Road Safety: Stika za Nenda kwa Usalama ni wizi, tuungane kuupinga

Hii hata mimi sikubaliani nayo. Wakati wa ku renew road licence gari inapaswa ikaguliwe kila kitu, sasa hizi sticker za nini?

Wabunge mnaopitia hapa, someni mchukuwe hatua. Siyo kwenda bungeni kubwabwaja bila mpango kama Mbowe.
 
Nimekutana na mtu mmoja katika kituo cha kujaza mafuta pale round about ya stand ya daladala Morogoro mjini anauza sticker za wiki ya nenda kwa usalama kwai Tshs 5,000 huku zikiwa zimeandikwa kiasi cha Tshs 3,000, nilipomwuliza kwanini unaziuza wewe raia wakati zilitakiwa zitolewe na kikosi cha usalama barabarani baada ya kufanya ukaguzi wa gari, akanambia hao usalama barabarani ndiyo wameniuzia zote nilizonazo mkononi.

Nimejiuliza swali huu utaratibu wa raia kuuza sticker umelipeleka jeshi la polisi hususani kikosi cha usalama barabarani likizo?

Kuna sababu gani kuuza stucker kama ukaguzi wa magari haufanyiki kama sheria inavyotaka?

Huyo kiongozi wa kikosi cha usalama barabarani aliyempa raia burungutu la sticker aziuze anatambua madhara yake?

Huyo kiongozi anayepaswa kuzitoa sticker hizo kwa magari yaliyo kaguliwa anafanya kazi gani kama kazi yake imekabidhiwa kwa raia?
Mimi niko ofisi Moja hapa Posta nimeshangaa Sana kumuona Dada mmoja anapita maofisini anapita.... TZ NI N NOMA.
 
Wewe umeiba vingapi!? Mbona hakuna aliyekuletea ukuda.! Take care utapotea.
 
Ninaandika barua ya wazi kwa Afande MPINGA Mkuu wa Usalama Barabarani kwa wizi na uonevu unaofanywa na Maaskari wa Usalama Barabarani kituo cha Mpakani mwa Mkoa wa Simiyu na Mkoa wa Mara.

Nilikuwa naenda kuhudhuria mazishi ya Ndugu yangu tarehe 28.2.2015 kule Tarime na nilikuwa na gari dogo la RAVA4. Nilipofika mpakani mwa Simiyu na Mara nikakaguliwa na askari namba G.9368 wa Usalama Barabarani.

Baada ya ukaguzi akanieleza kuwa sina STIKA na mimi nikakubali. Nikamweleza kagua gari na nilipie stika. Nikamuuliza kuwa stika ni shillingi ngapi?.

Akanieleza kuwa stika ni tshs.10,000 mimi nikamueleza kuwa mbona stika ni shs.2,000 na ukichelewa kama mimi inaweza kuwa tshs.5,000.

Yeye akanieleza kuwa nitoe tshs.10,000 ndipo anipe stika. Mimi nikagoma na baadaye akasema sasa ninakulipisha faini ya tshs.30,000 kwa kukosa stika.

Nikakubali sawa lakini nipe risiti. Yeye akanieleza kuwa hana risiti ila nitoe tshs.30,000. Nikamuuliza je faini si fedha za Serikali?. Akashindwa la kusema.

Baadaye nikaandikiwa kosa kwa ahadi ya kuchukua risiti kesho yake. Kesho yake nikafuatilia risiti kwa binde ndipo nikaipata.

Maaskari wa Usalama Barabarani wa kituo cha NASA na mpaka wa Simiyu na Mara wanaiibia Serikali sana kwa sababu hawatoi risiti pindi mwenye gari anapopatikana na kosa na fedha wanaweka mfukoni.

Nakushauri Afande MPINGA maaskari wote kwenye vituo nilivyovitaja wavuliwe vyeo mara moja na kuwa Maaskari wa kawaida.

Kwanza wanatesa sana wasafiri na siyo waaminifu mbele ya umma. Hasa Askari namba G.9368 wa kituo cha Wilaya ya Busega afukuzwe kazi mara moja.

Una majungu kama kweli ulidhurumiwa na hao traffic ulishindwa nini kupeleka malalamiko yako kwa Mpinga au Ocd wa eneo husika isije ikawa mnagombea demu na hao masoja hivyo unataka kulivenji.
 
Kumbe na wewe ni trafiki mla rushwa. Tutakunasa muda siyo mrefu.
 
Na huku LUDEWA wapo hivo hivo na wanakula pamoja na ocd sku moja wamelipisha fain eti rist uje kesho nikawambia inakuwaje upokee pesa wakati huna rist ngoja nikaulize PCCB kama ndo taratibu basi wakaanza ooh bhana usinde huko wakanipa wezi sana.
 
Matrafiki wote Tanzania ni wezi. Ingawa wengine kama huku Arusha wanadai kuwa serikali imewatuma kuwapora watu fedha kwa ajili ya uchaguzi. Hivyo si rahisi kuchukuliwa hatua.
 
Nimejaribu kufuatilia kwa miaka mitatu mfululizo nimegudua kwamba wiki ya nenda kwa usalama haina maana ila ni ulaji wa pesa tu, kwa miaka yote mitatu hakuna kinachofanyika cha kugagua magari ndio upewe stika ya kubadika kwenye gari kinachofanyika ni wewe mwenye gari au shirika la magari kwenda na list ya namba za magari yako na kununua stika hakuna cha kukagua magari kwa maana nyingine Trafic wanawaibia wananchi
 
Sabasaba
Nanenane
Mbio za mwenge
Bunge la katiba 2014
Hafla za kumuaga rais
ZOTE ME NASHAURI UKAWA MKIKAMATA NCHI ZIFUTENI
 
Siyo hivyo tuu. Hapa nilipo mimi kuna gari la matangazo linapita kuhamasisha ukaguzi wa magari. Cha kushangaza hao watangazaji wana stickers za nenda kwa usalama na wanaziuza 5000/ kila anapo pita ukimsimamisha anakupa sticker.
Hapa ndipo jeshi la polisi lilipo fikia.
Wako busy na kusema msizomee Ccm, msiandamane ila wao ni sawa kula rushwa.
Tujiunge tuseme sasa utawala wa aina hii basiii
 
Back
Top Bottom