Roho ni nini na ipo sehemu gani ya mwili?

Daaah mkuu unashusha nondo hatar yaan unaongea Ukweli wenyewe aise vitu vinatutokea kabsaa roho Huwa Inaumagaa Sana tena inakataa inasema huyu mtu achana nae akili nayo inagoma

Baadae unajutaa na kulia sanaa unasema nlisikia roho ikinikataza
Roho huweza kuona ambavyo macho ya mwili hayawezi kuona, hasa jambo au kitu kitakachotokea baadaye. Usishangae kuwa litakalotokea kesho roho yako inalijua leo!

Hata mke wa kuoa au mume wa kuolewa naye, unaweza kumfurahia kwa macho na kuvutiwa na kila kitu leo, lakini roho yako ikamkataa kabisa, na pengine kwa kuugua na kuumia sana jinsi unavyompenda wewe na akili yako, pasina kujua lolote.

Unaweza kushupaza shingo, lakini moto utakapoanza kuwaka ndani ya nyumba baada ya miaka kadhaa ya uvumilivu, utakumbuka na kuanza kusema: ndio maana roho ilisita, iligoma, iliuma, iliogopa, nk.; Inabaki kuwa majuto ni mjukuu!
 
Huwezi kuiona roho yako kwa macho kwa kuwa si mwili. Nikuulize kidogo ili uweze kunielewa: Je, umewahi kuuona upepo kwa macho? Hata kama hujawahi kuuona lakini sauti yake, matokeo au madhara yake, unayasikia na kuyaona kwa hakika.

Kwahiyo, uwepo wa kitu fulani si lazima ukione kwa macho. Hata sauti hujawahi kuziona lakini unazisikia kwa hakika!

Roho yako ndiyo wewe mwenyewe. Mwili ni koti tu lililoivaa roho, ikitoka unakuwa umekufa. Pia una nafsi (soul) ambayo hujumuisha akili (mind), hisia (emotions) na maamuzi (decisions). Nafsi hubeba utashi (conscience) ambao wanao watu tu, si wanyama.

Unafanya jambo lolote kwa utashi wako, kwa maamuzi yako na mtazamo au mapenzi yako. Tunu hiyo haipo kwa wanyama. Hata mnyama anapokunya hafikirii chochote - kunya kunamtokea tu popote!

Je, umewahi kutokewa ambapo unabishana na wewe mwenyewe? Akili yako inaamua kwenda mahali fulani, lakini ndani yako unasikia sauti ya chini inakukataza usiende! Ukiamua kwenda bila kuitii hiyo sauti ndani yako halafu ukapata shida huko uendako, utaanza kusema roho yangu ilinikataza! Roho yangu ilisita! Roho iligoma kwenda!

Kwahiyo, kila mtu ana sehemu tatu: Roho (spirit), Nafsi (soul) na Mwili wa damu, nyama, mifupa, nk (flesh). Kama hujanielewa nitafute ili nikupe ufafanuzi zaidi kadri Mungu atakavyonijaalia. Pia waweza kusoma 1 Thesalonike 5:23
Safi Sana. Mtu ni roho, yenye nafsi inayokaa kwenye mwili.
 
Roho (spirit) ndiye mtu halisi (real human beinpiapig), imevaa nafsi (soul) na mwili (flesh). Uwepo wako wa ndani kabisa ndiyo roho yako. Nafsi ina utashi ambako kuna akili, hisia na maamuzi
ndio nafsi pia inakufa

Roho (spirit) ndiye mtu halisi (real human being), imevaa nafsi (soul) na mwili (flesh). Uwepo wako wa ndani kabisa ndiyo roho yako. Nafsi ina utashi ambako kuna akili, hisia na maamuzi
ndio pia mtu anapokufa imaanisha pia nafsi yake imekufa kutia ndani uwezo wa kufikiri , mawazo na kila kitu...
roho ni nguvu ya utendaji tu kama nguvu za umeme haina uwezo wa kufikiri wala kumbukumbu
 
Roho huweza kuona ambavyo macho ya mwili hayawezi kuona, hasa jambo au kitu kitakachotokea baadaye. Usishangae kuwa litakalotokea kesho roho yako inalijua leo!

Hata mke wa kuoa au mume wa kuolewa naye, unaweza kumfurahia kwa macho na kuvutiwa na kila kitu leo, lakini roho yako ikamkataa kabisa, na pengine kwa kuugua na kuumia sana jinsi unavyompenda wewe na akili yako, pasina kujua lolote.

Unaweza kushupaza shingo, lakini moto utakapoanza kuwaka ndani ya nyumba baada ya miaka kadhaa ya uvumilivu, utakumbuka na kuanza kusema: ndio maana roho ilisita, iligoma, iliuma, iliogopa, nk.; Inabaki kuwa majuto ni mjukuu!
si kweli hizo ni hisia
 
Roho ni pumzi ya Mungu aliyokupulizia siku umeumbwa si hewa ya kawaida ndio uhai wenyewe.Roho ni sawa na nishati(energy)huwezi kuiona katika umbo lolote lile hapa wataalamu wa engine za magari watanielewa
 
Neno roho kwa wote sio geni sana. Kwa wanaojua wasaidie kujibu maswali, wasitumie imani za dini.

1: Roho ni nini?

2: Roho inapatikana wapi katika sehemu ya mwili?

3: Nani amewahi kuiona roho na inafananaje?

4: Moyo ndio kiungo kikuu Cha binadamu, binadamu akifariki tunasema roho imemtoka na sio moyo umesimama. Kwa Nini? Na roho ikimtoka binadamu inaenda?

5: Roho Safi ikoje na roho chafu zikoje?

6: Kama binadamu anaishi kwa kutegemea hewa Aina ya oxygen, kwanini binadamu roho ikimtoka ndio hufa? Na bado hewa ya oxygen inakuwepo bado.
Roho ni kiunganishi kati yako na ulimwengu wa Kiroho, nayo ndiyo inakufanya unakua conscious Bila roho unahesabika mfu, kwa maana nyingine roho ni nafsi ndani yako ndo maana siku ukifa watasema tunaenda kuaga Mwili wa Wilson inamaana Wilson Kuna mahali roho au (nafsi) yako imeenda, mfano wachawi wanapomchukua mtu msukule wanachukua nafsi nakuacha Mwili, nafsi haina Mwili wa nyama japo inafanana na ww copyright ata ktk Imani tunaambiwa Mbinguni tutakua tunafanana hivi tulivyo lkn si kwahii miili tuliyonayo, kwahiyo roho ( nafsi) haifi inaishi milele kwamaana hiyo Ata Mungu ni roho ndo maana tunaambiwa tumeumbwa kwa mfano wake ktk Imani ya ukiristu tunaambiwa Kuna Roho mtakatifu ambaye Yuko ndani yetu na ndiye anatuunganisha na ulimwengu wa Kiroho,
 
Neno roho kwa wote sio geni sana. Kwa wanaojua wasaidie kujibu maswali, wasitumie imani za dini.

1: Roho ni nini?

2: Roho inapatikana wapi katika sehemu ya mwili?

3: Nani amewahi kuiona roho na inafananaje?

4: Moyo ndio kiungo kikuu Cha binadamu, binadamu akifariki tunasema roho imemtoka na sio moyo umesimama. Kwa Nini? Na roho ikimtoka binadamu inaenda?

5: Roho Safi ikoje na roho chafu zikoje?

6: Kama binadamu anaishi kwa kutegemea hewa Aina ya oxygen, kwanini binadamu roho ikimtoka ndio hufa? Na bado hewa ya oxygen inakuwepo bado.
Kiungo muhimu ni ubongo si moyo. Moyo unaweza simama ukashtuliwa ukaamka tena. Ubongo ukisimama ndo tunasema huyu mtu hayupo.

Roho bila imani ya dini haipo. Roho na imani ni mapacha. Ukitoa imani, binadamu hana tofauti na mnyama mwingine yoyote.
 
Neno roho kwa wote sio geni sana. Kwa wanaojua wasaidie kujibu maswali, wasitumie imani za dini.

1: Roho ni nini?

2: Roho inapatikana wapi katika sehemu ya mwili?

3: Nani amewahi kuiona roho na inafananaje?

4: Moyo ndio kiungo kikuu Cha binadamu, binadamu akifariki tunasema roho imemtoka na sio moyo umesimama. Kwa Nini? Na roho ikimtoka binadamu inaenda?

5: Roho Safi ikoje na roho chafu zikoje?

6: Kama binadamu anaishi kwa kutegemea hewa Aina ya oxygen, kwanini binadamu roho ikimtoka ndio hufa? Na bado hewa ya oxygen inakuwepo bado.
Roho sio Moyo, Ubongo ndio kila kitu, Ubongo unaweza kusimama na moyo ukaendelea kufanya kazi,
Maelezo ni mengi ila nimalize tu kwa kisema, IMANI ni bora kuliko DINI, nadhani umenielewa
 
SIMPLe,roho ni uhai,uhai wa roho haushikiki,hauonekani, haufi ni wa milele.uhai wa mwili unaonekana ni wa damu na oxygen ,hufa ni wa muda.muhimu malaika wote wana uhai wa roho hawana wa mwili,wanyama,ndege najamii ya saamaki wana uhai wa mwili hawana uhai wa roho.in mwanadamu peke yake mwenye uhai was mwili na uhai wa roho,eemwanadamu jua kuna moto wa milele na kuna mbingu ya milele..nakusihi tenda mema ungali na uhai was muda wa uhaimwili.
We umejuaje yote haya,evidence please
 
Roho huweza kuona ambavyo macho ya mwili hayawezi kuona, hasa jambo au kitu kitakachotokea baadaye. Usishangae kuwa litakalotokea kesho roho yako inalijua leo!

Hata mke wa kuoa au mume wa kuolewa naye, unaweza kumfurahia kwa macho na kuvutiwa na kila kitu leo, lakini roho yako ikamkataa kabisa, na pengine kwa kuugua na kuumia sana jinsi unavyompenda wewe na akili yako, pasina kujua lolote.

Unaweza kushupaza shingo, lakini moto utakapoanza kuwaka ndani ya nyumba baada ya miaka kadhaa ya uvumilivu, utakumbuka na kuanza kusema: ndio maana roho ilisita, iligoma, iliuma, iliogopa, nk.; Inabaki kuwa majuto ni mjukuu!
Upo sahihi
 
Huwezi kuiona roho yako kwa macho kwa kuwa si mwili. Nikuulize kidogo ili uweze kunielewa: Je, umewahi kuuona upepo kwa macho? Hata kama hujawahi kuuona lakini sauti yake, matokeo au madhara yake, unayasikia na kuyaona kwa hakika.

Kwahiyo, uwepo wa kitu fulani si lazima ukione kwa macho. Hata sauti hujawahi kuziona lakini unazisikia kwa hakika!

Roho yako ndiyo wewe mwenyewe. Mwili ni koti tu lililoivaa roho, ikitoka unakuwa umekufa. Pia una nafsi (soul) ambayo hujumuisha akili (mind), hisia (emotions) na maamuzi (decisions). Nafsi hubeba utashi (conscience) ambao wanao watu tu, si wanyama.

Unafanya jambo lolote kwa utashi wako, kwa maamuzi yako na mtazamo au mapenzi yako. Tunu hiyo haipo kwa wanyama. Hata mnyama anapokunya hafikirii chochote - kunya kunamtokea tu popote!

Je, umewahi kutokewa ambapo unabishana na wewe mwenyewe? Akili yako inaamua kwenda mahali fulani, lakini ndani yako unasikia sauti ya chini inakukataza usiende! Ukiamua kwenda bila kuitii hiyo sauti ndani yako halafu ukapata shida huko uendako, utaanza kusema roho yangu ilinikataza! Roho yangu ilisita! Roho iligoma kwenda!

Kwahiyo, kila mtu ana sehemu tatu: Roho (spirit), Nafsi (soul) na Mwili wa damu, nyama, mifupa, nk (flesh). Kama hujanielewa nitafute ili nikupe ufafanuzi zaidi kadri Mungu atakavyonijaalia. Pia waweza kusoma 1 Thesalonike 5:23
 
ila ipo siku hii siri ya kifo itakuja kufichuka, maana wote wanabuni kulingna na imani zao..
 
Back
Top Bottom