Roho ni nini? inaenda wapi baada ya kufa?

Tafuta kitabu kinaitwa: The Philosophy of Teachings Of Islam cha M G Ahmad, ndani yake imetajwa roho ni nini, inaingiaje kwenye mwili, asili yake, mahusiano yake na mwili, wakati wa kifo inakuwa wapi, baada ya kuzikwa inafanya nini, zinaishi wapi baada ya kifo, athari za maisha ya dunia zikoje kwenye roho baada ya mwili kufa, roho itaishije bila mwili, siku ya kiyama maana yake nini, n.k vyote hivyo vimefafanuliwa na kujibiwa kwa undani sana kiasi ambacho huwezi kidoubt maisha baada ya kifo.
Hicho kitabu sijakisoma bado, ila hayo mambo hakuna falsafa, au sayansi inayoweza kuyathibitisha hayo. Imani ni kubwa kuliko sayansi.
 
Yesu ni sehemu ya MUNGU mkuu, yani katika zile roho Saba za MUNGU na YESu yupo ndani yake, hivyo huwezi kumtenga YESu na uungu, alivokuja duniani alificha ukuu wake ili afanane na sisi, kwasababu angekuja na uungu wake amini watu wangekimbia, hivyo ili atuokoe, ilibidi aje kwa kupitia prosesi za kibinadamu kabisaa, ili ulimwengu usihofu.
unaongea kama muumini, so you are biased. You can't find God logically. We only find True God if we become like little kids. Faith is enough
 
Wewe Mkristo wa wapi mkuu, mkatoliki, pentekoste, msabato, Anglikana, Lutheran, au shahidi wa Yehova?
Maana yeyote anayepinga kuwa Yesu si Mungu ni mpinga Kristo!
Hawa mashahidi wa Jehovah sio wakristo, kama wangekubaliana na mimi ningewashauri wawe waislam moja kwa moja. Na mkristo anaehamia huko huwa namwona ameshauchoka Ukristo wa kweli.

Wana Ukristo wa New Age.
 
Hali hii utegemee Alkaaba iwekwe msalaba!!!!
Mimi na wengine wenye kuangalia wakati huwa tunajiuliza tu swali moja huu ni wakati gani?
Pia unganisha kukua kwa Uislam na kurudi kwa Wayahudi kwenye nchi yao pamoja na kuzidi kuchukua makazi mapya Hebron, ramallah, west bank na mpango wa kuichukua Jerusalem.

Kama Wakristo wangeendelea kuwa majority lengo linalotakiwa kutimia lisingetimia, UISLAM upo kimalengo na baada ya lengo lake la kuwepo kutimia utafutika na utakuwa kama haukuwahi kuwepo.

Kuna kusudi, lengo na mpango wa kuwepo kwa uislam na linatakiwa litimie katika wakati.
 
Hawa mashahidi wa Jehovah sio wakristo,,,kama wangekubaliana na mimi ningewashauri wawe waislam moja kwa moja......Na mkristo anaehamia huko huwa namwona ameshauchoka Ukristo wa kweli.........

Wana Ukristo wa New Age.
Hata wasabato wamekaa katika uelekeo usioeleweka,,,wako kama popo,,Huwezi waelewa ni ndege au animalia,,,,hawako baridi wala moto nao pia utadhani ni tawi la uislam.

Wamejengwa kwenye msingi wa UONGO.
 
Hicho kitabu sijakisoma bado, ila hayo mambo hakuna falsafa, au sayansi inayoweza kuyathibitisha hayo. Imani ni kubwa kuliko sayansi.

Usijijibu kabla hujakisoma. Chenyewe kina majibu ambayo kama unataka kujifunza utafaidika mno. Ngoja nikupe link yake hapa:
 
Usijijibu kabla hujakisoma. Chenyewe kina majibu ambayo kama unataka kujifunza utafaidika mno. Ngoja nikupe link yake hapa:

https://www.alislam.org/swahili/Hekima-ya-Mafundisho-ya-Kiislam.pdf

d31e804864598df900f6d2989218503b.jpg
 
Mimi na wengine wenye kuangalia wakati huwa tunajiuliza tu swali moja huu ni wakati gani???
Pia unganisha kukua kwa Uislam na kurudi kwa Wayahudi kwenye nchi yao pamoja na kuzidi kuchukua makazi mapya Hebron,,ramallah,,west bank na mpango wa kuichukua Jerusalem.........Kama Wakristo wangeendelea kuwa majority lengo linalotakiwa kutimia lisingetimia,,,,,,,UISLAM upo kimalengo na baada ya lengo lake la kuwepo kutimia utafutika na utakuwa kama haukuwahi kuwepo,,,,
Kuna kusudi,,,lengo na mpango wa kuwepo kwa uislam na linatakiwa litimie katika wakati...
Usihame mada rafiki, Habar za wapinga kristo -(wayahudi ) zipo 'clear' baada ya kibano cha Hitler cha kuwaua milion 6 kule German na kuja huku kupokelewa na wapalestina baadae wanafanya ubabe wa kuwaondoa wenyeji wao zinajulikana!

Hoja ya uislam kufutika sahau, kwa taarifa yako ungekuwa umeshafutika!!, Allah alishaahidi ataulinda uislam mwenyewe na mwisho utashinda mifumo yote ya Maisha ya kubuniwa na wanadam.

Kitu ambacho wakristo wa kibongo hamjui ni kuwa hao wayahudi 'as a whole' sio wakristo, na walimkataa Yesu long time , ndio mana pamoja na ninyi kuwashobokea mkienda the so called hija Yenu , ni wapalestina -waislam ndio wanaowaeleza historia ya Yesu na kuwatembeza katika maeneo aliyokulia!!

Hii ndiyo changamoto ambayo umeshindwa kutoa andiko na si wewe tu maana Dunia nzima hakuna msomi wa dini ya Kikristo amewahi kujibu!
 
Siwezi kukimbia,,,,ila ni nani alikudanganya wayahudi ni wapinga Kristo?? Unaweza kuta hata wewe ni miongoni mwa walio katika mission ya mpinga Kristo bila kujijua,,,,,,,,wayahudi sio wakristo ila wanaplay role kubwa na ya kuzingatia katika kupitisha,,kuenea na kufanikiwa Ukristo........Na bado wanabaki kuwa watu wa muhimu na maalum katika heshma ya Ukristo.......Ref WARUMI 12:13-36

Ukiielewa hii mistari itakusaidia kuelewa kwa undani kwa nini Wakristo wa kweli wana mafungamano ya dhati na wayahudi.......


Wapinga Kristo wakubwa ni wale wanaosema,,,,,,,Yesu ni binadamu,,,Yesu alioa,,,,Yesu sio Mungu,,,,Yesu hakufa msalabani,,,,Yesu hakufufuka na conspiracy theory nyingine zisizo na mashiko zinazofanana na hizi...............

Sijaweka huo mstari hapa maana ni mrefu sana.Kama utapenda pitia uelewe baadhi ya vitu vya msingi kuhusu wayahudi na wakristo.

Sisi tunajua siku nyingi sana kwamba Wayahudi wengi sio Wakristo......ila unatakiwa ujue kwamba wapo wayahudi Wakristo pia ambao kwa idadi yao Huwezi wahesabu kwa siku tatu au nne ukawamaliza........ila sisi wayahudi kuwa Judaism sio tatizo kwetu maana ni Ndugu zetu na hawajawa walivyo kwa bahati mbaya...Mstari unaeleza....

Zaidi wayahudi kuzidi kuichukua nchi yao mtaa kwa mtaa sio bahati mbaya ila ndio Wakati utaendelea tu na baadae kila mmoja ataelewa nini maana ya hayo yote.
 
Siwezi kukimbia,,,,ila ni nani alikudanganya wayahudi ni wapinga Kristo?? Unaweza kuta hata wewe ni miongoni mwa walio katika mission ya mpinga Kristo bila kujijua,,,,,,,,wayahudi sio wakristo ila wanaplay role kubwa na ya kuzingatia katika kupitisha,,kuenea na kufanikiwa Ukristo........Na bado wanabaki kuwa watu wa muhimu na maalum katika heshma ya Ukristo.......Ref WARUMI 12:13-36

Ukiielewa hii mistari itakusaidia kuelewa kwa undani kwa nini Wakristo wa kweli wana mafungamano ya dhati na wayahudi.......


Wapinga Kristo wakubwa ni wale wanaosema,,,,,,,Yesu ni binadamu,,,Yesu alioa,,,,Yesu sio Mungu,,,,Yesu hakufa msalabani,,,,Yesu hakufufuka na conspiracy theory nyingine zisizo na mashiko zinazofanana na hizi...............

Sijaweka huo mstari hapa maana ni mrefu sana.Kama utapenda pitia uelewe baadhi ya vitu vya msingi kuhusu wayahudi na wakristo.

Sisi tunajua siku nyingi sana kwamba Wayahudi wengi sio Wakristo......ila unatakiwa ujue kwamba wapo wayahudi Wakristo pia ambao kwa idadi yao Huwezi wahesabu kwa siku tatu au nne ukawamaliza........ila sisi wayahudi kuwa Judaism sio tatizo kwetu maana ni Ndugu zetu na hawajawa walivyo kwa bahati mbaya...Mstari unaeleza....

Zaidi wayahudi kuzidi kuichukua nchi yao mtaa kwa mtaa sio bahati mbaya ila ndio Wakati utaendelea tu na baadae kila mmoja ataelewa nini maana ya hayo yote.
Probably sielewi nini maana ya mpinga kristo, kwa mahaba yako kwa wayahudi huwez kuongea vinginevyo!!, ila kukusaidia wayahudi wanafuata sheria ya Musa yote, Yesu alisema amekuja kutimiliza sheria ya Musa (torati) according to bible, lakin hadi leo hawajawahi kumkubali!!!
Kama mpinga Kristo unamaanisha anayeenda kinyume na mafundisho ya Yesu basi si wayahudi tu, hadi wewe ni mpinga kristo,

Maana kakataza kula nguruwe wewe unakula!

Kasema 'baba ni mkuu kuliko mimi ' wewe hutaki unasema yeye ndio Mungu mkuu!! Tito 2

Kasema anafanya miujiza kwa jina la Mungu wewe unasema anafanya mwenyewe!

Kasema yeye ni binadam (mtu) wewe unamwita Mungu!!!

Alisali kwenye masinagogi (misikiti) wewe unasali kanisani

Anavua viatu kabla ya sala (mahali pakatifu) wewe unavaa!!!

Anatawadha ( kuosha miguu , mikono n.k kabla ya sala ) wewe hufanyi hivyo

Ametahiriwa ..wewe unasema sio lazima!!

Amesalimia ' shalom leku' maana yake Amani Iwe kwenu yaan Asalaam alaykum wewe unasalimia 'Bw. Yesu asifiwe'

Amejisalimisha 'Elloi Elloi lama Sabaktan' yaani 'Allah Allah mbona waniacha' wewe unamwita ni Jehova , unabadilisha namna Yesu alivyomwita Mungu.

Ametabiri kuja kwa Mtume Muhammad kuwaambia kweli yote na kumtukuza yeye, Mtuma Muhammad Alikuja zaid ya miaka 1400 iliyopita amemtukuza wewe unamkataa!!!

NANI MPINGA KRISTO?
 
Yapo mengi sana huyafanyi aliyofundisha Yesu, bahati mbaya unasema una mpenda Yesu!!! Katika maisha yako hujawahi kumsujudia Mungu!! Lakin unampenda Yesu!!!!
 
Yapo mengi sana huyafanyi aliyofundisha Yesu, bahati mbaya unasema una mpenda Yesu!!! Katika maisha yako hujawahi kumsujudia Mungu!! Lakin unampenda Yesu!!!!
Mpinga Kristo ni neno pana 1John 4:1-16. Kumpinga Kristo ni mpango madhubuti wa kuaminisha watu kwamba alichokifanya Yesu kilikuwa uongo na kisichokuwa na maana yoyote, na pia kujaribu kumuundermine ili aonekane si kitu na kujaribu kuwaaminisha waliomfuata habari za uongo.

Lakini hayo yote yanakuwa sponsered na ulimwengu usioonekana ambako ndio mambo yote huanzia. Sinagogi sio msikiti wa kiislam kwa sababu moja tu ya msingi. Mungu wa wayahudi na wakristo sio huyo wanaemwabudu Waislam.

waislam wana Mungu wao na wakristo wana Mungu wao, kwa hio walioingia kwenye sinagogi hawamwabudu Mungu wa Waislam wala kufuata amri yake yoyote. Sisi huwa tunafuata alioamrisha Yesu na kuiga matendo yake(japo yahitaji kujicommit binafsi na kuongozwa na Roho ndani ambae hataki dhambi) / swala la kutahiriwa sio kwamba tunalichukulia kirahisi ila ni nadra ukute mkristo hakutahiriwa, mtoto akizaliwa wa kiume govi hukatwa Mapema kabisa.

Ukiusoma Ukristo kutafuta makosa utakuwa umepotea mazima, kwa sababu unaemletea hayo makosa anakuona kwamba umeyaona ni makosa kwa sababu hukuyaelewa kuna watu pia husoma biblia kutafuta lengo, dhamira na sababu za yalioandikwa. Ukimwambia Eti! Paulo mtume kaharibu Ukristo atakushangaa sana, kwa sababu anajua Mtume Paulo na mitume wengine walikuwa kwenye phase ipi wakikamilisha nini?

Haya Mambo pia ujue ni mambo yalioanzia kwenye vyanzo hayakutokea bahati mbaya.
 
Yesu Si Mungu. Na hawezi kuwa Mungu.

Mungu haonekani hivyo hana mfano.
Hizo nyingine ni simulizi.

Hakuna sababu inayofanya Yesu Awe Mungu Mkuu
Kumbuka unazungumzia Imani.Yesu kuwa Mungu au kutokuwa Mungu ni Imani haihitaji nguvu nyingi kuelezea waweza amini au usiamini ndo maana ya Imani.Binafsi naamini ni Mungu halisi kabisa.
 
Wewe umeisoma biblia kwa kuongozwa na roho mtakatifu? Hata lete mistari sasa siyo kuongea kwa ujumla wake. Kwa taarifa tu biblia haijaelezea ni wapi roho zinapohifadhiwa baada ya mauti. Kama unajua toa andiko!
Leo unaizungumzia biblia?Umeisoma kweli haina hivyo vifungu?Kwa kuwa umeisemea hata sikupi majibu isome vizuri na mwombe Roho Mtakatifu akuongoze utaviona hivyo vifungu .
 
Yesu alikuja kuitimiza torati kwa kuleta mfumo utakaoizuia dhambi kutoka chanzo chake, sio kuizuia dhambi kwa sheria na intimidation, kwa kuwa na Roho yenye nguvu ndani yako itakayokubadilisha utoke kwenye uelekeo, mawazo na asili ya kutenda dhambi (Agano jipya).

Agano jipya au mkataba mpya una tofauti na mkataba uliopita kwa maana ya damu inayotumika (hili ni somo linaloeleweka na wakristo) kwa hio kula nguruwe, sungura na ngamia au nyoka ni kitu ambacho hakiko kisheria tena.

Sheria ni kitu kizuri cha zamani ambacho kimehamishiwa mahakamani. Sheria zote Mungu alizihamishia mahakamani ili badala ya mtu kupigwa mawe afungwe miaka kumi na badala ya mtu kukatwa kichwa afungwe miaka 75, labda na akili itamrudia huko kifungoni atubie dhambi yake na Mungu alie mwingi wa rehma amsamehe na amkaribishe mbingu yake. Kwa sasa kuna namna nyingine Nzuri ya kuishinda dhambi na kufanya utakaso wa dhambi. Ambayo Yesu ni architecture na mitume wake wakamalizia kwa muendelezo.

Labda kuhusu nguruwe niseme kidogo, palipokatazwa nguruwe mbele yake kakatazwa ngamia, hivi imekuwaje ngamia kwenu waislam awe halali na pia kitoweo ghali wakati ana unajisi sawa na nguruwe, au hili ni tyiping error. Sisi Wakristo hatukatazwi kula nyama yoyote maana katika mkataba mpya namna ya kuishinda na kuitakasa dhambi imebadilika.
 
Mpalasinge support maelezo yako na aya za biblia unayoiamin, nakushangaa unaandika saaana lakin ni maneno yako mwenyewe!!!, Yesu anasema amekuja kutimiza torati na sio kubatilisha , wewe una narrate kitu different kabisa na hau support na aya yoyote!!! Hebu soma tena hapa ..unaweza pindisha kweli? Pole sana rafiki
PAULO AU YESU? IMANI AU MATENDO

12- PAULO AU YESU? IMANI AU MATENDO?

Hebu yazingatie Mahubiri ya Yesu aliyotoa juu ya Mlima wa Zaituni

Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza. Kwa maana, amin, nawaambia, Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukta moja ya torati haitaondoka, hata yote yatimie. Basi mtu ye yote atakayevunja amri moja katika hizi zilizo ndogo, na kuwafundisha watu hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni; bali mtu atakayezitenda na kuzifundisha, huyo ataitwa mkubwa katika ufalme wa mbinguni. Maana nawaambia ya kwamba, Haki yenu isipozidi hiyo haki ya waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.

Mathayo 5.17-20

Sasa Mpalasinge hebu
Futa hilo andiko kwa andiko la yeye mwenyewe Yesu. KARIBU.
 
Mpinga Kristo ni neno pana 1John 4:1-16.,,,,,,Kumpinga Kristo ni mpango madhubuti wa kuaminisha watu kwamba alichokifanya Yesu kilikuwa uongo na kisichokuwa na maana yoyote,,,,na pia kujaribu kumuundermine ili aonekane si kitu na kujaribu kuwaaminisha waliomfuata habari za uongo...Lakini hayo yote yanakuwa sponsered na ulimwengu usioonekana ambako ndio mambo yote huanzia.........Sinagogi sio msikiti wa kiislam kwa sababu moja tu ya msingi"""Mungu wa wayahudi na wakristo sio huyo wanaemwabudu Waislam"""" waislam wana Mungu wao na wakristo wana Mungu wao....kwa hio walioingia kwenye sinagogi hawamwabudu Mungu wa Waislam wala kufuata amri yake yoyote........ ......Sisi huwa tunafuata alioamrisha Yesu na kuiga matendo yake(japo yahitaji kujicommit binafsi na kuongozwa na Roho ndani ambae hataki dhambi)))/ swala la kutahiriwa sio kwamba tunalichukulia kirahisi ila ni nadra ukute mkristo hakutahiriwa,,,,mtoto akizaliwa wa kiume govi hukatwa Mapema kabisa..... ......

Ukiusoma Ukristo kutafuta makosa utakuwa umepotea mazima,,,,kwa sababu unaemletea hayo makosa anakuona kwamba umeyaona ni makosa kwa sababu hukuyaelewa kuna watu pia husoma biblia kutafuta lengo,,dhamira na sababu za yalioandikwa...Ukimwambia Eti!! Paulo mtume kaharibu Ukristo atakushangaa sana.. .kwa sababu anajua Mtume Paulo na mitume wengine walikuwa kwenye phase ipi wakikamilisha nini????

Haya Mambo pia ujue ni mambo yalioanzia kwenye vyanzo hayakutokea bahati mbaya.
Huo mpango madhubuti umefanywa na Paulo kuwaaminisha na kupindisha yote yaliyofanywa na Yesu.
 
Back
Top Bottom