Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,983
- 10,804
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA 14
ILIPOISHIA...
Tuliona Mkuki na Mei Lee wamefukuzwa nyumbani kwa Meja, wakiwa njiani Mkuki anamuokoa bibi mmoja wasiyemfahamu katika ajali ya ajali. Bibi anawaomba kuishi nao pamoja.
SOMA KILICHOJIRI...
Ni kama kile alichokizungumza kilikuwa na barafu kali, kilimgandisha Mkuki na kumfanya sasa afikirie kwamba inawezekana hiyo ikawa ni fursa pekee ya kumuacha Mei Lee pale na kumfuata jioni akiwa ameshafikiria ni wapi watakwenda. Lakini nafsi yake ilikinzana yenyewe ndani kwa ndani, alifikiria kumuacha Mei Lee pale, tena bila ya kukubaliana ama kumuuliza kwamba hilo litampendeza ilikuwa ni sawa na nusu ya kumtelekeza.
“Usijali bibi, tutakuja siku nyingine.” Akaamua Mkuki.
“Sawa. Nawashakuru sana kwa kunisaidia. Kwa sasa sina cha kuwapa lakini nawaahidi nitawaandalia kitu kizuri mtakapokuja hiyo siku nyingine.” Akasema Bibi, na baada ya hapo Mkuki na Mei Lee wakatoka wakimuacha bibi akifunga mlango na kurudi kuketi kwenye kiti chake akipendacho zaidi mle ndani.
Punde mlango ulibishwa hodi, bibi aliinuka kwenda kufungua na hapo akakutana na Mkuki na Mei Lee—waliamua kurudi baada ya kukubaliana kwamba ni vyema Mei Lee akabaki pale hadi jioni.
“Bibi, naomba mwenzangu abaki hapa. Nitamfuata jioni.” Akasema Mkuki na hilo halikuwa ombi kwa bibi, bali ni zawadi kubwa na ya muhimu sana ya kumuondolea ile hali ya upweke, hali ya kuwa mwenyewe kwa siku nzima.
Yeye alikuwa akiitwa Pin Ping, bibi kikongwe wa miaka takriban 80. Alikuwa akiishi peke yake kwa sababu kuu moja ambayo mwenyewe aliifanya kama siri.
Awali alikuwa akiishi Guanzouh na si hapa Hong Kong alipo leo, bali alikimbilia huko baada ya mwanae kumpelekea akaishi katika nyumba ya kulelea wazee. Hakuwa akiyataka maisha ya huko lakini hakutaka kuwakwaza wanawe na maamuzi yao. Alichoamua ni kutoroka akiwa huko kituoni, na akatumia pesa zake alizozihifadhi kwa siri kuhama Hong Kong, kupanga nyumba na kuanzisha maisha kwa kujificha ingawa alifahamu fika kwamba maisha ya aina hiyo yana ukingo wake.
“Sawa. Anaweza kubaki hapa.” Akasema bibi Pin Ping, hapo Mei Lee akamuaga Mkuki na kuingia ndani, kisha mwanaume akaondoka mbio mbio hadi mgahawani.
Alichelewa mno, na siku hiyo ilikuwa ni manusura afukuzwe kazi isipokuwa Meja alimtetea kwamba alikuwa na matatizo ya kiafya na ilibidi apite hospitali kwanza.
Kisha baada ya hapo Meja akamuita pembeni Mkuki na kumuomba msamaha zaidi wa kile kilichotokea. Hakika kilimuumiza lakini hakuwa na jinsi, ilikuwa ni lazima aegemee upande wa familia yake, upande wa mke wake.
Hata hivyo Mkuki sasa alimuelewa, hakuwa na kinyongo naye wala chuki dhidi yake, alijtahidi kusahau kila kilichotokea, na kuamua kuangalia mbele tu.
******************************
Jioni Mkuki alirudi kwa bibi Pin Pong, alibisha hodi na mlango ulifunguliwa na Mei Lee.
“Karibu.” Akasema Mei Lee. Mkuki akapita ndani, akaketi kwenye kiti.
“Bibi yuko wapi?” Mkuki akauliza.
“Kalala.” Akajibu Mei Lee.
“Muamushe umuage tuondoke.” Akasema Mkuki, alikuwa amepanga kwenda kulala na Mei Lee kwenye hoteli ndogo, alikuwa amepata vipesa kidogo siku hiyo.
“Mkuki, nimezungumza vitu vingi sana na bibi, nimemueleza kila kitu kuhusu maisha yetu, kasema tunaweza kuishi naye hapa.” Akaeleza Mei Lee huku akimtazama Mkuki machoni.
Mkuki alimtazama kana kwamba hakuelewa kile kilichosemwa; lakini ukweli ni kwamba alikipenda ingawa aliogopa kwa kiasi fulani kutokana na kwamba hawakuwa wakimfahamu uzuri yule bibi.
Lakini Mkuki hakuona sababu ya kupinga ofa ile hasa ukizingatia kwamba ilionekana hata bibi alikuwa anawahitaji, yaani kila mmoja alikuwa na umuhimu kwa mwenzake; bibi alichoka maisha ya upweke na Mkuki na Mei Lee hawakua na pahala pa kuishi.
********************************
Mkuki, Mei Lee na bibi Pin Ping walitengeneza familia bora sana yenye furaha hata kila mmoja akasahau mahangaiko aliyopitia. Na hivi ndivyo Mungu alivyo, mara zote hufanya njia pale pasipotarajiwa ili kuthibitisha uwepo na uwezo wake mkubwa wakufanya kile atakacho ndani ya nukta moja tu
Mkuki sasa akawa ndiye mleta huduma wa familia kama ambavyo alikuwa kwenye familia ya mzee Wong na hilo lilizidisha umuhimu wake katika familia hii.
Walikaa na bibi Pin Ping kwa miezi miwili; na kwa wiki ya kwanza ya kipindi chote hicho bibi Pin alipata kugundua kipaji kikubwa cha kuimba alichokuwa nacho Mei Lee. Mara kadhaa alimsifia na kuonesha hisia zake za wazi za jinsi ambavyo anafurahishwa na uimbaji wa msichana huyo, hata ukajengekea utamaduni wa kwamba kabla ya kulala ilibidi aimbiwe, aisikie sauti ya Mei Lee masikioni mwake ndipio usingizi uje.
Siku moja, baada ya miezi miwili ya kuishi kama familia , bibi Pin Ping alimuuliza Mei Lee jambo kuhusiana na muziki wake.
“Unajua kupiga chombo gani?” aliuliza bibi.
“Chombo cha muziki?”
“Ndiyo.”
“Hapana. Sijui kupiga chochote.”
“Mh! Kwanini? Hupendi?”
“Hapana. Napenda. Sikupata nafasi ya kujifunza tu.”
“Basi ngoja.” Akasema bibi Pin Ping, kisha akainuka kuelekea chumbani kwake akimuacha Mei Lee pale sebuleni walipokuwa. Punde alirejea akiwa na kitu fulani mkononi, ala ya muziki ambayo ilikuwa ni miongoni mwa ndoto za Mei Lee kwamba siku moja aimiliki na ajue kuitumia.
Lilikuwa ni gitaa, ala maarufu yenye kutengeneza muziki kwa kuvutwa nyuzi zake. Hili alilokuja nalo bibi Pin Ping lilikuwa ni gitaa lisilotumia umeme, lenyewe lilikuwa limetengenezwa kwa mbao nyepesi na kunakishiwa kwa rangi nyeusi, huku likiwa na vumbi kiasi kana kwamba lilihifadhiwa mahala kwa muda mrefu bila kutumika.
“Shika,” bibi akasema huku akimkabidhi Mei Lee lile gita. “Nenda kalisafishe, lifute vumbi kisha uje nalo.” Akamuelekeza.
Mei Lee akapokea, akainuka nalo na kwenda chumbani kwake akimucha bibi mwenyewe pale sebuleni. Alirudi sekunde chache baadae akiwa na gitaa lisilokuwa na vumbi sasa, alikwenda huko ndani kwa ajili ya kuchukua kitambaa kikubwa na kulisafisha.
“Tayari.” Akasema Mei Lee huku akimkabidhi bibi lile gitaa. Bibi akapoke taratibu, akalipaka kwenye mapaja yake akilitazama kwa makini kana kwamba lilimkumbusha jambo fulani murua lenye kusisimua lililopata kutokea katika maisha yake. Akafumba na macho kama mtu anayevuta hisia tamu, na hapo kiganja chake cha mkono kilipapasa gitaa lile.
Sekunde chache baadae akashusha pumzi ndefu, akafumbua macho, akamtazama Mei Lee.
“Hili gitaa linaitwa Caihong (Upinde wa Mvua),” akazungumza polepole na kwa hisia kali bibi Pin Ping na kuendelea. “kwangu ni kitu cha thamani zaidi kilichobaki kwenye uso wa dunia. Nilipewa kama zawadi na mume wangu, alinunua Uingereza alipokwenda kusoma. Sijui alifikiria nini hata akaamua kuniletea zawadi ya aina hii kwa sababu mimi na yeye, sote hatukuwahi kuwa wanamuziki; lakini niliipenda.
Basi nilitafuta mwalimu, akanifundisha jinsi ya kulitumia kwa usahihi na nilipohitimu tu nikawa nikitengeneza melodi nzuri kwa ajili ya kumliwaza mume wangu kila usiku.
Alifurahia sana, hata aliandika kwenye wosia wake kwamba akifa kabla yangu nimpigie melodi kadhaa kwenye mazishi yake.” alisimulia bibi Pin Ping na hadi kufikia hapa hisia zilimzidi. Akashindwa kujizuia, akajikuta akitokwa machozi.
Kile alichokisimulia kilimkumbusha mbali sana, kilimpa kumbukumbu za kusisimua za mapenzi. Alimkumbuka Lau, mwanaume aliyemuoa kwa ndao halali, ndoa iliyochochewa na upendo wa dhati wa kila mmoja kwa mwenzake. Alifariki kipindi ambacho bibi Pin Ping bado alikuwa ni mwanamke mwenye nguvu, hivyo baada ya pale alipata kuwa na wanamume wengine na hata kuolewa pia lakini bado nafasi ya Lau ilibaki kama ilivyo; hakuna shababi aliyefanikiwa kumfunika mwanaume huyo.
Bibi aliendelea kulia kwa machozi, Mei Lee alikuwa pale lakini hakuthubutu kusema neno, alielewa wakati mgumu namna ile aliokuwa akipitia bibi yake, hivyo aliamua kumpa uhuru wa kufanya vile alivyoamua, kutoa sumu za kumbukumbu zote za raha alizowahi kupewa na mumewe kipenzi Lau.
Baadae bibi alitulia mwenyewe, hapa sasa Mei Lee akapata nguvu ya kumsemesha na bibi akamuunga mkono kwa kumjibu na kisha mazungumzo mengine yakashika hatamu ambayo yalikuwa na sentensi mbili tu za kati kabla ya bibi kufikia kuelezea kwanini alikuja na lile gitaa.
“Ninataka nikufundishe kupigia gitaa.” Akasema bibi Pin Ping na hivyo ndivyo ilivyokuwa.
Bibi Pin Ping alimfunza barabara Mei Lee jinsi ya kutumia gitaa, na ndani ya wiki nne tu binti akawa tayari na uwezo wa kuchezesha vizuri vidole vyake na kutengeneza muziki mzuri. Alilielewa kwa muda mfupi sana hasa ukilinganisha na watu wengine jinsi ambavyo huchukua kipindi kirefu cha kujifunza matumizi ya dubwana hilo; lakini bila shaka yeye alifanikiwa kutokana na kiu aliyokuwa nayo.
Sasa ikawa kila jioni, baada ya chakula Mei Lee aliwaimbia Mkuki na bibi Pin Ping huku akipiga gitaa. Alifanya hivyo kwa ustadi mkubwa sana na hakika kila mmoja alifarikija kusikiliza nyimbo zake.
****************************************
Mei Lee alikuwa akilala chumba kimoja na bibi Pin Ping; na huko kikongwe huyo aligundua kitu nyeti kuhusu mjuu wake huyu ambacho ni zaidi ya sauti nzuri na kipaji kikubwa alichokuwa nacho.
Aligindua kwamba Mei Lee alikuwa na mapenzi makubwa mno na Mkuki, na si mapenzi ya kawaida, mapenzi ya kaka na dada, bali mapenzi ya Adam na Hawa; mapenzi yaliyopelekea leo hii dunia kuwa na idadi kubwa mno ya watu.
Hili halikuwekwa wazi na Mei Lee mwenyewe, isipokuwa bibi Pin Ping alikuwa shuhuda wa kuweweseka kwa Mei Lee na ndoto zake za kila siku usiku alizokuwa akiota na huku akimtaja Mkuki.
*****************************
ILIPOISHIA...
Tuliona Mkuki na Mei Lee wamefukuzwa nyumbani kwa Meja, wakiwa njiani Mkuki anamuokoa bibi mmoja wasiyemfahamu katika ajali ya ajali. Bibi anawaomba kuishi nao pamoja.
SOMA KILICHOJIRI...
Ni kama kile alichokizungumza kilikuwa na barafu kali, kilimgandisha Mkuki na kumfanya sasa afikirie kwamba inawezekana hiyo ikawa ni fursa pekee ya kumuacha Mei Lee pale na kumfuata jioni akiwa ameshafikiria ni wapi watakwenda. Lakini nafsi yake ilikinzana yenyewe ndani kwa ndani, alifikiria kumuacha Mei Lee pale, tena bila ya kukubaliana ama kumuuliza kwamba hilo litampendeza ilikuwa ni sawa na nusu ya kumtelekeza.
“Usijali bibi, tutakuja siku nyingine.” Akaamua Mkuki.
“Sawa. Nawashakuru sana kwa kunisaidia. Kwa sasa sina cha kuwapa lakini nawaahidi nitawaandalia kitu kizuri mtakapokuja hiyo siku nyingine.” Akasema Bibi, na baada ya hapo Mkuki na Mei Lee wakatoka wakimuacha bibi akifunga mlango na kurudi kuketi kwenye kiti chake akipendacho zaidi mle ndani.
Punde mlango ulibishwa hodi, bibi aliinuka kwenda kufungua na hapo akakutana na Mkuki na Mei Lee—waliamua kurudi baada ya kukubaliana kwamba ni vyema Mei Lee akabaki pale hadi jioni.
“Bibi, naomba mwenzangu abaki hapa. Nitamfuata jioni.” Akasema Mkuki na hilo halikuwa ombi kwa bibi, bali ni zawadi kubwa na ya muhimu sana ya kumuondolea ile hali ya upweke, hali ya kuwa mwenyewe kwa siku nzima.
Yeye alikuwa akiitwa Pin Ping, bibi kikongwe wa miaka takriban 80. Alikuwa akiishi peke yake kwa sababu kuu moja ambayo mwenyewe aliifanya kama siri.
Awali alikuwa akiishi Guanzouh na si hapa Hong Kong alipo leo, bali alikimbilia huko baada ya mwanae kumpelekea akaishi katika nyumba ya kulelea wazee. Hakuwa akiyataka maisha ya huko lakini hakutaka kuwakwaza wanawe na maamuzi yao. Alichoamua ni kutoroka akiwa huko kituoni, na akatumia pesa zake alizozihifadhi kwa siri kuhama Hong Kong, kupanga nyumba na kuanzisha maisha kwa kujificha ingawa alifahamu fika kwamba maisha ya aina hiyo yana ukingo wake.
“Sawa. Anaweza kubaki hapa.” Akasema bibi Pin Ping, hapo Mei Lee akamuaga Mkuki na kuingia ndani, kisha mwanaume akaondoka mbio mbio hadi mgahawani.
Alichelewa mno, na siku hiyo ilikuwa ni manusura afukuzwe kazi isipokuwa Meja alimtetea kwamba alikuwa na matatizo ya kiafya na ilibidi apite hospitali kwanza.
Kisha baada ya hapo Meja akamuita pembeni Mkuki na kumuomba msamaha zaidi wa kile kilichotokea. Hakika kilimuumiza lakini hakuwa na jinsi, ilikuwa ni lazima aegemee upande wa familia yake, upande wa mke wake.
Hata hivyo Mkuki sasa alimuelewa, hakuwa na kinyongo naye wala chuki dhidi yake, alijtahidi kusahau kila kilichotokea, na kuamua kuangalia mbele tu.
******************************
Jioni Mkuki alirudi kwa bibi Pin Pong, alibisha hodi na mlango ulifunguliwa na Mei Lee.
“Karibu.” Akasema Mei Lee. Mkuki akapita ndani, akaketi kwenye kiti.
“Bibi yuko wapi?” Mkuki akauliza.
“Kalala.” Akajibu Mei Lee.
“Muamushe umuage tuondoke.” Akasema Mkuki, alikuwa amepanga kwenda kulala na Mei Lee kwenye hoteli ndogo, alikuwa amepata vipesa kidogo siku hiyo.
“Mkuki, nimezungumza vitu vingi sana na bibi, nimemueleza kila kitu kuhusu maisha yetu, kasema tunaweza kuishi naye hapa.” Akaeleza Mei Lee huku akimtazama Mkuki machoni.
Mkuki alimtazama kana kwamba hakuelewa kile kilichosemwa; lakini ukweli ni kwamba alikipenda ingawa aliogopa kwa kiasi fulani kutokana na kwamba hawakuwa wakimfahamu uzuri yule bibi.
Lakini Mkuki hakuona sababu ya kupinga ofa ile hasa ukizingatia kwamba ilionekana hata bibi alikuwa anawahitaji, yaani kila mmoja alikuwa na umuhimu kwa mwenzake; bibi alichoka maisha ya upweke na Mkuki na Mei Lee hawakua na pahala pa kuishi.
********************************
Mkuki, Mei Lee na bibi Pin Ping walitengeneza familia bora sana yenye furaha hata kila mmoja akasahau mahangaiko aliyopitia. Na hivi ndivyo Mungu alivyo, mara zote hufanya njia pale pasipotarajiwa ili kuthibitisha uwepo na uwezo wake mkubwa wakufanya kile atakacho ndani ya nukta moja tu
Mkuki sasa akawa ndiye mleta huduma wa familia kama ambavyo alikuwa kwenye familia ya mzee Wong na hilo lilizidisha umuhimu wake katika familia hii.
Walikaa na bibi Pin Ping kwa miezi miwili; na kwa wiki ya kwanza ya kipindi chote hicho bibi Pin alipata kugundua kipaji kikubwa cha kuimba alichokuwa nacho Mei Lee. Mara kadhaa alimsifia na kuonesha hisia zake za wazi za jinsi ambavyo anafurahishwa na uimbaji wa msichana huyo, hata ukajengekea utamaduni wa kwamba kabla ya kulala ilibidi aimbiwe, aisikie sauti ya Mei Lee masikioni mwake ndipio usingizi uje.
Siku moja, baada ya miezi miwili ya kuishi kama familia , bibi Pin Ping alimuuliza Mei Lee jambo kuhusiana na muziki wake.
“Unajua kupiga chombo gani?” aliuliza bibi.
“Chombo cha muziki?”
“Ndiyo.”
“Hapana. Sijui kupiga chochote.”
“Mh! Kwanini? Hupendi?”
“Hapana. Napenda. Sikupata nafasi ya kujifunza tu.”
“Basi ngoja.” Akasema bibi Pin Ping, kisha akainuka kuelekea chumbani kwake akimuacha Mei Lee pale sebuleni walipokuwa. Punde alirejea akiwa na kitu fulani mkononi, ala ya muziki ambayo ilikuwa ni miongoni mwa ndoto za Mei Lee kwamba siku moja aimiliki na ajue kuitumia.
Lilikuwa ni gitaa, ala maarufu yenye kutengeneza muziki kwa kuvutwa nyuzi zake. Hili alilokuja nalo bibi Pin Ping lilikuwa ni gitaa lisilotumia umeme, lenyewe lilikuwa limetengenezwa kwa mbao nyepesi na kunakishiwa kwa rangi nyeusi, huku likiwa na vumbi kiasi kana kwamba lilihifadhiwa mahala kwa muda mrefu bila kutumika.
“Shika,” bibi akasema huku akimkabidhi Mei Lee lile gita. “Nenda kalisafishe, lifute vumbi kisha uje nalo.” Akamuelekeza.
Mei Lee akapokea, akainuka nalo na kwenda chumbani kwake akimucha bibi mwenyewe pale sebuleni. Alirudi sekunde chache baadae akiwa na gitaa lisilokuwa na vumbi sasa, alikwenda huko ndani kwa ajili ya kuchukua kitambaa kikubwa na kulisafisha.
“Tayari.” Akasema Mei Lee huku akimkabidhi bibi lile gitaa. Bibi akapoke taratibu, akalipaka kwenye mapaja yake akilitazama kwa makini kana kwamba lilimkumbusha jambo fulani murua lenye kusisimua lililopata kutokea katika maisha yake. Akafumba na macho kama mtu anayevuta hisia tamu, na hapo kiganja chake cha mkono kilipapasa gitaa lile.
Sekunde chache baadae akashusha pumzi ndefu, akafumbua macho, akamtazama Mei Lee.
“Hili gitaa linaitwa Caihong (Upinde wa Mvua),” akazungumza polepole na kwa hisia kali bibi Pin Ping na kuendelea. “kwangu ni kitu cha thamani zaidi kilichobaki kwenye uso wa dunia. Nilipewa kama zawadi na mume wangu, alinunua Uingereza alipokwenda kusoma. Sijui alifikiria nini hata akaamua kuniletea zawadi ya aina hii kwa sababu mimi na yeye, sote hatukuwahi kuwa wanamuziki; lakini niliipenda.
Basi nilitafuta mwalimu, akanifundisha jinsi ya kulitumia kwa usahihi na nilipohitimu tu nikawa nikitengeneza melodi nzuri kwa ajili ya kumliwaza mume wangu kila usiku.
Alifurahia sana, hata aliandika kwenye wosia wake kwamba akifa kabla yangu nimpigie melodi kadhaa kwenye mazishi yake.” alisimulia bibi Pin Ping na hadi kufikia hapa hisia zilimzidi. Akashindwa kujizuia, akajikuta akitokwa machozi.
Kile alichokisimulia kilimkumbusha mbali sana, kilimpa kumbukumbu za kusisimua za mapenzi. Alimkumbuka Lau, mwanaume aliyemuoa kwa ndao halali, ndoa iliyochochewa na upendo wa dhati wa kila mmoja kwa mwenzake. Alifariki kipindi ambacho bibi Pin Ping bado alikuwa ni mwanamke mwenye nguvu, hivyo baada ya pale alipata kuwa na wanamume wengine na hata kuolewa pia lakini bado nafasi ya Lau ilibaki kama ilivyo; hakuna shababi aliyefanikiwa kumfunika mwanaume huyo.
Bibi aliendelea kulia kwa machozi, Mei Lee alikuwa pale lakini hakuthubutu kusema neno, alielewa wakati mgumu namna ile aliokuwa akipitia bibi yake, hivyo aliamua kumpa uhuru wa kufanya vile alivyoamua, kutoa sumu za kumbukumbu zote za raha alizowahi kupewa na mumewe kipenzi Lau.
Baadae bibi alitulia mwenyewe, hapa sasa Mei Lee akapata nguvu ya kumsemesha na bibi akamuunga mkono kwa kumjibu na kisha mazungumzo mengine yakashika hatamu ambayo yalikuwa na sentensi mbili tu za kati kabla ya bibi kufikia kuelezea kwanini alikuja na lile gitaa.
“Ninataka nikufundishe kupigia gitaa.” Akasema bibi Pin Ping na hivyo ndivyo ilivyokuwa.
Bibi Pin Ping alimfunza barabara Mei Lee jinsi ya kutumia gitaa, na ndani ya wiki nne tu binti akawa tayari na uwezo wa kuchezesha vizuri vidole vyake na kutengeneza muziki mzuri. Alilielewa kwa muda mfupi sana hasa ukilinganisha na watu wengine jinsi ambavyo huchukua kipindi kirefu cha kujifunza matumizi ya dubwana hilo; lakini bila shaka yeye alifanikiwa kutokana na kiu aliyokuwa nayo.
Sasa ikawa kila jioni, baada ya chakula Mei Lee aliwaimbia Mkuki na bibi Pin Ping huku akipiga gitaa. Alifanya hivyo kwa ustadi mkubwa sana na hakika kila mmoja alifarikija kusikiliza nyimbo zake.
****************************************
Mei Lee alikuwa akilala chumba kimoja na bibi Pin Ping; na huko kikongwe huyo aligundua kitu nyeti kuhusu mjuu wake huyu ambacho ni zaidi ya sauti nzuri na kipaji kikubwa alichokuwa nacho.
Aligindua kwamba Mei Lee alikuwa na mapenzi makubwa mno na Mkuki, na si mapenzi ya kawaida, mapenzi ya kaka na dada, bali mapenzi ya Adam na Hawa; mapenzi yaliyopelekea leo hii dunia kuwa na idadi kubwa mno ya watu.
Hili halikuwekwa wazi na Mei Lee mwenyewe, isipokuwa bibi Pin Ping alikuwa shuhuda wa kuweweseka kwa Mei Lee na ndoto zake za kila siku usiku alizokuwa akiota na huku akimtaja Mkuki.
*****************************