Riwaya: Sala ya Sarah

Riwaya: Sala ya Sarah

soon ntazishusha episodes nyingine za sala ya Sarah, hicho ndo cha msingi, na ndo hasa lengo la huu uzi, kwa heshima ya wanaoifuatilia riwaya hii. Tuachane na hayo mengine mkuu

the Legend☆
Ushasomeka mkuu... ila..
Achana na dear... dear..dear..ndio nini...
Usione vyaelea... ...
Afu bora ushushe tu hizo episode mkuu na visirani vitatupungua ..ujuwe arosto ina effect mingi sana....
Asante kwa uelewa mkuu ...ila ndo ivo yaani..mawe yatakuja tu.. ...

Tunakusubiria Al - wattan..!
Mbavu zangu ...


Sent using Jamii Forums mobile app
 
RIWAYA : SALA YA SARAH.

MTUNZI : ALEX KILEO.

0766 404747

SEHEMU YA TISA.

ILIPOISHIA.

RIWAYA : SALA YA SARAH.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA NANE.

ILIPOISHIA.

Mishale ya saa tatu na dakika zake usiku, ndio ndege aliyopanda Sarah ilikuwa inatua katika ardhi ya uingereza kwenye jiji la London,

baada ya dakika kumi mlango wa ndege ulifunguliwa na Sarah akawa ni miongoni mwa watu wa mwanzo kutelemka, alikuwa chini ya uangalizi wa muhudumu wa kike wa ndege ambaye alikabidhiwa na Emily.

Sarah alipelekwa mpaka eneo wanalokaa watu wanaousubiri wageni wao, hapo ndipo walipomkuta kijana mmoja wa kizungu akiwa amebeba bango liliandikwa jina la Sarah, yule muhudumu akampeleka Sarah mpaka mwa kijana yule, kisha yule kijana akatoa shukrani kwa yule muhudumu na baada ya hapo yule kijana akimshika mkono Sarah na kutoka nae eneo la nje ya uwanja wa ndege, wakaelekea kwenye gari ambayo alikuja nayo yule kijana na wakaingia humo, safari ya makazi mapya ikaanza, ndani ya gari ukimya ulitawala,

"Mbona umepoa hivyo, au kwa kuwa Mark ameuawa?" Sarah aliuliza baada ya muda kidogo na kumfanya yule kijana ashtuke, kwa maana yule kijana aliambiwa mtoto huyo hajui chochote kuhusu kifo cha Mark na wala hasimpe taharifa hizo za kifo.

Sasa Sarah amejuaje?

*********ENDELEA**********

"Nani amekuambia jambo hilo?" Kijana wa kizungu aliuliza,

"Kuna mtu tulipakana nae kwenye siti niliyokaa, niliona hiyo habari kupitia simu yake" Sarah alijibu,

"Sawa, una umri gani?" Kijana wa kizungu aliuliza,

"Miaka sita" Sarah alijibu,

"Nilisikia familia yako iliteketea katika moto?, samahani lakini kama hili swali limekuumiza" Kijana wa kizungu aliongea,

"Baba na mama ndio waliteketea kwa moto" Sarah alijibu katika hali ya utulivu,

"Nilisikia na mdogo wako pia aliteketea" Kijana wa kizungu aliuliza huku akisimamisha gari mbele ya nyumba yenye geti jeusi na kupiga honi,

"Mdogo wangu hajafa, yupo, yupo hai" Sarah alitoa jibu jingine tata,

"Alishakufa bwana, yupo wapi unaposema wewe?" Kijana wa kizungu aliuliza huku akiingiza gari ndani ya geti,

"Napajua alipo, wakati ukifika kila mtu atajua ukweli" Sarah aliongea huku akitelemka kwenye gari baada ya yule kijana kumfungulia mlango,

" je huo wakati utafika lini?" Kijana wa kizungu aliuliza,

"Sijui, na sipendi kuulizwa zaidi" Sarah alijibu,

"Haya tumefika, hapa ndio nyumbani" Kijana wa kizungu aliongea huku akitelemsha begi la Sarah lililokuwepo katika buti la gari, lakini pia kijana was kizungu alijiuliza sana juu ya uwezo was Sarah katika kuongea.

Waliingia mpaka ndani na kukuta sebule kubwa ambayo ilikuwa na kochi za sofa na runinga iliyokuwa inaonesha,

"Kaa hapo, ngoja nikamuite anko" Kijana wa kizungu aliongea huku akielekea sehemu ya vyumbani, baada ya muda alirejea huku nyuma yake akifuatwa na Mzungu mwingine aliyevaa fulana nyeusi na chini alikuwa na suruali ya jeshi,

"Naitwa John, karibu sana Sarah" Mzungu alijitambulisha mbele ya Sarah huku akitabasamu,

"Nani amekuambia jina Langu?" Sarah aliuliza kitoto,

"Mimi nakujua, wewe ndio hunijui mimi" John alijibu huku akitabasamu,

"Hapa ni kwako?" Sarah aliuliza tena,

"Ndio, hapa ni kwangu" John alijibu huku akielekea kwenye friji,

"Wewe ni mwanajeshi? Mbona umevaa suruali ya jeshi?" Sarah aliuliza maswali mfululizo,

"Ndio, kwani na wewe unapenda jeshi?" John aliuliza huku akirudi kutoka kwenye friji na mkononi alibeba maziwa na kumpatia Sarah,

"Ndio, nataka kuwa mwanajeshi au muhubiri, sitaki kusoma" Sarah aliongea na kufanya wale wazungu wamshangae,

"Kwanini unasema hivyo Sarah? Si unajua kilichokuleta huku ni shule?" John aliuliza,

"Mimi nataka kuwa tu mwanajeshi kama wewe" Sarah aliongea,

"Basi soma, ukiwa mkubwa utakuwa mwanajeshi" John aliongea kwa upole,

"Au pale kambini kwenu si ipo shule?, akasomee pale" Kijana wa kizungu alimshauri John,

"Sasa kuna gharama ambazo zilitangulizwa kwenye ile shule ambayo ndio anatakiwa akasome" John aliongea,

"Kaongee nao tu, ni vizuri kumpatia mtoto kila anachokitaka" Kijana wa kizungu aliendelea kumshauri,

"Sawa, itabidi kesho niende kuongea nao" John alikubaliana na ushauri,

"Sarah twende nikupeleke chumbani kwako, alafu uoge na upumzike" Kijana wa kizungu aliongea huku akibeba begi la Sarah na kuelekea vyumbani huku Sarah akimfuata kwa nyuma.

Huo ndio ukawa mwanzo wa maisha ya Sarah ndani ya uingereza.

********†***********

Nchini Tanzania ndani ya hospitali kubwa binafsi, katika wodi moja alikuwepo Taita na harry pembeni ya kitanda alicholala Sebastian ambaye ndiye mdogo wake Sarah.

Baada ya muda alikuja Daktari,

"Kazi yenu tayari imeisha, mnaweza mkamchukua mtoto wenu" Daktari aliongea,

"Kwa hiyo hapa kila kitu kinaanza upya, hajui lolote, hata jina lake halijui?" Taita aliuliza,

"Kila kitu, yaani ni mpya huyo" Daktari alijibu,

"Sawa, tunashukuru" Taita aliongea huku akimbeba Sebastian kisha wakaagana na Daktari na kutoka mpaka nje ya hospitali na kuingia ndani ya gari waliyokuja nalo.

"Harry tunafanyaje sasa, sitaki huyu mtoto aishi nyumbani kwangu, si unajua mke wangu alivyo mkorofi?" Taita aliuliza kwa upole,

"Huyu inabidi umpeleke shule za kijeshi, tena za mbali kabisa, wewe si unataka huyu aje kuwa mrithi wako?" Harry aliongea,

"Ndio, ni wazo zuri, basi ngoja akakae kwako wiki chache wakati tunashughulikia hilo jambo" Taita aliongea,

"Kwangu?? hapana, akakae tu kwako, si wiki tu, mchakato wa kupata kila kitu kuhusu usafiri ni wiki tu, kwani unataka umpeleke nchi gani?" Harry aliuliza,

"Nadhani marekani, kule ndio itakuwa rahisi kuingia jeshini, maana nataka na uraia achukue wa uko" Taita alijibu,

"Ana umri gani?" Harry aliuliza,

"Miaka minne" Taita alijibu,

"Sawa kabisa, kupewa uraia inawezekana" Harry aliongea,

"Jina inabidi abadilishwe, nitamuita Vin, kuanzia leo hilo ndio jina lake" Taita aliongea na kufanya Harry atabasamu.

Wakaondoka eneo la hospitali na kurudi nyumbani kwa Taita, baada ya hapo wakaanza kushughulikia mpango wa kumsafirisha Vin.

Baada ya wiki Vin alifanikiwa kusafirishwa na alipewa mtu wa kumuangalia na kumsimamia kwa kila kitu. Huo ndio ukawa mwanzo wa Vin katika safari ya maisha yake, aliweza kufika Marekani na huko mipango ilienda kama ilivyopangwa, Vin akaanza shule ya jeshi, alisoma mpaka akamaliza elimu ya kati, kisha akajiunga na jeshi la marekani, akapata alama za juu katika mafunzo, akateuliwa kwenda kujifunza zaidi nje ya marekani, nako akapata alama ya juu, aliporejea marekani akapandishwa cheo, na muda wote alikuwa anawasiliana na Taita, ndiye aliyemtambua kuwa ni baba yake wa damu, na Taita alikuwa anaenda marekani kila apatapo muda na kumkumbusha Vin kuwa anatakiwa arudi Tanzania alinde Mali zake, yaani Mali za Taita ambaye alijua ndiye baba yake.

Ilikuwa ngumu kumshawishi Vin kuhusu jambo hilo, Vin hakutaka kabisa kusikia suala hilo, na tayari aliambiwa huku hana ndugu, yeye alizaliwa peke yake na mama yake alishakufa, aliuawa na watu wabaya, basi Vin hakuona umuhimu wa kurudi Tanzania kwa kuwa baba yake alikuwa anaonana nae kila anapomuhitaji.

Ndio maisha ya Vin yakawa hivyo, hapo Taita akaona alitumia muda mrefu kumuandaa Vin kwa ajili ya kumfanyisha kazi za kishenzi, alafu leo hii vin hataki kurudi kumtumikia, Taita hakuwa na la kufanya, maana alimpenda sana Vin, na Vin alimpenda sana Taita, tena alimpenda zaidi ya Taita anavyompenda.

*******************

BAADA YA MIAKA KUMI NA TISA.

Ndani ya uwanja wa ndege anatoka msichana mwembamba ndani ya jengo la uwanja wa ndege, huku akivuta begi kubwa la nguo na chini alivaa suruali ya jeans nyeusi iliyombana na kufanya umbo lake lijichore vizuri, baada ya kutoka nje alisimama kwa muda na kuiangalia anga kwa muda kisha akatabasamu huku machozi yakimtoka, akajifuta na kitambaa.

Akapiga hatua chache na kuelekea sehemu zilipoegeshwa taxi na kuingia,

"Habari yako" Dereva taxi akamsalimia yule Dada,

"Ni nzuri, nipeleke hotel yoyote kubwa ya karibu na hapa" Dada alijibu kwa lafudhi ya kigeni,

"Ya nyota ngapi?" Dereva taxi aliuliza,

"Si chini ya tatu, ila isiwe na msongamano wa watu" Dada alijibu,

"Poa" Dereva taxi alijibu kisha akawasha gari na kuliondoa kwa mwendo wa taratibu mpaka katika jengo moja la hotel na kuisimamisha gari, kisha akatelemka na kumfungulia mlango yule Dada, kisha yule Dada akatelemka na begi lake na kumlipa pesa dereva taxi, na akachukua namba ya simu ya dereva taxi, kisha wakaagana na yule Dada akaelekea mapikezi na kumsalimia Dada wa mapokezi,

"Naweza kupata chumba" Dada alimuuliza muhudumu,

"Vipo, karibu" Dada wa mapokezi alijibu,

"Napendaga vyumba vilivyo ghorofa ya juu kabisa" Dada aliongea huku akitabasamu,

"Vipo, hata usijali" Dada wa mapokezi aliongea huku nae pia akitabasamu,

"Haya, nipe funguo" Dada mgeni aliongea,

"Jina unaitwa nani?" Dada wa mapokezi aliuliza huku akibofya computer iliyokuwepo mbele yake,

"Andika Sarah, Sarah Isack" Dada alijibu huku akitabasamu....

*********ITAENDELEA*********

the Legend☆
 
RIWAYA : SALA YA SARAH.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA KUMI.

ILIPOISHIA.

Akapiga hatua chache na kuelekea sehemu zilipoegeshwa taxi na kuingia,

"Habari yako" Dereva taxi akamsalimia yule Dada,

"Ni nzuri, nipeleke hotel yoyote kubwa ya karibu na hapa" Dada alijibu kwa lafudhi ya kigeni,

"Ya nyota ngapi?" Dereva taxi aliuliza,

"Si chini ya tatu, ila isiwe na msongamano wa watu" Dada alijibu,

"Poa" Dereva taxi alijibu kisha akawasha gari na kuliondoa kwa mwendo wa taratibu mpaka katika jengo moja la hotel na kuisimamisha gari, kisha akatelemka na kumfungulia mlango yule Dada, kisha yule Dada akatelemka na begi lake na kumlipa pesa dereva taxi, na akachukua namba ya simu ya dereva taxi, kisha wakaagana na yule Dada akaelekea mapikezi na kumsalimia Dada wa mapokezi,

"Naweza kupata chumba" Dada alimuuliza muhudumu,

"Vipo, karibu" Dada wa mapokezi alijibu,

"Napendaga vyumba vilivyo ghorofa ya juu kabisa" Dada aliongea huku akitabasamu,

"Vipo, hata usijali" Dada wa mapokezi aliongea huku nae pia akitabasamu,

"Haya, nipe funguo" Dada mgeni aliongea,

"Jina unaitwa nani?" Dada wa mapokezi aliuliza huku akibofya computer iliyokuwepo mbele yake,

"Andika Sarah, Sarah Isack" Dada alijibu huku akitabasamu....

*********ENDELEA*********

"Sarah Isack" Dada wa mapokezi aliandika hilo jina huku akirudia kulitamka, kisha akamuelekeza Sarah namna ya kukifikia chumba na Sarah akaondoka zake taratibu na kuingia ndani ya lifti huku akiwa analivuta begi lake taratibu.

Alipoingia kwenye lifti alibonyeza vitufe vilivyopo pembeni ya mlango wa lifti na kisha lifti ikaanza kupanda juu, ilipanda mpaka ghorofa ya mwisho na kisha ikasimama na mlango ukafunguka, Sarah akatoka na kuelekea upande wa kushoto huku akiwa makini kuzisoma namba zilizopo katika kila mlango wa chumba anachopita, baada ya muda alikifikia chumba anachotakiwa akae, akaingiza funguo ndani ya tundu na kisha akaizungusha ile funguo, mlango ukafunguka, Sarah akaingia na kuanza kuangaza ndani ya kile chumba kwa nusu dakika, kisha akaurudishia mlango na kuelekea dirishani, akafungua vioo vya dirisha na kwa Mara ya kwanza akauona mji vizuri, mji aliouacha miaka kumi na Tisa iliyopita,

"Karibu tena Africa" Sarah aliongea peke yake kisha akatabasamu na kuvifunga vioo vya dirisha, kisha akavua suruali yake na kuchukua taulo, akaelekea mariwatoni kujiswafi mwili wake.

***************

Taita wa nyakati hizi utu uzima ulikuwa umemfikia, alikuwa na miaka takribani hamsini na kipindi hiki pesa ilikuwa ni rafiki yake mkubwa, alikuwa yupo karibu sana na serikali kutokana na misaada aliyokuwa anaisaidia serikali na pia alikuwa ni muarifu wa kuuza vitu haramu au vya magendo.

Taita alikuwa anaingiza dawa za kulevya nchini, Taita alikuwa ana kikundi kinajihusisha na ujambazi mkubwa hapa nchini na pia Taita alikuwa na makampuni makubwa makubwa aliyokuwa anayatumia kama njia ya kuficha maovu yake.

Katika kikundi chake kilikuwa vile vile, Harry kama mwanasheria wake ingawa na umri ulikuwa umeenda, na yeye pia alikuwa na fedha za kutosha kutokana na utajiri wa Taita.

Trigger alikuwepo, yeye ndiye alikuwa kiongozi wa vikundi vyote vya uharifu vilivyokuwa vinamilikiwa na Taita, ila safari hii waliongezeka vijana wengine watatu hatari, alikuwepo Sostenes, huyu alikuwa ni msomi aliyebobea katika masuala ya teknolojia, kila mawasiliano na vitu vyote vinahusu teknolojia huyu ndiye alikuwa mratibu na jina la utani aliitwa Tekso, yaani Tek ilisimama kama Teknolojia na So ilisimama kama sostenes ambao ndio jina lake.

Wa pili aliitwa Dula, huyu alisomea masuala ya mbinu na mipango katika kufanikisha jambo, kwa hiyo mipango yao yote ilikuwa inamtegemea huyu mtu, na sifa yake kuu ni kupenda kukaa peke yake muda Mrefu na wenzake wanapenda kumuita strategic, sijui wana maana gani?

Na wa tatu ni Toisa, huyu ni mjanja mjanja tu, hutumiwa sana kwenda kufanya upelelezi kipindi genge hili likiwa linataka kuvamia sehemu, na uzuri wa hawa watu ni kuwa wote walikuwa mafundi wa mapigano na shughuli za magendo walizifanya wote, iwe kusambaza madawa au kuvamia bank basi wote walishika mitutu na kutekeleza kazi chini ya kiongozi wao Trigger.

Hata mke wa Taita alikuwa ameshafiriki kutokana na saratani ya kizazi, kwa hiyo muda huu Taita alikuwa anaishi mwenyewe na mfanyakazi wa ndani kwa ajili ya kumfanyia kazi na kumpikia.

*************

Mida ya saa kumi jioni Sarah alimpigia simu dereva taxi na kumuita, baada ya dakika tano taxi ilikuwa imeshafika nje ya hoteli, Sarah akatelemka ghorofani na kwenda mpaka nje, kisha akaingia ndani ya ile taxi,

"Nipeleke mbezi, mbezi shamba" Sarah aliongea huku akijifunga mkanda wa gari, dereva akaiondoa gari,

"Wewe ni mwenyeji wa huku?" Dereva taxi alimuuliza Sarah,

"Kidogo, nimeshawahi kuishi hapa" Sarah alijibu huku akitabamu,

"Kwa hiyo ulikuwa nje ya nchi kwa ajili ya masomo?" Dereva taxi aliuliza,

"Uko ndipo ninapoishi kwa sasa, nilihama hapa zamani sana" Sarah alijibu,

"Vipi maisha ya uko nje?" Dereva taxi aliuliza,

"Uko maisha kawaida tu" Sarah alijibu,

"Sasa huku mbezi unaenda kwa nani?, au una ndugu?" Dereva taxi aliuliza,

"Hapana, naenda kuangalia kiwanja, kuna mtu anataka kuniuzia" Sara aliongea,

"Kule ni pazuri, pametulia na isitoshe kama hutaki kujenga unapafanya shamba" Dereva taxi aliongea,

"Ebu simamisha hapa, nadhani tumefika" Sarah aliongea na gari ikasimama, kisha Sarah akatelemka na kuiangalia hotel moja kubwa sana, ya ghorofa iliyokuwa inavutia, Sarah aliangalia kwa muda na kisha huzuni ukamjaa moyoni, eneo ambalo ipo hiyo hotel, ndiyo eneo ambao nyumba yao ilikuwepo, ndipo ambapo wazazi wake walichomwa ndani ya nyumba hiyo. Hiyo hotel ilikuwa inaitwa VIN hotel.

Sarah aliendelea kuangalia kwa dakika kadhaa kisha akarudi ndani ya gari,

"Mbona umeiangalia na kuishia nje?" Dereva taxi aliuliza,

"Kuna mtu nilikuwa namuangalia, nadhani hayupo maana gari yake siioni" Sarah aliongea,

"Mpigie simu" Dereva taxi alimshauri Sarah,

"Simu nimeiacha kule hotelini" Sarah alidanganya,

"Nipe namba yake nikusaidie kupiga" Dereva taxi aliongea huku akiitoa simu yake mfukoni,

"Namba yake sijaikariri, acha tu nirudi hotelini, waswahili hawajui kwenda na ahadi" Sarah aliongea na dereva Taxi akawasha gari na kuiondoa,

"Basi bahati mbaya, utamrudia baadae?" Dereva taxi aliuliza,

"Hapana, hii hotel ya nani?" Sarah aliuliza,

"Ile ni ya boss mmoja anaitwa Taita, na jina la hiyo hotel ni jina la mwanae, yupo marekani uko" Dereva taxi alitoa jibu lililoshtua moyo wa Sarah,

"Taita ndio amekuwa na pesa mpaka amejenga hoteli kubwa hivyo?" Sarah alijikuta anauliza bila kutegemea,

"Unamjua Taita kwani?" Dereva taxi aliuliza,

"Namsikiaga tu, toka nipo uingereza nasikia habari zake, sikudhani ana utajiri mkubwa kiasi hicho" Sarah alijibu,

"Ni tajiri mkubwa sana, anaisaidia mpaka serikali" Dereva taxi aliongea,

"Ana biashara gani nyingine tofauti na hotel?" Sarah aliuliza,

"Nyingi sana, anauza magari, ana mashamba makubwa na pia kuna habari anajihusisha na madawa ya kulevya" Dereva taxi alijibu,

"Uliniambia ana mtoto yupo marekani?" Sarah aliuliza,

"Ndio, anaitwa Vin" Dereva taxi alijibu,

"Aisee huyo mtu tajiri sana, anakaa wapi?" Sarah aliuliza,

"Anaishi osterbay, si unajua ndipo matajitiri wanapoishi huko" Dereva taxi alijibu,

"Itabidi nimtafute nifanye nae kazi, unaweza kunielekeza mtaa anaoishi?" Sarah aliuliza,

"Siujui kwa kweli, ila unaweza kutafuta namba zake, kaziweka tu mitandaoni kwa ajili ya biashara" Dereva taxi alijibu huku akiegesha gari nje ya jengo la hotel aliyofikia Sarah,

"Nashukuru kaka" Sarah aliongea huku akimkabidhi ujira wake dereva taxi na kisha akatelemka katika gari, akaingia ndani, alipofika alijitupa kitandani na kuanza kutafakari namna Taita alivyoidhurumu nyumba yao na kufungua hotel hiyo kubwa, ila swali alilojiuliza huyo mtoto wa Taita ni yupi? Mbona hakuwai kumuona kabla? Ila akapuuzia tu na akili yake akaiweka katika kutafuta ukweli wa wapi alipo mdogo wake aitwae Sebastian.

Baada ya muda Sarah alichukua simu yake na kutafuta jina la Vin hotel katika sehemu ya Google, alipoipata akaingia upande wa mawasiliano na kuongea nao kwa muda, alikuwa anaomba namba ya Taita, ilikuwa ngumu kupata ila alijitahidi kubembeleza mpaka akapewa.

Akaichukua ile namba na kuiingiza sehemu ya kutafutia ni wapi mwenye hiyo namba yupo muda huo, simu ikaonesha yupo osterbay, akatabasamu, akabadili nguo na kutoka nje, akaita bajaj na kumuelekeza ni wapi pa kwenda, bajaj ikaondoka mpaka katika duka linalouza Zawadi, Sarah akaingia na kuchukua Zawadi anayoijua yeye na kuiingiza katika box dogo na kumwambia dereva bajaj ampeleke osterbay.

Baada ya dakika kumi na tano, Bajaj ilikuwa imesimama nje ya nyumba kubwa yenye geti, Sarah akatelemka na kwenda getini, akabonyeza kengele, mlinzi akafungua geti,

"Habari yako?" Sarah alimsalimia mlinzi,

"Nzuri, karibu" Mlinzi aliongea,

"Mwenye nyumba nimemkuta?" Sarah aliuliza,

"Ametoka kidogo" Mlinzi alitoa jibu na kumfanya Sarah afikirie kidogo,

"Sawa, basi akija utampatia huu mzigo" Sarah aliongea huku akimkabidhi mlinzi mfuko wa nylon ambao ndani kulikuwa na lile box la zawadi alilolinunua,

"Nimwambie umetoka kwa nani?" Mlinzi aliuliza huku akiupokea,

"Mwambie umetoka umetoka marekani, kwa mwanae" Sarah alijibu,

"Umetoka kwa vini kumbe, saw a binti" Mlinzi alijibu na kisha Sarah akaingia kwenye bajaj na kuondoka huku akitabasamu.

***************

Taita alirudi nusu saa tu baada ya Sarah kuondoka, aliingiza gari ndani ya nyumba, na kisha mlinzi akamkabidhi ule mfuko,

"Umetoka Wapi huu?" Taita aliuliza,

"Kuna binti ameuleta, anasema umetoka marekani kwa vin" Mlinzi alijibu,

"Ooh kumbe vin ameniletea" Taita aliongea kwa furaha huku akiupokea na kuingia nao ndani, alipofika aliuweka mezani na kuufungua, akakuta box, akalichana, alichoona kilichopo ndani akajikuta anashangaa, tena mshangao sio wa kitoto.......

**********ITAENDELEA**********

the Legend☆
 
RIWAYA : SALA YA SARAH.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA KUMI NA MOJA.

ILIPOISHIA.

Taita alirudi nusu saa tu baada ya Sarah kuondoka, aliingiza gari ndani ya nyumba, na kisha mlinzi akamkabidhi ule mfuko

"Umetoka Wapi huu?" Taita aliuliza,

"Kuna binti ameuleta, anasema umetoka marekani kwa vin" Mlinzi alijibu,

"Ooh kumbe vin ameniletea" Taita aliongea kwa furaha huku akiupokea na kuingia nao ndani, alipofika aliuweka mezani na kuufungua, akakuta box, akalichana, alichoona kilichopo ndani akajikuta anashangaa, tena mshangao sio wa kitoto.......

**********ENDELEA**********

" ni nini hiki Vin anafanya?" Taita alijiuliza mwenyewe baada ya kukuta keki ndogo ndani ya lile box, akalifunga box na kutoka mpaka getini kwa mlinzi,

"Huyo binti aliyeleta mzigo alikutajia jina lake?" Taita alimuuliza mlinzi,

"Hapana" Mlinzi alijibu na kumfanya Taita amuangalie kwa muda,

"Kuwa makini sana" Taita aliongea huku akielekea ndani, machale yalianza kumcheza, aliingia chumbani kwake kisha akawasiliana na Vin ili kujua kama kweli ametuma lile box, lakini Vin alikataa na alidai hajui chochote kuhusu hilo box, Taita akakata simu na kuhisi huenda kuna mtu anamchezea akili, akawaza ingekuaje kama hilo box lingekuwa na Bomu?

"Huyu mlinzi nae mpumbavu" Taita aliongea peke yake huku akipanda kitandani na kujilaza kitandani.

*************

Sarah alirudi hotelini na kuingia chumbani kwake, akajitupa juu ya kochi na kutabasamu peke yake,

"Pale ni rahisi sana kuingia, mlinzi mwenyewe mmoja na pia ni rahisi sana kupenyeza kitu chochote cha hatari" Sarah aliongea mwenyewe na kuendelea kutabasamu, kisha akaiendea simu ya mezani na kuipiga, aliongea na wahudumu wa hotelini, alikuwa anahitaji chakula cha jioni muda huo.

Baada ya dakika kumi mlango wa chumbani kwake uligongwa na akaingia muhudumu huku akisukuma meza ya matairi iliyokuwa na chakula,

"Asante mrembo" Sarah aliongea wakati chakula chake kikiwekwa juu ya meza,

"Hutumii kilevi chochote?" Muhudumu alimuuliza Sarah,

"Hapana, uwa natumia mara moja moja. Kwanini umeniuliza hivyo?" Sarah aliuliza,

"Mara nyingi watu wanaoagiza chakula cha jioni hapa hotelini kwetu uwa wanapewa na kilevi cha ofa wanachohitaji, sasa nashangaa wakati naweka chakula chako hapa mezani sioni kilevi" Muhudumu alijibu,

"Sikutaka kuagiza, ila ipo siku nitaagiza" Sarah aliongea huku akicheka,

"Sawa, nakutakia mlo mwema na jioni njema" Muhudumu aliongea huku akiondoka,

"Shukrani, kazi njema" Sarah aliongea na kuiendea meza ya chakula na kisha akakifunua, akanawa mikono na kuanza kula.

Baada ya muda alimaliza kula na kuingia bafuni kuoga, alipomaliza alirudi na kujitupa kitandani. Siku yake iliisha hivyo.

***************

Asubuhi na mapema Sarah aliamka na kujiandaa kwa ajili ya kutoka, akampigia simu dereva taxi na kumuhitaji, baada ya muda dereva taxi aliwasili na Sarah akatoka ndani na kuingia kwenye taxi,

"Za tangu jana?" Sarah alimsalimia dereva taxi,

"Nzuri, leo wapi boss wangu?" Dereva taxi aliuliza,

"Nipeleke kinondoni makaburini" Sarah aliongea,

"Sawa boss" Dereva taxi alijibu na kisha akaiondoa gari taratibu kuelekea uko.

"Sijui itakuwa imebadilika hiyo kino?" Sarah aliuliza,

"Kwani tunapoelekea ni pale pale kwenye makaburi au eneo lingine?" Dereva taxi aliuliza,

"Naenda makaburini" Sarah alijibu,

"Kuna ndugu yako amezikwa pale" Dereva taxi aliuliza,

"Wazazi wangu wamezikiwa pale" Sarah alijibu,

"Ooh pole sana, wamezikwa sehemu moja?" Dereva taxi aliuliza,

"Hapana, wamezikwa sehemu tofauti ila eneo moja" Sarah alijibu na ukimya ukatawala.

Gari ilitembea mpaka makaburuni na kisha dereva akaiegesha nje ya uzio wa makaburi na Sarah akatelemka huku akiwa na maua makubwa mawili na mataji mawili, akatembea mpaka eneo la ndani la makaburi na kuanza kuangaza angaza sehemu yalipo makaburi ya wazazi wake, aliangaza kwa dakika kadhaa na kuyaona, yalikuwa yameshaanza kubomoka, ilionekana yalikaa muda Mrefu bila kufanyiwa matengenezo.

Sarah akayasogelea na kuyaangalia kwa muda, kisha akaweka maua kwenye kila kaburi na yale mataji akayaweka kwenye ile misalaba ya makaburi, kipindi hicho machozi yalikuwa yanamtoka, uchungu wa kuondokewa na wazazi ulimjaa na pia moyoni alisikitika wazazi wake kufa kifo cha kikatili tena kilichosababishwa na mtu ambaye ni wa karibu kwao.

Sarah alipomaliza kuweka mataji, alirudi hatua mbili nyuma, akatoa kitambaa na kujifuta machozi, kisha akapiga magoti katikati ya makaburi yale na kufumba macho,

"Baba na mama yangu, nadhani wakati wangu wa kulipa kile mlichofanyiwa umefika, nadhani wakati wa kuwapa furaha angalau kwa kiasi kidogo ni wakati huu ambao ninao sasa, naamini mtanipa ruhusa ya kulipa ubaya kwa ubaya.

"Mwenyezi Mungu nipe moyo wa moto, moyo wa kumuunguza kila aliye mbaya juu yangu" Sarah alimaliza kusali na kufungua macho yake, kisha akasimama na kupangusa magoti yake, akaelekea mpaka kwenye taxi,

"Hatuwezi pata mafundi ujenzi hapa?" Sarah alimuuliza dereva taxi,

"Ebu ngoja nikamuulize mlinzi wa hapa" Dereva taxi alijibu huku akitelemka na kuelekea kwenye kibanda kidogo kilichopo pembezoni mwa uzio wa makaburi.

Dereva taxi alipofika kwenye hicho kibanda alimkuta mzee akiwa amekaa huku akivuta goso, goso ni tumbaku iliyonyongorotewa kwenye karatasi na kuwa kama sigara,

"Shikamoo Mzee" Dereva taxi alimsalimia yule Mzee,

"Marahaba" Mlinzi aliitikia,

"Babu eti hapa ni eneo gani naweza kupata mafundi, nataka nirekebishe kaburi" Dereva taxi aliuliza na kisha mlinzi akamuelekeza sehemu mafundi wanapopatikana. Dereva taxi akamshukuru mlinzi na kuondoka zake.

Dereva taxi alipomfikia Sarah alimueleza alivyoelekezwa na mlinzi, Sarah akiongozana na dereva taxi waliambatana kwa miguu mpaka sehemu walipo mafundi, hapakuwa mbali na ndio maana waliacha gari.

Waliwakuta mafundi na kisha wakawachukua mpaka eneo la makaburi yanayotakiwa kukarabatiwa, mafundi wakapiga hesabu za tofali na saruji, Sarah akatoa pesa ya tofali na muda huo tofali zikaenda kununuliwa, tofali zilipokamilika, mafundi wakaanza kujengea makaburi ya Isack na mke wake, kipindi chote Sarah alikuwa hapo akifuatilia kila hatua.

Mafundi walitumia saa moja kukamilisha ile kazi, kisha wakalipwa pesa yao na kuondoka zao huku wakimsisitiza Sarah kuwa kesho akumbuke kumwagia maji yale makaburi kwa ajili ya kufanya ukuta uwe imara, Sarah akawakubalia.

Sarah na dereva wakarudi ndani ya gari,

"Wapi boss?" Dereva taxi akauliza,

"Nirudishe hotelini" Sarah akajibu na kisha dereva taxi akawasha gari na kuliondoa kistaharabu, safari ya kumrudisha Sarah hotelini ilianza.

*****************

Asubuhi mishale ya saa mbili, Baba Isack ambaye ni babu yake Sarah alionekana makaburini huku akiwa na mwanae, kitu kilichowashangaza ni kukuta maua juu ya makaburi na pia kukuta makaburi yakiwa yamekarabatiwa vizuri,

"Ni nani aliyejengea, au Taita?" Babu yake Sarah alimuuliza mwanae,

"Sasa mimi nitajuaje baba?, mpigie simu umuulize" Mwanae alijibu kwa mshangao,

"Ila Taita sijui, maana sidhani kama alishawahi kuja hapa toka tumewazika hawa, labda kwa kuwa amekuwa mtu mzima na busara zinaanza kumuingia" Babu Sarah aliongea huku akimtazama mwanae,

"Ebu mpigie umuulize, tuache kuishi kwa hisia" Mwanae aliongea na kisha babu Sarah akaitoa simu mfukoni na kumpigia Taita na kumuuliza kama ni yeye ndiye aliyejengea makaburi, kwanza Taita alishtuka lakini alikanusha na akaahidi kufika hapo muda mfupi ujao.

************

Asubuhi hii Sarah aliamka mida ya saa tatu na kukumbuka kuwa anahitajika kufika eneo la makaburini kwa ajili ya kumwagilizia tofali zilizojengwa siku iliyopita, akaoga na kumpigia siku dereva wake kwa ajili ya kwenda makaburini.

***************

Taita aliwasili makaburini saa nne kasoro na alikuwa na Harry na Trigger, walipofika walielekea moja kwa moja mpaka kwenye makaburi husika na kumkuta babu yake Sarah na mwanae, wakawasalimia,

"Kwa hiyo mzee nyie wenyewe hamjui aliyejengea?" Taita aliuliza huku akishangaa,

"Sisi tulijua ni wewe na ndio maana tulikupigia simu" Babu yake Sarah alijibu na kufanya Taita afikiri kidogo,

"Ebu nifuateni" Taita aliongea huku akielekea kwenye kibanda cha mlinzi, alipofika walimkuta yule Mzee ambaye ni mlinzi, wakampa salamu,

"Eti ndugu ni nani aliyeyajengea yale makaburi mawili?" Taita aliuliza huku akiyaoneshea kwa kidole yale makaburi,

"Ni kijana mmoja wa kiume na wa kike, walikuja jana na kujengea hayo makaburi" Mlinzi alijibu,

"Wapoje wapoje?, au walijitambulishaje?" Babu yake Sarah aliuliza kwa shauku,

"Hawajajitambulisha kwa kweli" Mlinzi alijibu,

"Mzee ulitakiwa uwaulize, wewe si ndio mwenye mamlaka hapa?" Taita aliuliza huku akimuangalia mlinzi, na wakati huo ile taxi anayoitumia Sarah ilikuwa ikiegeshwa nje ya uzio wa makaburini,

"Bora aisee, tena watu wenyewe wale pale kwenye ile gari" Mlinzi aliongea huku akiioneshea kidole ile taxi na kufanya watu wote waitolee macho na kuangalia ni wakina nani wataoshuka, ukafunguliwa mlango wa dereva akatelemka dereva, na kufanya wakina Taita wamtolee macho bila kumjua, na wakati huo mlango wa abiria ulikuwa ukifunguliwa, hapo kila mmoja akatupa karata yake kuona huyo atayeshuka watamtambua au lah????????????

********ITAENDELEA*********

the Legend☆
 
RIWAYA : SALA YA SARAH.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA KUMI NA MBILI.

ILIPOISHIA.

Taita aliwasili makaburini saa nne kasoro na alikuwa na Harry na Trigger, walipofika walielekea moja kwa moja mpaka kwenye makaburi husika na kumkuta babu yake Sarah na mwanae, wakawasalimia,

"Kwa hiyo mzee nyie wenyewe hamjui aliyejengea?" Taita aliuliza huku akishangaa,

"Sisi tulijua ni wewe na ndio maana tulikupigia simu" Babu yake Sarah alijibu na kufanya Taita afikiri kidogo,

"Ebu nifuateni" Taita aliongea huku akielekea kwenye kibanda cha mlinzi, alipofika walimkuta yule Mzee ambaye ni mlinzi, wakampa salamu,

"Eti ndugu ni nani aliyeyajengea yale makaburi mawili?" Taita aliuliza huku akiyaoneshea kwa kidole yale makaburi,

"Ni kijana mmoja wa kiume na wa kike, walikuja jana na kujengea hayo makaburi" Mlinzi alijibu,

"Wapoje wapoje?, au walijitambulishaje?" Babu yake Sarah aliuliza kwa shauku,

"Hawajajitambulisha kwa kweli" Mlinzi alijibu,

"Mzee ulitakiwa uwaulize, wewe si ndio mwenye mamlaka hapa?" Taita aliuliza huku akimuangalia mlinzi, na wakati huo ile taxi anayoitumia Sarah ilikuwa ikiegeshwa nje ya uzio wa makaburini,

"Bora aisee, tena watu wenyewe wale pale kwenye ile gari" Mlinzi aliongea huku akiioneshea kidole ile taxi na kufanya watu wote waitolee macho na kuangalia ni wakina nani wataoshuka, ukafunguliwa mlango wa dereva akatelemka dereva, na kufanya wakina Taita wamtolee macho bila kumjua, na wakati huo mlango wa abiria ulikuwa ukifunguliwa, hapo kila mmoja akatupa karata yake kuona huyo atayeshuka watamtambua au lah????????????

*********ENDELEA*********

Alishuka kijana mmoja ambaye hakuwa nadhifu, alishuka na kuelekea upande wa nyuma wa gari na kufungua buti kisha akatelemsha madumu mawili makubwa ya maji na kufunga buti, kisha wakaongea na dereva taxi na dereva taxi akaanza kuelekea sehemu yalipo makaburi ya wazazi wa Sarah na nyuma alifuatwa na yule kijana huku akiwa amebeba yale madumu ya maji.

Walifika mpaka yalipo makaburi na kisha yule kijana akaanza kumwagia maji yale matofali yaliyojengwa siku iliyopita.

Taita na wenzake wakasogea mpaka alipo dereva taxi na yule kijana,

"Habari zenu vijana?" Taita alisalimia,

"Salama, shikamooni" Dereva taxi alijibu kwa heshima baada ya kumtambua Taita,

"Marahaba, mbona mnalimwagia maji kaburi letu?" Taita aliuliza kwa sauti tulivu,

"Hili ni lenu? mimi nimeagizwa tu nilimwagie tu baada ya kujengwa jana" Dereva taxi alijibu,

"Nani amewaagiza wanangu?" Babu Sarah aliuliza huku akistaajabu,

"Ni msichana fulani hivi, uwa anaikodi gari yangu mara kwa mara ndio tumetokea kuzoeana" Dereva taxi alijibu kistaharabu,

"Anaitwa nani na anaishi wapi?" Taita aliuliza,

"Jina lake sikubahatika kulijua, ila anaishi hotelini kule mjini" Dereva taxi alijibu,

"Kwani Sarah amerudi?" Taita aliuliza huku akimgeukia babu yake Sarah,

"Sarah hajarudi, na jana tuliongea nae na amesema hawezi kuja hivi karibuni" Babu Sarah alijibu,

"Unaweza kutupeleka hiyo hotel anayoishi huyo binti?" Taita alimuuliza dereva taxi,

"Haina shida, twendeni" Dereva taxi alijibu na kisha akatoa hela kumlipa yule kijana aliyeenda nae pale, ni kijana alimkodi kwa ajili ya kumwagia ule ukuta wa makaburi, baada ya hapo dereva taxi alienda na kuingia kwenye gari lake ambapo pia kwenye hilo gari alipanda babu Sarah na mwanae na gari la pili alikuwepo Taita ambaye alikuwa na Harry.

Safari ilianza kwa mwendo wa wastani huku gari zile zikiongozana kistaharabu na kila mmoja alikuwa anawaza lake, wakati Taita, Harry na Babu Sarah wakiwa na shauku ya kumuona huyo binti, lakini dereva taxi yeye alichokuwa anakiwaza ni kuwa leo huyo binti atapata bahati ya kukutana na Taita, tajiri mkubwa Tanzania na aliamini yule binti atafurahi kwa maana alishamwambia ana wazo la kufanya biashara na Taita.

Dereva taxi alisimamisha gari nje ya hotel ambayo anaishi Sarah na kisha gari ya Taita ikapaki nyuma ya taxi na wote wakashuka kisha dereva taxi akatoa simu yake mfukokoni Ili ampigie Sarah na kumtaharifu juu ya ugeni huo, cha ajabu namba ya Sarah hakuikuta, akajaribu kuangalia namba alizowasiliana nazo siku hiyo, lakini bado namba hakuiona, akapata mfadhaiko kidogo,

"Vipi, hapatikani?" Babu Sarah alimuuliza dereva taxi,

"Namba yake siioni, sijui nimeifuta bila kujua" Dereva taxi alijibu,

"Ebu twendeni ndani" Taita aliongea huku akianza kupiga hatua na wenzake wakamfuata kwa nyuma, akiwepo na dereva taxi pia, walifika mpaka mapokezi na kumkuta muhudumu wa pale aliyekuwa amekaa, wakamsalimia kwa upole,

"Samahani, yule Dada ambaye uwa naondoka nae hapa nimemkuta?" Dereva taxi aliuliza,

"Ameondoka muda sio Mrefu" Dada wa mapokezi alijibu baada ya kumuelewa dereva taxi,

"Ila atarudi, si ndio?" Taita akauliza,

"Yaani ameondoka moja kwa moja, amerudisha na funguo" Dada wa mapokezi alijibu,

"Unaweza kutusaidia jina lake?" Taita aliuliza,

"Jina lake silijui" Dada wa mapokezi alijibu,

"Si uangalie kwenye record zenu, au Wateja wakiingia hapa uwa hamnakiri wasifu wao?" Taita aliuliza na kumfanya yule Dada aanze kubonyeza bonyeza computer, alifanya hivyo kwa dakika mbili,

"Eeh, sioni kitu kwa kweli, hata hii mimi imenishangaza" Dada wa mapokezi aliongea kwa mshangao,

"Yaani record zake hazionekani?" Taita aliuliza,

"Yaani zimefutika zote, hii inaweza kugharimu kazi yangu" Dada wa mapokezi aliongea kwa unyonge,

"Huyu mtu ni nani?" Babu Sarah aliuliza huku akijua kabisa hakuna mwenye jibu,

"Mi naondoka inawezekana tunapoteza muda kumfuatilia mtu asiyekuwa na maana" Taita aliongea huku akielekea nje na kufanya wenzake wamfuate, walitoka mpaka nje,

"Mzee tutawasiliana, acha niwahi majukumu" Taita aliongea huku akimtazama babu Sarah,

"Mwanangu ebu tupe lifti ya kutufikisha nyumbani, maana hali ya mifuko ni tete" Babu Sarah aliongea kwa upole,

"Chukueni taxi Mzee wangu" Taita aliongea huku akitoa pesa mfukoni na kumpatia babu Sarah,

"Asante mwanangu" Babu Sarah alipokea na kuzitia mfukoni kisha wakaagana na Taita.

Taita aliingia kwenye gari yake huku akiwa na Harry,

"Huyo binti ni nani?" Taita alimuuliza Harry,

"Sasa mimi nitajuaje mkuu?" Harry alihoji huku akimshangaa bosi wake huyo,

"Ujue hivi vitu hatupaswi kuviweka kichwani sana, inawezekana huyo binti amekosea au amesahau makaburi ya ndugu zake na ameyafananisha na yale ya kwetu" Taita aliongea,

"Hiyo pia inawezekana, ila usipuuze tu, mnatakiwa mumfuatilie" Harry aliongea,

"Tutamfuatiliaje wakati hatumjui?" Taita aliuliza,

"Ila sawa, huenda uliyosema ni sawa" Harry aliongea,

"Niliyosema yapi?" Taita aliuliza,

"Hayo ya kufananisha makaburi" Harry alijibu,

"Ebu tuachane na hayo mambo. Umeshakunywa chai?" Taita alimuuliza mwenzake,

"Bado" Harry alijibu,

"Basi ngoja tupitie hotelini tukanywe" Taita aliongea,

"Ni jambo zuri" Harry aliitikia kisha Taita akakanyaga mafuta ya gari na gari ikaongeza mwendo.

*******************

Sarah alishajua kitakachotokea baada ya kujenga makaburi, alihisi kabisa kama kuna ndugu wangeenda kuangalia makaburi yale ni lazima wangepata viulizo vya maswali ya kuwa ni nani aliyeyajengea makaburi yale, kwa hiyo alichofanya ni kumtuma dereva taxi akayamwagilie, kitu ambacho hakukijua dereva taxi ni kuwa muda aliopewa pesa, kiliwekwa na kinasa sauti ambacho kilikuwa kinafikisha sauti kwa Sarah, kwa hiyo wakati dereva akiwa anahojiwa na Taita makaburuni, ndio huo muda Sarah aliosikia kuhusu watu hao kwenda hotelini hapo, alichofanya Sarah ni kubeba mabegi yake na kwenda kukabidhi funguo mapokezi na kulipia kila kitu, mkoni alikuwa na kifaa kidogo cheusi alikishika, kwa hiyo wakati yule muhudumu akijaza file la Sarah kwenye computer, kila kitu kilienda vizuri, ila kilifutika baada ya muhudumu kutoka tu kwenye file lile, naam; hivyo ndivyo Sarah alivyoucheza huo mchezo kwenye computer ya hotel hiyo na mchezo huo huo aliucheza kwenye simu ya dereva taxi.

Sarah alitoka nje ya hotel na kwenda kwenye mgahawa wa kitalii uliopo mbele ya hotel hiyo, akaagiza juisi na kisha akakaa katika kiti kinachotazama mlango, mlango wenyewe ulikuwa wa kioo, kwa hiyo aliweza kupaona nje vizuri.

Aliweza kuona namna Taita alivyokuja huku akiambatana na babu yake, aliweza kusikia vyote walivyoongea, aliendelea kuwaangalia mpaka walivyoondoka, ila neno ambalo lilimuuma ni kitendo cha babu yake kumuomba pesa Taita, aliona namna babu yake alivyoisha kwa umasikini, roho ilimuuma Sarah ila hakuwa na papara. Taita alivyoondoka na kisha babu yake alivyoondoka, Sarah alitoka mgahawani hapo na kuchukua bajaji kisha akaiamuru bajaj hiyo impelekee eneo lolote la uswahilini lililo na guest.

Dereva bajaj aliondoa bajaj na kuanza kuelekea maeneo anayoyajua yeye, ilimchukua takribani dakika ishirini ndipo dereva bajaj aliposimamisha bajaj yake nje ya guest iliyochoka,

"Hapa patakufaa dada?" Dereva bajaj alimuuliza Sarah,

"Nahisi patafaa, nitelemshie begi" Sarah aliongea huku akishuka, kisha dereva bajaj akamshushia begi lake,

"Nisubiri, nataka unipeleke mahali" Sarah aliongea huku akilivuta begi lake na kuingia ndani ya guest, alifika mapokezi na kukaribishwa, akapata chumba na kuweka mizigo yake, kisha akatoka na kumwambia dada wa guest kuwa atarudi muda si Mrefu.

Akatoka nje na kupanda ndani ya bajaj,

"Nipeleke osterbay" Sarah aliongea na dereva akawasha bajaj na safari ya osterbay ikaanza chini ya maelekezo ya Sarah.

Bajaj ilifika mpaka osterbay mtaa ule ule anaoishi Taita, Sarah akashuka na kumlipa dereva bajaj pesa yake, dereva bajaj akapokea na kuondoka zake.

Sarah akapiga hatua mpaka katika nyumba ya Taita, alipofika nje ya geti akagonga geti mlinzi akafungua,

"Nimekuja tena" Sarah aliongea huku akitabasamu,

"Karibu" Mlinzi aliongea,

"Taita nimemkuta?" Sarah aliuliza,

"Ametoka" Mlinzi alijibu,

"Naomba nimsubiri" Sarah aliongea,

"Pita ndani ya geti" Mlinzi aliongea kisha Sarah akaingia ndani ya geti,

"Nyumba nzuri, kubwa" Sarah aliisifia nyumba ya Taita huku akitabasamu,

"Twende ndani" Mlinzi aliongea huku akitangulia na kumpeleka Sarah sebuleni, Mlinzi akamuita mfanyakazi wa ndani na kumkabidhisha Sarah kisha mlinzi akarudi getini.

Sarah akasalimiana na mfanyakazi wa ndani, kisha Sarah akajitambulisha yeye ni mchumba wa Vin ili kumtoa hofu yule binti, baada ya huo utambulisho, mfanyakazi wa ndani alielekea jikoni kuendelea na kazi na kumuacha Sarah akitazama runinga.

************

Taita na Harry walipotoka kupata kifungua kinywa waliamua waelekee nyumbani kwa Taita, walifika getini na kisha mlinzi akafungua geti, Taita akaingiza gari na kuiegesha kisha akashuka,

"Kuna mpya gani?" Taita aliuliza wakati alifunga mlango wa gari,

"Yule binti aliyeleta Zawadi siku ile, amekuja tena" Mlinzi alijibu na kufanya Taita amuwekee umakini,

"Ameleta nini leo?" Taita aliuliza huku akiwa amemkazia macho mlinzi,

"Leo amekuja mwenyewe tu, yupo sebuleni" Mlinzi alijibu,

"Unamuamini vipi mpaka umempeleka sebuleni?" Taita aliuliza,

"Kama ni mgeni unadhani angekaribishwa wapi?" Harry aliingilia kati,

"Sio kila mtu anaaminika" Taita alijibu huku akianza kupiga hatua za kuelekea sebuleni na pia alikuwa na shauku kubwa ya kumjua huyo binti.

Alitembea mpaka alipoufikia mlango wa sebuleni na kuufungua taratibu, baada ya kufungua akajikuta anatoa mguno wa mashaka.......

********ITAENDELEA**********

the Legend☆
 
RIWAYA : SALA YA SARAH.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA KUMI NA TATU.

ILIPOISHIA.

Taita na Harry walipotoka kupata kifungua kinywa waliamua waelekee nyumbani kwa Taita, walifika getini na kisha mlinzi akafungua geti, Taita akaingiza gari na kuiegesha kisha akashuka,

"Kuna mpya gani?" Taita aliuliza wakati alifunga mlango wa gari,

"Yule binti aliyeleta Zawadi siku ile, amekuja tena" Mlinzi alijibu na kufanya Taita amuwekee umakini,

"Ameleta nini leo?" Taita aliuliza huku akiwa amemkazia macho mlinzi,

"Leo amekuja mwenyewe tu, yupo sebuleni" Mlinzi alijibu,

"Unamuamini vipi mpaka umempeleka sebuleni?" Taita aliuliza,

"Kama ni mgeni unadhani angekaribishwa wapi?" Harry aliingilia kati,

"Sio kila mtu anaaminika" Taita alijibu huku akianza kupiga hatua za kuelekea sebuleni na pia alikuwa na shauku kubwa ya kumjua huyo binti.

Alitembea mpaka alipoufikia mlango wa sebuleni na kuufungua taratibu, baada ya kufungua akajikuta anatoa mguno wa mashaka.......

**********ENDELEA**********

Hakukuta mtu, Taita ikabidi amuite mfanyakazi wa ndani, mfanyakazi akaja sebuleni,

"Nimeambiwa kuna mgeni, yupo wapi?" Taita aliuliza,

"Ameondoka muda si Mrefu" Mfanyakazi alijibu,

"Ameondoka?" Taita aliuliza kwa mshangao,

"Ametoka, kwani mlinzi hajakwambia?" Mfanyakazi akauliza,

"Yeye ndio ameniambia yupo ndani" Taita akajibu huku akishangaa,

"Ameshaondoka, au labda wakati akitoka mlinzi hakuwa getini" Mfanyakazi akajibu,

"Mmeongea nae nini huyo mgeni?" Taita akauliza,

"Alikuwa anataka akusalimie, ameniambia yeye ni mchumba wa Vin" Mfanyakazi akajibu,

"Ndicho hicho tu?" Taita akauliza,

"Hajaniambia kingine" Mfanyakazi akajibu,

"Sawa, kuweni makini sana na wageni, sio kila mtu unamuamini" Taita aliongea huku akielekea nje, alitoka mpaka getini kwa mlinzi,

"Vipi nifungue geti?" Mlinzi akauliza,

"Mbona ndani sijakuta mgeni, nimeambiwa ameondoka" Taita aliongea huku akimuangalia mlinzi,

"Ameondoka?" Mlinzi aliuliza,

"Unaniuliza mimi tena, ina maana wewe hukumuona wakati akiondoka?" Taita aliuliza huku hasira zikianza kumpanda,

"Kweli bosi, nimekumbuka kuwa alitoka, nisamehe nilisahau" Mlinzi aliamua kudanganya ili asionekane mzembe kazini,

"Una mawazo gani mpaka unasahau kwamba kuna mgeni ametoka?" Taita aliuliza kwa ukali,

"Nisamehe sana mkuu, nilipitiwa tu" Mlinzi aliongea huku kichwa chake kikikataa kabisa kuamini kuwa yule msichana ameondoka,

"Kuwa makini" Taita aliongea huku akielekea ndani,

"Sawa mkuu" Mlinzi alijibu huku akimtazama bosi wake anavyoondoka, Taita alivyoingia ndani tu, mlinzi akaelekea nyuma ya nyumba na kuanza kukagua usalama, alipata wasiwasi baada ya kuambiwa mgeni ameondoka wakati yeye hakumuona akipita getini.

Mlinzi baada ya kukagua upande wa nyuma na kuridhika kuwa hakuna kitu chochote kilichotokea, aliamua arudi zake getini.

"Tutakaribisha mpaka majini sasa" Mlinzi aliongea peke yake huku akikaa juu ya kiti pembeni ya geti.

*************************

Sarah alivyoenda kwa Taita, alijua kabisa Taita hayupo, alichofanya ni kwenda kusoma ramani ya ndani na pia alifanikisha kuweka vinasa sauti kwenye sehemu mbili ndani ya sebule ya Taita, na alipomaliza kuweka vinasa sauti hivyo, alimuita Dada wa kazi na kumuaga, ingawa dada wa kazi alishangaa kitendo cha Sarah kuondoka ndani ya muda mfupi, Sarah aligundua hilo na kumdanganya kuwa amepigiwa simu na anahitajika haraka ila atarudi hapo siku yoyote, Dada wa kazi hakuwa na neno, akakubali kumruhusu Sarah aende.

Wakati Sarah anafungua mlango wa sebuleni, aliweza kuna gari ikisimama nje ya geti, akahisi huenda hiyo gari ni ya Taita, alichofanya Sarah ni kutoka kwa mwendo wa haraka na kuelekea nyuma ya nyumba, uko akaangalia mazingira na kugundua anaweza kutoka nje kwa kutumia ukuta ingawa ukuta ulikuwa Mrefu kiasi, alichofanya Sarah alirudi nyuma hatua nne, kisha kwa kasi ya ajabu akauendea ukuta na kuurukia, mikono ikagusa kingo za juu za ukuta, Sarah akajivuta na kupanda juu, kisha akajitupa na kutua upande wa pili, akaangalia kushoto na kulia na hakuona mtu, akatabasamu na kuanza kutembea taratibu mpaka kwenye Barabara ya lami.

Aliendelea kutembea kwa mwendo wa madaha huku akiwa amevaa headphone kama anasikiliza muziki, kumbe alikuwa anasikiliza maongezi yote yaliyokuwa yanaendelea ndani ya sebule ya Taita.

Sarah alitembea kwa mwendo wa madaha mpaka kwenye barabara inayopitisha magari mengi, akaita bajaj na kuingia ndani na kisha akajirudisha mpaka guest ya uswailini kule alipofikia.

Akaingia ndani na kujifungia mlango na kisha akajitupia kitandani na kuanza kufikiria namna anavyopiga hatua zake katika kulipa kisasi, hakuona kama kuna hatua amekosea ila alichofurahi ni mambo kwenda kama anavyotaka yeye,

"Inafuata hatua ya usumbufu sasa" Sarah aliongea peke yake kisha akavua headphones, akasimama na kutoa nguo mwilini kisha akafungua begi lake na kutoa taulo na kujifunga, akaelekea bafuni.

Alitumia muda Mrefu kujisafi mwili, alipotoka bafuni alirudi chumbani na kutafuta suruali ilioushika mwili wake na kuivaa, kisha juu akavaa fulana nyepesi, akatoka mpaka sehemu ya mapokezi,

"Hapa ni wapi naweza kupata madalali wa nyumba?" Sarah alimuuliza Dada wa mapokezi,

"Wapo kule, shika iyo njia inayoelekea kushoto, mwisho kule utakuta kuna kijiwe cha kahawa, hapo ndipo walipo madalali wa nyumba" Dada wa mapokezi alimuelekeza Sarah,

"Nashukuru" Sarah aliongea huku akiondoka na kufuata maelekezo ya yule Dada, alienda moja kwa moja mpaka kwenye kijiwe cha kahawa na kumpata kijana mmoja, akatoka nae katikati ya kundi la watu,

"Kaka mimi natafuta nyumba" Sarah aliongea baada ya salamu,

"Nyumba au chumba?" Dalali aliuliza huku akimuangalia Sarah,

"Nataka nyumba nzima" Sarah aliongea kwa msisitizo,

"Hiyo nyumba unataka upange au unanunua kabisa?" Dalali aliendelea kuuliza,

"Nahitaji ya kununua kabisa" Sarah alijibu,

"Unataka iweje?" Dalali akatupa swali jingine,

"Nataka iwe na vyumba vitatu, kimoja kiwe master, alafu iwe na jiko, stoo, varanda na choo kingine cha ndani kwa ajili ya watu " Sarah aliongea,

"Kitapatikana, unahitaji uhamie lini?" Dalali aliuliza,

"Siku yoyote kitakapopatikana, alafu kinatakiwe kiwe nje ya mji" Sarah aliongea,

"Yaani mjini ila pembezoni, sio katikati ya mji?" Dalali aliuliza,

"Nje ya mji, hata ukipata porini ni sawa, sio lazima iwe Dar es salaam, hata nje ya Dar, ili mradi niwe jirani na Dar" Sarah alitolea ufafanuzi kauli yake,

"Nimekuelewa, nipe namba yako ya simu ili nikifanikisha kukipata, nikutaharifu" Dalali aliongea,

"Sina simu, ukitaka kunipata nenda guest moja inaitwa "SHUMBE" ipo hii barabara niliyotokea, nipo hapo muda wote, ukifika pale ulizia Sarah" Sarah aliongea,

.

"Sawa Dada, ngoja hiyo kazi niianze leo" Dalali aliongea,

"Sawa, jitahidi ukamilishe haraka" Sarah aliongea kisha wakaagana na Dalali, Sarah akarudi Guest kwenda kupumzisha akili.

Alipofika mapokezi alimkuta dada wa mapokezi,

"Vipi umempata dalali?" Dada wa mapokezi alimuuliza Sarah,

"Nimempata, nashukuru kwa msaada wako" Sarah alijibu,

"Asante kushukuru" Dada wa mapokezi alijibu,

"Naenda kupumzika, akija mtu yoyote kuniulizia, muoneshe chumba changu apitilize mpaka ndani" Sarah alimwambia dada wa mapokezi huku akiamini hakuna mtu atayekuja kumuulizia zaidi ya dalali,

"Sawa" Dada wa mapokezi alijibu na Sarah akaelekea chumbani kwake kupumzika.

*****************

Taita hakuridhika na wala hakutaka kuamini huyo msichana aliyekuja ni mchumba wa Vin, kwanza aliamini kama huyo msichana ni mchumba wa Vin, basi Vin angempa taharifa baba yake juu ya ujio wa msichana huyo.

Taita akatoa simu yake mfukoni na kumpigia mwanae huyo na kumuuliza kama ana mchumba Tanzania, lakini Vin alikataa katakata na kwanza alishangaa kusikia hivyo. Taita akakata simu na kuanza kuhisi huenda kuna adui yake katika biashara amemtuma huyo dada kumchunguza.

Taita akatoka mpaka sebuleni na kuanza kukagua kama pako Salama, katika kupekua pekua ndipo alipokiona kinasa sauti kidogo sana pembeni ya kochi, Taita akachukua simu yake na kumpigia kijana wake ambaye ni mtaalam wa teknolojia, huyo kijana anaitwa Sostenes, ila wanamuita Tekso.

Baada ya dakika kumi Tekso alifika na kuoneshwa hicho kinasa sauti, akakichunguza kisha akakizima kwa utaalam, alafu akachukua waya mmoja na kuugeuza, akaupachika kwenye kifaa chake kilichopo kama computer, hapo ndipo alipoweza kugundua huyo mtu aliyeweka hicho kinasa sauti yupo wapi muda huo,

"Tumeshampata huyu" Tekso aliongea huku akitabasamu,

"Ngoja nimuite kijana mmoja uongozane nae, mkaniletee huyo binti" Taita aliongea,

"Mwite aende mwenyewe, mimi nitakuwa hapa namuelekeza kupitia mtambo wangu" Tekso alijibu kisha Taita akamuita kijana wake mmoja aliyejaa jaa mwili.

"Kuna kazi ya ghafla imetokea" Taita alimwambia yule kijana,

"Nipo tayari, niagize mkuu" Kijana aliongea kikakamavu,

"Kuna mtu unatakiwa ukamchukue" Taita aliendelea,

"Yupo wapi?" Kijana aliuliza,

"Tekso ndio atakuwa anakuelekeza kupitia simu, mpaka hiyo sehemu alipo huyo mtu" Taita aliongea,

"Nitamjuaje kama ndiye yeye?" Kijana aliuliza,

"Ni binti, mwembamba kiasi, ukimkuta tofauti na huyo pia mchukue, inawezekana nae ni muhusika" Taita aliongea,

"Nitaenda peke yangu au nitaambatana na wenzangu?" Kijana aliuliza,

"Utaenda mwenyewe tu, chukua gari nenda" Taita aliongea na kisha kijana akapewa maelekezo mengine machache na Tekso, alafu akaondoka zake.

Kijana aliondoka huku akiwa anawasiliana na Tekso muda wote ili aweze kufika sehemu Salama.

Kijana alifanikiwa kufika hilo eneo alilopo Sarah, alifika mpaka nje ya Guest, akasimamisha gari na kuanza kupiga hesabu za kuingia ndani kama atakutana na pingamizi lolote,

Mwisho akaamua kutumia ubabe endapo kutakuwa na kikwazo chochote, kijana akashuka kwenye gari na kuingia moja kwa moja ndani ya Guest, ambapo alimkuta dada wa mapokezi akisinzia sinzia kaunta,

"Karibu kaka, unahitaji chumba?" Dada wa mapokezi alimuuliza,

"Hapana, kuna dada mmoja nimemfuata, nataka kumuona" Kijana alijibu na kumfanya dada wa mapokezi akumbuke kuwa Sarah ndiye aliyesema kuna mgeni wake atakuja kumuulizia,

"Aah yupo, nenda chumba namba nne" Dada wa mapokezi alijibu na kisha yule kijana akaenda mpaka chumba namba nne, akagonga hodi na baada ya muda mchache mlango ulifunguliwa, ulifunguliwa na Sarah mwenyewe, Sarah akapata mshtuko baada ya kukutana na sura ngeni mlangoni,

"Karibu" Sarah aliongea huku akiwa amesimama mlangoni,

"Naweza kupita ndani?" Kijana aliuliza,

"Hapana, kama una shida unaweza kuongea hapo hapo" Sarah alijibu,

"Nina shida, ila nitahitaji tuongee ndani" kijana aliongea,

"Siwezi kumkaribisha chumbani kwangu mtu nisiyemjua" Sarah aliongea huku akiwa amesimama mlangoni,

"Ebu pisha bwana" Kijana aliongea na kumsukuma Sarah na kufanya Sarah apepesuke huku akirudi nyuma, kijana akajitoma ndani kibabe.............

***********ITAENDELEA*************

the Legend☆
 
RIWAYA : SALA YA SARAH.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA KUMI NA NNE.

ILIPOISHIA.

Kijana aliondoka huku akiwa anawasiliana na Tekso muda wote ili aweze kufika sehemu Salama.

Kijana alifanikiwa kufika hilo eneo alilopo Sarah, alifika mpaka nje ya Guest, akasimamisha gari na kuanza kupiga hesabu za kuingia ndani kama atakutana na pingamizi lolote,

Mwisho akaamua kutumia ubabe endapo kutakuwa na kikwazo chochote, kijana akashuka kwenye gari na kuingia moja kwa moja ndani ya Guest, ambapo alimkuta dada wa mapokezi akisinzia sinzia kaunta,

"Karibu kaka, unahitaji chumba?" Dada wa mapokezi alimuuliza,

"Hapana, kuna dada mmoja nimemfuata, nataka kumuona" Kijana alijibu na kumfanya dada wa mapokezi akumbuke kuwa Sarah ndiye aliyesema kuna mgeni wake atakuja kumuulizia,

"Aah yupo, nenda chumba namba nne" Dada wa mapokezi alijibu na kisha yule kijana akaenda mpaka chumba namba nne, akagonga hodi na baada ya muda mchache mlango ulifunguliwa, ulifunguliwa na Sarah mwenyewe, Sarah akapata mshtuko baada ya kukutana na sura ngeni mlangoni,

"Karibu" Sarah aliongea huku akiwa amesimama mlangoni,

"Naweza kupita ndani?" Kijana aliuliza,

"Hapana, kama una shida unaweza kuongea hapo hapo" Sarah alijibu,

"Nina shida, ila nitahitaji tuongee ndani" kijana aliongea,

"Siwezi kumkaribisha chumbani kwangu mtu nisiyemjua" Sarah aliongea huku akiwa amesimama mlangoni,

"Ebu pisha bwana" Kijana aliongea na kumsukuma Sarah na kufanya Sarah apepesuke huku akirudi nyuma, kijana akajitoma ndani kibabe.............

***********ENDELEA**********

"Unataka nini kutoka kwangu?" Sarah aliuliza huku akionekana ana hasira,

"Sihitaji maswali, unachotakiwa kufanya ni kusikiliza amri kutoka kwangu tu" Kijana alijibu huku macho yake yakiangaza ndani ya chumba kile cha guest,

"Ndio useme sasa unachokitaka" Sarah aliongea,

"Unatakiwa uambatane na mimi mpaka sehemu ninayotaka uende. Sitaki swali jingine" Kijana aliongea,

"Sehemu gani hiyo? kwanza wewe ni nani?" Sarah aliuliza,

"Nimekwambia sitaki maswali, fanya ninachotaka" Kijana aliongea huku akimuendea Sarah,

"Sawa, naomba utoke nibadilishe nguo" Sarah aliongea,

"Badili tu, mimi siwezi kutoka, tutatoka wote" Kijana aliongea huku amemkazia macho Sarah,

"Sawa endelea kuniangalia" Sarah aliongea huku akiliendea begi lake la nguo na kulifungua, kisha akaingiza mkono, bila hata kutegemea ule mkono ulitoka na bastola na kumuelekezea yule kijana, kijana akapigwa na butwaa, maana hakutegemea kitu kama hicho,

"Kaa hapo kwenye kiti" Sarah aliongea huku akimuangalia yule kijana, kijana akatii huku akiendelea kushangaa namna mchezo ulivyombadilikia ghafla namna ile, akakiri ni uzembe mkubwa ameufanya kwa kumdharau mwanamke yule.

Sarah akamsogelea yule kijana,

"Toa earphone hizo, tupa hapo chini" Sarah aliongea na yule kijana akatii na kuitupa chini ile earphone, Sarah akaikota na kuiangalia kwa muda, kisha akaikata kata,

"Lete simu" Sarah aliongea na yule kijana akaitoa simu na kuitupa jirani na miguu yake, Sarah akaiendea akainama ili aiokote, Kijana alirusha teke lililoipiga bastola ya Sarah, kisha akarusha ngumi nyingine kumuendea Sarah, kwa ukali wa ile ngumi ilikuwa ngumu sarah kuidaka ingawa alikuwa na uwezo huo, alichofanya Sarah ni kurudi nyuma kisha akaachia teke jepesi kulenga tumbo la yule kijana, kijana akaudaka mguu wa Sarah, na hicho ndicho Sarah alichokikusudia, baada ya mguu wake kudakwa, Sarah aliruka sarakasi na kujibinua kisha ule mguu wake mwingine ukaenda kukipiga kidevu cha yule kijana, kijana akajikuta anayumba huku akirudi nyuma, Sarah akamuendea kwa kasi na kumpiga teke Kali la shingo na yule kijana akajikuta anatua chini kama mzigo huku akipambana na macho yake yaliyokuwa yanaona maluweluwe.

Sarah akarudi nyuma na kuikota bastola yake kisha akakaa kitandani huku akimuangalia yule kijana aliyekuwa ahamini kitu kilichofanywa na huyo binti muda mchache uliopita,

"Taita amekutuma si ndio?" Sarah aliuliza huku akiwa amemkazia macho,

"Hapana" Kijana alijibu huku macho yake yakipingana na jibu lake,

"Nimesikia kila mlichoongea na kila ulichoagizwa, napenda sana mtu mkweli. Ulitumwa unichukue?" Sarah aliuliza tena,

"Ndio" Kijana alijibu,

"Twende unipeleke" Sarah aliongea huku akimtazama yule kijana aliyekuwa anashangaa kujiamini kwa binti huyo,

"Nyanyuka wewe, hakuna muda wa kushangaana, ongoza mbele na usithubutu kugeuza shingo nyuma" Sarah aliongea kwa sauti kali na kumfanya Kijana asimame na kuanza kuelekea nje huku akifuatwa na Sarah.

Walipofika jirani na kaunta, Sarah akaificha bastola,

"Unatoka Bibie?" Dada wa mapokezi alimuuliza Sarah,

"Yap, nitarudi muda si mrefu" Sarah alijibu bila kugeuka na huku akisonga mbele. Walielekea moja kwa moja mpaka nje pembeni ya gari,

"Panda gari, wewe ndio dereva" Sarah aliongea na kijana akaingia upande wa dereva kisha Sarah akaingia siti za nyuma, kijana akawasha gari na kuiondoa kwa mwendo wa taratibu kulingana na maelezo ya Sarah.

Gari ilitembea kwa dakika kadhaa mpaka ilipoanza kuingia mitaa ya osterbay,

"Simamisha gari" Sarah aliongea na kijana akatii, kisha Sarah akaendelea,

"Kwa umri ulionao unaona kipi bora kati ya uhai na kifo" Sarah aliuliza,

"Uhai" kijana alijibu,

"Kuanzia sasa una machaguo mawili, chaguo la kwanza ni kufikisha ujumbe nitaokupa ili uendelee kuishi, na chaguo la pili ni kutofukisha ujumbe nitaokupa alafu ufe" Sarah aliongea kisha akameza mate,

"Nitafikisha ujumbe" Kijana aliongea kwa uoga,

"Kamwambie Taita kuwa yeye ni mpumbavu, huo ndio ujumbe unaotakiwa kuufikisha" Sarah aliongea na kukaa kimya,

"Sawa nitamwambia" Kijana aliongea,

"Hiyo ni juu yako wewe, ila matokeo yake nimeshakwambia. Ukifika nitakupa dakika tano za kumwambia, ukishindwa kumwambia ndio kifo chako kitatimia" Sarah aliongea kisha akampiga ngumi kali ya shingo yule kijana, kijana akapoteza fahamu na hakujua kitu chochote kilichoendelea.

Kijana alifungua macho na kujikuta amekaa siti ya nyuma ya gari, na alipoangalia siti ya dereva hakuona mtu, ndipo alipokurupuka na kuchungulia nje na kujikuta yupo kama nyumba ya tatu kutoka kwa Taita, Kijana akatelemka katika gari na kwenda moja kwa moja mpaka kwenye geti la Taita, akaingia na kupitiliza moja mwa moja mpaka sebuleni na kumkuta Taita na vijana wengine wakiwa kama na kikao, walipomuona mwenzao walishtuka,

"Yaani tulikuwa tunaangalia namna ya kukupata, maana ulipotea ghafla mtandaoni" Tekso aliongea huku akimuangalia yule kijana,

"Aisee yule Dada sio wa kawaida" Kijana aliongea,

"Kwanini unasema hivyo?" Taita aliuliza,

"Amejipanga kupambana" Kijana alijibu huku akikikumbuka kichapo alichopigwa,

"Yupo wapi sasa?" Taita aliuliza,

"Sijui, tulikuja nae ila alinipiga na nikapoteza fahamu, niliposhtuka nikajikuta nipo peke yangu" Kijana alitoa maelezo,

"Kuna ujumbe wowote amekupa?" Taita aliuliza,

"Hapana, hapana hajanipa" Kijana alijibu, sio kwamba hakuwa na kumbukumbu kwa alichoagizwa na Sarah, ila alimuheshimu sana bosi wake kwa hiyo aliona ni dharau sana kumuita bosi wake mpumbavu na ndio maana hakutaka kumwambia.

"Lakini umejua anapokaa?" Tekso akamuuliza yule kijana,

"Ndio, anaishi guest" Kijana alijibu,

"Guest? Tukienda tutamkuta kweli?" Taita aliuliza,

"Twendeni haraka, tukimkosa tunaweza kupata mwanga wowote wa kumjua" Tekso aliongea,

"Gari ipo wapi?" Taita alimuuliza yule kijana,

"Gari ipo, ipo nyumba ya tatu kutoka hapa" Kijana alijibu

"Nyumba ya tatu kutoka hapa? Kwanini umeiegesha uko?" Taita aliuliza,

"Sio mimi, ni huyo Dada, alinipiga nikazimia ndio nikajikuta ameegesha gari hapo" Kijana alijibu,

"Kaisogeze hapa basi hiyo gari" Taita aliongea na kisha kijana akatoka kwenda kuifuata hiyo gari, alipoifikia alifungua mlango na kuingia ndani ya gari, alilikagua hilo gari kama limetegwa bomu ila hakukuta kitu, akajiridhisha kupo Salama, akawasha gari na kuisogeza mpaka nje ya geti la Taita. Akafungua mlango ili ashuke, ila akaiona simu yake iliyokuwa kwenye siti ya pembeni ikiita, akaichukua na kuangalia jina la mpigaji ila hakukuta jina isipokuwa namba tu, akabofya kitufe cha kupokelea,

"Halow" Kijana aliongea,

"Ulichagua kufikisha ujumbe niliokupa, ila umeshindwa kufikisha" Ilikuwa ni sauti ya Sarah iliyofanya kijana ajiulize kuwa huyo binti amejuaje kuwa ujumbe haujafika,

"Wewe Malaya usiniendeshe, huo ujumbe ungeupeleka mwenyewe" Kijana alijibu kibabe,.

"Umefeli, angalia chini ya kiti ulichokalia" Sarah aliongea kisha akakata simu, yule kijana akainuka na kufunua kiti, papo hapo ukatokea mlipuko mkubwa wa bomu, yaani ile gari ililipuka na yule kijana akiwa ndani ya gari, huo ndio ukawa mwisho wa yule kijana.

Kule mlipuko wa bomu uliwastua mpaka Taita na vijana wake, wakatoka sebuleni ili kuelekea getini, wakakuta geti na ukuta wake vyote vipo chini na gari aliyokuwemo yule kijana ilikuwa ikiwaka moto.

Taita akaonekana dhahiri amechanganyikiwa kutokana na lile tukio,

"Mlinzi wa geti yupo wapi?" Taita aliuliza ila hakuna mtu aliyemjibu kwa maana kutokana na watu kutojua ni wapi mlinzi alipo kwa muda huo.

Na kipindi hicho watu wengine walikuwa wakianza kujisogeza eneo la tukio, na polisi pia walifika kwa ajili ya kuja kuangalia tukio hilo.

Baada ya muda, vijana wa Taita wakaanza kutoa matofali yaliyokuwa yamezagaa hapo, ni matofali ya ukuta wa geti ulioangushwa na Bomu.

Baada ya kumaliza walinyanyua geti, chini ya geti ndipo walipomkuta mlinzi akiwa amelaliwa na geti na hakuwa na fahamu,

"Bosi mlinzi huyu hapa" kijana mmoja alimwambia Taita, Taita akasogea na kumkuta mlinzi akiwa amelala na mwili umejaa damu, bahati nzuri na gari ya hospitali ilikuwa hapo, ikambeba mlinzi na kuondoka nae.

Polisi wakachukua maelezo kidogo kwa Taita kisha nao wakaondoka zao.

Baada ya muda kidogo watu wakiwa wameshasambaa na muda huo vijana wa Taita wakiwa bize na shughuli za hapo, ndipo simu ya Taita ikaanza kuita, alipoangalia kioo cha simu akakutana na namba ngeni,

"Hallow" Taita aliongea baada ya kupokea,

"Pole kwa tukio, ila huo ni mwanzo tu, watakufa watu wengi kwa ajili yako ila mwisho ni kwamba mimi naitaka roho yako" ilikuwa ni sauti ya Sarah, iliongea maneno machache ila yalikuwa makali,

"We ni nani?" Taita aliuliza,

"Unanijua vizuri tu" Sarah alijibu na kuzidi kumchanganya Taita,

"Ningekuwa nakujua nisingekuuliza" Taita aliongea,

"Kwa hiyo unataka kuniona kwa Mara nyingine tena?" Sarah aliuliza,

"Ndio" Taita alijibu kwa shahuku,

"Geuka, nipo nyuma yako" Sarah aliongea na Taita akageuka, ndipo alipomuona msichana akiwa amesimama huku akitabasamu na sikioni alikuwa na simu aliyoishika kwa kiganja chake, alikuwa ni Sarah,

"Nahisi umeniona sasa" Sarah aliongea huku akitabasamu na kufanya Taita atoe macho.......................

*********ITAENDELEA********

the Legend☆
 
RIWAYA : SALA YA SARAH.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA KUMI NA NNE.

ILIPOISHIA.

Kijana aliondoka huku akiwa anawasiliana na Tekso muda wote ili aweze kufika sehemu Salama.

Kijana alifanikiwa kufika hilo eneo alilopo Sarah, alifika mpaka nje ya Guest, akasimamisha gari na kuanza kupiga hesabu za kuingia ndani kama atakutana na pingamizi lolote,

Mwisho akaamua kutumia ubabe endapo kutakuwa na kikwazo chochote, kijana akashuka kwenye gari na kuingia moja kwa moja ndani ya Guest, ambapo alimkuta dada wa mapokezi akisinzia sinzia kaunta,

"Karibu kaka, unahitaji chumba?" Dada wa mapokezi alimuuliza,

"Hapana, kuna dada mmoja nimemfuata, nataka kumuona" Kijana alijibu na kumfanya dada wa mapokezi akumbuke kuwa Sarah ndiye aliyesema kuna mgeni wake atakuja kumuulizia,

"Aah yupo, nenda chumba namba nne" Dada wa mapokezi alijibu na kisha yule kijana akaenda mpaka chumba namba nne, akagonga hodi na baada ya muda mchache mlango ulifunguliwa, ulifunguliwa na Sarah mwenyewe, Sarah akapata mshtuko baada ya kukutana na sura ngeni mlangoni,

"Karibu" Sarah aliongea huku akiwa amesimama mlangoni,

"Naweza kupita ndani?" Kijana aliuliza,

"Hapana, kama una shida unaweza kuongea hapo hapo" Sarah alijibu,

"Nina shida, ila nitahitaji tuongee ndani" kijana aliongea,

"Siwezi kumkaribisha chumbani kwangu mtu nisiyemjua" Sarah aliongea huku akiwa amesimama mlangoni,

"Ebu pisha bwana" Kijana aliongea na kumsukuma Sarah na kufanya Sarah apepesuke huku akirudi nyuma, kijana akajitoma ndani kibabe.............

***********ENDELEA**********

"Unataka nini kutoka kwangu?" Sarah aliuliza huku akionekana ana hasira,

"Sihitaji maswali, unachotakiwa kufanya ni kusikiliza amri kutoka kwangu tu" Kijana alijibu huku macho yake yakiangaza ndani ya chumba kile cha guest,

"Ndio useme sasa unachokitaka" Sarah aliongea,

"Unatakiwa uambatane na mimi mpaka sehemu ninayotaka uende. Sitaki swali jingine" Kijana aliongea,

"Sehemu gani hiyo? kwanza wewe ni nani?" Sarah aliuliza,

"Nimekwambia sitaki maswali, fanya ninachotaka" Kijana aliongea huku akimuendea Sarah,

"Sawa, naomba utoke nibadilishe nguo" Sarah aliongea,

"Badili tu, mimi siwezi kutoka, tutatoka wote" Kijana aliongea huku amemkazia macho Sarah,

"Sawa endelea kuniangalia" Sarah aliongea huku akiliendea begi lake la nguo na kulifungua, kisha akaingiza mkono, bila hata kutegemea ule mkono ulitoka na bastola na kumuelekezea yule kijana, kijana akapigwa na butwaa, maana hakutegemea kitu kama hicho,

"Kaa hapo kwenye kiti" Sarah aliongea huku akimuangalia yule kijana, kijana akatii huku akiendelea kushangaa namna mchezo ulivyombadilikia ghafla namna ile, akakiri ni uzembe mkubwa ameufanya kwa kumdharau mwanamke yule.

Sarah akamsogelea yule kijana,

"Toa earphone hizo, tupa hapo chini" Sarah aliongea na yule kijana akatii na kuitupa chini ile earphone, Sarah akaikota na kuiangalia kwa muda, kisha akaikata kata,

"Lete simu" Sarah aliongea na yule kijana akaitoa simu na kuitupa jirani na miguu yake, Sarah akaiendea akainama ili aiokote, Kijana alirusha teke lililoipiga bastola ya Sarah, kisha akarusha ngumi nyingine kumuendea Sarah, kwa ukali wa ile ngumi ilikuwa ngumu sarah kuidaka ingawa alikuwa na uwezo huo, alichofanya Sarah ni kurudi nyuma kisha akaachia teke jepesi kulenga tumbo la yule kijana, kijana akaudaka mguu wa Sarah, na hicho ndicho Sarah alichokikusudia, baada ya mguu wake kudakwa, Sarah aliruka sarakasi na kujibinua kisha ule mguu wake mwingine ukaenda kukipiga kidevu cha yule kijana, kijana akajikuta anayumba huku akirudi nyuma, Sarah akamuendea kwa kasi na kumpiga teke Kali la shingo na yule kijana akajikuta anatua chini kama mzigo huku akipambana na macho yake yaliyokuwa yanaona maluweluwe.

Sarah akarudi nyuma na kuikota bastola yake kisha akakaa kitandani huku akimuangalia yule kijana aliyekuwa ahamini kitu kilichofanywa na huyo binti muda mchache uliopita,

"Taita amekutuma si ndio?" Sarah aliuliza huku akiwa amemkazia macho,

"Hapana" Kijana alijibu huku macho yake yakipingana na jibu lake,

"Nimesikia kila mlichoongea na kila ulichoagizwa, napenda sana mtu mkweli. Ulitumwa unichukue?" Sarah aliuliza tena,

"Ndio" Kijana alijibu,

"Twende unipeleke" Sarah aliongea huku akimtazama yule kijana aliyekuwa anashangaa kujiamini kwa binti huyo,

"Nyanyuka wewe, hakuna muda wa kushangaana, ongoza mbele na usithubutu kugeuza shingo nyuma" Sarah aliongea kwa sauti kali na kumfanya Kijana asimame na kuanza kuelekea nje huku akifuatwa na Sarah.

Walipofika jirani na kaunta, Sarah akaificha bastola,

"Unatoka Bibie?" Dada wa mapokezi alimuuliza Sarah,

"Yap, nitarudi muda si mrefu" Sarah alijibu bila kugeuka na huku akisonga mbele. Walielekea moja kwa moja mpaka nje pembeni ya gari,

"Panda gari, wewe ndio dereva" Sarah aliongea na kijana akaingia upande wa dereva kisha Sarah akaingia siti za nyuma, kijana akawasha gari na kuiondoa kwa mwendo wa taratibu kulingana na maelezo ya Sarah.

Gari ilitembea kwa dakika kadhaa mpaka ilipoanza kuingia mitaa ya osterbay,

"Simamisha gari" Sarah aliongea na kijana akatii, kisha Sarah akaendelea,

"Kwa umri ulionao unaona kipi bora kati ya uhai na kifo" Sarah aliuliza,

"Uhai" kijana alijibu,

"Kuanzia sasa una machaguo mawili, chaguo la kwanza ni kufikisha ujumbe nitaokupa ili uendelee kuishi, na chaguo la pili ni kutofukisha ujumbe nitaokupa alafu ufe" Sarah aliongea kisha akameza mate,

"Nitafikisha ujumbe" Kijana aliongea kwa uoga,

"Kamwambie Taita kuwa yeye ni mpumbavu, huo ndio ujumbe unaotakiwa kuufikisha" Sarah aliongea na kukaa kimya,

"Sawa nitamwambia" Kijana aliongea,

"Hiyo ni juu yako wewe, ila matokeo yake nimeshakwambia. Ukifika nitakupa dakika tano za kumwambia, ukishindwa kumwambia ndio kifo chako kitatimia" Sarah aliongea kisha akampiga ngumi kali ya shingo yule kijana, kijana akapoteza fahamu na hakujua kitu chochote kilichoendelea.

Kijana alifungua macho na kujikuta amekaa siti ya nyuma ya gari, na alipoangalia siti ya dereva hakuona mtu, ndipo alipokurupuka na kuchungulia nje na kujikuta yupo kama nyumba ya tatu kutoka kwa Taita, Kijana akatelemka katika gari na kwenda moja kwa moja mpaka kwenye geti la Taita, akaingia na kupitiliza moja mwa moja mpaka sebuleni na kumkuta Taita na vijana wengine wakiwa kama na kikao, walipomuona mwenzao walishtuka,

"Yaani tulikuwa tunaangalia namna ya kukupata, maana ulipotea ghafla mtandaoni" Tekso aliongea huku akimuangalia yule kijana,

"Aisee yule Dada sio wa kawaida" Kijana aliongea,

"Kwanini unasema hivyo?" Taita aliuliza,

"Amejipanga kupambana" Kijana alijibu huku akikikumbuka kichapo alichopigwa,

"Yupo wapi sasa?" Taita aliuliza,

"Sijui, tulikuja nae ila alinipiga na nikapoteza fahamu, niliposhtuka nikajikuta nipo peke yangu" Kijana alitoa maelezo,

"Kuna ujumbe wowote amekupa?" Taita aliuliza,

"Hapana, hapana hajanipa" Kijana alijibu, sio kwamba hakuwa na kumbukumbu kwa alichoagizwa na Sarah, ila alimuheshimu sana bosi wake kwa hiyo aliona ni dharau sana kumuita bosi wake mpumbavu na ndio maana hakutaka kumwambia.

"Lakini umejua anapokaa?" Tekso akamuuliza yule kijana,

"Ndio, anaishi guest" Kijana alijibu,

"Guest? Tukienda tutamkuta kweli?" Taita aliuliza,

"Twendeni haraka, tukimkosa tunaweza kupata mwanga wowote wa kumjua" Tekso aliongea,

"Gari ipo wapi?" Taita alimuuliza yule kijana,

"Gari ipo, ipo nyumba ya tatu kutoka hapa" Kijana alijibu

"Nyumba ya tatu kutoka hapa? Kwanini umeiegesha uko?" Taita aliuliza,

"Sio mimi, ni huyo Dada, alinipiga nikazimia ndio nikajikuta ameegesha gari hapo" Kijana alijibu,

"Kaisogeze hapa basi hiyo gari" Taita aliongea na kisha kijana akatoka kwenda kuifuata hiyo gari, alipoifikia alifungua mlango na kuingia ndani ya gari, alilikagua hilo gari kama limetegwa bomu ila hakukuta kitu, akajiridhisha kupo Salama, akawasha gari na kuisogeza mpaka nje ya geti la Taita. Akafungua mlango ili ashuke, ila akaiona simu yake iliyokuwa kwenye siti ya pembeni ikiita, akaichukua na kuangalia jina la mpigaji ila hakukuta jina isipokuwa namba tu, akabofya kitufe cha kupokelea,

"Halow" Kijana aliongea,

"Ulichagua kufikisha ujumbe niliokupa, ila umeshindwa kufikisha" Ilikuwa ni sauti ya Sarah iliyofanya kijana ajiulize kuwa huyo binti amejuaje kuwa ujumbe haujafika,

"Wewe Malaya usiniendeshe, huo ujumbe ungeupeleka mwenyewe" Kijana alijibu kibabe,.

"Umefeli, angalia chini ya kiti ulichokalia" Sarah aliongea kisha akakata simu, yule kijana akainuka na kufunua kiti, papo hapo ukatokea mlipuko mkubwa wa bomu, yaani ile gari ililipuka na yule kijana akiwa ndani ya gari, huo ndio ukawa mwisho wa yule kijana.

Kule mlipuko wa bomu uliwastua mpaka Taita na vijana wake, wakatoka sebuleni ili kuelekea getini, wakakuta geti na ukuta wake vyote vipo chini na gari aliyokuwemo yule kijana ilikuwa ikiwaka moto.

Taita akaonekana dhahiri amechanganyikiwa kutokana na lile tukio,

"Mlinzi wa geti yupo wapi?" Taita aliuliza ila hakuna mtu aliyemjibu kwa maana kutokana na watu kutojua ni wapi mlinzi alipo kwa muda huo.

Na kipindi hicho watu wengine walikuwa wakianza kujisogeza eneo la tukio, na polisi pia walifika kwa ajili ya kuja kuangalia tukio hilo.

Baada ya muda, vijana wa Taita wakaanza kutoa matofali yaliyokuwa yamezagaa hapo, ni matofali ya ukuta wa geti ulioangushwa na Bomu.

Baada ya kumaliza walinyanyua geti, chini ya geti ndipo walipomkuta mlinzi akiwa amelaliwa na geti na hakuwa na fahamu,

"Bosi mlinzi huyu hapa" kijana mmoja alimwambia Taita, Taita akasogea na kumkuta mlinzi akiwa amelala na mwili umejaa damu, bahati nzuri na gari ya hospitali ilikuwa hapo, ikambeba mlinzi na kuondoka nae.

Polisi wakachukua maelezo kidogo kwa Taita kisha nao wakaondoka zao.

Baada ya muda kidogo watu wakiwa wameshasambaa na muda huo vijana wa Taita wakiwa bize na shughuli za hapo, ndipo simu ya Taita ikaanza kuita, alipoangalia kioo cha simu akakutana na namba ngeni,

"Hallow" Taita aliongea baada ya kupokea,

"Pole kwa tukio, ila huo ni mwanzo tu, watakufa watu wengi kwa ajili yako ila mwisho ni kwamba mimi naitaka roho yako" ilikuwa ni sauti ya Sarah, iliongea maneno machache ila yalikuwa makali,

"We ni nani?" Taita aliuliza,

"Unanijua vizuri tu" Sarah alijibu na kuzidi kumchanganya Taita,

"Ningekuwa nakujua nisingekuuliza" Taita aliongea,

"Kwa hiyo unataka kuniona kwa Mara nyingine tena?" Sarah aliuliza,

"Ndio" Taita alijibu kwa shahuku,

"Geuka, nipo nyuma yako" Sarah aliongea na Taita akageuka, ndipo alipomuona msichana akiwa amesimama huku akitabasamu na sikioni alikuwa na simu aliyoishika kwa kiganja chake, alikuwa ni Sarah,

"Nahisi umeniona sasa" Sarah aliongea huku akitabasamu na kufanya Taita atoe macho.......................

*********ITAENDELEA********

the Legend☆
Mambo yanaanza kunoga
 
RIWAYA : SALA YA SARAH

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA KUMI NA TANO.

ILIPOISHIA.

Baada ya muda kidogo watu wakiwa wameshasambaa na muda huo vijana wa Taita wakiwa bize na shughuli za hapo, ndipo simu ya Taita ikaanza kuita, alipoangalia kioo cha simu akakutana na namba ngeni,

"Hallow" Taita aliongea baada ya kupokea,

"Pole kwa tukio, ila huo ni mwanzo tu, watakufa watu wengi kwa ajili yako ila mwisho ni kwamba mimi naitaka roho yako" ilikuwa ni sauti ya Sarah, iliongea maneno machache ila yalikuwa makali,

"We ni nani?" Taita aliuliza,

"Unanijua vizuri tu" Sarah alijibu na kuzidi kumchanganya Taita,

"Ningekuwa nakujua nisingekuuliza" Taita aliongea,

"Kwa hiyo unataka kuniona kwa Mara nyingine tena?" Sarah aliuliza,

"Ndio" Taita alijibu kwa shahuku,

"Geuka, nipo nyuma yako" Sarah aliongea na Taita akageuka, ndipo alipomuona msichana akiwa amesimama huku akitabasamu na sikioni alikuwa na simu aliyoishika kwa kiganja chake, alikuwa ni Sarah,

"Nahisi umeniona sasa" Sarah aliongea huku akitabasamu na kufanya Taita atoe macho.......................

*********ENDELEA********

Taita alipigwa na butwaa, ila ubaya ni kuwa Sarah alikuwa amesimama umbali mrefu kutoka yeye aliposimama, tena mbali sana na ilikuwa ngumu sana kuiona hata sura yake.

Taita aliendelea kumuangalia binti yule huku hasira zikimpanda taratibu,

"Nadhani umeniona, kwaheri" Sarah aliongea kisha akakata simu na kuondoka zake kwa kufuata kona iliyopo jirani na aliposimama, alifanya hivyo ili kumpoteza Taita.

Taita kuona binti huyo amepotelea kwenye kona, ndipo akili zikamjia, akamwambia Trigger atoke na gari, Trigger akatii akatoa gari ndani na kisha Taita akaingia ndani ya gari,

"Twende mpaka kwenye kona ilee" Taita aliongea kisha Trigger akaiondoa gari kwa kasi mpaka kwenye hiyo kona na kuisimamisha gari, Taita akatupa macho upande alipoelekea Sarah ili aweze kuona kama atamuona, lakini hakuona mtu kabisa upande huo,

"Twende upande huo" Taita aliongea na kisha Trigger akakunja kona kuelekea ule upande alioambiwa na Taita. Gari ilitembea kwa mwendo wa wastani kwa muda Mrefu mpaka walipotokezea sehemu iliyokuwa na pilika pilika za watu wengi, Taita akamuamuru Trigger asimamishe gari, Trigger akatii.

Taita akatelemka na kuanza kuangaza angaza kila upande ili aone kama ataabatika kumuona binti anayemtaka, lakini hakupata bahati hiyo, Taita akapiga paji lake la uso kwa hasira kisha akarudi ndani ya gari,

"Geuza gari turudi nyumbani" Taita aliongea na kisha Trigger akafuata amri ya bosi wake na kuigeuza gari na kuishika njia aliyokuja nayo.

"Kwani vipi?" Trigger alimuuliza Taita baada ya kuona kama hamuelewi vile,

"Yule binti niliyewaambieni anatufuatilia, ndio amehusika na ule mlipuko pale nyumbani" Taita aliongea huku akikuna uwaraza wake,

"Nani amekuambia?" Trigger aliuliza,

"Ndio amenipigia simu muda mfupi uliopita na kujinasibu kuwa amefanya hivyo, na cha ajabu nilimuona kwa macho yangu" Taita aliongea,

"Ungempiga risasi" Trigger aliongea kwa hamaki,

"Alikuwa mbali, ndio maana nikakwambia utoke na gari na hapa nilikuwa namfuatilia, ila bahati mbaya sijampata, sasa sijui nae alikuwa na usafiri?" Taita aliuliza bila kuwa na jibu,

"Hivi huyu mtu ni nani na kwanini afanye hivi? ni lazima tuwe makini nae, maana kwa hili shambulio inaonesha yupo upande wa hatari zaidi" Trigger aliongea,

"Inahitajika tufanye mkutano wa haraka ili tujipange, huyu mtu inaelekea anatujua vizuri" Taita aliongea wakati gari ikisimama nje ya nyumba yake,

"Tena leo hii hii, maana tukingoja mpaka kesho inaweza kuwa matatizo zaidi" Trigger aliongea,

"Leo hii, wewe wasiliana na watu muhimu wa kundi, waambie tukutane Vin hotel, saa moja jioni" Taita aliongea kisha akatelemka katika gari na kumuacha Trigger akibonyeza bonyeza vitufe vya siku yake, nadhani ndio alikuwa anajiandaa kutoa taarifa za kikao kwa wenzake.

********************

Sarah alipotoka mtaa anaohishi Taita, alirudi moja kwa moja katika guest aliyofikia, alichokiwaza muda huo ni kuwa ni lazima vijana wa Taita wataenda eneo hilo kwa kuwa walishajua ni wapi alipo kutokana na mawasiliano waliyokuwa wanayafanya na yule kijana wa kwanza.

Sarah aliwaza kuhama muda huo, na alipanga aende guest nyingine tofauti na hiyo ila iwe mafichoni kama hiyo.

Sarah akarudishia nguo zake kwenye begi kisha akakusanya kila kitu chake na akaanza kutoka nje ya chumba chake, alitoka mpaka mapokezi na kumkuta Dada wa mapokezi akisinzia,

"Dada mimi naondoka" Sarah aliongea na kumshtua yule Dada toka usingizini,

"Mbona ghafla hivyo, au tayari umepata nyumba?" Dada wa mapokezi aliuliza,

"Hapana, nahamia kwa rafiki yangu, si unajua kukaa guest kila siku ni gharama sana" Sarah alidanganya huku akitabasamu,

.

"Kweli lakini. Sawa dada, karibu tena" Dada wa mapokezi alijibu kwa huzuni,

"Hauendi kukagua hata chumba kama kipo Salama?" Sarah alimuuliza yule dada,

"Nakuhamini bwana" Dada wa mapokezi alijibu huku akitabasamu,

"Nenda kakague, ndio unaniamini ila fuata utaratibu wa kazi" Sarah alimsihi yule dada, dada wa mapokezi akaona bora aende,

"Haya ngoja nikakague, ila naamini pako Salama tu" Dada wa mapokezi aliongea huku akielekea chumbani, Sarah akatumia mwanya huo kuingiza mkono chini ya meza ya kaunta na kutoa daftari la wageni, kisha akatafuta karatasi iliyokuwa na jina lake na kuling'oa lile karatasi, kisha akarudisha daftari.

Baada ya dakika Dada wa mapokezi akarejea huku akitabasamu,

"Ndani kupo Salama, mimi nakuamini" Dada wa mapokezi aliongea huku akitabasamu,

"Sidaiwi kwa maana uwa nalipa kila asubuhi" Sarah aliongea,

"Huna deni, hilo nalijua" Dada wa mapokezi aliongea kichangamfu,

"Shika hii utakunywa soda, kwaheri" Sarah aliongea huku akimpatia noti ya elfu kumi yule dada wa kaunta,

"Asante shoga" Dada wa mapokezi aliongea huku akipokea ile hela huku akifurahi, maana ilikuwa bahati kubwa sana kupewa pesa kubwa kama ile.

Sarah alitoka mpaka nje huku akibuluta begi lake la matairi, alipofika mbele ya guest kama bahati vile alikutana na dalali yule aliyemuagiza amtafutie chumba, dalali alikuwa ndani ya gari ndogo ambayo umbo la gari hiyo na bei nahisi vililingana,

"Dada ndio nimekufuata, tena nimekuwahi maana naona unaondoka" Dalali aliongea huku akitabasamu,

"Nilikuwa naondoka ila nilitaka nianzie kijiweni kwako kukuangalia ulipofikia. Vipi umefanikisha?" Sarah alimuuliza dalali,

"Ndio, nyumba imepatikana na hapa nilikuja kukuchukua ukapaangalie" Dalali aliongea,

"Haina shida, je naweza kuhamia leo endapo nitapapenda?" Sarah aliuliza,

"Leo?" Dalali aliuliza huku akishangaa,

"Ndio, nataka nihamie leo kama patanipendeza" Sarah alijibu,

"We twende tukapaangalie, kama mtafikiana makubaliano na mwenye nyumba, utahamia tu" Dalali alijibu,

"Niingie kwenye gari au?" Sarah alimuuliza dereva,

" ingia twende" Dalali alijibu.

"Naruhusiwa kukaa mbele?" Sarah aliuliza,

"Ni wewe tu uamuzi wako" Dalali alijibu,

"Nadhani nyuma ni pazuri" Sarah alijibu.

**************************

Ingawa Taita na vijana wake walikubaliana kuwa saa moja ndipo kuwe na kikao pale Vin hotel kwa ajili ya kumjadili binti msumbufu aliyewafanyia shambulio, lakini kuna mkali anaitwa Tekso, yeye aliamini kuwa tayari anapokaa Sarah kumejulikana, basi ni lazima vijana waende muda huo kuangalia uwezekano wa kumpata Sarah.

Tekso alitoa mpaka ramani kutokana tu na mawalisiliano ya hawali baina ya Tekso na kijana aliyetumwa akamchukue Sarah hawali, pia vile vinasa sauti alivyovitega Sarah kwenye nyumba ya Taita na baadae Tekso alipokuja kuvichakachukua ndipo alipoweza kugundua huyo mtu aliyevitega hivyo vinasa sauti anapatikana Wapi.

Tekso baada ya muswada wake kupitishwa na Taita, Tekso aliwachukua vijana takribani sita na kuingia nao ndani ya gari aina ya land cruiser, wakaondoka kwa kasi ili kujaribu kumuwahi Sarah.

Land cruiser waliyopanda vijana wa Taita iliwasili katika maeneo jirani na guest aliyokuwa akihishi Sarah, walichofanya vijana wa Taita ni kuzuia ile Barabara yote ambayo ilikuwa inaingiza na kutoa magari yaendayo kule mtaa wenye guest, uzuri ni kwamba barabara yenyewe ilikuwa moja tu, kama ni kamari basi walikuwa wametupa kete ya ushindi.

kisha Tekso alitelemka na kuanza kutembea kwa mguu kuelekea kwenye hiyo guest, aliamua kufanya hivyo mara baada ya simu yake kuonesha kuwa yupo jirani tu na hiyo guest. Tekso aliambatana na vijana wengine wawili.

Vijana wengine walibaki na gari, tena gari yenyewe walikuwa wameisimamisha katikati ya barabara kwa ajili ya kuweza kusimamisha gari zote ili wazikague kama huyo binti wanaemtafuta atakuwepo, ingawa hawakumjua ila walipewa wajihi wake kwa nje, waliambiwa ni mwembamba na ana kimo cha wastani, kwa hiyo walichokuwa wanafikiri wale vijana ni kukamata wasichana wote wembamba wenye kima cha wastani wataowahisi kwa namna moja au nyingine.

Baada ya dakika moja tu ya kukaa barabarani kwa vijana wa Taita na gari yao, walishuhudia gari ndogo ikitokea upande ule wa guest na kuelekea upande walipo wao, vijana hawakuwa na pupa, waliisubiri ile gari ilivyokuja mpaka ilipowakaribia, ile gari ndogo ikasimama kutokana na kutokuwa na nafasi ya kupita, vijana wa Taita wakashuka na kwenda kugonga kwenye kioo cha dereva wa ile gari ndogo kwa maana ile gari ilikuwa na vioo vya Giza.

Dereva wa gari ndogo akashusha kioo, alikuwa ni yule dalali wa Sarah, vijana wa Taita wakamsalimia,

"Unaweza kutufungulia milango kuna mtu tunamtafuta" Kijana wa Taita aliongea huku akimuangalia Dalali,

"Hakuna mtu zaidi yangu ndani ya gari" Dalali alijibu baada ya kufikiria kwa muda, vijana wa Taita wakamtilia shaka,

"Basi fungua milango" kijana mmoja akaongea kwa hasira,

"Hakuna mtu, si nimeshawaambia" Dalali aliongea,

"Mbona mnambeleleza sana" kijana mwingine aliongea huku akimuwekea bastola usawa wa kichwa yule dereva,

"Haya fungua milango" Kijana aliongea huku akiwa hana mzaha hata kidogo, dalali akalegeza kamba, aka unlock milango yote, kisha kwa pupa vijana wa Taita wakakimbilia kufungua milango ya nyuma ya ile gari ya dalali.........

**********ITAENDELEA**************

the Legend☆
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom