Riwaya: Sala ya Sarah

Riwaya: Sala ya Sarah

Mi naona Sarah kashakufa.......ila nikikumbuka amepiga somo kwa jeshi la bwana Trump naona bado Kuna nafasi ya kuendelea kuishi .......nahofia tuu asije ishiwa hela manake ataanza kudanga hapa bongo

Sent using Jamii Forums mobile app
Sifikirii hawezi kufa kirahisi hivyo. Ni kudanga sio rahisi.mtu ameweza kununua nyumba chap chap baadae aishie kudanga. Revenge inaendelea. Akiungana na mdogo nguvu zitaongezeka
 
Sifikirii hawezi kufa kirahisi hivyo. Ni kudanga sio rahisi.mtu ameweza kununua nyumba chap chap baadae aishie kudanga. Revenge inaendelea. Akiungana na mdogo nguvu zitaongezeka
Ni kweli mkuu. tatizo mdogo ake ndo hivyo kashafutwa kumbukumbu, na wanaeza wakamjaza upepo. kumshawishi akubali taita sio baba ake bila shaka haitakua rahisi

the Legend☆
 
Ni kweli mkuu. tatizo mdogo ake ndo hivyo kashafutwa kumbukumbu, na wanaeza wakamjaza upepo. kumshawishi akubali taita sio baba ake bila shaka haitakua rahisi

the Legend☆
Maneno atakayopewa na sister wake yatamuingia tu.subiri uone ( kwa kuwa wewe ndio mleta story maybe unajua mwisho wake
 
Oya mwamba mbona hudondoshi vitu au mpaka raia tuanze kulitajataja jina lako ndio uanze tupia kipande moja moja....

Sent using Jamii Forums mobile app
Nlikua na maana yangu kusema tangu mwanzo ratiba ya kuweka episodes za hii 'sala ya Sarah' kua ni muda wowote kuanzia saa 10 jioni, especially siku za katikati ya wiki. Kuna majukumu mengine mkuu

the Legend☆
 
Uwe muelewa mkuu ameshasema anapoitoa bado haijapostiwa yeye sio mtunzi
Nlikua na maana yangu kusema tangu mwanzo ratiba ya kuweka episodes za hii 'sala ya Sarah' kua ni muda wowote kuanzia saa 10 jioni, especially siku za katikati ya wiki. Kuna majukumu mengine mkuu

the Legend☆
Basi nimeelewa.. manake Kuna wale jamaaa wanaanzishaga story alaf ghafla wanapotea unaskia anatuita WhatsApp group huwa wananikataga handas kinyama japokuwa Ni biashara

Sent using Jamii Forums mobile app
 
RIWAYA : SALA YA SARAH.

MTUNZI : ALEX KILEO

SEHEMU YA KUMI NA TISA.

ILIPOISHIA.

Gari ilivyopotea machoni pa Toisa, Toisa hakutaka kuingia ndani ya geti, alichofanya alijifanya anatembea mpaka akafika upande wa nyuma wa nyumba, akaruka ukuta na kuingia ndani ya uzio, akawa anachungulia kila dirisha la chumba, hakuona mtu, ila alipofika kwenye dirisha la sebuleni, aliweza kumuona Sarah akiwa amelala kwenye sofa huku akitazama runinga, Toisa akaelekea kwenye mlango wa kuingilia na kuminya kitasa kwa taratibu, mlango ukafunguka na Toisa akatokea sebuleni,

"Leo umepatikana kirahisi" Toisa aliongea na kufanya Sarah ashtuke na kugeuka nyuma, hapo ndipo Sarah alipokutana na mdomo wa bastola ukimuangalia............

***********ENDELEA***********

"Sidhani kama upo sahihi kusema hivyo" Sarah aliongea huku akirudisha macho yake kwenye runinga na kumfanya Toisa ajiulize ni kipi kinachompa kiburi huyu binti?

"Mikono juu, au nakufyatua risasi" Toisa aliongea kwa sauti kubwa kidogo ila Sarah wala hakujali, badala yake Sarah alimgeukia Toisa na huku mkononi akiwa na remote,

"Unaona hii? hii ni remote ya Bomu, mtoto wa Harry yupo ndani nimemfunga bomu" Sarah aliongea kwa sauti tulivu ila iliyobeba maana ya kile alichokizungumza, Toisa kusikia hivyo kidogo akapoa, ila hakutaka kushusha bastola chini,

"Mtoto yupo wapi?" Toisa aliuliza,

"Yupo ndani kalala" Sarah alijibu,

"Sasa kalala na bomu? likimlipukia je?" Toisa aliuliza kwa mshangao,

"Haliwezi kulipuka mpaka liruhusiwe" Sarah alijibu huku akitabasamu, tabasamu alilitoa baada ya kuona tayari amemuweza Toisa,

"Kamlete, nimuone" Toisa aliongea,

"Kwanza weka bastola chini alafu uisukume kwangu kwa mguu" Sarah alimwambia Toisa ambaye alitii,

"Haya kamlete mtoto nimuone" Toisa aliongea huku akiwa amemkazia macho Sarah.

Sarah akaikota ile bastola na kuishika yeye, kisha akaangaza macho kushoto na kulia, akakiendea kiti cha mbao kilichopo pembezoni mwa ukuta na kukibeba kisha kumpa Toisa,

"Kaa hapo nikufunge kamba" Sarah aliongea kwa jeuri huku akimtazama,

"Wewe mpumbavu nini, makubaliano ni kumleta mtoto na wala sio kufungana kamba" Toisa aliongea kwa hasira, Sarah akakinyanyua kile kiti na kumpiga nacho Toisa begani, Toisa akataka apambambane,

"Ukithubutu hata kutingishika nakufumua mwili" Sarah aliongea huku akiwa ameishika ile bastola ya Toisa, ila Toisa hakutaka kuitii ile amri ya Sarah, Toisa akarusha teke Kali kumuelekea Sarah, Sarah akainama kisha akanyanyuka kwa kasi na kuushika mguu wa Toisa kabla haujafika chini, alafu akachukua bastola na kupiga risasi goti la Toisa, Toisa akatoa ukelele wa maumivu huku asiamini kile anachofanyiwa,

"Nilikwambia usithubutu kutingishika, ukapuuza" Sarah aliongea huku akimsukuma Toisa na kumuangushia kwenye kiti, na kipindi hicho mtoto wa Harry alikuwa anatoka ndani, nadhani sauti ya bastola ndio ilimshtua.

Mtoto wa Harry alipotoka ndani hakuonekana kuwa na dalili yoyote ya kufungwa bomu, Toisa akajiona mpumbavu kwa kitendo chake cha kuamini pasipo kuona,

"Aunty umemfanya nini Toi?" Mtoto wa Harry aliuliza baada ya kumuona Toisa akitoka damu gotini huku akiugulia maumivu,

"Princess kumbe unamjua huyu?" Sarah alimuuliza mtoto wa harry huku akimshika begani,

" Anko Toi, rafiki ake baba" Princess alijibu, princess ndio jina la mtoto wa Harry,

"Anko Toi ameumia, ameanguka" Sarah aliongea kirafiki na princes,

"Pole anko Toi, nenda hospital" Princess aliongea kwa huruma huku akimshika Toisa,

"Usijali princess, nitampekeka. Unataka juice au chocolate?" Sarah alimuuliza Princess,

"Oooh, chocolate" Princess alijibu kwa furaha,

"Nenda kachukua kwenye droo ya kitanda, usije huku mpaka nikuite ee?" Sarah alimwambia Princess,

"Sawa aunty" Princess alijibu huku akikimbilia chumbani na kuwaacha Toisa na Sarah.

"Sitokuumiza tena endapo utanijibu vizuri maswali nitayokuuliza" Sarah aliongea huku akimuangalia Toisa aliyekuwa ameshikilia goti lake,

"Kwenye kundi lenu mpo wangapi?" Sarah aliuliza huku akimtupia jicho Toisa, ila Toisa hakujibu,

"Unajifanya kiburi sio?" Sarah aliuliza huku akiitoa bastola yake chini ya kochi na ile bastola ya Toisa akaitupa pembeni,

"Nakuuliza kwa mara ya mwisho, mpo wangapi kundini?" Sarah aliuliza huku akifunga kiwambo cha sauti katika mdomo wa bastola ili akifyatua risasi sauti isitoke.

Toisa hakujibu tena swali hilo, Sarah akaelekeza mdomo wa bastola katika goti la pili la Toisa na kumfyatulia risasi nyingine iliyofanya Toisa apige kelele kubwa zaidi ya aliyopiga mwanzo,

"Nauliza kwa mara ya tatu, mpo wangapi?" Sarah aliuliza huku akiielekezea bastola kwenye kiwiko cha mkono wa Toisa,

"Niue tu, yanini unitese hivi" Toisa alijibu kijeuri,

"Kifo na mateso ni kipi bora?" Sarah aliuliza huku akitabasamu,

"Niue Malaya wewe, sitaki maswali" Toisa aliongea kwa ukali na kumtemea mate usoni Sarah,

"Naheshimu chaguzi yako" Sarah aliongea kisha akajifuta mate usoni kwa kiganja cha mkono, kisha akamfyatulia risasi kichwani Toisa, Toisa akafa pale pale.

Sarah akambeba Toisa mpaka katika chumba kimojawapo ndani ya nyumba yake. Chumba kilikuwa kimejaa visu, misumeno na vitu vingi vya kifundi selemala. Sarah akachukua kisu na kukikata kichwa cha Toisa, kisha akaenda kwenye kona moja iliyokuwa na friji, akakiingiza kile kichwa ndani ya friji.

Sarah akaurudia mwili wa Toisa na kuanza kuukata kata vipande vipande, kisha akaviingiza katika mifuko mikubwa mieusi miwili na kuiweka kwenye pembe ya kile chumba, baada ya hapo akarudi sebuleni na kusafisha damu iliyotapakaa pale sakafuni kisha akamuita Princess.

"Anko Toi ameenda hospitali?" Princess aliuliza baada ya kufika sebuleni,

"Ameondoka, unampenda ee?" Sarah alimuuliza huku akimuangalia,

"Ndio, ananipaga soda" Princess alijibu na kumfanya Sarah ahisi uchungu.

"Atakuja baadae, atakuletea soda" Sarah aliongea kisha akambeba Princess na kumpakata.

"Atakuja na baba?" Princess aliuliza,

"Ndio, watakuja wote" Sarah alijibu,

"Alafu aunty, nataka chocolate tena" Princess aliongea,

"Kwa siku unatakiwa kule chocolate tatu tu, ukila nyingi meno yako yataoza, sawa?" Sarah alimuuliza Princess,

"Sawa aunty" Princess alijibu,

"Leo umekula ngapi?" Sarah alimuuliza Princess,

"Tatu" Princess alijibu,

"Kachukue maziwa kwenye friji, chocolate utakula kesho" Sarah alimwambia Princess kisha Princess akaelekea kwenye friji ya pale sebuleni na kutoa pakiti ya maziwa.

***************

Baada ya siku tatu ya Sarah kumteka Princess na siku mbili za kutoonekana kwa Toisa, kambi ya Taita iliingia na hofu juu ya mtu wanaetaka kupambana nae, kwa upande wa Harry alichofanya ni kutoa taharifa katika vyombo vya habari juu ya kupotea kwa binti yake, na akatangaza pesa kubwa kwa mtu yoyote atayefanikisha kupatikana kwa mtoto wake.

Siku hiyo kila gazeti lililotoka lilitoka na tangazo hilo linalohusiana na kupotea kwa mtoto wa Harry, muda huu gazeti lilishikwa na dalali wa Sarah, baada ya kuona picha ya Princess pale kwenye gazeti, dalali alishtuka kwa maana huyo mtoto anamuona kila siku yupo na Sarah kule nyumbani kwa Sarah, ila kilichomtatiza Dalali ni ile pesa iloyowekwa kwa mtu atakayefanikisha kupatikana kwa mtoto huyo, Dalali tamaa ikamuingia. Uzuri ni kwamba katika magazeti yote yaliyotolewa juu ya habari za kupotea Princess, ziliwekwa na namba za Harry.

"Kwani mama yangu yule, tumefahamiana kwa ajili ya kazi tu, acha niongee ninachokijua, pesa yote hiyo kweli niiache?" Dalali aliongea na moyo wake kisha akaachia tabasamu laini kutoka moyoni ila likapenya mpaka mdomoni na kufanya meno yake meupe yaonekane.

Dalali akajinyanyua kutoka kwenye kijiwe cha kahawa na kulifuata gari lake akaingia. Alikuwa anatafuta eneo lenye utulivu ili aweze kusikilizana na baba wa mtoto.

Dalali baada ya kuingia katika gari, alichukua simu yake na kuipiga ile namba ya Harry ila simu ya dalali ikaonesha haina salio la kutosha, akakopa mtandaoni na kupata kifurushi, kisha ukaingia ujumbe wa maneno kutoka kampuni ya simu uliomtahadharisha kukumbuka kulipa deni hilo.

Dalali akaenda kwenye kumbukumbu ya watu aliowapigia na kuikuta ile namba ya Baba wa mtoto, akapiga na simu ikaanza kuita, moyo wa dalali ukafurahi kwa hatua hiyo aliyofikia.

Simu ikapokelewa na Harry mwenyewe,

"Hallow" Harry aliongea kinyonge,

"Hallow, hali yako kaka?" Dalali alimsalimia Harry,

"Salama, naongea na nani?" Harry aliuliza,

"Mimi ni msamalia mwema, nimeona tangazo lako kwenye gazeti" Dalali aliongea,

"Eee, niambie" Harry aliongea huku akiwa na shahuku ya kutaka kujua ni kipi kitazungumzwa,

"Aisee kaka huyo mtoto nimemuona katika nyumba moja hivi anaishi na mdada" Dalali alitoa neno lililomfanya Harry ashushe pumzi, maana hakuamini kusikia kuwa mwanae bado anaishi,

"Maeneo gani?" Harry aliuliza,

"_mimi nitakupeleka, kwanza nataka unipe uhakika wa kupata pesa uliyoitangaza" Dalali aliongea na kunyamaza,

"Pesa ipo, pesa kwangu si kitu, ninachotaka ni mwanangu tu" Harry aliongea kwa jazba,

"Tufanye makubaliano kwanza, nikifika utanipa nusu, na ukimuona mwanao utamalizia iliyobaki" Dalali aliongea,

"Sawa, upo wapi nije?" Harry alimuuliza Dalali,

"Nielekeze ulipo nije kukuchukua, maana nina gari" Dalali aliongea,

"Nipo osterbay, nyumba namba 53" Harry alijibu,

"Nipe robo saa, nitakuwa hapo" Dalali alijibu kisha akakata simu, akatoa tabasamu jingine la pesa, maana aliamini muda mchache ujao atakuwa tajiri mkubwa katika ukoo wao.

Kwa upande wa Harry baada ya simu kukatwa, akamtupia jicho Taita, maana muda huo walikuwepo wote wakijadili jambo hilo na pia juu ya kupotea ghafla kwa Toisa. Simu ya dalali ilipokatwa, Taita na wenzake wakakusanya vijana wapatao kumi, ndio wakapanga wataongozana na huyo msamalia ataekuja kuwapeleka kwa huyo Dada anateishi na mtoto wa Harry.

Harry alikuwa na haraka na mchecheto wa kutaka kumuona mtoto wake, na muda huo alikuwa anahesabu kiasi cha pesa ili amkabidhi huyo msamalia mwema atakayekuja, kwake Harry pesa hakuona tamu muda huo, alimuhitaji binti yake tu.

Vijana wa Taita wakiwa getini pamoja na wakuu zao, ndipo walipoiona gari ndogo ikisimama mbele yako na dereva wa gari ile akashusha kioo, ila cha ajabu watu wote pale walikuwa wamepigwa na butwaa na kumfanya Dalali ashindwe kuelewa sababu ya watu wale kumtolea macho,

"Mkamateni mpumbavu huyu" Harry aliwaamrisha vijana wa Taita kwa hasira na kufanya Dalali achoke kabisa, akahisi amegeukwa...........

*********ITAENDELEA***********

the Legend☆
 
RIWAYA : SALA YA SARAH.

MTUNZI : ALEX KILEO

SEHEMU YA ISHIRINI.

ILIPOISHIA.

Harry alikuwa na haraka na mchecheto wa kutaka kumuona mtoto wake, na muda huo alikuwa anahesabu kiasi cha pesa ili amkabidhi huyo msamalia mwema atakayekuja, kwake Harry pesa hakuona tamu muda huo, alimuhitaji binti yake tu.

Vijana wa Taita wakiwa getini pamoja na wakuu zao, ndipo walipoiona gari ndogo ikisimama mbele yako na dereva wa gari ile akashusha kioo, ila cha ajabu watu wote pale walikuwa wamepigwa na butwaa na kumfanya Dalali ashindwe kuelewa sababu ya watu wale kumtolea macho,

"Mkamateni mpumbavu huyu" Harry aliwaamrisha vijana wa Taita kwa hasira na kufanya Dalali achoke kabisa, akahisi amegeukwa...........

***********ENDELEA***********

Bumbuwazi likaamia kwa dalali sasa, akawa anajiuliza kule ni kugeukwa ama ni kitu gani? Dalali akiwa bado katikati ya maswali, tayari vijana wa Taita walikuwa wameshamkamata na kumshusha kwenye gari kwa amri ya Harry.

Kipindi chote hicho Taita mwenyewe alikuwa akishangaa huku akiwa hajui ni kwanini msamalia mwema huyo anafanywa hivyo,

"Mpelekeni chumba cha mateso" Harry aliamrisha vijana,

"Mateso tena?" Dalali aliuliza huku akiwa ahamini kinachomtokea,

"Kaa kimya, hutakiwi kuongea" Harry alifoka kwa hasira,

"Lazima niongee kama naona jambo haliendi sawa" Dalali aliongea ila safari hii hakujibiwa kwa mdomo, alijibiwa na makofi kutoka kwa vijana wa Taita waliokuwa wamemshika na kumpeleka ndani, katika chumba cha mateso.

Huku nje alibaki Harry, Trigger, Taita na Tekso ambao walikuwa makini kufuatilia kile kinachofanywa na vijana wao,

"Harry sielewi ni kwanini unamfanya hivi huyu mtu ambaye ni msamalia mwema" Taita aliongea huku mshangao ukijionesha dhahiri machoni pake,

"Hii gari aliyokuja nayo ndio gari ambayo ilikuwa ikinifuatilia siku ile nilipovamiwa nyumbani kwangu" Harry aliongea na kumfanya Taita ashtuke sasa,

"Yeah, gari ndio hili hili tulilokuwa tunalifuatilia kutokana na maelekezo ya yule Dada wa guest kule" Tekso aliongea huku akitingisha kichwa chake,

"Sasa mtekaji si ni mwanamke? kwanini mnataka kumuadhibu huyo mwanaume?" Taita aliuliza swali la kipumbavu,

"Kama gari iliyotumika ni moja, basi inawezekana kabisa wanafahamiana" Tekso alitoa jibu,

"Twendeni ndani tukamuhoji" Harry aliongea huku akielekea ndani na wenzake wakamfuata, walielekea moja kwa moja mpaka ndani ya chumba cha mateso na kumkuta bwana dalali akiwa amewekwa juu ya kiti huku mikono yake ikifungwa kwa nyuma kwa kutumia kamba ngumu.

"Ndugu yangu, hatutaki kukutesa wala kukuumiza, tunachotaka ni ukweli wako tu" Harry aliongea huku akiwa amesimama mbele ya Harry,

"Ukweli upi? Kama ukweli niliouongea umenifikisha hapa na kufanywa mateka" Dalali aliongea huku akitabasamu, halikuwa tabasamu la furaha,

"Hiyo gari uliyokuja nayo ni ya nani?" Harry aliuliza,

"Ni gari yangu" Dalali alijibu,

"Unafanya kazi gani?" Tekso aliingilia kati na kuuliza,

"Mimi ni dalali, tena maarufu sana" Dalali alijibu,

"Ndiyo huyu huyu" Tekso aliongea huku akimgeukia Taita na kufanya Dalali ajiulize maswali kibao,

"Tofauti na wewe, ni nani anayeendeshaga gari yako?" Harry alimtupia swali Dalali,

"Ndio huyo Dada sasa ambaye ndio yupo na huyo mtoto wa kike mnayemtafuta" Dalali alijibu,

"Huyo Dada mna uhusihano naye gani?" Taita aliuliza,

"Mimi ndiye nilimsaidia kupata nyumba ambayo anaishi mpaka sasa, ndipo tukafahamiana mpaka leo" Dalali alitoa jibu na kufanya Harry na Trigger watazamane,

"Unaweza kutupeleka anapoishi?" Trigger aliuliza,

"Ndicho kilichonileta hapa, ila sio bure, maana tangazo lenu linasema msamalia mwema atalipwa" Dalali alijibu,

"Utalipwa" Harry alijibu,

"Sasa kulikuwa na sababu gani ya kunikamata na kunifunga?" Dalali aliuliza,

"Sababu umeshaijua, mfungueni" Trigger alijibu kisha akatoa amri iliyotekelezwa na vijana, Sasa Dalali alikuwa hana kamba tena mwilini, alikuwa huru,

"Tupeleke sasa" Harry aliongea,

"Ngojeni kwanza, ni nani nilikuwa naongea nae kwenye simu?" Dalali aliuliza huku akimtupia macho kila mmoja,

" ni mimi hapa" Harry alijibu,

"Nipe advansi kwanza kabla sijawapeleka uko, alafu mkishampata mtoto wenu mtanimalizia pesa iliyobaki" Dalali aliongea huku akimtazama Harry,

"Twende wewe, ujue tumekuheshimu sana ndio maana hatujakudhuru?" Tekso aliongea huku akimvuta Dalali kwa lengo la kumuinua kwenye kiti,

"Muache kwanza" Harry aliongea kisha akatoa pesa kwenye mifuko yake ya suruali na kumkabidhi Dalali, Dalali akaanza kuzihesabu,

"Hapo sawa, maana hii ni biashara" Dalali aliongea huku akitabasamu,

"Haya tupeleke sasa" Taita aliongea na kisha Dalali akasimama na kutangulia mbele huku wakina Taita wakimfuata kwa nyuma mpaka nje ambapo ndipo kulikuwepo na magari,

"Lete funguo ya gari lako, nitaendesha mimi na wewe utakaa pembeni utakuwa ukinielekeza" Harry aliongea huku akiwa amesimama kwenye mlango wa dereva wa gari la Dalali,

"Sawa, ni wewe tu bosi" Dalali aliongea huku akitabasamu na kumpa funguo Harry. Harry akaingia ndani ya gari na kuiwasha, ila kabla hajaondoka simu yake ilianza kuita, akaitoa mfukoni na kuangalia namba ya mpigaji, haikuwa ngeni, aliikumbuka kuwa ni ile aliyowahi kutumia mtekaji baada ya kumteka mwanae, Harry akapokea na kuweka simu sikioni huku akiwa na wasiwasi,

"Nakupa siri Harry, toka mwenyewe na uangalia kwenye injini,ya hilo gari ulilokuwepo alafu ukimaliza nitakupigia" Sauti ya kike iliongea na kukata simu, Harry akataka amshirikishe dalali ila akasita, akahisi lao moja, Harry akazima gari na kutoka na funguo, akaenda mpaka mbele ya gari na kufungua boneti, hapo ndipo alipoliona Bomu likiwa limepachikwa pembeni ya rejeta, Harry akapiga kelele huku akikimbia na kufanya wenzake wahisi kuna hatari. Dalali akabaki anashangaa huku akiwa ahisi kitu, ila alichofanya ni kufungua mlango ili atoke aulize, alipofungua tu mlango tena kabla hajashusha hata mguu, bomu likaitika, tena lililipuka kwa nguvu na kuirusha ile gari juu angani na kuitupa chini na kuiacha ikiwaka moto.

Muda huo Taita na wenzake walikuwa wamelala chini ya magari yao huku wakiushuhudia ule mchezo wa hatari uliokuwa ukifanyika mbele ya macho yao, na Harry alikuwa kwa mbali akilitazama lile tukio huku akiwa amepoteza matumaini ya kumpata binti yake.

Harry akaanza kuwasogelea wenzake huku akiliangalia lile gari likiteketea na chini alikuwepo yule bwana Dalali akiwa amelala huku akiwa hana miguu na mwili wake ulionekana hauna dalili tena za uhai.

Harry akiwa amewakaribia kabisa wakina Taita, simu yake iliita, alipoiangalia namba alikuta ni ile ya mtekaji, Harry akapokea haraka,

"Kwanini unataka kuniua?" Harry aliuliza kwa hasira baada ya kupokea simu,

"Ningetaka kukuua wala nisingekuambia uangalie kwenye injini, ningelipua tu bomu na ungekufa" Sarah aliongea kisha akacheka,

"Na kwanini hukutaka nife?" Harry aliuliza huku akishangaa jibu la huyo mwanadada,

"Najua hupendi kufa, ila sikutaka ufe kwa sababu nataka nikuumize kihisia, kisaikolojia na kimwili mpaka utakapoona ni bora ufe, hapo ndipo nitakuua" Sarah alijibu katika sauti tulivu na kumfanya Harry jasho limtoke,

"Hivi wewe ni nani na unatutaka nini sisi?" Harry aliuliza kwa upole,

"Mtanijua wakati ukifika, na siku ambayo mtanijua, ndiyo hiyo siku nitaanza kuwaua nyie viongozi wa kakikundi chenu cha kishenzi, acha nidili na vibaraka kwa sasa" Sarah alijibu,

"Nikupe nini ili umuache mwanangu?" Harry aliuliza,

"Sitaki chochote, mwanao nitamrudisha kesho, kesho jioni" Sarah alijibu,

"Nakuomba ufanye hivyo" Harry aliongea,

"Nipe niongee na Taita, namuona yupo upande wako wa kushoto" Sarah aliongea na kufanya Harry ageuke huku akiamini Sarah yupo eneo hilo, Harry akampa simu Taita kisha Harry akamfuata Tekso na kumnong'oneza afanye kitu katika mtandao ili wajue Sarah yupo upande gani? Tekso akatoa simu yake kisha akabonyeza bonyeza na hapo ile sauti ya Sarah ikawa inasikika ndani ya simu mbili, yaani simu ya Harry ambayo alikuwa anaongea nayo Taita, na simu ya pili ni simu ya Tekso.

"Taita, Taita, vijana wako waambie mimi sio mtu wa kawaida, wajiangalie namna ya kunifuata, vinginevyo nitawamaliza wote" Sarah aliongea kisha akaweka kituo,

"Mbona hakuna kijana wangu anaekufuatilia" Taita aliongea huku akiwa hajiamini,

"Toisa nipo nae hapa, au sio kijana wako huyu?" Sarah aliuliza,

"Sina mtu anaeitwa hilo jina" Taita alijifanya hamjui kijana wake,

"Sawa, nitamleta kesho pamoja na mtoto wa Harry, ili umkane akiwa anakusikia. Nawatakia majukumu mema, tchao" Sarah aliongea kisha akakata simu.

Kipindi hicho ambacho Sarah alikuwa akiongea na Taita, tayari Tekso akiwa na vijana wawili walikuwa wanafuatilia eneo ambao mpiga simu huyo alionekana kuwepo, kwa maelezo ya simu ya Tekso yalionesha mpigaji yupo mtaa huo huo, na hata Sarah alipokata simu bado simu ya Tekso iliendelea kusoma alipo mpigaji.

Tekso na wenzake walitembea mpaka katika nyumba moja iliyopo mtaa huo huo na kusimama getini, wakaanza kugonga, ila hawakujibiwa, wakaamua waruke ukuta na kuingia ndani. Bado simu ya Tekso ilikuwa ikaendelea kuonesha na muda huu iliekekeza mpigaji yupo kwenye kajumba cha pembeni yao, baada ya kukachunguza kale kajumba waligundua ni choo cha nje, wakajipanga mlangoni na kuvamia kwa fujo, hawajakuta mtu isipokuwa simu tu iliyokuwa juu ya sinki la choo,

"Aaaagh shit, ichukue hiyo line" Tekso aliongea kwa hasira na kutoka zake nje na kumuacha kijana wake mmoja akiokota mfuko wa nylon na kuuvaa ili aichukue ile simu.

***************

Kitu ambacho Sarah alikifanya ni kufunga vinasa sauti kila sehemu ya gari la Dalali, na pia hata lile bomu aliliweka siku nyingi huku akiamini ni lazima ipo siku lile gari linaweza kumuweka hatiani, ila hakujua kuwa yule Dalali pia anaweza kumuingiza matatizoni.

Na hata Dalali alipowasiliana na Harry, Sarah alisikia kila kitu, alichofanya ni kusogea tu eneo ambalo Harry alimuelekeza Dalali ajongee. Sarah alipofika aliingia kwenye nyumba ya tano kutoka nyumba ya Taita na kuanza kufuatilia namna Taita na wenzake wanavyojipanga kwa ajili ya kwenda kumvamia yeye Sarah.

Sarah alichofanya ni kuilipua ile gari ya Dalali huku Dalali akiwa ndani kwa maana aliamini mtu mwenye ramani ya kuwafikisha maadui kwake ni dalali peke yake, pia alifanya hivyo kwa maana aliona dalali hakuwa mtu mwema tena kwake, Sarah aliiamini sana ile misemo ya "dawa ya ubaya ni ubaya na dawa ya moto, ni moto".

Baada ya hiyo, Sarah akaiweka simu chooni na kuondoka zake baada ya kugundua kuna vijana wa Taita wanamfuata eneo lile.

************

Siku iliyofuata ambayo ndio Sarah aliahidi kumrudisha mtoto wa Harry.

Mida ya saa kumi jioni mlinzi wa Taita aliingia sebuleni huku akiwa amebeba mabox mawili, moja kubwa na jingine dogo, na yote yalikuwa yamefungwa na karatasi za kuwakawaka au karatasi za zawadi "gift paper". Sebuleni walikuwepo wote, walikuwa wanasubiri kupigiwa simu na Sarah, maana waliamini hivyo kwa kuwa Sarah aliwaahidi kuwapelekea mtoto wao.

"Zimetoka wapi?" Taita aliuliza kwa uoga huku akiwa hajiamini kabisa,

"Zimeletwa na gari za airport, zile zinazoletaga bahasha mizigo kutoka kwa Vin" Mlinzi alijibu,

"Aah sawa" Taita alijibu kisha akabeba box moja lile kubwa na kuiondoa ile karatasi ya Zawadi,

"Box zito hilo, sijui vin amenitumia nini?" Taita aliongea kisha akakichomoa kikaratasi kidogo kilicho na maneno kilichokuwa juu ya box, kilikuwa kimeandikwa. "Kubwa ni lako, na dogo ni la Harry"

Baada ya kusoma hivyo, Taita akatabasamu,

"Leo Vin amekukumbuka" Taita aliongea huku akimpa kile kikaratasi Harry aliyekuwa na mawazo, Harry akakisoma kisha lile box dogo akalivutia kwake,

"Fungua tuone zawadi" Trigger alimtania Harry huku akicheka ila Harry wala hakujisumbua kutaka kufungua lile box.

Mzee mzima Taita alikuwa akiendelea kupasua lile box, na sasa ilifika hatua moja tu ya kulifungua ili ajue zawadi iliyomo, macho ya watu wote yalikuwa ndani ya ilo box, Taita akalifungua, wote wakashtuka baada ya kukuta kichwa cha mtu, tena Taita aliruka kidogo adondoke,

"Kitoe" Taita alimwambia Trigger huku Taita akiwa amesimama mbali kabisa, Trigger akakitoa kile kichwa, hapo ndipo wate walipigwa na mshangao, kilikuwa kichwa cha Toisa, kilitisha kwa kweli na puani kiliwekewa karatasi iliyokuwa na maneno yaliyoandikwa "ndio haki ya mwenye dhambi, kila damu yenye dhambi itaigharimu familia yake. Mchuma janga hula na ndugu zake"

Hayo maneno na kilichomo ndani ya box lile kubwa kilimtisha sana Harry pamoja na wengine.

Harry akaamini sasa lile box dogo litakuwa na kichwa cha mwanae. Harry akalifungua kwa pupa na kukuta karatasi iliyoandikwa "leo ni siku ya kukumbukwa katika familia yako, hii Zawadi haijatoka kwa Vin, ni zangu mimi mtu mbaya kabisa"

Baada ya Harry kusoma maneno hayo, nguvu zikaanza kumuishia na kushindwa kufungua box, Trigger akaliendea box na kulifungua, Harry akashindwa hata kuangalia, machozi yalikuwa yakimtoka huku Trigger aliyekuwa jirani na box akibaki na mshangao.............

*********ITAENDELEA**********

the Legend☆
 
RIWAYA : SALA YA SARAH.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA.

ILIPOISHIA............

Hayo maneno na kilichomo ndani ya box lile kubwa kilimtisha sana Harry pamoja na wengine.

Harry akaamini sasa lile box dogo litakuwa na kichwa cha mwanae. Harry akalifungua kwa pupa na kukuta karatasi iliyoandikwa "leo ni siku ya kukumbukwa katika familia yako, hii Zawadi haijatoka kwa Vin, ni zangu mimi mtu mbaya kabisa"

Baada ya Harry kusoma maneno hayo, nguvu zikaanza kumuishia na kushindwa kufungua box, Trigger akaliendea box na kulifungua, Harry akashindwa hata kuangalia, machozi yalikuwa yakimtoka huku Trigger aliyekuwa jirani na box akibaki na mshangao.............

*********ENDELEA**********

Mshangao aliokuwa nao Trigger ulikuwa mkubwa sana, akawageukia wenzake na kuwakuta nao wakimtazama yeye kwa maana wao walikuwa mbali huku wakitegemea kuwa na lile box dogo litakuwa na kichwa cha mtu, tena kichwa cha Princess ambaye ni mtoto wa Harry.

Trigger akarudisha macho kwenye box na kuingiza mkono kisha akalichana zaidi lile box na kilichopo ndani kikaonekana, ilikuwa ni keki iliyokuwa na neno "HAPPY BIRTHDAY PRINCESS HARRY", hapo Harry akasogea jirani na Trigger kisha akatabasamu peke yake, alikumbuka kuwa ni kweli hiyo tarehe ya leo ni siku ya kuzaliwa binti yake huyo.

Harry alitabasamu lakini hakuwa na furaha, kwa maana hakuwa na uhakika na uhai wa mwanae ingawa alipewa hiyo keki na mtekaji kama Zawadi ya mwanae, Harry akiwa amesimama tu huku akiwa hajui afanye nini, simu yake ilianza kuita, alipoitazama alikuta ni namba ya mtekaji, tena ile ile ya kila siku, Harry akaipokea simu kwa pupa,

"Pole kwa presha mwanasheria, chukua hiyo keki ipeleke nyumbani kwako, utamkuta mwanao" Sarah aliongea kisha akakata simu na kumuacha Harry akiitazama simu yake, Harry akaamua ampigie mke wake ili amuulize kama kweli Princess amerudishwa, lakini simu ya mke wake ikawa haipatikani,.

"Vipi kuna usalama?" Taita alimuuliza Harry,

"Sijajua bado, ila mtekaji amenipigia simu na kuniambia mtoto mmempeleka nyumbani" Harry alijibu Taita,

"Mpigie mkeo umuulize" Taita alimwambia Harry,

"Simu yake haipo hewani" Harry alijibu,

"Basi twende kwako" Taita alimshauri Harry,

"Sawa twende" Harry aliongea huku akitangulia kutoka nje na Taita akimfuata kwa nyuma, walipofika nje wakaingia ndani ya gari na kuliondoa.

*******************

Sarah alikuwa ndani ya bajaj huku akiwa amempakata Princess. Bajaj ilipofika katika mtaa anaoishi Harry, nyumba ya tano kutoka nyumba ya Harry, Sarah aliiamuru bajaj isimame, kisha Sarah akatelemka na kumlipa pesa yake dereva bajaj, kisha bajaj ikaondoka,

"Unapajua nyumbani?" Sarah alimuuliza Princess,

"Ndio, palee" Princess alijibu huku akionesha kwa kidole nyumba yao,

"Haya nenda" Sarah alimwambia Princess,

"Twende wote aunty, unataka kunitoroka" Princess aliongea huku akiwa amemshika mkono Sarah,

"Tangulia Princess, ngoja nikanunue chocolate" Sarah aliendelea kumbembeleza Princess,

"Sitaki aunty, unataka kuniacha" Princess aliendelea kumshika Sarah huku akilia,

"Shika hii, ipeleke ndani alafu urudi ili tuondoke wote tukanunue chocolate" Sarah aliongea huku akiivua saa yake na kumpa Princess,

"Sitaki aunty" Princess aligoma, tayari alimpenda Sarah kwa namna alivyoishi nae vizuri,

"Shhhhhh.....si unajua sipendi mtoto mkorofi? Nenda ndani kwanza" Sarah aliongea kwa ukali na kumfanya Princess akubali kuondoka ila kwa shingo upande, Sarah alisimama huku akimuangalia Princess aliyekuwa anatembea huku kila muda akigeuka nyuma kuangalia kama Sarah bado yupo. Princess alivyoingia tu ndani ya geti, Sarah akageuka na kuanza kuondoka taratibu na muda huo alikuwa anapishana na gari aliyokuwepo Harry na Taita, Sarah aliwaona akatabasamu peke yake ingawa wanaume hao hawakuweza kumgundua Sarah kutokana mavazi aliyovaa, alivaa dela pana na kichwani alijifunga ushungi huku macho yake yakiwa yamefunikwa na miwani pana za kisasa.

Harry alipofika getini alishuka taratibu huku akiwa hana uhakika kama kweli mtoto wake amerudishwa. Harry alipofika getini ili asukume mlango, alishangaa kuona mlango ukifunguka, ulifunguliwa na mke wake ambaye nae alikuwa anatoka mbio huku akiwa amemshika mkono Princess,

"Yupo wapi?" Mke wa Harry alimuuliza Princess,

"Aunty alikuwepo pale, atakuwa ameenda dukani kununua chocolate" Princess alijibu huku akionesha kwa kidole eneo ambalo alikuwa amesimama Sarah hapo hawali,

"Nani, eti Princess?" Harry aliuliza kwa wasiwasi huku akimbeba mwanae,

"Anadai amekuja na aunty yake, ndio nataka anioneshe yupo wapi huyo aunty yake?" Mke wa Harry alijibu,

"Twendeni ndani" Harry aliongea huku akisukumia mkewe ndani, nae akaingia huku Taita akija kwa nyuma.

Safari yao iliishia sebuleni kwa Harry,

"Princess amekuja muda gani?" Harry aliuliza,

"Sawa hivi yaani, hana hata dakika tatu" Mke wa Harry alijibu,

"Toto hujaumizwa?" Harry alimuuliza mtoto wake huku akimgeuza geuza,

"Sijaumia" Princess alijibu,

"Ulikuwa wapi?" Harry alimuuliza,

"Kwa aunty" Princess alijibu,

"Wapi?" Harry aliuliza tena,

"Kwenye nyumba yake, kuna chocolate na maziwa, anko Toisa anapajua" Princess alijibu na kufanya Taita amtazame Harry,

"Anko Toisa ulimuona kumbe?" Harry aliuliza,

"Alikuja alafu akaondoka kuniambia, alinitotoka" Princess alijibu,

"Acha maswali na wewe, twende tukatoe taharifa polisi" Mke wa Harry aliongea, kisha Harry akaondoka na mke wake na wakaelekea kituoni kutoa taharifa.

Taita alirudi moja kwa moja kwake na kukuta vijana wake wakiwa wamesimama tu wakikiangalia kichwa cha Toisa,

"Trigger na wewe umekuaje siku hizi, yaani umekosa maarifa ya kukifanya hiki kichwa?" Taita aliuliza kwa ukali,

"Tumeshakubaliana kuwa tutakizika na shimo tumeshachimba, ila sasa tulikuwa tunakusubiri ili tuone kama una wazo tofauti na letu" Trigger alijitetea,

"Kazikeni tu, tena kwa uangalifu sana" Taita aliongea huku akielekea chumbani kwake,

"Alafu kuna ujumbe mwingine chini ya box" Trigger aliongea na kumfanya Taita asimame,.

"Umeandikwaje?" Taita aliuliza,

"Mungu naomba nikiwa mkubwa niwe nawaka kama moto" Trigger alisoma ujumbe ulivyosomeka na kumfanya Taita afikirie kidogo kwa muda,

"Hayo maneno kama nayajua, sijui nimewahi kuyaona wapi?" Taita alijiuliza mwenyewe,

"Sio kwenye biblia?" Trigger aliuliza,

"huenda" Taita alijibu na kuupuuza na kuingia zake ndani na kuwaacha vijana wake wakikibeba kichwa cha Toisa na kuelekea nacho nyuma ya nyumba.

******************

Jumapili moja tulivu, Sarah alielekea makaburini kule walipozikwa baba na mama yake, akaenda moja kwa moja na kupiga magoti katikati ya makaburi, akafunga macho,

"Sidhani kama ninachokifanya kinaudhi, naimani mnakifurahia kwa maana sifanyi kwa ajili yangu, bali kwa ajili yenu. Kazi niliyoianza sio rahisi, ni ngumu sana na inahitaji utulivu wa mwili na akili. Nimeficha sana wajihi wangu kwa maadui, sasa nadhani nahitaji kujionesha, nahitaji wanijue ili wajue kwanini nafanya hivi" Sarah aliongea kwa mtindo wa sala kisha akafungua macho yake na kuvitoa vikaratasi viwili vyenye maneno na kuvibandika juu ya makaburi ya wazazi wake.

Sarah alipotoka hapo alielekea kanisani, lile kanisa ambalo alitoa Sarah ambayo ilifanya watu wote waangue kicheko. Sarah akaomba aonane na askofu mkuu wa kabisa, akaelekezwa ofisi ilipo na kuingia,

"Naitwa Sarah, mimi ndiye niliyeomba ile sala iliyobandikwa pale mbele katika kabisa, nilifanya hivyo miaka kumi na Tisa iliyopita" Sarah aliongea na kufanya askofu ashangae,

"Ulikuwa Wapi muda wote? tulikutafuta sana kwa maana walitokea watu waliovutiwa na kile ulichokiomba na wengi walikuwa wanataka kukudhamini, ni raia wa nje" Askofu alimuuliza Sarah,

"Nilikuwa uingereza, nimerudi kutimiza ile Sarah" Sarah aliongea na kumfanya Askofu amshangae,

"Kivipi? kwa hiyo sasa hivi unawaka kama moto?" Askofu aliuliza,

"Ndio, naweza kumuunguza yoyote" Sarah aliongea kisha akacheka ili kufanya maongezi yake yawe kama utani,

"Karibu Sarah, umetuletea kutoka uingereza?" Askofu aliuliza,

"Sijaleta kitu kwa kweli, ila nitawafanyia kitu kabla sijarudi uingereza" Sarah aliongea,

"Ooh kumbe sio mkaaji tena nchini, unasoma uko?" Askofu aliuliza,

"Hapana, ni mfanyakazi wa serikali ya uingereza" Sarah alijibu,

"Hongera sana Sarah, itabidi nikakutambulishe kwa maana sala yako bado maarufu mpaka leo" Askofu aliongea,

"Sawa" Sarah alijibu huku akitabasamu.

Askofu alimchukua Sarah na kuongozana nae mpaka ndani ya kanisa, uzuri walikuta misa ya kwanza ikielekea ukingoni na pale ulikuwa muda wa kusoma matangazo.

Askofu akaenda mpaka kwa padri aliyekuwa anaongoza misa na kuongea nae kidogo kisha wakakaa kimya wakimsubiri mtoa matangazo amalize.

Baada ya muda yule bwana aliyekuwa anatoa matangazo alikuwa amemaliza na sasa askofu akachukua kipaza sauti, kisha akawasalimu waumini waliohudhuria ibada, baada ya hapo akairudia ile sala iliyowahi kuombwa na Sarah miaka mingi iliyopita, wakati akiirudia ile sala, Taita alishtuka, tena uzuri alikuwa amekaa kiti cha mbele kabisa pamoja na Harry ambaye nae alipata mshtuko,

Masikio na mwili wa Taita vikapata ubaridi kwa pamoja wakati askofu akiirudia ile sala, Taita akakumbuka na ule ujumbe aliouona kwenye box upande wa chini, box ambalo kiliwekwa kichwa cha Toisa, ila bado Taita alisubiri kusikia ni kipi askofu ataongea baada ya kuirudia sala ile,

"Sasa baada ya kuirudia sala hii iliyowahi kuombwa na mtoto mdogo miaka kumi na Tisa iliyopita, leo hii huyu mtoto yupo hapa, namuomba asogee mbele" Askofu aliongea kisha Sarah akawa anajongea mbele huku waumini wakimpigia makofi. Sarah alipofika mbele akapewa kipaza sauti,

"Naitwa Sarah, Sarah Isack" Sarah aliongea kisha akatupia macho mahali walipokaa Taita na Harry na kuwaona namna walivyopata mshtuko, tena sio kidogo........

**********ITAENDELEA***********

the Legend☆
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom