya kuidharaulisha Russia, lakini ulipofika wakati na kuelezwa ukweli kwamba ni muda muafaka akae pembeni kupisha mtu mwingine, Boris Yeltsin hakuifanya shingo yake kuwa ngumu.



Roman Abramovich akakutana na ma-oligarch wenzake. Akawapa pendekezo lake la nani anadhani anafaa kuwa rais mpya wa Russia. Akaweka sababu zake mezani… ma-oligarch wakakubaliana naye.



Nilieleza kwamba wale wanaojiita ‘The Family’ ambao ni ma-oligarch na wanafamilia ya Yeltsin kimsingi ndio ambao walikuwa wanaendsha nchi. Na ndani ya The Family kulikuwa na ule ‘Utatu Mtakatifu’… Abramovich, Tatyana na Yumachev. Na katika kipindi hiki Abramovich alikuwa na nguvu ya ushawishi kwa Yeltsin kuwazidi wote hata ndani ya The Family na Utatu Mtakatifu.

Kwa hiyo ulipofika wakati wa kuzungumza suala hili zito na Yeltsin… ni Abramovich pekee yake… yeye na Yeltsin pekee walijifungia ofisini na ‘kuyajenga’.

Kwanza Abramovich alimueleza Yeltsin kwa nini huu ni muda muafaka yeye kukaa pembeni na kumpisha kiongozi mpya. Baada ya Yeltsin kuukubaliana na hili, Abramovich akamueleza kuhusu pendekezo la mrithi wake. Abramovich akamueleza kwamba anapendekeza Vladimir Vladimirovich Putin, Mkurugenzi Mkuu wa FSB aanze kuandaliwa kurithi kiti hicho cha Urais. Kama ambavyo aliwafafanulia ma-oligarch ndivyo pia ambavyo alimfafanulia Rais Boris Yeltsin.



Tarehe 9 August mwaka 1999 Rais Boris Yeltsin alimteua Vladimir Putin kuwa Naibu wa Kwanza wa Waziri Mkuu. Yaani kipindi hicho ilikuwa kunakuwa na Waziri Mkuu alafu anakuwa na Manaibu watatu au wawili. Yaani mfano mzuri kama Zanzibar walivyo na ‘Makamu wa Kwanza na Makamu wa Pili wa Rais’. Kwa hiyo Putin aliteuliwa kuwa Naibu wa Kwanza wa Waziri Mkuu wa Russia. Nimeeleza kwamba kipindi hiki Russia ilikuwa kwenye mparaganyiko fulani hivi wa kimfumo. Wakati Putin alikuwa anateuliwa kuwa Naibu wa Kwanza wa Waziri Mkuu lakini nafasi ya Waziri Mkuu ilikuwa wazi. Ndani ya muda wa chini ya miezi kumi na tatu, walikuwa wameteuliwa Mawaziri Wakuu wane tofauti na kufukuzwa. Uteuzi huu wa Putin kuwa Naibu wa Kwanza wa Waziri mkuu ulitangazwa asubuhi ya tarehe hiyo 9… lakini ajabu sana ilipofika majira ya jioni siku hiyo hiyo Putin aliteuliwa kuwa Waziri Mkuu wa Russia.





Mkakati… Abramovich… Abracadabra…



Uteuzi wa Putin kuwa Waziri Mkuu mwanzoni haukushitua sana watu japokuwa hakuwa na umaarufu kwa wanasiasa wala wananchi kwa sababu kama ambavyo nimeeleza kuwa kwa muda wa kama miezi kumi na tatu tu tayari kulikuwa na Mawaziri Wakuu wane walioteuliwa na kufutwa kazi. Kwa hiyo watu walikuwa wanamuhesabia siku tu Putin kabla yay eye pia ‘kutumbuliwa’… ni kama vile hapa kwetu nchini, ukiteuliwa kuongoza Wizara ya Maliasili na Utalii au Wizara ya Nishati na Madini… watu wanakuhesabia miezi tu.



Lakini siku tatu tu baada ya uteuzi wa Putin, Rais Boris Yeltsin alifanya kitu cha tofauti kulinganisha na Mawaziri Wakuu waliopita ambao aliwahi kuwateua. Katika hotuba yake kwa wananchi alitamka kwamba anatamani Putin awe mrithi wake wa kiti cha Urais siku akiondoka kwenye cheo hicho… wenye kusoma alama za nyakati wakaelewa nini kilikuwa kinaendelea. Hii haikuwa ile ‘teau kisha fukuza’. Putin alikuwa anaandaliwa kuchukua nchi.



Kwa hiyo wapinzania wa Yeltsin au tuseme wapinzani wa ‘The Family’ wakaanza kujipanga kuzuia hicho ambacho kilikuwa kinataka kutokea. Iikuwa wazi kwamba Yeltsin amebakiza muda mchache madarakani, kwa wapinzani wa ma-oligarch hii ilikuwa habari njema kwao kwamba walau sasa na wao watapata zamu yao kufaidi mema ya nchi. Lakini baada ya kauli ya Yeltsin kwamba anatamani kurithiwa kiti cha Urais na Putin walielewa kwamba huu ulikuwa ni mkakati wa kuanza kumnadi Putin kwa wananchi. Kwahiyo nao wakaanza mipango ya kukwamisha suala hilo lisifanikiwe.



Sasa,

nimeeelza kwenye sehemu zilizopita kwamba Yeltsin alikuwa na upinzani mkubwa sana kwa wanasiasa wengine. Upinzani huu ulikuwa na historia ndefu hata kabla hajaanza kuwalimbikizia mali ma-oligarch.



Tutazame kidogo kwa ufupi sana… Shirikisho la Russia lilivunjika December, 1991. Kama mwezi mmoja hivi baadae, yaani January, 1992 Rais Yeltsin alianzisha program mpya kukabiliana na hali ya mbaya ya kiuchumi ambayo ilisababishwa na kuvunjika kwa Shirikisho la Russia. Badala ya program ile kusaidia badala yake ilifanya hali ya kiuchumi kuwa mbaya zaidi. Yeltsin alipingwa vikali mno kwa sera hizo mpya ambazo alizianzisha kiasi kwamba mpaka makamu wake wa Rais alikuwa anazikosoa hadharani kabisa. Likatokea wimbi la wanasiasa wengi hata wa chama chake kujiweka mbali na Yeltsin na kujipambanua kupinga sera hizo mpya za kiuchumi za Yeltsin. Matokeo yake ni kwamba Yeltsin alikuwa akipeleka miswada au mapendekezo Bungeni ili yapitishwe yalikuwa yanakwamishwa makusudi ili kumkata makali ya kutekeleza sera zake za kiuchumi. Kipindi hicho Bunge la Russia lilikuwa linaitwa “Supreme Soviet”. Baada ya mvutano wa muda mrefu kati ya Yeltsin na Bunge hatimaye Yeltsin akatangaza kulivunja Bunge. Sasa katiba ya Russia kipindi hicho ilikuwa haimpi mamlaka Rais kulivunja Bunge, kwa hiyo wabunge wakagoma na wakawa wanaendelea na shughuli za kibunge. Yeltsin akaingiza vifaru vya kijeshi kwenye viwanja vya bungeni kutaka kuwatoa wabunge kwa lazima. Wabunge wakagoma… wafuasi wao wakaandamana mitaani pale Moscow… kukatokea mapigano makali kati ya wananchi waliokuwa wanaunga mkono bunge dhidi ya wafuasi wa Yeltsin na jeshi. Inakadiriwa karibia watu 1,500 walipoteza maisha kwenye yale mapigano na kuyafanya kuwa moja ya tukio baya zaidi kwenye historia ya Russia.



Loh.! Nanogewa nichambue zaidi historia hii ya Russia… but let’s cut a long story short. Mapigano yale yalidumu kwa muda wa kama wiki mbili hivi kabla ya Rais Yeltsin na Bunge kufikia muafaka. Bunge walimpa masharti kadhaa ili waendelee kufanya naye kazi ‘smoothly’ na yeye Rais Yeltsin akatoa matakwa yake.

Moja ya makubaliano makuu ilikuwa ni kuunda upya mfumo wa Bunge la ‘Supreme Soviet’. Yeltsin alihisi kwamba Bunge lilikuwa limepewa mamlaka makubwa mno kutokana na mfumo wa kijamaa ambao ulikuwa unatumika kuendesha nchi huko nyuma. Chini ya mfumo huu mpya, kwanza ‘supreme soviet’ litavunjwa na kuundwa ‘Federal assembly’ ambayo itakuwa na ‘chamber’ mbili. Kutakuwa na ‘Lower House’ kwa jina State Duma (au GosDumas kama warusi wenyewe wanavyooita), na pia kutakuwa na ‘Upper House’ kwa jina la Council of the Federation. (Mfumo huu bado ungali unatumika mpaka sasa).



Kwanini nimegusia historia hii? Kuna vitu viwili ambavyo nataka uvione… kwanza ni uhasama wa Bunge na rais Yeltsin kwani hata baada ya mfumo mpya kuwekwa Bunge bado lilikuwa na kinyongo naye kutokana na kile ambacho kilitokea.

Na jambo la pili nataka tufahamu kwamba ile lower house ya Bunge (State Duma) ndiyo ambayo ilikuwa na malamlaka ya kumthibitisha Waziri Mkuu mara baada ya kuteuliwa na Rais.



Sasa,



Bada ya kauli ya Yeltsin kwamba anatamani Putin awe mrithi wake wa kiti cha Urais, wapinzani wa ‘The Family’ wakaanza kampeni ya chini kwa chini kushawishi wabunge wa GosDumas kumpiga chini Putin.



Putin alikuwa anahitaji kura 226 ili kuthibitishwa kuwa Waziri Mkuu.



Kambi ya Yeltsin ikagundua njama hii na mara moja wakaanza kuifanyia kazi. Wanasema pesa sabuni ya roho… haijalishi ni kabila gani au nchi gani… pesa inaweza kubadili moyo wa binadamu. Ma-oligarch wakaingia kazini kumwaga fedha kwa wabunge wa GosDuma.

Siku ya August 16 kura zilipopigwa Putin aliponea chupu chupu kwa kupata kura 233. Kura saba tu zaidi.



Kwa hiyo rasmi sasa Putin alikuwa ni waziri Mkuu wa Russia.



Hatua ambayo ilikuwa inafuata ilikuwa ni kumjenga Putin kwenye mioyo ya wananchi. Kama ambavyo nimeeleza… vyombo vya habari vyote vilikuwa vinamilikiwa na ma-oligarch. Kwa hiyo kila siku vilikuwa vinaandaliwa vipindi malumu vya redio na televisheni… makala kwenye magazeti na makongamano na mikutano ya hadhara… vyote kumuhusu Vladimir Putin.

Lakini moja ya matukio ambayo yalisaidia kumuweka Putin kwenye mioyo ya warusi ilikuwa ni namna ambavyo alishughulikia tafrani ambayo ilitokana na kulipuka kwa mabomu kwenye nyumba za kupanga kwenye miji mitatu nchini urusi… tukio ambalo linajulikana kwa jina maarufu la ‘Russia Appartment Bombings’. Tukio ambalo lilizua hofu kubwa ndani ya Urusi. Putin alionyesha ukakamavu wa hali ya juu na umahiri kulishughulikia suala hilo mpaka mwisho. Lakini pia Putin aliwakosha warusi kwa msimamo wake thabiti juu ya vita waliyokuwa wanaipigana Chechenya.



Miezi mitatu baadae, yaani mwezi December 1999 Rais Boris Yeltsin alijiuzulu ghafla na kwa mujibu wa katiba ya Rusia Waziri Mkuu ndiye anachukua nafasi yake na kuikaimu mpaka uchaguzi mkuu uitishwe.



Yeltisn alijiuzulu tarehe 31 December 1999… siku hiyo hiyo Putin akatangazwa kuwa Kaimu Rais wa Russia. Na siku hiyo hiyo akasaini ‘decree’ ya kwanza na muhimu sana kwenye historia ya Urusi. Decree hii ilikuwa na kichwa kinachosema, “On Guarantees of former President of the Russian federation and members of his family”. Decree hii iikuwa inatoa kinga kwa Rais Yeltsin na wanafamilia wake wote kwamba hawatashtakiwa kwa makosa yoyote yale kama ikionekana labda kulikuwa na makosa yoyote ambayo yalitendeka kipindi cha Urais wa Yeltsin.

Na hii ilikuwa ni moja ya makubaliano kati ya Yeltsin na Abramovich kwa niaba ya ma-oligarch wenzake walipomtaka aachie ngazi… alitaka ahakikishiwe kwamba mali zake hatopokonywa na kamwe asishtakiwe.



Miezi mitatu baadae, Putin aliitisha uchaguzi mkuu ambao alishinda kiulaini kabisa. Tarehe 7 May 2000, Vladimir Vladimirovich Putin alikula kiapo kuwa Rais wa Russia.



Kazi ilikuwa imekamilika…. Abramovich… abracadabra.!!



Swahiba wake ambaye ‘amemfinyanga’ kwa mikono yake na kumtengenezea njia sasa alikuwa amekalia kiti cha urais wa nchi.



Kuna kitabu kitakatifu kinasema “tunakua kutoka utukufu mpaka utukufu”. Na haswaaa, hii ndio hulka yetu binadamu… haijalishi tuko kileleni kiasi gani… siku zote tunataka kuipanda ngazi inayofuata. Hata uwe na kikubwa kiasi gani, nafsini tunaona tulichanacho bado hakitoshi… haijalishi tunacho kingi kiasi gani. Tunatamani, tunatafuta, tunakipata alafu tunataka zaidi… wanadamu tumeumbwa na kiu ya “kukua kutoka utukufu mpaka utukufu”.



Huu sasa ulikuwa ni wakati wa Abramovich kuhamia katika hatua ya pili ya ndoto zake… ndoto kubwa zaidi. Unaweza kudhani kumiliki Sibneft kampuni kubwa zaidi ya kuzalisha mafuta nchini Russia ilikuwa inatosha.. la hasha… Roman Abramovich alikuwa anataka zaidi, na alichikuwa anakitaka safari hii kilikuwa kimono zaidi pale Russia.. Abrfamovich alikuwa anataka kujimilikisha sekta ya Aluminum ndani ya nchi ya Russia. Sekta yenye utajiri mkubwa zaidi nchini Russia lakini pia ikiwa ni sekta hatari zaidi.

Kuingia kwa Abramovich kwenye sekta hii kutakuja kuibua moja ya nyakati za hatari zaidi kuwahi kushuhudiwa nchini Russia na Ulaya mashsriki yote kiasi kwamba mpaka leo hii kipindi hicho kinajulikana kama nyakati za ‘Vita za Aluminum’.



Tutajadili…




Kuhusu ishu ya Vitabu...



Noana kuna jambo nasisitizwa sana, VITABU.

Niliwahi kutangaza kutoa kitabu lakini sijawapa tena update yeyote.



Kuna changamoto imetokea na nilikuwa sitaki kuizungumzia ndio maana kwa mwaka mzima sijasema chochote kuhusu kile kitabu ambacho niliwapostia mpaka picha yake kwamba tayari kinachpwa. Lakini nadhani ni vyema nilisemee mara moja ili walau mnielewe nini kimetokea…

Ni kwamba kwenye kile kitabu kuna hii makala ya ya Ujasusi Sebuleni Kwetu na makala ya The Richest Man. Hizi makala zote zinahusu masuala ya kiusalama hapa Afrika Mashariki.

Nadhani mnaona hali za kiuslama hapa katikati ilikuwa tete kidogo Afrika Mashariki… Kuna mabwana wakubwa wanahisi kwamba hizo makala zina taarifa sensitive na kwamba si vyema zikienda public... so kitabu kikapigwa stop kabla ya kuuza hata nakala moja. Nikafosi kutoa nakala mia moja tu na kuwapa watu waliopo kwenye group langu whatsapp kwa masharti. But sijawahi kumpatia mtu mwingine yeyote nje ya hao na ndio maana hata humu sijawahi kuwaeleza kinapatikanaje.







Taarifa gani hizo sensitive? Wajua, mie humu JF nikionana akiana 'chogo' wanakuja kubeza sijui oooh hii iko google sijui nini nini... huwa nawaangalia nabaki nacheka tu hiiiiiiii... ubaya tumekutana tu hapa JF hakuna anayejua undani wa mwenzake.



Niseme tu kwa haya masuala ya intelijensia Afrika Mashariki nina access ya kupata taarifa kubwa ambazo hata haziko mitandaoni au mtaani. Na kwa kusema hivyo sitaki kumaanisha kwamba labda mie niko pale Oysterbay/K.nyama... hapana, siko huko na sijawahi kuwepo. But nikihitaji intelijensia kuhusu masuala ya Afrika Mashariki najua naipataje… wale mlioko kwenye group nadhani mnafahamu vitu ambavyo mara kadhaa huwa najadili kule kuhusu masuala ya ulinzi na usalama hapa Afrika Mashariki.



Anyways… hiki ndicho kilitokea na sababu kwa nini mpaka sasa nashindwa kutoa kitabu. Ningeweza kutoa kitabu kwa kuondoa makala hizo mbili but nahisi ule ‘umaalumu’ wa kitabu utaondoka. Kwa hiyo bado nakomaa, maana kuna watu wapya pale sasa hivi naamini tutaenda sawa…na mimi mtiifu sana kwa nchi yangu, nawasubiri wao wanipe go ahead ndio nikitoe...



Sikutaka kusema haya muda wote huu maana JF imejaa wajuaji na ungeibuka mjadala ambao hauna maana wala tija… but imebidi niseme maana naona kama hapo juu kuna comment nyingi sana kuhusu kitabu na kwa nini sikitoi wakati nilishatangaza.






Bold - 0718096811

To Infinity and Beyond
Mkuu The bold,

Hongera sana kwa uandishi wa makala zako nzuri zenye kusisimua, kuburudisha, kuelimisha na kutafakarisha,

Ushauri wangu kwako Mimi kama mdogo wako ni kwamba, "Hakuna ulazima wa wewe kuweka wazi kuwa una access ya taarifa za kiusalama za hapa Afrika mashariki, wakati huo huo unafahamika kwa majina na mawasiliano yako, ni hatari sana lakini kwa sasa unaweza usilione hilo jambo"

Endelea kutupa vitu kimya kimya wakisema unatoa google hio ni nzuri zaidi sababu inamchanganya mtu kubaini vyanzo vyako vya maarifa.

Ahsante.
 
79 Reactions
Reply
Back
Top Bottom