Don san tan
JF-Expert Member
- May 23, 2015
- 562
- 433
- Thread starter
- #41
RIWAYA: HUJUMA 20
MTUNZI: richard MWAMBE
“Sharon, usiku wa leo tuna wageni wengi uwanja wa ndege, naomba uchague vijana watano wazuri katika usalama uwaweke pale, wakiongozwa na wewe mwenyewe, msako wa huyo Hayawani muachie Fasendy, na vijana wengine wanakuja kushika nafasi za hao watano,” ilimaliza sauti ya Shalaba.
§§§§§§
Baada ya kuliacha gari alilokuwa amepanda kama mita mia tano hivi mtaa wa pili nyuma ya kile kituo cha mabasi, Amata alipita kwenye vibaraza vya maduka na kutokea nkwenye barabara kubwa inayoelekea katika kituo kile. Alisimama mbele ya duka kubwa la vyombo akitazama huku na kule, alijua kwa vyovyote vile lazima wamuwekee mtego katika gari lake, hivyuo aliamua kuwacheza shere, alikodi tax na moja kwa moja akaelekea hotelini kwake.
Mbele ya hoteli ile alijaribu kusoma sura za watu na akagundua kuwa kuna sura ambazo hawezi kuziamini hata kidogo, aliamua kuwabadilishia mchezo. Ilikuwa lzima afike katika chumba chake kwani kuna dokumenti alizokuwa akizihitaji kwa usiku huo.
Akazunguka nyuma ya hoteli na kuichunguza akagundua kuna mlango wa kutokea upande huo wa nyuma, akajaribu kuutikisa akakuta umefungwa, akatulia kimya kufikiri mara mbili la kufanya. Nukta hiyohiyo akasikia sauti za watu wanaoongea wakija upande wa nyuma wa hoteli ile, akajibana katikati ya mabomba mawili ya uchafu, yanayotiririsha majitaka toka juu kuleta chini. Walikuwa ni walinzi wa hoteli hiyo, walipompita aliamua kukwea kupitia yale mabomba. Chumba chake hakikuwa juu sana ilikuwa ni ghorofa ya tatu tu, hivyo haikumchukua muda kwa mtu kama yeye kufika usawa wa chumba chake, pale kulikuwa na kaukuta kalikojitokeza ambako kalikuwa kamebeba ndoo kadhaa za maua, akakanyaga kwa uangalifu kabisa asije kudondosha hata moja, alipohakikisha kuwa yuko usawa wa dirisha la chumba chake akalitikisa kidogo na lenyewe likatii amri, taratibu akaingia kupitia dirisha hilo kubwa lililoundwa kwa aluminiam safi, akatua ndani ya chumba hicho kwa madaha bila kufanya kelele yoyote kwani alijua kuwa lazima wapo wengine walio ndani.
Akakiendea kitanda chake na kukibonyezabonyeza, kilikuwa kimetulia kama kilivyo. Kamanda Amata akalisogelea kabati kubwa la nguo. Akashika kitasa cha mlango huo tayari kuuvuta lakini kengele za hatari kichwani mwake ziligonga, akajiandaa, kisha akavuta kwa nguvu ule mlango. Hakuwa tofauti na hisia zake, alipofuangua mlango tu, mtu mmoja aliyekuwa amejificha ndani ya kabati hilo alijitokeza kwa minajiri ya kumpamia Kamanda Amata, lo, Kamanda alipoufungua ule mlango tayari alikuwa kajiweka kando hivyo yule mtu akapitiliza peke yake na kumpita Amata ambaye alinyanyua mguu na kumpiga ngwala maridadi iliyomfanya mtu yule atue kwa uso katika sakafu na kuvunja mwamba wa pua. Kabla hajajigeuza, mguu mzito ulitua nyuma ya shingo yake na kumfanya mtu huyo kugugumia kwa maumivu. Amata akamwinamia palepale alipo na kumtazama mtu yule ambaye alikuwa chini, damu zikimvuja puani huku akilia kwa uchungu, lakini hakuweza hata kujigeuza kutokana na uzito wa guu la Amata.
“Wenzako wako wapi?” Kamanda alimuuliza.
“Niko pe-pe-ke ya-ngu,” alijibu kwa shida huku akijaribu kujiinua, lakini hakuweza kufanya hivyo.
“Unanitania sio?” Kamanda aliuliza na kumkanyaga kwa nguvu, yule mjinga pale chini alianza kutupatupa miguu na mikono kwa kutafuta pumzi.
“Ni-niiii-takwa-mbi-i-a,” alijibu. Kamanda Amata akalegeza mguu kidogo.
“Haya sema,”
“Wa-po nje,” akajibu.
“Wangapi?” Kamanada akahoji.
“Si- si… unaniumiza bwana,” yule mtu akashindwa kutoa jibu na badala yake akamtamkia maneno hayo Kamanda.
“Niambie, yule komandoo na wale wengine mmewaweka wapi?” akauliza tena.
“Si si – sijui mi-mi,” akajibu.
Muda huohuo saa ya Kamanda Amatav ikaanza kumfinya kwa fujo kuashiria kuna ujumbe ulikuwa ukiingi. Ni nafasi hiyohiyo ambayo yule mjinga pale chini aliitumia, alijigeuza kwa nguvu na kuwa chali akitaka sasa kusimama, teke moja kali nla Amata lilikuwa likienda kupiga korodani, yule bwana akaipanga mikono yake kwa mtindo wa x na kuchanua viganja vyake chini kidogo ya kiuno chake kusha akabonyea kufanya kama anachuchumaa, teka la Amata halikuwa pata lilipokusudiwa bali lilikingwa kwa hiyo mikono kwa usatdi kabisa. Kamanda Amata akaona akile ta mchezo hapo kazi itakuwa ngumu, wakati yule jamaa akiushusha mguu wa Amata chini mara tu baada ya kulipangua lile pigo kwa akili zote, kamanda Amata alishusha kichwa cha nguvu na katika paji ola uso la yule mjinga. Nyota zilimzunguka maana aliona kama kadondoshewa tofali, alipepesuka na kujibwaga kitandani, akajisjika pale alipopigwa kama kumepasuka lakini alishuhudia nundu lililojitokeza bila hata kushauriwa.
Yule mjinga kutoka pale kitandani alijirusha kinyumenyume sarakasi inayoitwa ‘back’, akatua upande wa pili na wakati huohuo alichomoa visu viwili na kuvirusha kwa umahiri kumwelekea Amata ambaye aliviona na kujitupa chini sakafuni na kuruhusu visu vile kukutana na ukuta. Kama ni kosa yule mjinga alilifanya hapo, alirukia kitandani ili atue upande wa pili ambapo alijua Kamanda Amata yuko chini, na Kamanda Amata alikwishajua nini yule bwana atafanya baada ya yeye kujitupa chini, na ndivyo ilivyokua, yule bwana alikanyaga kitanda na kujirusha upande wa pili, kabla hajafika chini, Kamanda Amata alirusha teke kali la na kiatu chake upande wa mbele kikapiga kwenye pingili za mwisho za uti wa mgongo ‘sacrum’ karibu na nyonga, yule bwana akajikuta kama anaishiwa nguvu za miguu, alijibamiza ukutani na kujibwaga chini kiama gunia, marehemu.
Kamanda Amata akasonya na kuiweka saa yake vizuri, kisha katika lile kabati akachukua kijitabu kidogo kutoka katika vitu vya Marehemu Gwamaka, akatia mfukoni, akajiongezea na vikolokolo vichache katika mifuko yake ya akiba, kisha akatoka kwa jinsi ileile aliyoingilia.
Walinzi waliowekwa doria upande wa chini, walikuwa bado wakizungukazunguka kutafuta wapi windo lao litatokea, labda hapa au pale lakini walikuta usiku unazidi kuwa mwingi na hakuna dalili za windo hilo kurudi.
Kiongozi wa kundi lile lililokuwa likiweka doria chini ya hoteli hiyo aliinua simu yake ya upepo na kupiga kwa mtu ambaye alimuweka ndani ya chumba cha hoteli ili kutoa taarifa pindi tu windo lao litakapofika. Simu iliita na kuita lakini hakuna jibu lolote.
“Hamsud, huyu jamaa mbona hapokei simu, hebu panda juu umwangalie,” akatoa maagizo kwa kijana mwingine. Yule aliyeagizwa akaweka pembeni bunduki yake na kutwaa bastola moja na kuipachika kiunoni, akashuka garini na kuzijongea ngazi za jengo hilo. Sekunde chache tu aliufikia mlango wa chumba kile, akagonga na kugonga lakini hakuna jibu lolote. Akatoa funguo Malaya, akajaribu kuufungua ule mlango, ukafunguka, lo, hakuamini alichokiona, alitazama mwili wa swahibaye uliokuwa umelala bila uhai.
“Shiiiiiiittttt!!!!” akang’aka kwa hasira, akarudisha mlango na kuufunga kama ulivyokuwa. Kisha kwa hatua fupifupi kama za mtu aliyelewa, Hamsud alijivuta na kuteremka chini.
“Vipi?” yule kiongozi alimuuliza.
“Hakuna mtu, amekufa,” Hamsud akajibu.
“What?” yule kiongozi alijishika kichwa kwa mshangao, akawa anazungukazunguka huku na kule. Akampiga kijikofi Hamsud na kuelekea naye ndani, walifika katika chumba na kutazama maafa waliyoyakuta. Yule kiongozi akaugeuza ule mwili wa yule marehemu. Akatikisa kichwa, na mikono yake akaiweka kiunoni mwake. Ametuzidi kete mwanaharamu huyu, yule kiongozi alijiwazia. Wakapekua makabati na kukuta peupe, Kamanda Amata aliondoka na kila kitu chake mle chumbani, kwa ujumla alihama, lakini hakuna aliyemuona kutoka nje.
§§§§§
Shabalah alishusha simu masikioni mwake akiwa amefura kwa hasira, alitamani amuone huyo mtu anyeitwa Amata ili amtafune kama ikibidi. Kama kuna kitu kilichomuuzi sana ni kitendo cha mtu wake kuuawa ndani ya hoteli pasina muuaji kuonekana. Shalabah alichanganyikiwa, akainua simu yake na kuwapa taarifa wengine wote ili kukomaza doria usiku huo, wakiwa wamepewa amri ya kuhakikisha Amata anapatikana ama mfu au hai.
Kituo cha mabasi cha W Sheikh Abaadir
KAMANDA Amata akatulia kwenye kona moja ya jengo lililokuwa na watu wengi, kila akitazama saa yake alikuwa akiona muda unamkimbia na wakati huo alikuwa akilitaka gari lake, alijua wazi kuwa kwa vyovyote wapo wanaomtega katika eneo hilo. Kamanda Amata aliamua la kuamua, akajivuta taratibu mpaka kwenye gari yake akainua mkono na kuitazama saa yake, akaizungusha kwa namna ya pekee kidogo, lengo ilikuwa ni kutazama kama kuna kitu chochote cha hatari ambacho kimetegwa katika gari hilo, alipoona kuna usalama, akafungua buti ili kuweka mabegi yake, lo, alijikuta akitazamana na mtutu wa shot gun, uso kwa uso, Kamanda Amata akamtazama mtu huyo aliyekuwa amelala ndani ya buti lile.
“Tumekukamata sasa, mshenzi wewe, umeshatuulia wenzetu wengi tu lakini leo hii ni zamu yako,” sauti ilitoka nyuma yake, alipogeuka tu alijikuta akikutana na konde zito lililotua shavuni mwake, hakuyumba, alisimama kidete akimtazama huyo aliyepiga konde hilo, Amata akajifuta pale lilipotua konde hilo. Wale waliofuatana na mtu huyo wakacheka kwa kitendo kile, Amata alichukizwa sana kwa hilo aliona kama anazihakiwa.
“Mpekue…” amri ilitoka.
Kamanda akapekuliwa na wakatoa bastola yake iliyokuwa kwenye kikoba maalumu.
“Yuko safi,” akajibu yule aliyekuwa akimpekua huku akimkabidhi yule kiongozi wao ile bastola. Kisha Kamanda Amata akafungwa pingu na kuingizwa kwenye land cruiser iliyofika wakati huo, kisha mmoja wale maharamia akatakiwa kuiendesha ile gari ya Amata. Kamanda Amata akawapatia rimoti kwa ajili ya kuendeshea gari ile, gari iliyokuwa ikitumia rimoti tu.
“Lala chini, unaangalia nini?” mtu mwingine alimuamuru Amata huku akimpiga na teke moja kali la usoni ambalo lilimpeleka chini, kisha wale jamaa wakasimama juu yake. Ile land cruiser ikawashwa..
MTUNZI: richard MWAMBE
“Sharon, usiku wa leo tuna wageni wengi uwanja wa ndege, naomba uchague vijana watano wazuri katika usalama uwaweke pale, wakiongozwa na wewe mwenyewe, msako wa huyo Hayawani muachie Fasendy, na vijana wengine wanakuja kushika nafasi za hao watano,” ilimaliza sauti ya Shalaba.
§§§§§§
Baada ya kuliacha gari alilokuwa amepanda kama mita mia tano hivi mtaa wa pili nyuma ya kile kituo cha mabasi, Amata alipita kwenye vibaraza vya maduka na kutokea nkwenye barabara kubwa inayoelekea katika kituo kile. Alisimama mbele ya duka kubwa la vyombo akitazama huku na kule, alijua kwa vyovyote vile lazima wamuwekee mtego katika gari lake, hivyuo aliamua kuwacheza shere, alikodi tax na moja kwa moja akaelekea hotelini kwake.
Mbele ya hoteli ile alijaribu kusoma sura za watu na akagundua kuwa kuna sura ambazo hawezi kuziamini hata kidogo, aliamua kuwabadilishia mchezo. Ilikuwa lzima afike katika chumba chake kwani kuna dokumenti alizokuwa akizihitaji kwa usiku huo.
Akazunguka nyuma ya hoteli na kuichunguza akagundua kuna mlango wa kutokea upande huo wa nyuma, akajaribu kuutikisa akakuta umefungwa, akatulia kimya kufikiri mara mbili la kufanya. Nukta hiyohiyo akasikia sauti za watu wanaoongea wakija upande wa nyuma wa hoteli ile, akajibana katikati ya mabomba mawili ya uchafu, yanayotiririsha majitaka toka juu kuleta chini. Walikuwa ni walinzi wa hoteli hiyo, walipompita aliamua kukwea kupitia yale mabomba. Chumba chake hakikuwa juu sana ilikuwa ni ghorofa ya tatu tu, hivyo haikumchukua muda kwa mtu kama yeye kufika usawa wa chumba chake, pale kulikuwa na kaukuta kalikojitokeza ambako kalikuwa kamebeba ndoo kadhaa za maua, akakanyaga kwa uangalifu kabisa asije kudondosha hata moja, alipohakikisha kuwa yuko usawa wa dirisha la chumba chake akalitikisa kidogo na lenyewe likatii amri, taratibu akaingia kupitia dirisha hilo kubwa lililoundwa kwa aluminiam safi, akatua ndani ya chumba hicho kwa madaha bila kufanya kelele yoyote kwani alijua kuwa lazima wapo wengine walio ndani.
Akakiendea kitanda chake na kukibonyezabonyeza, kilikuwa kimetulia kama kilivyo. Kamanda Amata akalisogelea kabati kubwa la nguo. Akashika kitasa cha mlango huo tayari kuuvuta lakini kengele za hatari kichwani mwake ziligonga, akajiandaa, kisha akavuta kwa nguvu ule mlango. Hakuwa tofauti na hisia zake, alipofuangua mlango tu, mtu mmoja aliyekuwa amejificha ndani ya kabati hilo alijitokeza kwa minajiri ya kumpamia Kamanda Amata, lo, Kamanda alipoufungua ule mlango tayari alikuwa kajiweka kando hivyo yule mtu akapitiliza peke yake na kumpita Amata ambaye alinyanyua mguu na kumpiga ngwala maridadi iliyomfanya mtu yule atue kwa uso katika sakafu na kuvunja mwamba wa pua. Kabla hajajigeuza, mguu mzito ulitua nyuma ya shingo yake na kumfanya mtu huyo kugugumia kwa maumivu. Amata akamwinamia palepale alipo na kumtazama mtu yule ambaye alikuwa chini, damu zikimvuja puani huku akilia kwa uchungu, lakini hakuweza hata kujigeuza kutokana na uzito wa guu la Amata.
“Wenzako wako wapi?” Kamanda alimuuliza.
“Niko pe-pe-ke ya-ngu,” alijibu kwa shida huku akijaribu kujiinua, lakini hakuweza kufanya hivyo.
“Unanitania sio?” Kamanda aliuliza na kumkanyaga kwa nguvu, yule mjinga pale chini alianza kutupatupa miguu na mikono kwa kutafuta pumzi.
“Ni-niiii-takwa-mbi-i-a,” alijibu. Kamanda Amata akalegeza mguu kidogo.
“Haya sema,”
“Wa-po nje,” akajibu.
“Wangapi?” Kamanada akahoji.
“Si- si… unaniumiza bwana,” yule mtu akashindwa kutoa jibu na badala yake akamtamkia maneno hayo Kamanda.
“Niambie, yule komandoo na wale wengine mmewaweka wapi?” akauliza tena.
“Si si – sijui mi-mi,” akajibu.
Muda huohuo saa ya Kamanda Amatav ikaanza kumfinya kwa fujo kuashiria kuna ujumbe ulikuwa ukiingi. Ni nafasi hiyohiyo ambayo yule mjinga pale chini aliitumia, alijigeuza kwa nguvu na kuwa chali akitaka sasa kusimama, teke moja kali nla Amata lilikuwa likienda kupiga korodani, yule bwana akaipanga mikono yake kwa mtindo wa x na kuchanua viganja vyake chini kidogo ya kiuno chake kusha akabonyea kufanya kama anachuchumaa, teka la Amata halikuwa pata lilipokusudiwa bali lilikingwa kwa hiyo mikono kwa usatdi kabisa. Kamanda Amata akaona akile ta mchezo hapo kazi itakuwa ngumu, wakati yule jamaa akiushusha mguu wa Amata chini mara tu baada ya kulipangua lile pigo kwa akili zote, kamanda Amata alishusha kichwa cha nguvu na katika paji ola uso la yule mjinga. Nyota zilimzunguka maana aliona kama kadondoshewa tofali, alipepesuka na kujibwaga kitandani, akajisjika pale alipopigwa kama kumepasuka lakini alishuhudia nundu lililojitokeza bila hata kushauriwa.
Yule mjinga kutoka pale kitandani alijirusha kinyumenyume sarakasi inayoitwa ‘back’, akatua upande wa pili na wakati huohuo alichomoa visu viwili na kuvirusha kwa umahiri kumwelekea Amata ambaye aliviona na kujitupa chini sakafuni na kuruhusu visu vile kukutana na ukuta. Kama ni kosa yule mjinga alilifanya hapo, alirukia kitandani ili atue upande wa pili ambapo alijua Kamanda Amata yuko chini, na Kamanda Amata alikwishajua nini yule bwana atafanya baada ya yeye kujitupa chini, na ndivyo ilivyokua, yule bwana alikanyaga kitanda na kujirusha upande wa pili, kabla hajafika chini, Kamanda Amata alirusha teke kali la na kiatu chake upande wa mbele kikapiga kwenye pingili za mwisho za uti wa mgongo ‘sacrum’ karibu na nyonga, yule bwana akajikuta kama anaishiwa nguvu za miguu, alijibamiza ukutani na kujibwaga chini kiama gunia, marehemu.
Kamanda Amata akasonya na kuiweka saa yake vizuri, kisha katika lile kabati akachukua kijitabu kidogo kutoka katika vitu vya Marehemu Gwamaka, akatia mfukoni, akajiongezea na vikolokolo vichache katika mifuko yake ya akiba, kisha akatoka kwa jinsi ileile aliyoingilia.
Walinzi waliowekwa doria upande wa chini, walikuwa bado wakizungukazunguka kutafuta wapi windo lao litatokea, labda hapa au pale lakini walikuta usiku unazidi kuwa mwingi na hakuna dalili za windo hilo kurudi.
Kiongozi wa kundi lile lililokuwa likiweka doria chini ya hoteli hiyo aliinua simu yake ya upepo na kupiga kwa mtu ambaye alimuweka ndani ya chumba cha hoteli ili kutoa taarifa pindi tu windo lao litakapofika. Simu iliita na kuita lakini hakuna jibu lolote.
“Hamsud, huyu jamaa mbona hapokei simu, hebu panda juu umwangalie,” akatoa maagizo kwa kijana mwingine. Yule aliyeagizwa akaweka pembeni bunduki yake na kutwaa bastola moja na kuipachika kiunoni, akashuka garini na kuzijongea ngazi za jengo hilo. Sekunde chache tu aliufikia mlango wa chumba kile, akagonga na kugonga lakini hakuna jibu lolote. Akatoa funguo Malaya, akajaribu kuufungua ule mlango, ukafunguka, lo, hakuamini alichokiona, alitazama mwili wa swahibaye uliokuwa umelala bila uhai.
“Shiiiiiiittttt!!!!” akang’aka kwa hasira, akarudisha mlango na kuufunga kama ulivyokuwa. Kisha kwa hatua fupifupi kama za mtu aliyelewa, Hamsud alijivuta na kuteremka chini.
“Vipi?” yule kiongozi alimuuliza.
“Hakuna mtu, amekufa,” Hamsud akajibu.
“What?” yule kiongozi alijishika kichwa kwa mshangao, akawa anazungukazunguka huku na kule. Akampiga kijikofi Hamsud na kuelekea naye ndani, walifika katika chumba na kutazama maafa waliyoyakuta. Yule kiongozi akaugeuza ule mwili wa yule marehemu. Akatikisa kichwa, na mikono yake akaiweka kiunoni mwake. Ametuzidi kete mwanaharamu huyu, yule kiongozi alijiwazia. Wakapekua makabati na kukuta peupe, Kamanda Amata aliondoka na kila kitu chake mle chumbani, kwa ujumla alihama, lakini hakuna aliyemuona kutoka nje.
§§§§§
Shabalah alishusha simu masikioni mwake akiwa amefura kwa hasira, alitamani amuone huyo mtu anyeitwa Amata ili amtafune kama ikibidi. Kama kuna kitu kilichomuuzi sana ni kitendo cha mtu wake kuuawa ndani ya hoteli pasina muuaji kuonekana. Shalabah alichanganyikiwa, akainua simu yake na kuwapa taarifa wengine wote ili kukomaza doria usiku huo, wakiwa wamepewa amri ya kuhakikisha Amata anapatikana ama mfu au hai.
Kituo cha mabasi cha W Sheikh Abaadir
KAMANDA Amata akatulia kwenye kona moja ya jengo lililokuwa na watu wengi, kila akitazama saa yake alikuwa akiona muda unamkimbia na wakati huo alikuwa akilitaka gari lake, alijua wazi kuwa kwa vyovyote wapo wanaomtega katika eneo hilo. Kamanda Amata aliamua la kuamua, akajivuta taratibu mpaka kwenye gari yake akainua mkono na kuitazama saa yake, akaizungusha kwa namna ya pekee kidogo, lengo ilikuwa ni kutazama kama kuna kitu chochote cha hatari ambacho kimetegwa katika gari hilo, alipoona kuna usalama, akafungua buti ili kuweka mabegi yake, lo, alijikuta akitazamana na mtutu wa shot gun, uso kwa uso, Kamanda Amata akamtazama mtu huyo aliyekuwa amelala ndani ya buti lile.
“Tumekukamata sasa, mshenzi wewe, umeshatuulia wenzetu wengi tu lakini leo hii ni zamu yako,” sauti ilitoka nyuma yake, alipogeuka tu alijikuta akikutana na konde zito lililotua shavuni mwake, hakuyumba, alisimama kidete akimtazama huyo aliyepiga konde hilo, Amata akajifuta pale lilipotua konde hilo. Wale waliofuatana na mtu huyo wakacheka kwa kitendo kile, Amata alichukizwa sana kwa hilo aliona kama anazihakiwa.
“Mpekue…” amri ilitoka.
Kamanda akapekuliwa na wakatoa bastola yake iliyokuwa kwenye kikoba maalumu.
“Yuko safi,” akajibu yule aliyekuwa akimpekua huku akimkabidhi yule kiongozi wao ile bastola. Kisha Kamanda Amata akafungwa pingu na kuingizwa kwenye land cruiser iliyofika wakati huo, kisha mmoja wale maharamia akatakiwa kuiendesha ile gari ya Amata. Kamanda Amata akawapatia rimoti kwa ajili ya kuendeshea gari ile, gari iliyokuwa ikitumia rimoti tu.
“Lala chini, unaangalia nini?” mtu mwingine alimuamuru Amata huku akimpiga na teke moja kali la usoni ambalo lilimpeleka chini, kisha wale jamaa wakasimama juu yake. Ile land cruiser ikawashwa..