Riwaya: Ukurasa wa gaidi

Mkuu, kwanza nikupongeze, pili weka uandishi ktk parandensi, tatu ahidi kwa maneno yako ni siku zipi utaweka hii hadithi, na kisia kwa mtililiko huo unatataji kuimaliza lini?
 
Mkuu, kwanza nikupongeze, pili weka uandishi ktk parandensi, tatu ahidi kwa maneno yako ni siku zipi utaweka hii hadithi, na kisia kwa mtililiko huo unatataji kuimaliza lini?
Nieleweshe kuhusu hili neno parandesi lina maana gani
Uongo mbaya moja ya masomo niliofeli ni kiswahili na uandishi ni hobi yangu tu nielekeze Chief

Nitaweka riwaya kila niwapo na salio kama sina hamataniona ova
 
Nieleweshe kuhusu hili neno parandesi lina maana gani
Uongo mbaya moja ya masomo niliofeli ni kiswahili na uandishi ni hobi yangu tu nielekeze Chief

Nitaweka riwaya kila niwapo na salio kama sina hamataniona ova
Parandensi ni paragraph au aya mkuu tuliosoma kipindi cha analogia tulijifunza enzi hzo ukimaliza la saba sawa na form 6 ya sasa,

Natania tu mkuu..

Utanipiem no ntakuwa nakutumia bando...
 
IRINGA
SAFE HOUSE
Hadi kufikia siku iliyofuata asubuhi, idara yote ilikuwa imehamia Iringa katika moja ya nyumba ambazo inazimiliki Tanzania. Katika mikoa yote iliyo jirani na mikoa iliyo mpakani mwa nchi,C.T.I ilimiliki nyumba moja kama hii. Kwa kuwa mkoa wa Mbeya unapakana na nchi ya Malawi na Zambia, nyumba ilijengwa katika mkoa jirani wa Iringa.
Kiuhalisia si kwamba nyumba ilikuwa mpya. Nyumba ile ilikuwa imefanyiwa ukarabati kutoka kuwa ghala la chakula na kurekebishwa kuwa jumba la kisasa sana.Jumba hili lilikuwa na vyumba kadhaa vya kulala pamoja na ofisi kubwa na ofisi ndogo ndogo pamoja na vitu vingine vingi sana.Hata namna ya kuingia katika nyumba ile haikuwa kazi nyepesi. Kulikuw na vitasa vya kisasa katika nyumba hii ambavyo vilihitaji namba ya siri, alama za vidole pamoja na mtazamo wa mboni ya jicho ili kufungua.Walio weza kuingia ndani ya nyumba hii ni wale wahusika tu. Hawa ndio pekee ambao teknolojia inayohusika kwa sababu za usalama katika nyumba hii ilikuwa imelishwa taarifa zao.
Maajenti wa idara hii ya CTI,walikuwa wamekusanyika katika ofisi kubwa ya pamoja wakifanya hili na lile pamoja na kupanga hiki na kile ili mradi kuweka mambo sawa.Chumba hiki cha ofisi, kilikuwa kimetawaliwa na kompyuta kadhaa zilizounganishwa kwa utaalamu wa hali ya juu huku zikitumia 'soft wares' za kisasa kabisa zinazohusika na kazi hii ya upelelezi. Yaani kwa kifupi kazi ilikuwa inaanza kuoamba moto rasmi wakati huu.
********************************************************
"Clara, hebu jaribu ku-hack mfumo wa kamera za CCTV za jeshi kikosi cha jkt Mafinga uangalie kilichorekodiwa kwa muda wa wiki moja nyuma kabla ya tukio kutokea." Aliongea Mick na kusikika kwa ajenti Clara upande wa pili kupitia kifaa cha mawasiliano alichokivaa sikioni.
"Ok acha nifanye yangu ".Alijibu Clara kutoka upande wa pili na kisha sauti ya vitufe vya kompyuta ikaanza kusikika ikibonyezwa bonyezwa kwa kasi ya ajabu.
Wakati huu ambao wawili hao walikuwa wanawasiliana, Clara alikuwa yupo ofisini wakati Mick yupo msituni,mahali ambapo palitokea tukio siku mbili tatu nyuma.Tukio lililosababisha wanaidara wa C.T.I kujikuta wana jukumu zito la kufanya mara baada ya kuwa na majukumu ya kawaida tu kwa muda mrefu.
Tangu asubuhi,wakati idara yote ya C.T.I ilipokuwa imewasili katika eneo hili, Mick alikwenda mahali pale na kuanza kazi yake eneo la tukio mara moja.Akiwa amekwishapata taarifa za awali za nini kilichojiri,moja kwa moja Mick alijua ni wapi pa kuanzia. Alikumbuka moja ya kauli mbiu ya idara yake iliyosema "katika tukio lolote, ni vizuri na lazima upelelezi uanzie eneo la tukio kwa sababu ndiyo mahali pekee ambapo utapata ushahidi au fununu zitakazokupeleka kwenye ushahidi". Na ni ukweli mtupu unaoongelewa katika kauli mbiu hii.Idara yoyote ya usalama duniani inapofanya upelelezi wa tukio fulani,ni lazima itafika eneo la tukio kwa sababu ya mambo mawili.Ushahidiau fununu au kama mataifa ya magharibi yaliyotufundisha mambo haya wanavyosema kwa lugha yao 'either clue or evidence'.
Kwanza kabisa baada ya kufika eneo la tukio,ajenti Mick alimuhoji mmoja wa askari waliokuwa wanalinda eneo hilo.Wakati alipomuhoji,Mick aliweza kung'amua kuwa magaidi wale walikhwapo muda mrefu,pengine masaa mawili matatu kabla ya msafara kupita na kushambuliwa.Aling'amua kuwa magaidi wale walikuja kwa pamoja eneo hilo na kisha wakatawanyika kila upande nyuma ya misitu ya eneo lile la tukio na ndiyo maana ilikuwa vigumu kupambana nao.Pia alihisi,kwa jinsi eneo lilivyokuwa msituni basi magaidi hawa yawezekana waliletwa eneo lile kwa usafiri fulani mahali pale.Kwa maelezo ya askari aliyehojiwa Mick ,aliweza kung'amua upande ambao inawezekana ndiko magaidi wale walikoikia kabla ya kutawanyika kuzingira eneo lote.
Ndiyo.Ilikuwa ni rahisi kwa Mick kung'amua mambo haya kutokana na maelezo ya askari yule wa weledi wa E.C.S waliokuwa chini ya C.T.I ambaye alikuwa miongoni mwa askari waliokuwa wakilinda eneo lile la tukio ili ushahidi usipotee.Kilichopelekea askari yule kutoa maelezo kwa kina ni kwa kuwa pia alikuwa ni miongoni mwa askari waliosindikiza msafara uke uliovamiwa.Askari yule alimueleza ajenti Mick upande ambao risasi nzito zaidi kutoka kwa adui ziliwashambulia.Na ni upande huo huo ambako upinzani mkubwa ulitokea kuliko upande wowote.Mick aliposikia hayo aliweza kuhisi kuwa yawezekana upande huo ndiko upande ambao adui walikuwa wengi zaidi.Pia yawezekana risasi nzito kwa maelezo ya askari,zilitokea katika bunduki nzito nzito zilizofungwa katika magari ya adui.Basi kwa kusikiliza hayo na kuyachambua kichwani Mick aliuhisi upande huo na kuanza kufuatilia,akitokea barabara ya lami na kuingia msituni.
Mick alipasua msitu na kuukabili hadi kilometa moja na nusu msitu ukipoishia. Wakati huu wote,alikuwa anafuata njia za vumbi ambazo zilitawaliwa na tope katika msimu huu wa mvua Akitumia gari alilokabidhiwa,aina ya Range rover sport nyeusi iliyong'ara sana,Mick alifuatisha barabara ya vumbi iliyokuwa inapita nyuma,upande wa pili wa msitu huu kwa umbali wa kilomita moja tena. Kama ingepigwa picha kutoka juu sana,ama kama ilivyoonekana kwa picha za satelite, barabara hii ilikuwa upande wa pili wa msitu huu wa 'mipaina' ikionekana kwenda ki-msambamba na barabara ya lami.
Kilomita moja mbele ,Mick aliweza kung'amua alama za matairi ya magari zinazoingia msituni.Kilichompa dukuduku zaidi kuwa huenda hicho ndicho alichokuwa ankitafuta,ni kuwa alama zile zilizojichora katika tope zilionesha kuwa magari zaidi ya nane yalipita eneo hili na kuchepuka kuingia msituni.Alama hizi zilinoga zaidi eneo la miti michanga ambapo miti ilikanyagwa sana.Akiwa ameshuka kutoka garini,kwa miguu yake Mick alipasua pori na kuanza kufuatilia matairi hayo huku bastola yake aina ya bereta ikiwa kiunoni na ile ndogo ya 'colt 45' ikiwa imepachikwa katika soksi mguu wa kulia.Kufuatilia huku kulimpeleka hadi mita 300 ndani ya msitu ule,eneo ambalo alama za matairi ya magari yale ziliishia.Hapo Mick aliona kitu ambacho kilimuhakikishia kuwa adui walifikia katika eneo hili na kisha kutawanyika.Eneo lilikuwa limetawaliwa na maganda ya risasi kwa uwingi hasa. Maganda ya risasi kutoka katika bunduki nzito nzito yalikuwa yametawanyika katika eneo hili.Bunduki ambazo aidha zilikuwa zimefungwa kwenye magari au hata kama zilibebwa na magaidi wale basi wasingeweza kutembea nazo kwa umbali mrefu kutoka katika gari kutokana na uzito wake.Hili nalo lilizidi kumthibitishia kuwa hapa ndipo maadui walifikia nakutawanyika kufanya mashambulizi.
Baada ya kujihakikishia kwa hili,Mick alirudi katika gari lake na kuanza kufuatilia alama zile.za magari zilizokatisha msituni na kuishia mahali alikokuta maganda ya risasi mengi,upande zilikotokea kabla yakukatisha porini hapo.
Akiwa anaendesha gari lake huku akifuatilia alama za matairi za magari haya mahali zilikotokea, alama hizi zilimpeleka kilomita nane mbele,mahali ambako barabara hii ilipita nyuma ya kambi la jeshi la kujenga taifa.Kambi ya Mafinga.
Hapa Mick aliona alama za matairi zikiwa zimechepuka kidogo na kisha mbele kurudi usawa wa mwanzo.Alama hii ilikuwa ni ya matairi ya gari dogo.Mick alipaki gari pembeni, akashuka na kuchuchumaa kuangalia kwa umakini alama zile huku akionekana kutafakari jambo.
"Hapa yalipita magari madogo mawili na makubwa au labda malori sita.Kati ya haya magari makubwa kulikuwa na magari aina ya TATA mawili, IVECO mawili na ISUZU mawili.Hapa alama za matairi zinazoonekana kwenda pembeni kidogo nakisha kurudi usawa wa mwanzo na kutengeneza 'curve', kuna gari moja kati ya magari makubwa lilipaki kando na kisha kuendelea na safari,labda kuna jambo wahusika walifanya nje ya gari."Aliwaza ajenti Mick ndani ya kichwa chake.Kisha akageuka nyuma na kuona ukuta wa fensi upande wa nyuma wa kambi hilo ulivyo mrefu.Kisha baada ya ukuta huo kwa ndani kulikuwa na msitu wa miti mingi aina ya milingoti na miti ya matunda mingi. Majengo hayakuonekana labda utumie kiona mbali kutokana na msitu ulivyoshona mahali hapo,hivyo Mick akatambua kuwa si rahisi kwa walio ndani kujua nini kinaendelea nje.Lakini alipokaza macho vizuri, aliona kamera za CCTV zilizofungwa kwa juu katika jengo hilo ambapo kama si utaalamu na uzoefu wa kazi yake pengine asingeziona.
Na hapo ndipo alipowasiliana na ajenti Clara ili amsaidie kwa utundu wa kompyuta kuingilia mfumo wa kamera hizi na ikiwezekana kuibia mambo yaliyorekodiwa nyakati za tukio lile lilipotokea.
Mara baada ya kuwasiliana na ajenti Clara,Mick alirudi katika gari lake na kuendelea kufuatilia alama za matairi alizokuwa anazifuatilia tangu mwanzo.Alifuatilia zilikotokea kabla ya eneo hili alikotoka.Mbelealimaliza eneo la usawa wa jeshi.Mbele kidogo ya hapo alikutana na magari yanayobeba mbao yakitokea katika upande mmoja wa barabara hii ya tope na kwenda porini kwa kufuata barabara nyingine.Hii barabara iliyofuatwa na malori haya na ile inayotoka nyuma ya jeshi zimeunganishwa kwa barabara moja huko zilikotokea.Kwa sababu hiyo ikawa siyo rahisi kwa Mick kuweza kuendelea kung'amua alama zile za matairi alizokuwa anazifuatilia kwani zilichanganyika na alama za matairi za malori yale naa pengine zilifutwa kabisa na kubaki alama za malori yale.
Akiwa amekata tamaa ya kufuatilia kile alichokuwa anakifuatilia,akaona si vibaya akiuliza kitu kutoka kwa bwana mmoja aliyekuwa akibadilisha tairi katika roli lake lililokuwa tupu.Bwana huyu alionekana kama ndiye dereva wa gari lile na kwa upande ambao gari lake lilitazama,ilionekana kuwa ndiyo anaenda kufuata mzigo wa mbao.
"Samahani braza".Mick alianzisha mazungumzo na dreva yule ambaye ndiyo kwanza alikuwa amegundua kuwa kuna mtu nyuma yake.
"Bila samahani kaka sijui nikusaidie nini".Alijibu kwa staha dreva yule hasa kutokana na unadhifu wa huyu mgeni wa ghafla(Mick).Ama kwa hakika jinsi dreva huyu alivyoongea kwa adabu ungeweza kudhani kuwa madreva wa malori ni watu wa staarabu sana.Lakini kumbe...........
"Hivi ni kwa nini mnapita njia ndefu na malori yenu. Mbona kuna njia fupi hii inayopita nyuma ya jeshi au wajeda wanamaindi nini.?" Alihoji Mick.
Yule dreva aliyeulizwa swali hili akamuangalia Mick usoni kwa sekunde kadhaa kwa kukereka kisha akafungua mdomo wake.
"Hivi blaza mbona unapenda kusumbua watu kwa maswali ya kiboya.Mi nilikuona kama mstaarabu kumbe hovyo tu.Au tuseme hujui kusoma.Pita uone utakavyo chezea vitasa hadi ujinyee".Alijibu kwa jazba dreva yule huku akinyoosha kidole mahali fulani kama vile anataka Kumuonesha Mick kitu fulani upande wa kushoto kwake.
Mick alipogeuka kutazama upande ule ndiyo kwanza aliona kibao kilichoandikwa " ILANI. NI MARUFUKU KUPITA BARABARA HII NYUMA YA KAMBI.UKIPATIKANA UTAONA CHA MOTO."Kibao kile kilijieleza.
"Bas poa blaza.Shika hii ya maji."Aliongea tena Mick huku akimkabidhi dreva yule noti tatu za shilingi elfu kumi kumi.Ustaarabu wa dreva yule alioonekana nao mara ya kwanza ukarudi tena wakati huu alipokuwa akipokea fedha hii na kushukuru huku akiwa kama haaminikama kuulizwa swali moja tu la kipuuzi ambalo amejibu kwa jazba kumempa pesa yote hii kabla hata ya mchana.Tabasamu lilichomoza usoni mwa dreva huyu ambaye sekunde chache zilizopita alimjibu Mick kwa ghadhabu.Ama kweli pesa ni sabuni ya roho.
"Hawa madreva wa magari makubwa sijui wana matatizo gani.Yaani akili zao wanazijua wenyewe".Aliwaza Mick wakati akiwa amerudi ndani ya gari lake.
"Lakini mbona mimi nimepita barabara ile na nimeshuka na kukaa zaidi ya dakika ishirini bila kubugudhiwa na mtu.Au kamera zimekufa."Alijiuliza Mick.Alihisi taa nyekundu kuwaka kichwani mwake.Yeye kama mwana usalama yeyote,alihisi kuwepo kwa mchezo mchafu.Ndiyo.Kwa nini kamera ziharibiwe.Kwa nini magaidi walipita njia ile.Alipojaribu kuunganisha mambo haya,Mick alihisi kuwa kuna jambo limejificha nyuma yake,hii haikuwa 'Coincidence'.
Mick aliendesha gari lake kurudi ' safe house' huku akiwaza jambo hili na lile.Mwisho aliamua kuwa muda utatoa majibu muafaka wa maswali aliyojiuliza kichwani mwake,japo muda hausubiri mtu.
tupo pamoja
 
Kwanza nikufahamishe ndugu sijawahi kuweka fb

Lakini kubwa nambie wapi niliweka uzi sikumaliza? Au siposti baada ya kuweka? Chief busara jambo jema sana kuliko mihemko ya hisia lakini ewe bwana MTENGETI umeona alichoandika huyo mtu na mimi kumjibu? Nakuheshimu naomba tuishie hapa si vyema kulumbana bila sababu
Hakuna mihemko wala mizuka kama ya kina bashite Na Rais Magufuli!! Ukweli Ni kuwa ctor zako haziishi mkuu;! Huu Ni untyanyasaji!! Ila kwa SBB unaonekana una PhD ya ubish hamna noma! Embu pitia comment za wadau kuanzia ya kwanza hadi ya tano ya uzi huu utaona ninachokisema! Tunawapenda watunzi wetu humu jf! Na kazi zenu zikiwa mtaani kwenye vitabu au magazet tuna nunua ila hampendi mashabiki wenu! Na kwa upendo huo huo nikuchane mubashara " acha kunyanyasa wasomaji wa jf; kamilisha kazi zako " mwisho wa mchano. Kama bundle linasumbua ingia hapa bure bila MB : www.freebasic.com kuna link ya jf hapo! Post,jenga jina then lete hard copy mtaani
 
[HASHTAG]#Tater[/HASHTAG],shabani lee,donlucchese,kichwa kikubwa,soud35,swahiba92,madame s,moneytalk,Tumosa,muya ataho,MTENGETI,macson3#shunie,songa heri,ADK#
 
J.K.T MAFINGA
Saa kumi na mbili na nusu jioni.
Ndani ya moja kati ya ofisi za Jeshi la Kujenga Taifa (JKT),mlango uligongwa gongwa na mtu aliye nje.Sauti nzito ya mtu aliyekuwa ndani ilisikika ikisema "karibu".Mlango ulifunguliwa kisha ajenti Mick-reuben akiwa amevaa suti nyeusi iliyomkaa vyema ikisindikizwa na shati jeupe na tai nyeusi huku sikioni akiwa amevaa kifaa maalum cha mawasiliano kinachoitwa 'Tube Coiled Earpiece'.Kijana huyu alifunga mlango nyuma yake baada ya kuingia kisha akakaa katika kiti kilichokuwa mbele ya meza huku akitazamana na yule aliyekaa nyuma ya meza, mtu mzima mmoja ambaye alionekana kama mwenye umri kati ya miaka 50 hadi 55 hivi.
"Naitwa Mick-reuben kutoka C.T.I, nadhani ulipata ujumbe kuhusu ujio wangu".Aliongea kwa nidhamu kijana huyu huku akiwa katika hali ya utulivu wa hali ya juu.
"Ok, nimepata habari kutoka makao makuu na ndiyo maana niko ofisini hadi sasa.Mimi naitwa Aloyce Mwasambili.Ni mkuu wa kambi hili la Hapa mafinga.Nimepewa maagizo nikupe ushirikiano kwa kila utakachokitaka.Sijui nikusaidie nini kijana wangu."Aliongea kwa nidhamu pia mzee huyu ambaye mabegani alichafuka kwa nyota kadhaa.Alionekana kuwa mtu kwenye cheo cha juu.
"Kubwa hapa ni kuhusu tukio lililotokea na ambalo bado ni la moto kwa taifa letu na mataifa mengine.Tukio la kutoroka kwa gaidi wa kimataifa Omar al-Mahmood. Namna pekee ya kujua aliko kirahisi ni kwa kuwatambua baadhi ya watu wanaotuhumiwa kusaidia kutoroka kwake. Moja ya watu wanaotuhumiwa kuhusiana na tukio hili ni mtu ambaye hapo mwanzo alidhaniwa kuwa ji marehemu tangu mwaka 1998.Lakini katika upelelezi imegundulika kuwa yupo hai na anahusishwa moja kwa koja kwa kuhusika na tukio hili kwa namna moja au nyingine.Tumemtambua mtu huyu,kwa jina anaitwa John Karobota.Kwa kuwa hakufariki, ninaweza kusema kuwa alipotea akiwa na cheo cha luteni katika jeshi la wananchi,yaani JWTZ."Alianza kujieleza Mick kisha akaacha kwa muda kidogo kumuacha mwenyeji wake ayatafakari haya kabla hajaendelea kumueleza kwa kina.
"Sasa picha iliyopatikana inayotushuhudia kuwa mtu huyu yupo hai , imerekodiwa na kamera za kambi hii kwa hiyo tunaamini mtu huyu alikuwapo ndani ya kambi hii aidha kwa muda mrefu au kwa muda mfupi.Picha yenyewe ya mtu huyo ni hii hapa,sijui kama unaweza kuitambua".Alimaliza kueleza Mick huku akitoa 'Tablet' kutoka katika mfuko wa suruali aliyoivaa, kisha akapapasa kioo hapa na pale kisha picha waliyoipata ya John Karobota ikaonekana vizuri kabisa.Ni picha ya muda mrefu,lakini mkuu wa kambi hii bwana Aloyce alionekana kuitambua mara baada ya kuiangalia kwa sekunde chache tu.
"Picha hii siyo ngeni kwangu......Ahaa....Nadhani nimekumbuka kitu.Miezi kama mitatu hivi iliyopita,nilipigiwa simu kutoka makao makuu ofisi ya C.D.F(Mkuu wa Majeshi Tanzania). Simu hii ilipigwa na katibu muhtasi wa C.D.F, ambaye alinipa maagizo kuhusiana na ujio wa mtu huyu, kwamba atakuja katika kambi hii kwa muda mfupi kwa sababu ya kazi maalum anayoifanya katika mipaka ya nchi upande huu wa nyanda za juu kusini,yaani katika mkoa wa Mbeya kisha ataondoka.Kwamba hapa ndiyo itakua kituo chake kikuu wakati wote atakaokuwa akifanya kazi hiyo. "Alijieleza kwa maelezo ya mwanzo mkuu huyu wa kambi kisha akanyamaza kidogo akionekana kufikilia jambo fulani kwa kina kabla hajaendelea.
"Nilitambulishwa jina lake.Anaitwaaaaaaaa (huku akitafuta kitu katika makabrasha mengi yaliyokuwa katika droo za meza yake na kisha kutoa bahasha moja ya ukubwa wa 'A4'.akaifungua haraka na kutoa karatasi mbili zilizounganishwa kisha akaiangalia kwa haraka), yes....Anaitwa Jeremiah Mwakibinga.Cheochake ni Luteni. Lakini hiyo picha uliyonionesha haina utofauti sana na sura yake.Labda tu hiyo picha naweza kusema inamuonesha akiwa kijana zaidi ya alivyokuja hapa, au labda kama ni ndugu yake aliyefanana kwa asilimia mia."
"Na hii ni barua yake aliyokuja nayo na pia nilitumiwa ' email' kwa anwani ya makao makuu ya jeshi( huku akibonyeza hapa na pale katika keyboard ya kompyuta iliyo mezani pake) ambayo ni hii hapa".Alimaliza kuongea mkuu huyu wa kambi huku akimgeuzia Mick kompyuta yake ili aweze kuona barua pepe ile.
"Wewe umewahi kuzungumza na katibu muhtasi wa C.D.F kabla"Alihoji Mick Reuben.
"Ndiyo nimewahi kuzungumza naye zaidi ya mara ya tatu na hii ilikuwa ni ya nne.Tena kwa namba hiihii tangu nilipoteuliwa kuwa mkuu wa kambi hii miaka mitano iliyopita."Alijibu mkuu huyu wa kambi hii ya JKT.
Kisha mara tu alipojibu akaonekana kukumbuka kitu kwa ghafla ambacho ni kama kilimshitua kidogo.
"Lakini, kuna kitu nimekumbuka ambacho sijawahi kukifikiria hapo mwanzo.Nilipoongea naye mara ya mwisho,sauti yake ilikuwa kama inakwaruza hivi, siyo ile niliyowahi kuisikia kabla.Na siku ile alikuwa akiongea kama mtu aliyechangamka sana tena kirafiki kuliko kawaida ya siku zingine ambapo huwa anazungumza akiwa yupo siriasi , tena kwa sauti kama ya ki-amri amri hivi."Alimalizia kuongea mkuu huyu wa kambi,Aloyce Mwasambili.
Kengere ya hatari ikalia katika kichwa cha Mick.Tayari alikwishaunganisha maelezo haya na mambo ambayo yeye alikuwa akiyahisi, na kung'amua jambo katika kichwa chake.
"Ahsante.Ila kwa kukumbushana tu nadhani unafahamubkuwa tuliyoongea hapa ni siri kubwa na hakuna mtu anatakiwa kufahamu.Nikikuhitaji tena nitakutafuta.Naomba niondoke na barua hii kwa upelelezi zaidi pia naomba unitumie barua pepe hiyo uliyotumiwa katika anwani hii( huku akimuandikia anuani ile)." Akamaliza kuongea Mick.
"Haina shida.Nafurahi tu kama maelezo yameweza kukusaidia kwa lolote.Wakati wowote utakaponihitajiunakaribishwa sana".Aliongea mkuu wa kambi kisha wakapeana mikono na Mick.Mick akaondoka huku akionekana kufikiria mambo kadhaa kichwani.
******;********************************************************************************************
"Nimefanyia utafiti ile barua uliyokuja nayo pamoja na barua pepe.Nikianza na barua.Imefanana na barua za makao makuu ya jeshi kwa asilimia kubwa sana.Asilimia chache zilizobaki kufika asilimia mia iko katika muhuri uliopigwa katika barua hii.Kama unavyoona, muhuri wa jeshi uko katika umbo la duara.Lakini nikifananisha na barua nyingine kutoka makao makuu ya jeshi, zinatofautiana kidogo katika kipenyo kwa milimita moja na nusu.Pia umbali kati ya herufi na herufi umetofautiana kwa umbali ambao haiwezekani kutambua kwa macho ya kawaida.Mimi mwenyewe nimeng'amua hayo baada ya kui'scan' katika kompyuta na kutumia programu maalum ya kompyuta inayoweza kupima vitu hivyo."
"Nimeitafiti barua pepe ambayo ilitumwa kwa mkuu wa kambi ya jeshi Mafinga.Nimetafiti pia na namba ya simu ambayo mkuu wa kambi ya JKT Mafinga anadai kuwa ilipigwa kutoka makao makuu ofisi ya C.D.F na katibu wake.Vyote hivyo,yaani barua pepe na simu vilitumika kuwasiliana kutokea eneo la ofisi za mamlaka ya mapato (TRA) Mbeya. Ninadhani mpigaji simu na mtumaji wa barua pepe hiyo alikuwa mtaalamu au aliwezeshwa na mtaalamu wa teknolojia ya habari na mawasiliano na inawezekana alitumia programu maalum kufanya mawasiliano hayo.Programu hiyo inamsaidia mtumiaji kuingilia mawasiliano ya mtu mwingine,na hivyo nadhani mawasiliano ya ofisi ya C.D.F yaliingiliwa. Nathubutu kusema mtaalam wa teknolojia aliyehusika kufanya haya yawezekana ni mtaalamu wa hali ya juu sana kuweza ku-'hack' hata mawasiliano ya taasisi kubwa kama ofisi ya mkuu wa majeshi".
"Kwa sababu hiyo ninaweza kuhitimisha kuwa mawasiliano hayo pamoja na barua ile ni feki na wala hazihusiani na ofisi ya C.D.F."Alimaliza kuongea Clara.Wasikilizaji wake walikuwa ni ajenti Mick,mkurugenzi wa C.T.I, Maajenti wengine watatu wa C.T.I pamoja na mtu mmoja aliyekuja pamoja na mkurugenzi wa C.T.I ambaye wengine walikuwa bado hawajamfahamu.
"Kwanza naomba niwatambulishe mgeni wetu huyu. Kutokana na majukumu kuwa mengi, raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania mheshimiwa George Katumba amemteua Josephat Moses kutoka idara ya usalama kitengo cha ulinzi wa rais,kuwa makamu mkurugenzi wa idara ya C.T.I. Sahani kwa kuwa mpaka wakati huu amekwisha kuhudhuria kikao chake cha kwanza ndani ya idara bila nyinyi kumgundua.Hii ni kwa sababu rais ameagiza aanze kazi mara moja."Aliongea mkurugenzi wa C.T.I na wanaidara waliokuwemo katika kikao hiki wakapiga makofi kama ishara ya kumkaribisha mgeni huyu.
"Lakini pia ,kutokana na alichokigundua Mick pamoja na maelezo haya ya ajenti Clara, basi ninadhani kuna umuhimu wa ajenti Mick na ajenti Clara kwenda kwenda huko Mbeya ofisi za mamlaka ya mapato TRA mkaanzie hapo.Wengine tutaendelea kutoa usaidizi kutokea hapahapa ofisini. Mtapata usaidizi wote mtakaouhitaji."Alimaliza kuongea mkurugenzi wa C.T.I.
Dakika ishirini baadaye,Ajenti Mick pamoja na Ajenti Clara walikuwa ndani ya helkopta iliyo na chapa ya polisi wakielekea Mbeya .
***************************************
 
J.K.T MAFINGA
Saa kumi na mbili na nusu jioni.
Ndani ya moja kati ya ofisi za Jeshi la Kujenga Taifa (JKT),mlango uligongwa gongwa na mtu aliye nje.Sauti nzito ya mtu aliyekuwa ndani ilisikika ikisema "karibu".Mlango ulifunguliwa kisha ajenti Mick-reuben akiwa amevaa suti nyeusi iliyomkaa vyema ikisindikizwa na shati jeupe na tai nyeusi huku sikioni akiwa amevaa kifaa maalum cha mawasiliano kinachoitwa 'Tube Coiled Earpiece'.Kijana huyu alifunga mlango nyuma yake baada ya kuingia kisha akakaa katika kiti kilichokuwa mbele ya meza huku akitazamana na yule aliyekaa nyuma ya meza, mtu mzima mmoja ambaye alionekana kama mwenye umri kati ya miaka 50 hadi 55 hivi.
"Naitwa Mick-reuben kutoka C.T.I, nadhani ulipata ujumbe kuhusu ujio wangu".Aliongea kwa nidhamu kijana huyu huku akiwa katika hali ya utulivu wa hali ya juu.
"Ok, nimepata habari kutoka makao makuu na ndiyo maana niko ofisini hadi sasa.Mimi naitwa Aloyce Mwasambili.Ni mkuu wa kambi hili la Hapa mafinga.Nimepewa maagizo nikupe ushirikiano kwa kila utakachokitaka.Sijui nikusaidie nini kijana wangu."Aliongea kwa nidhamu pia mzee huyu ambaye mabegani alichafuka kwa nyota kadhaa.Alionekana kuwa mtu kwenye cheo cha juu.
"Kubwa hapa ni kuhusu tukio lililotokea na ambalo bado ni la moto kwa taifa letu na mataifa mengine.Tukio la kutoroka kwa gaidi wa kimataifa Omar al-Mahmood. Namna pekee ya kujua aliko kirahisi ni kwa kuwatambua baadhi ya watu wanaotuhumiwa kusaidia kutoroka kwake. Moja ya watu wanaotuhumiwa kuhusiana na tukio hili ni mtu ambaye hapo mwanzo alidhaniwa kuwa ji marehemu tangu mwaka 1998.Lakini katika upelelezi imegundulika kuwa yupo hai na anahusishwa moja kwa koja kwa kuhusika na tukio hili kwa namna moja au nyingine.Tumemtambua mtu huyu,kwa jina anaitwa John Karobota.Kwa kuwa hakufariki, ninaweza kusema kuwa alipotea akiwa na cheo cha luteni katika jeshi la wananchi,yaani JWTZ."Alianza kujieleza Mick kisha akaacha kwa muda kidogo kumuacha mwenyeji wake ayatafakari haya kabla hajaendelea kumueleza kwa kina.
"Sasa picha iliyopatikana inayotushuhudia kuwa mtu huyu yupo hai , imerekodiwa na kamera za kambi hii kwa hiyo tunaamini mtu huyu alikuwapo ndani ya kambi hii aidha kwa muda mrefu au kwa muda mfupi.Picha yenyewe ya mtu huyo ni hii hapa,sijui kama unaweza kuitambua".Alimaliza kueleza Mick huku akitoa 'Tablet' kutoka katika mfuko wa suruali aliyoivaa, kisha akapapasa kioo hapa na pale kisha picha waliyoipata ya John Karobota ikaonekana vizuri kabisa.Ni picha ya muda mrefu,lakini mkuu wa kambi hii bwana Aloyce alionekana kuitambua mara baada ya kuiangalia kwa sekunde chache tu.
"Picha hii siyo ngeni kwangu......Ahaa....Nadhani nimekumbuka kitu.Miezi kama mitatu hivi iliyopita,nilipigiwa simu kutoka makao makuu ofisi ya C.D.F(Mkuu wa Majeshi Tanzania). Simu hii ilipigwa na katibu muhtasi wa C.D.F, ambaye alinipa maagizo kuhusiana na ujio wa mtu huyu, kwamba atakuja katika kambi hii kwa muda mfupi kwa sababu ya kazi maalum anayoifanya katika mipaka ya nchi upande huu wa nyanda za juu kusini,yaani katika mkoa wa Mbeya kisha ataondoka.Kwamba hapa ndiyo itakua kituo chake kikuu wakati wote atakaokuwa akifanya kazi hiyo. "Alijieleza kwa maelezo ya mwanzo mkuu huyu wa kambi kisha akanyamaza kidogo akionekana kufikilia jambo fulani kwa kina kabla hajaendelea.
"Nilitambulishwa jina lake.Anaitwaaaaaaaa (huku akitafuta kitu katika makabrasha mengi yaliyokuwa katika droo za meza yake na kisha kutoa bahasha moja ya ukubwa wa 'A4'.akaifungua haraka na kutoa karatasi mbili zilizounganishwa kisha akaiangalia kwa haraka), yes....Anaitwa Jeremiah Mwakibinga.Cheochake ni Luteni. Lakini hiyo picha uliyonionesha haina utofauti sana na sura yake.Labda tu hiyo picha naweza kusema inamuonesha akiwa kijana zaidi ya alivyokuja hapa, au labda kama ni ndugu yake aliyefanana kwa asilimia mia."
"Na hii ni barua yake aliyokuja nayo na pia nilitumiwa ' email' kwa anwani ya makao makuu ya jeshi( huku akibonyeza hapa na pale katika keyboard ya kompyuta iliyo mezani pake) ambayo ni hii hapa".Alimaliza kuongea mkuu huyu wa kambi huku akimgeuzia Mick kompyuta yake ili aweze kuona barua pepe ile.
"Wewe umewahi kuzungumza na katibu muhtasi wa C.D.F kabla"Alihoji Mick Reuben.
"Ndiyo nimewahi kuzungumza naye zaidi ya mara ya tatu na hii ilikuwa ni ya nne.Tena kwa namba hiihii tangu nilipoteuliwa kuwa mkuu wa kambi hii miaka mitano iliyopita."Alijibu mkuu huyu wa kambi hii ya JKT.
Kisha mara tu alipojibu akaonekana kukumbuka kitu kwa ghafla ambacho ni kama kilimshitua kidogo.
"Lakini, kuna kitu nimekumbuka ambacho sijawahi kukifikiria hapo mwanzo.Nilipoongea naye mara ya mwisho,sauti yake ilikuwa kama inakwaruza hivi, siyo ile niliyowahi kuisikia kabla.Na siku ile alikuwa akiongea kama mtu aliyechangamka sana tena kirafiki kuliko kawaida ya siku zingine ambapo huwa anazungumza akiwa yupo siriasi , tena kwa sauti kama ya ki-amri amri hivi."Alimalizia kuongea mkuu huyu wa kambi,Aloyce Mwasambili.
Kengere ya hatari ikalia katika kichwa cha Mick.Tayari alikwishaunganisha maelezo haya na mambo ambayo yeye alikuwa akiyahisi, na kung'amua jambo katika kichwa chake.
"Ahsante.Ila kwa kukumbushana tu nadhani unafahamubkuwa tuliyoongea hapa ni siri kubwa na hakuna mtu anatakiwa kufahamu.Nikikuhitaji tena nitakutafuta.Naomba niondoke na barua hii kwa upelelezi zaidi pia naomba unitumie barua pepe hiyo uliyotumiwa katika anwani hii( huku akimuandikia anuani ile)." Akamaliza kuongea Mick.
"Haina shida.Nafurahi tu kama maelezo yameweza kukusaidia kwa lolote.Wakati wowote utakaponihitajiunakaribishwa sana".Aliongea mkuu wa kambi kisha wakapeana mikono na Mick.Mick akaondoka huku akionekana kufikiria mambo kadhaa kichwani.
******;********************************************************************************************
"Nimefanyia utafiti ile barua uliyokuja nayo pamoja na barua pepe.Nikianza na barua.Imefanana na barua za makao makuu ya jeshi kwa asilimia kubwa sana.Asilimia chache zilizobaki kufika asilimia mia iko katika muhuri uliopigwa katika barua hii.Kama unavyoona, muhuri wa jeshi uko katika umbo la duara.Lakini nikifananisha na barua nyingine kutoka makao makuu ya jeshi, zinatofautiana kidogo katika kipenyo kwa milimita moja na nusu.Pia umbali kati ya herufi na herufi umetofautiana kwa umbali ambao haiwezekani kutambua kwa macho ya kawaida.Mimi mwenyewe nimeng'amua hayo baada ya kui'scan' katika kompyuta na kutumia programu maalum ya kompyuta inayoweza kupima vitu hivyo."
"Nimeitafiti barua pepe ambayo ilitumwa kwa mkuu wa kambi ya jeshi Mafinga.Nimetafiti pia na namba ya simu ambayo mkuu wa kambi ya JKT Mafinga anadai kuwa ilipigwa kutoka makao makuu ofisi ya C.D.F na katibu wake.Vyote hivyo,yaani barua pepe na simu vilitumika kuwasiliana kutokea eneo la ofisi za mamlaka ya mapato (TRA) Mbeya. Ninadhani mpigaji simu na mtumaji wa barua pepe hiyo alikuwa mtaalamu au aliwezeshwa na mtaalamu wa teknolojia ya habari na mawasiliano na inawezekana alitumia programu maalum kufanya mawasiliano hayo.Programu hiyo inamsaidia mtumiaji kuingilia mawasiliano ya mtu mwingine,na hivyo nadhani mawasiliano ya ofisi ya C.D.F yaliingiliwa. Nathubutu kusema mtaalam wa teknolojia aliyehusika kufanya haya yawezekana ni mtaalamu wa hali ya juu sana kuweza ku-'hack' hata mawasiliano ya taasisi kubwa kama ofisi ya mkuu wa majeshi".
"Kwa sababu hiyo ninaweza kuhitimisha kuwa mawasiliano hayo pamoja na barua ile ni feki na wala hazihusiani na ofisi ya C.D.F."Alimaliza kuongea Clara.Wasikilizaji wake walikuwa ni ajenti Mick,mkurugenzi wa C.T.I, Maajenti wengine watatu wa C.T.I pamoja na mtu mmoja aliyekuja pamoja na mkurugenzi wa C.T.I ambaye wengine walikuwa bado hawajamfahamu.
"Kwanza naomba niwatambulishe mgeni wetu huyu. Kutokana na majukumu kuwa mengi, raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania mheshimiwa George Katumba amemteua Josephat Moses kutoka idara ya usalama kitengo cha ulinzi wa rais,kuwa makamu mkurugenzi wa idara ya C.T.I. Sahani kwa kuwa mpaka wakati huu amekwisha kuhudhuria kikao chake cha kwanza ndani ya idara bila nyinyi kumgundua.Hii ni kwa sababu rais ameagiza aanze kazi mara moja."Aliongea mkurugenzi wa C.T.I na wanaidara waliokuwemo katika kikao hiki wakapiga makofi kama ishara ya kumkaribisha mgeni huyu.
"Lakini pia ,kutokana na alichokigundua Mick pamoja na maelezo haya ya ajenti Clara, basi ninadhani kuna umuhimu wa ajenti Mick na ajenti Clara kwenda kwenda huko Mbeya ofisi za mamlaka ya mapato TRA mkaanzie hapo.Wengine tutaendelea kutoa usaidizi kutokea hapahapa ofisini. Mtapata usaidizi wote mtakaouhitaji."Alimaliza kuongea mkurugenzi wa C.T.I.
Dakika ishirini baadaye,Ajenti Mick pamoja na Ajenti Clara walikuwa ndani ya helkopta iliyo na chapa ya polisi wakielekea Mbeya .
***************************************
Endelea mkuu
 
  • Thanks
Reactions: ADK
Hata mie nani subiria kama vipi twende chemba
Chief chemba nilishawahi kukufikia sema labda kwa sababu ya tatizo la simu yako hukuona notifikesheni
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom