Road licence Kufutwa

Road licence Kufutwa

Mie 2009, na nipo nipo sana.

Ni kama ule mkopo wa chuo, silipi hata kwa upinde.

Ya kwangu iliisha 2008 na mpaka leo nadunda na corolla yangu kama kawaida...! Road Licence ni sawa sawa na ile iliyokuwa inaitwa "kodi ya kichwa"...! Ni wizi tu...!
 
Mkuu Kiriku siku hizi utawakuta traffic wakiwa pamoja na mijamaa ya TRA na ile mijamaa mingine ya fire yaani Tanzania kuna kodi nyingi hadi kichwa kinauma.

Kodi nyingi halafu makusanyo yote yanaishia kugharamia safari za kishenzi za mzinzi zisizo na faida hata kwa wilaya moja achilia mbali taifa kwa ujumla, unajua inauma?
 
Last edited by a moderator:
Kuna dalili ya kuingia mjini kwa kibali cha jiji kama bodaboda! Serikali inatafuta mbinu zote kuingiza mapato ya nchi.

Hawa wahuni wanatafuta mapato ili waweze kwenda kustarehe huko New-York wakati wake na dada zetu wanazalia sakafuni!!!
 
Mkuu kama ni kweli watakuwa wamefanya jambo jema sana maana hiyo kodi inaumiza sana, kwa mfano unakuta mtu anashindwa kulipia compressive insurance anaishia kulipia third part wakati analipa hela inayokaribia hiyo kwenye road license pamoja na fire.
Tukirudi miaka ya 80 wakati Cleopa Msuya akiwa waziri wa fedha alianzisha road toll kukawa na vituo vya kulipia sehemu mbali mbali kwenye barabara kuu mwisho wa siku ikawa inatajirisha wafanyakazi wa hivyo vituo ikabidi ifutwe ndio ikaingizwa kwenye mafuta.
Kama kumbukumbu zangu zipo sahihi road license ilianzishwa na Zakia Meghji akiwa waziri wa fedha kama nimekosea mtanisahihisha wadau, hii ya kulipia kwenye mafuta ni nzuri kwa sababu "use more pay more" tutapunguza safari zisizo na tija.


Sent from my iPhone using JamiiForums mobile app
 
Hawa wahuni wanatafuta mapato ili waweze kwenda kustarehe huko New-York wakati wake na dada zetu wanazalia sakafuni!!!

Halafu "wakimnjunjia" vimada wake utaona reaction yake yenye true vengeance na mateso kwa wasio na hatia kama ilivyomtokea mzee wa watu Nguza.
 
Ajabu sana kama mtu unai park gari kwa sababu zako na iko ndani kwanini ulipe? Sheria hii sio sahihi kwani ilikuwa kama haipiti barabarani why pay,
 
Gari yangu hailipiwi hzo kodi ndogondogo na hata plate namba natumia fake na sijawahi kuulizwa na nmeingia nalo hadi posta mara kibao tu nadhani hua wanaangalia na mtu mwenyewe lkn mm hua ukinisimamisha napiga lugha ya malkia mwanzo mwisho na hv wengi wao vilaza tena naminya ulimi mwisho nasiki MR AROVERA GO!
Mhhh..ngoja nichanganye na zangu......
 
Mbona itakuwa vizuri.Kwamaana mimi sijaona faida yake na kila mwaka nikilipa.Na hapo watabuni kitu kingine kama ktk mafuta mbona tunaibiwa tu.
 
tusubirie mfumuko wa bei kama Zimbabwe,madhara ya kiuchumi yanaweza kuwa makubwa kuliko hiyo kodi wanayotaka kukusanya
 
Mkuu hii ndio tutalia zaidi.......kupitia mafuta ndio tutaumia zaidi........wanatujua watanzania....hatujali....kama PAYE tunakatwa lakini haituumi utadhani tunalipiwa na mwajiri.......

Fikiria waongeze hata 300 kwa lita.....kama unatumia lita 5 kwa siku utalipia 1500 then kwa mwaka Approx 540,000

Mkuu Mtazamo solution ni kutumia usafiri kama wangu. ImageUploadedByJamiiForums1401874603.567037.jpg


Sent from my iPhone using JamiiForums mobile app
 
Samahani wakuu, road licence inayojadiliwa hapa ni ile Motor Vehicle Licence ? ama ipi ?
 
picchu naona kama kuna point hapo. Gari iko garage na unaokoteza mchuzi 2yrs hapo hapo na hii road license wapi na wapi? Waanzishe na garage license basiiii
 
Last edited by a moderator:
Kwa waziri huyu wa fedha na manaibu wake wahuni sidhani. labda kama lile jembe lililofariki ndio lililoleta hilo wazo
 
Ngoja nivute subira ya kukomenti juu ya hili
 
Halafu "wakimnjunjia" vimada wake utaona reaction yake yenye true vengeance na mateso kwa wasio na hatia kama ilivyomtokea mzee wa watu Nguza.

Kamanda ebu funguka kidogo huyu Nguza alifungwa kwasababu ya SHORI yupi?
 
Nchi hii ya kipuuzi sana! Mafuta yana matumizi mengi kwa watu wengi. Wapunguze tuu hiyo kodi. Mafuta ndio uchumi wa nchi,kuongeza kodi kwenye mafuta ni kudidimiza maendeleo.
Mtasikia sasa hivi petrol ni 3000 lita!!
 
Nimemshangaa sana, mie fees hizi nalipa nikiamua.



Kuvunja sheria ni hobby na haifundishiki, kuna raha yake. Hasa kama kosa lenyewe dogo kama hili.
Na ukitaka kujipima, jiulize, shuleni ulikuwa kati ya watiifu au watukutu? Kama ni mtukutu, ulikuwa mtukutu kwa hiari au kwa kulazimishwa na mazingira. Kama ulikuwa mtukutu wa hiari, trafiki hakushiki kwa road licence tu.

Kamata like 5.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom