SIRI
MTUNZI : PATRICK CK
SEASON 9: EPISODE 11
Baada ya kutoka katika
kambi yao,Austin
aliwapeleka akina Mathew
hadi katika nyumba Fulani
iliyokuwa na ukuta wa
mawe.Haikuwa nyumba
kubwa sana ilikuwa na
vyumba vitatu vya kulala
sebule jiko chumba kidogo
cha kupumzika na chumba
cha kusomea.
“Karibuni ndani jamani”
akasema Austin na
kumsaidia Gosu Gosu
kumbeba Edger na
kumuingiza ndani
wakampeleka katika moja
wapo ya chumba na
kumfunga pingu mkononi
katika dirisha lililokuwa
karibu na kitanda
alicholazwa.
“Whats’s going on
Austin?akauliza Mathew
“Wakati ukiendelea
kumuhoji Edger nilipokea
simu kutoka kwa Rais
akanieleza kwamba anatuma
mtu kuja kumchukua Edger
Kaka kwani amefanya
maamuzi ya kumkabidhi kwa
magaidi.Alinielekeza
kwamba nisiwataarifu
kuhusu jambo hili.Baada ya
simu ile nilitafakari nikaona
haitakuwa sawa.Huyu mtu
amewahi kuwa kiongozi na
ana mahusiano na magaidi
yawezekana akawa ni
pandikizi na alikuwa
anatumiwa kuwapa magaidi
siri za nchi.Kuna mambo
mengi ambayo
hatuyafahamu kuhusu Edger
kaka hivyo nikaamua
kupingana na Rais na
kumchukua Edger kumleta
hapa.Naamini baada ya
kugundua kwamba
nimemtorosha Edger Rais
atakasirika sana na mpaka
sasa nimekwisha poteza kazi
yangu na tayari nimeingia
katika mgogoro mkubwa na
mkuu wa nchi lakini hilo si
tatizo kwangu kwani
nilichoamua kukifanya ni
kwa manufaa ya
taifa.Maamuzi ya Rais ni
maamuzi ya uoga na yanafaa
kupuuzwa.Ni maamuzi ya
kutatua tatizo kwa muda
mfupi bila kufahamu kama
kuna mtandao mkubwa wa
IS hapa nchini.Kuanzia sasa
mimi ni mwenzenu
tutashirikiana pamoja katika
kupambana na hawa magaidi
wanaotishia amani na
usalama wa nchi yetu”
akasema Austin
“Dah ! akasema Mathew
akiwa katika mshangao
“Nimekosa neno la
kusema kwa hiki alichotaka
kukifanya Rais.Austin una
hakika kweli ni Rais ndiye
aliyekupa maelekezo hayo na
si mtu mwingine aliyetumia
simu ya Rais?akauliza
Mathew
“Ni Rais.Nimekuwa
nazungumza na Rais mara
kwa mara na kama
angekuwa ni mtu mwingine
ametumia simu yake
ningegundua lakini
aliyenipigia simu na kunipa
maelekezo yale ni Rais Dr
Evans” akasema Austin
“Oh my God ! ni akili
yake kweli au kuna mtu
kamshauri afanye
hivi?Tumeyaweka maisha
yetu rehani kwa ajili ya
kwenda kumkomboa Edger
Kaka nchini Kenya lakini
kumbe alikuwa na mipango
yake,amenisikitisha sana
sikutegemea kabisa kama
angeweza kutufanyia kitu
kama hiki.Ahsante sana
Austin kwa hiki
ulichokifanya,usijali kuhusu
kazi hapa tunalitanguliza
taifa kwanza.Kuanzia sasa
tutambue kwamba
operesheni hii tuko peke yetu
na hatuna tena msaada wa
Rais” akasema Mathew
“Kwa namna
ninavyomfahamu Dr Evans
akigundua kwamba
tumemtorosha Edger tayari
tutakuwa maadui zake na
atatumia nguvu kubwa
kutusaka.We must prepare
ourselves for that” akasema
Devotha.
“Vipi kuhusu Ruby na
Yule mke wa balozi?
Akauliza Gosu Gosu
“We must go get
her.Ruby ni muhimu sana
katika operesheni hii.”
akasema Mathew
“So what’s the
plan?akauliza Austin
“Plan ya kwanza ni
kuwakomboa watoto
waliotekwa ambao tayari IS
ameanza kuwaua.Naamini
Rais amewaahidi kuwa
atawapa mtu wao lakini
baada ya kumkosa hali
itakuwa mbaya lazima
watawachinja watoto kwa
hasira.Tunatakiwa
tusimamishe mauaji hayo na
kuwakomboa
watoto”akasema Mathew
“How are we going to do
it?akauliza Devotha
“We have Edger
kaka.Huyu atatusaidia sana
kuweza kuufahamu mtandao
wao” akasema Mathew
“Mathew unadhani
anaweza akafunguka kwa
haraka na tukazuia mauaji
yale ya watoto
yasiendelee?Tayari wameua
mmoja na wametishia
kuendelea kuua kila baada
ya muda Fulani”akasema
Austin
“Let me try once
again.Lazima kila mbinu
itumike kuhakikisha Edger
anaongea.Guys let’s not
waste time.Gosu Gosu na
Devotha mnakwenda
kuwachukua Ruby na mke
wa balozi mimi na Austin
tutaendelea hapa” akasema
Mathew
“Mathew I don’t think
that’s a good idea.Laiti kama
ungekuwepo ingesaidia
lakini nikienda peke yangu
na Gosu Gosu anything can
happen.Ruby bado ana
hasira na mimi”akasema
Devotha
“I’ll go.Nitakwenda
badala ya Devotha” akasema
Austin na Mathew hakuwa
na kipingamizi wakaondoka
akabaki na Devotha.Mathew
akamuacha Devotha
akichunga usalama yeye
akaingia katika chumba
alimo Edger Kaka
“Edger kaka
tumelazimika kukuhamisha
na kukuleta hapa kwa
sababu maalum.Israel tayari
wamekwishafahamu
kwamba ni sisi tuliokuteka
nyara na hivi tunavyoongea
umeibuka mzozo mkubwa
sana kati yao na sisi ndiyo
maana Rais akaelekeza
tukuondoe pale haraka
sana.Wewe ni Raia wa
Tanzania na hatuwezi
kukukabidhi kwa Israel
kwani watakuua.Rais ana
mpango mzuri sana juu yako
Edger anataka kukusaidia ili
uweze kuishi maisha mazuri
yenye amani ukiwa na
mwanamke umpendaye
Olivia.Lakini ili tukusaidie
nawe pia hauna budi
kutusaidia kufahamu
mtandao wa IS hapa
Tanzania na kuwapata
Olivia pamoja na watoto
waliotekwa usiku wa
leo.Edger wasichana wale
hawana hatia yoyote na
tayari IS wamekwisha anza
kuua mtoto mmoja baada
mwingine kwa kuwakata
vichwa.Huu ni ukatili
mkubwa sana na
usiovumilika.Wasichana
wale hawafahamu chochote
na hawastahili kutendewa
ukatili wa namna
hii.Wasichana sitini na sita
wote watauawa kama
hatutafanya juhudi za
kuwakomboa” akasema
Mathew na Edger
akaendelea kumtazama bila
kusema chochote.Mathew
akasema
“Edger nataka kujua kitu
kimoja toka
kwako.Uliendesha harakati
kubwa sana hapa nchini za
kufichua ufisadi uliokuwa
unafanywa na watu mbali
mbali serikalini ukajenga
jina kubwa na wananchi
wakakuamini.Nataka
kufahamu je mambo yale
uliyokuwa unayafanya ni
kweli uliyafanya kwa
dhamira ya dhati ya
kupambana na kufichua
ufisadi au ilikuwa ni moja ya
njia zako ya kutafuta
umaarufu ili kuficha maovu
yako?
Bado Edger Kaka
alikuwa kimya
“Edger please.Muda
unakimbia nijibu swali langu
ni kweli ulikuwa na dhamira
ya dhati ya kupambana na
ufisadi au ilikuwa ni moja ya
mipango yako kujenga
taswira nzuri mbele ya jamii
ili kuficha mambo yako
unayoyafanya? akasema
Mathew na kumtazama
Edger machoni
“Don’t say it.Tayari
nimepata jibu.It was all
lies.Mapambano yale
yalikuwa ni kiini macho
kuwalaghai
wananchi,kujenga jina lako
katika jamii.Nini hasa
lilikuwa lengo lako au lengo
lenu?Naamini haukuwa peke
yako katika hili.Mlikuwa na
mipango gani?akauliza
Mathew Edger aliendelea
kuwa kimya
“Nani ni kiongozi wa
mtandao wenu hapa
Tanzania? Naamini si wewe
bali yupo mkubwa wako na
wewe ulikuwa unatumika
tu.Nani kiongozi
wako?akauliza Mathew
lakini bado Edger aliendelea
kuwa kimya akimtazama
Mathew
“Edger unaniudhi sana
ninapokuuliza unakaa
kimya.Ninao uwezo wa
kukuharibu hapa hapa lakini
ninayaheshimu maelekezo ya
Rais wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania
ambaye ana malengo mazuri
ya kukusaidia ili
ukaishimaisha mazuri
mahala ambako hakuna
atakayekugundua.Nataka
unisaidie tuweze
kuwakomboa wale wasichana
ambao wanakatwa shingo
kikatili huku watu
wakishuhudia mtandaoni.Ni
kitendo cha kikatili sana
walichokifanya.Watoto wale
wanaouawa wana ndoto zao
ambazo wanataka kuzitimiza
katika maisha yao lakini
wanakatishwa ndoto zao
kikatili.Edger your not a
killer.You are not like
them.Macho yako
yanaonyesha haujawahi
kutoa roho ya mtu hivyo basi
waonee huruma watoto wale
wanaouawa bila kuwa na
kosa lolote.Naomba utusaidie
tuwapate wale watoto”
akasema Mathew.Edger
akainamisha kichwa
akaonekana kuzama
mawazoni
“Edger hakuna tena kitu
cha kuficha kuhusu
IS.Hawana msaada tena
kwako.Kwao umekwisha
fariki na hauna thamani tena
hivyo ni wewe na sisi
tu.Tusaidie na sisi tukusaidie
ili uishi maisha yenye raha
mustarehe mahala ambako
hakuna atakayekufahamu
ukiwa na mwanamke Yule
umpendaye” akasema
Mathew na baada ya dakika
mbili Edger akainua kichwa
akaonekana kusikitika na
kusema
“Fine,let’s end
this.Nitawaeleza kile
ninachokifahamu lakini
ninataka kuzungumza na
rais ili nipate uhakika
kutoka kwake kwamba
baada ya kuwapa kile
mnachokitaka nitapatiwa
kile ninachokitaka” akasema
Edger
“Baada ya kitisho cha
magaidi ulinzi wa Rais
umeongezeka na hivi
tunavyozungumza Rais yuko
mahala pa siri na hakuna
namna utakayoweza
kuzungumza naye kwa
sasa.Niko hapa kwa niaba
yake hivyo utazungumza na
mimi.Rais tayari amekwisha
weka wazi kuwa anataka
kukusaidia.Zungumza nami
nieleze chochote
unachokitaka na utakipata”
akasema Mathew.
“I need a new passport
with new name,I need a
house.Si nyumba tu mradi
nyumba nataka nyumba
nzuri ya ghorofa yenye hadhi
huko Uswisi.I need two
cars,luxury ones.Nahitaji
mtaji mkubwa
utakaoniwezesha kuwekeza
katika kilimo,mwisho
namuhitaji
Olivia.Mkinihakishia
kwamba nitapata hivyo vyote
niko tayari kuwasaidia
kuwapa taarifa”akasema
Edger
“Edger,Rais wa jamhuri
ya muungano wa Tanzania
yuko tayari kufanya chochote
kile utakachokihitaji ili
uweze kutupa taarifa
muhimu.Hesabu kwamba
haya yote umeyapata”
akasema Mathew
“Not so simple
Mr…what’s your name
again?akauliza Edger
“Mathew ..Mathew
Mulumbi”
“Mr Mathew Mulumbi
mambo hayaendi kirahisi
namna hiyo.Nahitaji uhakika
kutoka kwa Rais pekee na si
mtu mwingine” akasema
Edger
“Kama nilivyokwambia
kwamba Rais haitawezekana
kuzungumza naye kwa sasa
kutokana na kupelekwa
sehemu salama kufuatia
vitisho vya mashambulio ya
kigaidi na badala yake nipo
mimi.Usihofu mambo yako
yote yatatekelezwa.Lakini
wakati hayo yakitekelezwa
kwa nini tusianze kwanza
kumtafuta Olivia? Kila
unachokitaka kitapatikana
lakini kitakosekana kimoja
tu,Olivia Themba.Nipe
taarifa ambazo zitatusaidia
kumuokoa
Olivia.Ninakuhakikishia kila
kile unachokihitaji
kitapatikana.I give you my
word” akasema Mathew
“Mathew wewe
mwenyewe unafahamu
namna mambo haya
yanavyokwenda ninahitaji
uhakika kwamba kweli yale
ninayoyataka yanakwenda
kutekelezwa.Convince me!
Akasema Edger
Kaka.Mathew akamtazama
usoni kwa makini halafu
akasema
“Unataka kutumia jina
gani jipya?
Edger akafikiri kidogo na
kusema
“Nickson Robert”
“Sawa nisubiri
nitarejea”akasema Mathew
na kutoka
“Bastard ! akasema
Mathew kwa ukali.
“Nini
kimetokea?akauliza Devotha
“Edger yuko tayari
kufunguka lakini kuna
masharti ametoa” akasema
Mathew
“Ametoa sharti gani?
“Anataka nyumba ya
kifahari Uswisi,anataka
magari mawili ya kifahari
anataka mtaji wa kuwekeza
katika kilimo na anataka
hati mpya ya kusafiria yenye
jina jipya na mwisho kabisa
anataka kuondoka na Olivia
Themba.Tukimtekelezea
hayo yote yuko tayari kutupa
maelezo ya kutusaidia
kuwakomboa watoto pamoja
na Olivia”
“Vitu alivyovitaka ni
vikubwa mno viko nje ya
uwezo wetu.Tutafanya nini
kuvipata na mahusiano yetu
na Rais yamevunjika?Kama
bado tungekuwa na
mahusiano naye,Rais anao
uwezo wa kutekeleza hayo
yote”akasema Devotha
“Forget about
president.We’ll move on
without him.Edger anahitaji
kitu cha kumridhisha
kwamba maombi yake
yanafanyiwa kazi”
“What are we going to do
Mathew?
“I need to call my wife in
Paris”
“Your wife? Akauliza
Devotha
“Ndiyo”
“Mkeo anaingiaje katika
sakata hili?
“Ni bilionea
mkubwa.Anafahamiana na
matajiri wakubwa sehemu
mbali mbali duniani,nataka
anisaidie kupata nyumba ya
kununua nchini Uswisi
ambayo itanunuliwa kwa
jina la Nickson Robert
ambalo amechagua Edger”
“Mathew kwa nini
unataka kuingia hasara?
“I don’t care
ninachohitaji ni kupata
taarifa za kutuwezesha
kuwakomboa Olivia,Coletha
na watoto
waliotekwa.Tuwasubiri
akina Gosu Gosu warejee na
vifaa ili niweze kupiga simu
kwa mke wangu.Tukinunua
nyumba hiyo ataridhika na
atatueleza kila kitu”
akasema Mathew