Riwaya: Ukurasa wa gaidi

Riwaya: Ukurasa wa gaidi

Sasa naanza kusoma

Chief wew ukiona simulizi yangu usiwe na Shaka jua inaisha,sinaga ubabaishaji kama wana jamvi wengi walivyokariri ila huwa natoa tangazo kwa yeyote tu anashindwa kusubiri tunawasiliana nampa stor mwanzo mwisho

Tukutane kuanzia tareh ishirini Chief mzigo mwingine unakuja
 
Woyooooooo shemela wewe mkali hatari,shukrani sana nahongera kwa kipaji
 
Mara baada ya kushuka kutoka katika gari, Mick alitembea kuelekea kule aliko James Omolo.Alikwenda kwa namna ambayo hakuna aliyedhani kuwa kuna mtu anamfuata.Alipokuwa umbali wa hatua tatu kutoka alipo James Omolo ndipo alipoanza kuzungumza kwa sauti ya juu na kuwafanya watu wasiopenda shari wasogee pembeni.
inaendelea.........

"James Omolo, gaidi uliyesumbua sana Afrika na dunia kiujumla,uko chini ya ulinzi kuanzia sasa.Ukijaribu kubisha nina ruhusa ya kukumaliza hapahapa."
Baadhi ya watu walidhani ni utani na kama ilivyo jadi ya watanzania,baadhi hata walisogea kushangaa ni nini kilichoendelea.Ghafla Omolo alisimama na kutoa vitu vyote vya bandia alivyovivaa na kufanya aonekane katika uhalisia wake.Mara baadaa ya watu kumtambua, hawakujiuliza mara mbili.Walikimbia na kwenda kusimama mbali kabisa na eneo hilo.Kila mtu ndani na nje ya Afrika alimjua vizuri Omolo na matukio yake ya kigaidi na kikatili aliyowahi kuhusika nayo.
Mara baada ya kusimama, Omolo alianza kushuka ngazi na kumfanya Mick arudi chini kwa kushuka ngazi kinyume nyume hadi walipofika mwasho wa ngazi, mahali palipo na uwanja uliotengenezwa na lami.
Sasa hata watu waliopitaa barabarani walipaki magari yao pembeni na kuendelea kushuhudia mambo haya.
" I once heard that you are number one agent in your agency with the highest capability.But i'm yet to see what you got to be given such high position. I think your government is stupid and dumb.And your agency is useless.To day is your last day to breath.(Niliwahi kusikia kuwa wewe ni mpelelezi namba moja na mwenye uwezo wa juu katika idara yenu.Lakini sijaona bado ni kwa nini ulipewa nafasi hiyo ya juu.Nadhani serikali yako ni pumbavu.Na idara yako haina maana yoyote. Na leo nadhani ndiyo itakuwa ndiyo siku yako ya mwisho kuishi duniani)." Aliongea James Omolo kwa kejeli akiwa na lafudhi ya watu wa Afrika Magharibi.
"Fare well Mr. Omolo(Kwa heri bwana Omolo)."Aliongea Mick huku akitabasamu na kujiweka tayari kwa mapigano.
Omolo ndiye aliyeanzisha mapigano kwa kurusha makonde na mateke mazito mazito kwa ghafla.Lakini Mick aliyaona yote hayo.Aliyapangua kwa ustadi sana,japo baadhi yalimpata kutokana na ughafla alioanza nao Omolo.
Baada ya kujiweka sawa Mick naye akamshambulia Omolo kwa mapigo ambayo Omolo aliyaona na kuyakwepa na kupangua baadhi.Mapigano haya yaliendelea huku kila mmoja akibadili mitindo adhimu zaidi ya mapigano na bado hakuna aliyedondoshwa chini.
"Mr.Mick, i told you that you are useless.Say hello to the hell(Bwana Mick nilikwambia wewe huna lolote.Sasa wasalimie kuzimu).James Omolo alizungumza kwa kejeli.
Mick hakujibu kitu.Alitabasamu kwa muda kisha akaamua kuonesha sura ya kazi.Sasa alitambua kuwa muda wa maneno matupu umekwisha. Akajiweka katika mpangilio wa mapigano kisha akamuita James Omolo kwa ishara ya mkono.James akamfuata Mick kwa kasi ya ajabu huku akirusha ngumi na mateke kwa namna ya mchezo wa kung-fu. Mick aliyaona yote hayo na kuyakwepa huku akijibu mashambulizi kwa kuibia.
Mtindo huu alioutumia sasa Mick ulizaa matunda haraka.Mtu yeyote ambaye angemshuhudia Mick akipambana asingesita kutambua kuwa Mick alikuwa anajua anachokifanya kwa hali ya juu sana.Kila wakati ambao James Omollo alijaribu kurusha ngumi moja,alijikuta imekingwa kiustadi na kushambuliwa na ngumi mbili au tatu za haraka.Kama alidhani yeye ni mjuaji,basi leo alikutana na mjuvi wa mambo wa hali ya juu.
James Omollo alijaribu kutumia ujuzi wake na ujanja wake wote hata ule ambao kwa kawaida huwa anauweka akiba,lakini Mick alikuwa mbele yake hatua kadhaa kila wakati.Hakuwahi kukutana na upinzani kama huu tangu kuzaliwa kwake.Mara ya kwanza wakati wanaanza kupambana, James alidhani Mick alikuwa anapambana kwa uwezo wake wote na ndiyo kaana alimkejeli.Lakini sasa alitambua kuwa ule wa mwanzo haukufaa hata kuitwa uwezo mbele ya Mick. Kejeli na dharau zilikuwa zimemponza.
Sasa James Omolo alionekana dhahiri kuwa amezidiwa ubavu japo aliendelea kujikakamua.Lakini bado aliendelea kutoa matusi na kauliza dharau kwa Mick na nchi ya Tanzania kiujumla hukuakisema kuwa Tanzania haitaweza kushinda vita ya ugaidi ambayo imeichokonoa kamwe.Na badala yake,Tanzania itajutia kuanzisha vita hii.
Sasa Mick aliamua kummaliza kabisa.Kwanza akamuhadaa kama anataka kumpiga teke.James alipolikinga teke lile akajikuta amepigwa kwa ngumi nzito sana mbili za haraka za kifuani huku akimaliziwa na teke lililomvunja mbavu upande wa kulia.Kisha akapigwa ngwala na kuanguka chini.Kila alipojaribu kuamka akakutana na teke la mbavu tena.Mara apigwe kifuani.Mara akaanza kutapika damu Kwa wingi.Hapo Mick akaona haina haja ya kumkawiza, akamkaba shingoni kwa kiwiko.Kila Omolo alipojaribu kujinasua alishindwa kabisa.Mara akaanza kupoteza pumzi pole pole.
"Kawasalimie kuzimu."Mick aliongea kisha akamnyonga shingo hadi aliposikia sauti ya mvunjiko.Gaidi la kimataifa James Omolo alikuwa ni marehemu tayari.
Watu waliokuwapo eneo hilo bado walikuwa katika mshangao mkubwa sana.Walikuwa wameshuhudia mapambano haya ya ana kwa ana kwa muda wa nusu saa sasa.Walimshangaa kijana huyu aliyevalia nadhifu na akiwa na haiba na mvuto sana,namna alivyo mmaliza gaidi huyo kwa mapigano ya ana kwa ana. Muda wote walikuwa wakishangaa namna alivyopigana kwa ufundi mkali namna ile.Ilikuwa ni zaidi ya muvi kali sana ya mapigano.
Mara Mick alipommaliza James Omolo, aliubeba mwili wake na kuuweka katika gari aina ya Range rover ambalo alikuja nalo kisha akaondoa gari kwa kasi sana.Alikuwa anaelekea katika kambi la jeshi la JWTZ Mbalizi.
Alifika Mbalizi dakika chache sana baadaye. Taarifa za kufika kwa Mick zilikwisha fika kabla.Jina lililotambulika kwa sasa ni Luteni Juma Ahmedi.Askari wa Pale kambini wakamsaidia kutoa mwili na kuubeba kuupeleka maabara ambako maiti ingefanyiwa utafiti zaidi.
MASAA MAWILI NYUMA
Wakati ambao Mick alikuwa bado amepaki gari nje ya hospitali ya Meta, alipata kuwasiliana na ajenti Paul.Ajenti Paul alikuwa ana Taarifa Muhimu sana kwa Mick.
"Oya, tumembana James Peter kwa mbinu zilizoboreshwa na tumefanikiwa kumtapisha mambo mengi sana.Moja wapo ni kuhusu 'book of codes'. Ametuambia kuwa 'book of codes' ni mali ya James Omolo na ameificha mahali ambako hakuna anayejua.Ila pia ametuambia kuwa huwa mara zote alipo Omolo ndipo ilipo 'book of codes'."Ajenti Paul alitoa taarifa.
"Ok,bado niko katika harakati za kumpata huyo mwanaharamu.Nikimtia mikononi nitahakikisha kwanza nang'amua wapi alikoficha 'book of codes'."Mick alijibu.
Mara Mick alipokutana na Omolo nje ya jengo la TAZARA na kabla hata hawajaanza kupambana,Mick aligundua kitu tayari.Katika mkono wa kushoto juu kidogo ya kiwiko cha mkono,James Omolo alikuwa na kovu la jeraha lililoonekanakuwahi kushonwa.Mick alipolitazama kwa umakini wa kuibia,aligundua kuwa halikuwa kovu la jeraha lililotokea kiajali ajali.Kwa namna lilivyonyooka,Mick aligundua haraka kuwa inawezekana Omolo aliwahi kujikata kwa makusudi mahali hapo na kisha kujishona. Kwa uzoefu wa kazi ya kupambana na wahalifu kama hawa,Mick alijua kuwa inawezekana kabla ya kujishona mara baada ya kujikata kwa makusudi, James Omolo alificha kitu fulani kidogo mahali hapo alipojikata kisha akashonea kwa juu.Labda alishonea kitu ambacho ni cha siri sana au kingemuelekeza kuelekea kwenye kitu kilichofichwa kwa siri sana.Na labda kuna uhusiano na 'book of codes'.
Hata hivyo,Mick alitambua kuwa asingeweza kumtapisha siri yoyote James Omolo,hivyo akaamua kumuua kisha aendelee kutafuta 'book of codes' mwenyewe.
******************************
Maabara ndogo, Hospitali ya jeshi-JWTZ Mbalizi.
Mick alikuwa mbele ya mwili wa James Omolo ndani ya maabara hii.Macho yake yalikuwa yakiangalia katika mkono wa kulia juu kidogo ya kiwiko.Alikuwa akiangalia tena kile alichokiona kwa mara ya kwanza wakati akipambana naye nje ya jengo la ukumbi wa abiria TAZARA.
Wakati huu alikuwa ameshika kiwembe cha kufanyia operesheni mbele ya mwili huo. Mick aliushika mkono wa kulia wa marehemu James Omolo,kisha akauchana katika eneo lile la kovu lililokuwa na rangi nyeusi.Kisha akaingiza vidole vyake viwili katika sehemu ile alipopakata.Hapo alihisi ameshika kitu kigumu. Akakivuta na kukitoa.Kilikuwa ni kikasha kidogo cha plastiki ambacho kilijaa damu kwa nje.Mick alikifuta kikasha hicho kwa pamba safi iliyokuwa pembeni yake.Hapo kikasha kile kikaangaza kuonesha ndani kilikuwa na kitu.
Mick akakifungua kikasha kile.Ndani akakutana na kikadi kidogo cha kutunza kumbukumbu(Memory chip).Mick akatoa 'memory chip' na kuipachika katika simu yake ya kisasa kabisa kisha akajaribu kuminya hapa na pale ili kuifungua 'memory chip' ile. 'Memory chip' ikataka neno siri ili iweze kufunguka.Mick akaona isiwe shida.Alipanda gari lake na kuanza kuliendesha kwa kasi kuelekea Iringa,katika ofisi ya idara ya C.T.I ya muda.
MASAA MANNE BAADAYE.
Wataalamu wa kompyuta wa C.T.I walikwishafanyakazi yao. Morris na Clara walikwishafanikiwa kuifungua 'memory chip' iliyoletwa na ajenti Mick kwa ujanja ujanja wa udukuzi wa data na taarifa.
Mara baada ya kuifungua 'memory chip' ile,nyuso za tabasamu zilitawala ghafla katika nyusi zao.
"Bingo. 'Book of codes' .Sasa kilichobaki ni kumalizia kazi hii." Alizungumza Mick kwa furaha ya kukamilisha kazi hiyo kwa mafanikio mengi japo siyo yote.
Ndiyo.Mafanikio hayakufikia asilimia mia mbele ya dunia nzima kwa kuwa mlengwa mkuu wa mtafutano huu tangu mwanzo, Omar Al-Mahmood alikuwa bado hajakamatwa na kutiwa nguvuni kaa ambavyo ilitakiwa.Lakini kwa upande wa Tanzania,mtafutano huu uliibua maovu mengi yaliyowahi kufanyika na ambayo yalitarajia kufanyika.
Wataalamu wa kompyuta wa C.T.I sasa walibakisha kazi moja ili kuhakikisha mafanikio makubwa ya operesheni hii.Ilikuwa ni kutumia 'book of codes' kuyatambua majina ya wahusika wa uovu huu uliokuwa unatarajiwa kutimizwa, ambao ilisemekana walikiwa wako nddaniya serikali na baadhi ya watu maarufu zaidi nchini.Walikuwa katika kuhitimisha.
SOMALIA
Hali ya hewa ilikuwa ni upepo mkali sana na mvua za rasha rasha katika mtaa wa Madina jijini Mogadishu.Ndani ya jyumba moja ,baba mmoja pamoja na familia yake walikuwa katika wakati mgumu sana. Dakika chache zilizopita,familia hii ilipata ugeni ambao hawakuutarajia.Ugeni huu uliwahusisha watu wawili warefu, wembamba huku mikononi wakiwa wameshika bunduki aina ya AK 47.
"Jamani nisameheni,naahidi sitakamatwa na hata nikikamatwa sitatoa siri hadi siku nitakapokufa."Baba huyu wa familia aliyebeba tumbo kubwa lililotokana na kutumbua mali wakati alipokuwa madarakani nchini kwake kabla ya kutorokea katika nchi hii,alijaribu kujitetea.
"Wewe ako jinga sana.Sisi habana wesa achia wewe.Umesababisha mupango ya bosi yetu kuharibika kabisa.Wewe ametoroka ameacha makabrasha mengi muhimu yenye siri nyingi na sasa ako mikononi mwa serikali na amesha weza kutafsiri siri zetu.Sisi habana mucheso.Tutakachokusaidia tutakuua wewe peke ako.Hii ni nadra sana.Kawaida sisi alitakiwa kuua familia ote."Alijibu mmoja kwa kiswahili kibovu kilicho na lafudhi ya kisomali.
Baba yule hakuwa na la kusema zaidi ya kujutia kushirikiana na watu hawa ili kujineemesha na hata kutaka kuhusika kuiangamiza nchi yake kwa faida zake binafsi. Familia yote ililia sana lakini watu wale walitoka nje pamoja na mzee yule kisha wakafunga mlango nyuma yao.
Risasi nane zilimiminwa katika kifua cha baba yule wa familia na huo ndiyo ukawa mwisho wa maisha yake. Waziri wa ulinzi wa Tanzania ambaye aliisaliti nchi yake,alikiwa amepata hukumu ya kifo kutoka kwa watu wabaya ambao alishirikiana nao hapo awali.
*************************************
IKULU-Magogoni, Dar es salaam.
Rais George Katumba alikuwa katika kikao cha siri na mkurugenzi wa C.T.I pamoja na wanausalama wote kutoka ndani ya idara hii.Mkurugenzi wa C.T.I , alikuwa anakabidhi majina ya wasaliti waliotaka kuiuza serikali ya nchi mikononi mwa Magaidi wa Al-shabaab.Majina maarufu yalikuwa mengi.Yalijumuisha mawaziri,manaibu waziri,Wakuu wa mikoa,wafanyabiashara wakubwa na hata wakuu wa vyombo vya usalama.Mnyororo ulikuwa mrefu sana na ulihusisha wengi sana.
"Mumefanya kazi nzuri sana.Nimepigiwa simu kutoka Marekani,wamewapa sifa sana.Japokuwa hamjamkamata Omar Al-Mahmood, lakini mumemkamata Abdallah Yusoof,mtubaliyemfanikisha sana Omar Al-Mahmood.Pia mumefanikiwa kumuangamiza James Omolo, gaidi aliyesumbua dunia kwa muda mrefu.Mumeteketeza vikosi vya kigaidi ambavyo vingeweza kuja kuwa mwiba mchungu kwa serikali na nchi kiujumla.Mumefanikiwa kuwatambua wasaliti wa nchi hii. Ninawahakikishia kuwa ninawaamini sana.Waliopo katika majina haya watafilisiwa hadi senti ya mwisho na kisha watahukumiwa kwa mujibu wa sheria na watajuta kujihusisha na ugaidi wakati dunia nzima inaupinga."
"Sasa najua magaidi wataleta chokochoko nyingi huko mbeleni.Mimi ninawaahidi kuwa ofisi maalum ya rais itawasaidia na itawaboresha zaidi na zaidi kuliko hivi sasa."Alimaliza kuzungumza Rais George Katumba.
Wanausalama wa C.T.I nao waliongea mambo mbalimbali yanayohusu mipango ya usalama ya mbeleni hasa kwa upande wa vita dhidi ya ugaidi.Baada ya hapo kulifanyika tafrija ya siri ndani ya ikulu hiyo.Hakika ilikuwa siku ya furaha.
*************************************
"Mick unakwenda wapi kipindi hiki cha likizo?"Aliuliza Mkurugenzi wa C.T.I bwana Eliakim Makassy.Wakati huu maajenti wa C.T.I waalikiwa wakila chakula cha jioni katika hoteli moja kubwa ya kitalii ndani ya jiji la Dar es salaam.
"Narudi Ibiza kula bata na watoto wazuri mzee.Si unakumbuka ulikatisha likizo yangu."Alijibu Mick kwa masihara.
"Acha uhuni wewe.Inabidi uoe sasa.Vinginevyoutakufa kwa ngoma."Alidakia Paul.Naye aliongea kwa masihara.
"Amenishindwa mtu hatari Omolo,ngoma itaniwezea wapi babuuu"
"Alikushindwa wapi wakati alikuonea huruma ulivyokuwa unalialia."Aliongea Paul
"Nyie bakini hapa nchini.Omar Al-Mahmood akija tena mjiandae kukatwa vichwa."Mick aliongea kwa kucheka.
"Hahaaaaaa." Wote wakacheka kwa sauti huku wakigonganisha viganja.
**TAMATI**

Mwisho wa stori hii ni mwanzo wa stori nyingine.....stori inayofuata itakuwa na muendelezo wa mtafutano kati ya idara matata ya C.T.I na magaidi akiwamo Omar ambaye bado hajakamatwa...
Thanks kudo
 
Mara baada ya kushuka kutoka katika gari, Mick alitembea kuelekea kule aliko James Omolo.Alikwenda kwa namna ambayo hakuna aliyedhani kuwa kuna mtu anamfuata.Alipokuwa umbali wa hatua tatu kutoka alipo James Omolo ndipo alipoanza kuzungumza kwa sauti ya juu na kuwafanya watu wasiopenda shari wasogee pembeni.
inaendelea.........

"James Omolo, gaidi uliyesumbua sana Afrika na dunia kiujumla,uko chini ya ulinzi kuanzia sasa.Ukijaribu kubisha nina ruhusa ya kukumaliza hapahapa."
Baadhi ya watu walidhani ni utani na kama ilivyo jadi ya watanzania,baadhi hata walisogea kushangaa ni nini kilichoendelea.Ghafla Omolo alisimama na kutoa vitu vyote vya bandia alivyovivaa na kufanya aonekane katika uhalisia wake.Mara baadaa ya watu kumtambua, hawakujiuliza mara mbili.Walikimbia na kwenda kusimama mbali kabisa na eneo hilo.Kila mtu ndani na nje ya Afrika alimjua vizuri Omolo na matukio yake ya kigaidi na kikatili aliyowahi kuhusika nayo.
Mara baada ya kusimama, Omolo alianza kushuka ngazi na kumfanya Mick arudi chini kwa kushuka ngazi kinyume nyume hadi walipofika mwasho wa ngazi, mahali palipo na uwanja uliotengenezwa na lami.
Sasa hata watu waliopitaa barabarani walipaki magari yao pembeni na kuendelea kushuhudia mambo haya.
" I once heard that you are number one agent in your agency with the highest capability.But i'm yet to see what you got to be given such high position. I think your government is stupid and dumb.And your agency is useless.To day is your last day to breath.(Niliwahi kusikia kuwa wewe ni mpelelezi namba moja na mwenye uwezo wa juu katika idara yenu.Lakini sijaona bado ni kwa nini ulipewa nafasi hiyo ya juu.Nadhani serikali yako ni pumbavu.Na idara yako haina maana yoyote. Na leo nadhani ndiyo itakuwa ndiyo siku yako ya mwisho kuishi duniani)." Aliongea James Omolo kwa kejeli akiwa na lafudhi ya watu wa Afrika Magharibi.
"Fare well Mr. Omolo(Kwa heri bwana Omolo)."Aliongea Mick huku akitabasamu na kujiweka tayari kwa mapigano.
Omolo ndiye aliyeanzisha mapigano kwa kurusha makonde na mateke mazito mazito kwa ghafla.Lakini Mick aliyaona yote hayo.Aliyapangua kwa ustadi sana,japo baadhi yalimpata kutokana na ughafla alioanza nao Omolo.
Baada ya kujiweka sawa Mick naye akamshambulia Omolo kwa mapigo ambayo Omolo aliyaona na kuyakwepa na kupangua baadhi.Mapigano haya yaliendelea huku kila mmoja akibadili mitindo adhimu zaidi ya mapigano na bado hakuna aliyedondoshwa chini.
"Mr.Mick, i told you that you are useless.Say hello to the hell(Bwana Mick nilikwambia wewe huna lolote.Sasa wasalimie kuzimu).James Omolo alizungumza kwa kejeli.
Mick hakujibu kitu.Alitabasamu kwa muda kisha akaamua kuonesha sura ya kazi.Sasa alitambua kuwa muda wa maneno matupu umekwisha. Akajiweka katika mpangilio wa mapigano kisha akamuita James Omolo kwa ishara ya mkono.James akamfuata Mick kwa kasi ya ajabu huku akirusha ngumi na mateke kwa namna ya mchezo wa kung-fu. Mick aliyaona yote hayo na kuyakwepa huku akijibu mashambulizi kwa kuibia.
Mtindo huu alioutumia sasa Mick ulizaa matunda haraka.Mtu yeyote ambaye angemshuhudia Mick akipambana asingesita kutambua kuwa Mick alikuwa anajua anachokifanya kwa hali ya juu sana.Kila wakati ambao James Omollo alijaribu kurusha ngumi moja,alijikuta imekingwa kiustadi na kushambuliwa na ngumi mbili au tatu za haraka.Kama alidhani yeye ni mjuaji,basi leo alikutana na mjuvi wa mambo wa hali ya juu.
James Omollo alijaribu kutumia ujuzi wake na ujanja wake wote hata ule ambao kwa kawaida huwa anauweka akiba,lakini Mick alikuwa mbele yake hatua kadhaa kila wakati.Hakuwahi kukutana na upinzani kama huu tangu kuzaliwa kwake.Mara ya kwanza wakati wanaanza kupambana, James alidhani Mick alikuwa anapambana kwa uwezo wake wote na ndiyo kaana alimkejeli.Lakini sasa alitambua kuwa ule wa mwanzo haukufaa hata kuitwa uwezo mbele ya Mick. Kejeli na dharau zilikuwa zimemponza.
Sasa James Omolo alionekana dhahiri kuwa amezidiwa ubavu japo aliendelea kujikakamua.Lakini bado aliendelea kutoa matusi na kauliza dharau kwa Mick na nchi ya Tanzania kiujumla hukuakisema kuwa Tanzania haitaweza kushinda vita ya ugaidi ambayo imeichokonoa kamwe.Na badala yake,Tanzania itajutia kuanzisha vita hii.
Sasa Mick aliamua kummaliza kabisa.Kwanza akamuhadaa kama anataka kumpiga teke.James alipolikinga teke lile akajikuta amepigwa kwa ngumi nzito sana mbili za haraka za kifuani huku akimaliziwa na teke lililomvunja mbavu upande wa kulia.Kisha akapigwa ngwala na kuanguka chini.Kila alipojaribu kuamka akakutana na teke la mbavu tena.Mara apigwe kifuani.Mara akaanza kutapika damu Kwa wingi.Hapo Mick akaona haina haja ya kumkawiza, akamkaba shingoni kwa kiwiko.Kila Omolo alipojaribu kujinasua alishindwa kabisa.Mara akaanza kupoteza pumzi pole pole.
"Kawasalimie kuzimu."Mick aliongea kisha akamnyonga shingo hadi aliposikia sauti ya mvunjiko.Gaidi la kimataifa James Omolo alikuwa ni marehemu tayari.
Watu waliokuwapo eneo hilo bado walikuwa katika mshangao mkubwa sana.Walikuwa wameshuhudia mapambano haya ya ana kwa ana kwa muda wa nusu saa sasa.Walimshangaa kijana huyu aliyevalia nadhifu na akiwa na haiba na mvuto sana,namna alivyo mmaliza gaidi huyo kwa mapigano ya ana kwa ana. Muda wote walikuwa wakishangaa namna alivyopigana kwa ufundi mkali namna ile.Ilikuwa ni zaidi ya muvi kali sana ya mapigano.
Mara Mick alipommaliza James Omolo, aliubeba mwili wake na kuuweka katika gari aina ya Range rover ambalo alikuja nalo kisha akaondoa gari kwa kasi sana.Alikuwa anaelekea katika kambi la jeshi la JWTZ Mbalizi.
Alifika Mbalizi dakika chache sana baadaye. Taarifa za kufika kwa Mick zilikwisha fika kabla.Jina lililotambulika kwa sasa ni Luteni Juma Ahmedi.Askari wa Pale kambini wakamsaidia kutoa mwili na kuubeba kuupeleka maabara ambako maiti ingefanyiwa utafiti zaidi.
MASAA MAWILI NYUMA
Wakati ambao Mick alikuwa bado amepaki gari nje ya hospitali ya Meta, alipata kuwasiliana na ajenti Paul.Ajenti Paul alikuwa ana Taarifa Muhimu sana kwa Mick.
"Oya, tumembana James Peter kwa mbinu zilizoboreshwa na tumefanikiwa kumtapisha mambo mengi sana.Moja wapo ni kuhusu 'book of codes'. Ametuambia kuwa 'book of codes' ni mali ya James Omolo na ameificha mahali ambako hakuna anayejua.Ila pia ametuambia kuwa huwa mara zote alipo Omolo ndipo ilipo 'book of codes'."Ajenti Paul alitoa taarifa.
"Ok,bado niko katika harakati za kumpata huyo mwanaharamu.Nikimtia mikononi nitahakikisha kwanza nang'amua wapi alikoficha 'book of codes'."Mick alijibu.
Mara Mick alipokutana na Omolo nje ya jengo la TAZARA na kabla hata hawajaanza kupambana,Mick aligundua kitu tayari.Katika mkono wa kushoto juu kidogo ya kiwiko cha mkono,James Omolo alikuwa na kovu la jeraha lililoonekanakuwahi kushonwa.Mick alipolitazama kwa umakini wa kuibia,aligundua kuwa halikuwa kovu la jeraha lililotokea kiajali ajali.Kwa namna lilivyonyooka,Mick aligundua haraka kuwa inawezekana Omolo aliwahi kujikata kwa makusudi mahali hapo na kisha kujishona. Kwa uzoefu wa kazi ya kupambana na wahalifu kama hawa,Mick alijua kuwa inawezekana kabla ya kujishona mara baada ya kujikata kwa makusudi, James Omolo alificha kitu fulani kidogo mahali hapo alipojikata kisha akashonea kwa juu.Labda alishonea kitu ambacho ni cha siri sana au kingemuelekeza kuelekea kwenye kitu kilichofichwa kwa siri sana.Na labda kuna uhusiano na 'book of codes'.
Hata hivyo,Mick alitambua kuwa asingeweza kumtapisha siri yoyote James Omolo,hivyo akaamua kumuua kisha aendelee kutafuta 'book of codes' mwenyewe.
******************************
Maabara ndogo, Hospitali ya jeshi-JWTZ Mbalizi.
Mick alikuwa mbele ya mwili wa James Omolo ndani ya maabara hii.Macho yake yalikuwa yakiangalia katika mkono wa kulia juu kidogo ya kiwiko.Alikuwa akiangalia tena kile alichokiona kwa mara ya kwanza wakati akipambana naye nje ya jengo la ukumbi wa abiria TAZARA.
Wakati huu alikuwa ameshika kiwembe cha kufanyia operesheni mbele ya mwili huo. Mick aliushika mkono wa kulia wa marehemu James Omolo,kisha akauchana katika eneo lile la kovu lililokuwa na rangi nyeusi.Kisha akaingiza vidole vyake viwili katika sehemu ile alipopakata.Hapo alihisi ameshika kitu kigumu. Akakivuta na kukitoa.Kilikuwa ni kikasha kidogo cha plastiki ambacho kilijaa damu kwa nje.Mick alikifuta kikasha hicho kwa pamba safi iliyokuwa pembeni yake.Hapo kikasha kile kikaangaza kuonesha ndani kilikuwa na kitu.
Mick akakifungua kikasha kile.Ndani akakutana na kikadi kidogo cha kutunza kumbukumbu(Memory chip).Mick akatoa 'memory chip' na kuipachika katika simu yake ya kisasa kabisa kisha akajaribu kuminya hapa na pale ili kuifungua 'memory chip' ile. 'Memory chip' ikataka neno siri ili iweze kufunguka.Mick akaona isiwe shida.Alipanda gari lake na kuanza kuliendesha kwa kasi kuelekea Iringa,katika ofisi ya idara ya C.T.I ya muda.
MASAA MANNE BAADAYE.
Wataalamu wa kompyuta wa C.T.I walikwishafanyakazi yao. Morris na Clara walikwishafanikiwa kuifungua 'memory chip' iliyoletwa na ajenti Mick kwa ujanja ujanja wa udukuzi wa data na taarifa.
Mara baada ya kuifungua 'memory chip' ile,nyuso za tabasamu zilitawala ghafla katika nyusi zao.
"Bingo. 'Book of codes' .Sasa kilichobaki ni kumalizia kazi hii." Alizungumza Mick kwa furaha ya kukamilisha kazi hiyo kwa mafanikio mengi japo siyo yote.
Ndiyo.Mafanikio hayakufikia asilimia mia mbele ya dunia nzima kwa kuwa mlengwa mkuu wa mtafutano huu tangu mwanzo, Omar Al-Mahmood alikuwa bado hajakamatwa na kutiwa nguvuni kaa ambavyo ilitakiwa.Lakini kwa upande wa Tanzania,mtafutano huu uliibua maovu mengi yaliyowahi kufanyika na ambayo yalitarajia kufanyika.
Wataalamu wa kompyuta wa C.T.I sasa walibakisha kazi moja ili kuhakikisha mafanikio makubwa ya operesheni hii.Ilikuwa ni kutumia 'book of codes' kuyatambua majina ya wahusika wa uovu huu uliokuwa unatarajiwa kutimizwa, ambao ilisemekana walikiwa wako nddaniya serikali na baadhi ya watu maarufu zaidi nchini.Walikuwa katika kuhitimisha.
SOMALIA
Hali ya hewa ilikuwa ni upepo mkali sana na mvua za rasha rasha katika mtaa wa Madina jijini Mogadishu.Ndani ya jyumba moja ,baba mmoja pamoja na familia yake walikuwa katika wakati mgumu sana. Dakika chache zilizopita,familia hii ilipata ugeni ambao hawakuutarajia.Ugeni huu uliwahusisha watu wawili warefu, wembamba huku mikononi wakiwa wameshika bunduki aina ya AK 47.
"Jamani nisameheni,naahidi sitakamatwa na hata nikikamatwa sitatoa siri hadi siku nitakapokufa."Baba huyu wa familia aliyebeba tumbo kubwa lililotokana na kutumbua mali wakati alipokuwa madarakani nchini kwake kabla ya kutorokea katika nchi hii,alijaribu kujitetea.
"Wewe ako jinga sana.Sisi habana wesa achia wewe.Umesababisha mupango ya bosi yetu kuharibika kabisa.Wewe ametoroka ameacha makabrasha mengi muhimu yenye siri nyingi na sasa ako mikononi mwa serikali na amesha weza kutafsiri siri zetu.Sisi habana mucheso.Tutakachokusaidia tutakuua wewe peke ako.Hii ni nadra sana.Kawaida sisi alitakiwa kuua familia ote."Alijibu mmoja kwa kiswahili kibovu kilicho na lafudhi ya kisomali.
Baba yule hakuwa na la kusema zaidi ya kujutia kushirikiana na watu hawa ili kujineemesha na hata kutaka kuhusika kuiangamiza nchi yake kwa faida zake binafsi. Familia yote ililia sana lakini watu wale walitoka nje pamoja na mzee yule kisha wakafunga mlango nyuma yao.
Risasi nane zilimiminwa katika kifua cha baba yule wa familia na huo ndiyo ukawa mwisho wa maisha yake. Waziri wa ulinzi wa Tanzania ambaye aliisaliti nchi yake,alikiwa amepata hukumu ya kifo kutoka kwa watu wabaya ambao alishirikiana nao hapo awali.
*************************************
IKULU-Magogoni, Dar es salaam.
Rais George Katumba alikuwa katika kikao cha siri na mkurugenzi wa C.T.I pamoja na wanausalama wote kutoka ndani ya idara hii.Mkurugenzi wa C.T.I , alikuwa anakabidhi majina ya wasaliti waliotaka kuiuza serikali ya nchi mikononi mwa Magaidi wa Al-shabaab.Majina maarufu yalikuwa mengi.Yalijumuisha mawaziri,manaibu waziri,Wakuu wa mikoa,wafanyabiashara wakubwa na hata wakuu wa vyombo vya usalama.Mnyororo ulikuwa mrefu sana na ulihusisha wengi sana.
"Mumefanya kazi nzuri sana.Nimepigiwa simu kutoka Marekani,wamewapa sifa sana.Japokuwa hamjamkamata Omar Al-Mahmood, lakini mumemkamata Abdallah Yusoof,mtubaliyemfanikisha sana Omar Al-Mahmood.Pia mumefanikiwa kumuangamiza James Omolo, gaidi aliyesumbua dunia kwa muda mrefu.Mumeteketeza vikosi vya kigaidi ambavyo vingeweza kuja kuwa mwiba mchungu kwa serikali na nchi kiujumla.Mumefanikiwa kuwatambua wasaliti wa nchi hii. Ninawahakikishia kuwa ninawaamini sana.Waliopo katika majina haya watafilisiwa hadi senti ya mwisho na kisha watahukumiwa kwa mujibu wa sheria na watajuta kujihusisha na ugaidi wakati dunia nzima inaupinga."
"Sasa najua magaidi wataleta chokochoko nyingi huko mbeleni.Mimi ninawaahidi kuwa ofisi maalum ya rais itawasaidia na itawaboresha zaidi na zaidi kuliko hivi sasa."Alimaliza kuzungumza Rais George Katumba.
Wanausalama wa C.T.I nao waliongea mambo mbalimbali yanayohusu mipango ya usalama ya mbeleni hasa kwa upande wa vita dhidi ya ugaidi.Baada ya hapo kulifanyika tafrija ya siri ndani ya ikulu hiyo.Hakika ilikuwa siku ya furaha.
*************************************
"Mick unakwenda wapi kipindi hiki cha likizo?"Aliuliza Mkurugenzi wa C.T.I bwana Eliakim Makassy.Wakati huu maajenti wa C.T.I waalikiwa wakila chakula cha jioni katika hoteli moja kubwa ya kitalii ndani ya jiji la Dar es salaam.
"Narudi Ibiza kula bata na watoto wazuri mzee.Si unakumbuka ulikatisha likizo yangu."Alijibu Mick kwa masihara.
"Acha uhuni wewe.Inabidi uoe sasa.Vinginevyoutakufa kwa ngoma."Alidakia Paul.Naye aliongea kwa masihara.
"Amenishindwa mtu hatari Omolo,ngoma itaniwezea wapi babuuu"
"Alikushindwa wapi wakati alikuonea huruma ulivyokuwa unalialia."Aliongea Paul
"Nyie bakini hapa nchini.Omar Al-Mahmood akija tena mjiandae kukatwa vichwa."Mick aliongea kwa kucheka.
"Hahaaaaaa." Wote wakacheka kwa sauti huku wakigonganisha viganja.
**TAMATI**

Mwisho wa stori hii ni mwanzo wa stori nyingine.....stori inayofuata itakuwa na muendelezo wa mtafutano kati ya idara matata ya C.T.I na magaidi akiwamo Omar ambaye bado hajakamatwa...
Leo nimefufua tena hili kaburi....aiseeh nime enjoy sana.

Hongera bwana Kudo, kwa utunzi mahiri.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom